Thursday, May 12, 2011

SI HAKI KUFUNGA SHULE KWA UTOFAUTI WA ITIKADI ZA VYAMA

Wabunge Chadema wageuka mbogo  Send to a friend
Wednesday, 11 May 2011 21:27
0diggsdigg
Boniface Meena, Kwela
WABUNGE wawili wa Chadema jana walikuwa mbogo baada ya kufanya ziara katika Kijiji cha Lusaka, Jimbo la Kwela, mkoani Rukwa na kubaini  Shule ya Sekondari Lusaka imefungwa bila maelezo.Mbali na hilo wabunge hao waliwaeleza wananchi kwamba wamebaini mbolea ya ruzuku inayotolewa na serikali ni ufisadi mtupu kwa sababu wananchi wanatozwa fedha nyingi kununua mbolea ya ruzuku.

Wananchi wa Kijiji cha Lusaka walilalamika mbele ya wabunge hao kwamba Serikali imekuwa ikiwanyanyasa na kibaya zaidi imefunga Shule ya Sekondari ya Kijiji hicho baada ya wananchi wa eneo hilo kumchagua Diwani wa Chadema.

Mbali na hilo wananchi hao walilalamika mbele ya wabunge hao kwamba shule hiyo iko moja tu katika eneo hilo na ilifungwa ghafla miezi mitatu iliyopita na viongozi wa Seriklali wa Manispaa ya Sumbawanga Vijijini bila kutoa maelezo yoyote.

Baada ya kusikia malalamiko ya  wananchi wa eneo hilo, Mbunge wa Viti Maalumu kutoka mkoani Arusha, Joyce Mukya na Raya Ibrahimu kutoka Zanzibar walikwenda katika shule hiyo na kuwaona madiwani wakiendelea na kikao na kushindwa kupata maelezo kutoka kwa madiwani na mbunge wa jimbo hilo.

Mukya aliwaambia wananchi hao kwamba atapambana na viongozi wa halimashauri hiyo ili ajue ni kwa nini shule hiyo imefungwa bila maelezo na kusababisha wanafunzi kutokwenda shuleni.

"Yani ni aibu, nitakufa nao kwa kuwa wamefunga shule halafu wanafanyia vikao vya madiwani kwenye majengo ya shule bila kujali haki za wanafunzi kusoma, hawa watu sijui ni wa aina gani,"alisema Mukya.

Alisema hilo ni moja ya maswali atakayowasilisha bungeni kwenye maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu ili aelezwe ni kwa nini shule hiyo imefungwa."Kata ina vijiji vitano, tunataka tujue ni kwa nini shule imefungwa, tutaliwasilisha bungeni kutaka kujua hilo. Inashangaza sana kwa nini mbunge wenu ananyamaza kuhusu shule kufungwa na anafanya mikutano huko ndani bila hata kujali,"alisema.

Raya Ibrahimu alionekana kuchukizwa na kitendo hicho na kuishambulia serikali kwa kushindwa kuwajali wananchi wake hasa wanachanga fedha zao kujenga shule, lakini zimekuwa zikifungwa bila wananchi kuelezwa sababu za kufanya hivyo.

"Unajua hawa watu wanatia aibu, mimi sijui ni wa aina gani watu wazima wanafunga shule bila kufikiria madhara gani wanafunzi wanapata, halafu wakikimbilia mijini wanalalamika," alisema.

Alisema kitendo kilichofanywa na Serikali kinatia aibu kwa kuwa kinasababisha vijana kukimbilia mijini kwa ajili ya kuuza pipi na biskuti.

Raya alisema suala la huduma za jamii limekuwa ni vituko kijijini ambako kuna barabara mbovu na aliwashauri wananchi kuipunzisha CCM ili wajifunze kuwajali wananchi wao.

Kuhusu mbolea alisema ni bora serikali ikaondoa ruzuku kwenye mbolea ili ishuke bei na wananchi wanunue kwa bei ya chini."Serikali iondoe vocha za ruzuku kwa kuwa zinafaidisha watu wachache na kuwaumiza wananchi wengi ambao ni masikini,"alisema Mukya.

Alisema nchi inanuka rushwa kwa sababu wananchi wamekwua wakilalamika kutopata mbolea kwa kuwa kila mtu ni mla rushwa."Viongozi wa CCM wanachukua zile vocha wanajigawia. mwananchi maskini akitaka vocha mpaka utoe rushwa, mbolea ni kwa ajili yenu ninyi watu maskini ili mjikomboe kwa vijana kufanya shughuli za kilimo, lakini inashindikana kutokana na ufisadi unaofanyika kwenye vocha hizo,"alisema Mukya.

LOLIONDO IKIWEKEWA MIKAKATI MIZURI INAWEZA KULIINGIZIA TAIFA PESA NYINGI ZA KIGENI,WAZIRI WA UTALII UNAMPANGO GANI?

Marais, mfalme watarajiwa kutua Samunge kwa Babu  Send to a friend
Wednesday, 11 May 2011 21:50
0diggsdigg
Abiria waliofika kwa mchungaji Ambilikile Mwasapila katika kijiji ch Samunge kunywa dawa jana, wakiteremka kutoka katika helikopta inayomilikiwa na kampuni ya Akagera aviation ya Rwanda. Picha na Mussa Juma
Mussa Juma, Samunge
MARAIS kadhaa wa nchi za Afrika akiwamo mfalme, wanatarajiwa kwenda Samunge, Loliondo kupata tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Ambilikile Mwasapila.

Kutokana na ujio huo, ulinzi umeimarishwa kuanzia jana. Ofisa mmoja wa polisi wa Wilaya ya Ngorongoro, alithibitisha ujio wa wakuu hao bila ya kutaka kutoa maelezo zaidi. Hakutaja siku wala muda ambao watawasili hapa.
Jana kulikuwa na idadi kubwa zaidi ya polisi kijijini hapa. Ofisa mwingine wa polisi ambaye pia hakutaka jina lake liandikwe alisema, wamepokea taarifa za ujio wa marais hao na walitegemea kwamba wangewasili Samunge kuanzia jana.

 "Ni kweli, kuna wageni watakuja. Nadhani ni wakubwa bado taarifa kamili hazijatufikia watatua lini," alisema.
Helikopta kutoka Rwanda inayomilikiwa na Kampuni ya Akagera Aviation, imeanzisha safari za kwenda Samunge kila siku ikitokea Uwanja wa Ndege wa Arusha.

Helikopta hiyo ni kubwa kuliko nyingine ambazo zimekuwa zikitua Samunge kuleta wagonjwa kupata tiba ya kikombe kwa Babu.Ujio wa helikopta hiyo, sasa unalifanya anga la Samunge kutawaliwa na helikopta nne, zinazofanya safari takriban mara tatu kwa siku kwenda na kutoka Samunge.

Gharama za nauli kwa abiria mmoja kutoka Arusha hadi Samunge kwa helikopta hiyo ya Rwanda ni Dola za Marekani 1,000 hivyo kufanya usafiri huo kuwa wa watu wenye uwezo mkubwa kifedha.
 Baada ya kuongezeka wimbi la viongozi kutoka nchi jirani ya Kenya wanaofika Samunge na habari zao kuandikwa, sasa vigogo wengi wa huko wamebuni njia nyingine ya kufika kijijini hapo bila kujulikana.

Vigogo hao sasa wanafika Samunge kupitia mpaka wa Narock ambako huenda moja kwa moja hadi Loliondo na kukodi magari ya wenyeji ili kuwapaleka Samunge.  Kwa takriban wiki mbili sasa, viongozi kadhaa wa Serikali ya Kenya, wakiwamo maofisa wa Ikulu ya Kenya, mawaziri na wabunge wamekuwa wakitua Samunge.

Babu: Wagonjwa waruhusiwe
Mchungaji Mwasapila ameomba vituo vinavyoratibu magari yanayokwenda Samunge, kuruhusu magari zaidi kupeleka wagonjwa ili wapate huduma kutokana na kupungua kwa foleni.Msaidizi wa Mchungaji Mwasapila, Frederick Nisajile alisema jana kwamba kutokana na huduma kuboreshwa, idadi ya magari yanayopaswa kuingia Samunge kwa siku yanapaswa kuongezeka.

"Tunaomba wawe na mawasiliano na sisi ya mara kwa mara kwani sasa kama unavyoona hakuna foleni, lakini kuna magari yamezuiwa maeneo ya vituo yasije huku," alisema Nisajile.

Jana, zaidi ya magari 500 yakiwamo mabasi makubwa kutoka Mikoa ya Kigoma, Dodoma, Mwanza na Arusha yalifika Samunge na abiria kupata kikombe na kuondoka.Hadi majira ya tisa jioni jana, foleni ya magari ilielekea kumalizika kabisa.

Bei ya kikombe iko palepale
Mchungaji Mwasapila jana alitoa ufafanuzi kuhusu malipo ya kikombe akieleza kuwa hajawahi kupandisha gharama zake tangu mwanzo. Alisema Watanzania wanalipa Sh500 na wageni kutoka nje ya nchi, wanalipa Dola moja au Sh1,500.

JE KAULI NAPE WA CCM INAATHARI KWA CHADEMA?

Chadema, CCM sasa ni kulipuana  Send to a friend
Wednesday, 11 May 2011 21:53
0diggsdigg
Gasper Andrew, Singida na Boniface Meena, Nkasi
VITA ya maneno baina ya vyama vikubwa vya siasa nchini CCM na Chadema, imezidi kushika kasi kwa vyama hivyo kurushiana tuhuma katika mikutano ya hadhara inayoendelea katika maeneo mbalimbali nchini.CCM kinawaita Chadema wanafiki na Chadema kinaendelea kudai kuwa chama hicho tawala ndicho kinachoisababishia nchi umasikini.

Jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM, Nape Nnauye alidai kuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa ni mnafiki kwa kula matapishi yake anapodai kuwa chama tawala kinafuja mali ya umma huku naye (Dk Slaa) akiwa katika mwelekeo huohuo.

Alidai kuwa Dk Slaa ameingia mikataba ya kukishinikiza chama chake kimlipe Sh7.5 milioni kila mwezi wakati alipokuwa mbunge alikuwa akiilalamikia serikali kwamba inawabebesha wananchi mzigo mkubwa kwa kuwalipa wabunge kila mmoja Sh milioni sita. Nape alisema hayo jana alipokuwa akizungumza kwenye mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika katikia Kituo Kikuu cha mabasi cha zamani mjini Singida.

Alisema anazo nyaraka halali za chama hicho zinazoonyesha kwamba baada ya Dk Slaa kuukosa urais, sasa amekigeukia chama chake na kuanza kukishinikiza kimlipe mshahara mkubwa kuliko aliokuwa akiupata alipokuwa mbunge.Nape alisema madai kwamba Dk Slaa haombi alipwe si ya kweli akidai kwamba ndiye anayeshiniza kulipwa kiasi hicho kwa vile ameachishwa ubunge na ameukosa urais.

"Anashangaza sana bungeni alikuwa akipanua mdomo hadi mwisho kupotosha jamii kuwa wabunge pamoja na posho, mishahara na marupurupu mengine, wanalipwa shilingi milioni sita kiasi ambacho alidai kuwa kinawaumiza wananchi. Kwa hiyo ndiyo tuseme Sh7.5 milioni ni kiwango ambacho hakitawaumiza wanachama wa Chadema na walipa kodi wengine," alihoji Nape huku akishangiliwa na wananchi waliohudhuria.

 Katibu huyo alisema kwa kitendo chake hicho cha kushinikiza alipwe kila mwezi mamilioni hayo, anapaswa kuwaomba radhi Watanzania kwa kuwadanganya alipokuwa bungeni kuwa Sh milioni sita ni mshahara mkubwa mno.
 Aidha, alisema kuwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe naye aliwahi kutoa msaada wa Fuso (malori aina ya Mitsubishi Fuso) tatu ili zikisaidie chama hicho katika shughuli mbalimbali za ustawi wake lakini sasa anakidai Sh500 milioni za ununuzi.

Madai ya Nape kuhusu mshahara wa Dk Slaa yaliwahi kutolewa maelezo na Chadema ambacho kilisema kilifikia uamuzi wa kumlipa, Dk Slaa mshahara na maslahi yanayolingana na anayopata mbunge kwa sababu ndicho kilichomshawishi aache kugombea ubunge katika Jimbo la Karatu mkoani Arusha, ambako alikuwa na nafasi kubwa ya kushinda na kumtaka agombee nafasi ya urais ambayo mgombea wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alishinda.

Kilisema uamuzi huo ulifuata taratibu zote ikiwa ni pamoja na vikao vikuu vya chama hicho, kama vile Kamati Kuu, kuidhinisha malipo hayo.Kuhusu malori Chaadema kilisema kiliamua kufanya mkakakti wa kununua magari matatu ambayo Mbowe aliyanunua na kuyatoa kwa muda ili yakisaidie kwenye kampeni.

Mbowe: CCM wanajipa mamlaka ya uungu mtu
Wakati Nape akisema hayo Mbowe amesema viongozi wa Serikali ya CCM wamelewa madaraka na kujivika mamlaka ya uungu watu na kusahau kuwatumikia Watanzania: "viongozi wa nchi hii, wanajipa mamlaka ya umungu-mtu na wananchi wanawaogopa."
Mbowe, ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alisema hayo jana alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika Uwanja wa mji mdogo wa Namanyere, Wilaya ya Nkasi, Rukwa, ikiwa ni sehemu ya operesheni ya Chadema ya kuishinikiza serikali kusikiliza kilio cha wananchi.

Alitoa mfano akisema, iwapo wananchi wa Wilaya ya Nkasi watajengewa barabara, wajue kuwa hiyo ni haki yao na pia wana haki ya kuiuliza serikali sababu za kuchelewa kujengewa kwa miaka 50 ya uhuru.
Alisema katika mkoa kama wa Kilimanjaro, wamekuwa wakijengewa barabara za lami kwa kadri inavyohitajika, tofauti na Mikoa kama ya Rukwa, Iringa, Mbeya na Ruvuma ambayo imeachwa nyuma kimaendeleo, licha ya kuzalisha chakula kinachohifadhiwa katika Hifadhi ya Chakula ya Taifa.

Kutokana na hali hiyo, alisema iwapo wananchi wa Mkoa wa Rukwa hawatapiga kelele kudai maendeleo, kamwe hawezi kushuka Malaika Gabriel kuwapigia kelele."Kwa hiyo ndugu zangu, si kila kitu ni cha kupongeza, muwatume wabunge wenu wakapige kelele," alisema Mbowe.Alisema tangu Chadema ianze kupiga kelele Rukwa, imefanikiwa kutoa Mbunge mmoja tu, Said Arfi na barabara zikianza kutengenezwa.

Mbowe alisema serikali imeshindwa kusimamia reli ya kati kiasi ambacho wananchi wanaotaka kusafiri kulazimika kutumia gharama kubwa kupata usafiri wa ndege.Alisema kuwa baadhi ya wabunge kutumia muda mwingi bungeni kuishukuru serikali katika mambo ambayo ni wajibu wake kuwatekelezea wananchi.Alisema wabunge hao wamekuwa wakifanya hivyo, huku wakijua wazi kuwa ni kinyume na jukumu la mbunge, ambalo ni kuisimamia serikali kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi.
"Kitendo cha kuishukuru serikali, ndicho kinatuchelewesha kupata maendeleo. Wananchi wanaiomba serikali, wabunge wanaishukuru..." alisema.Alisema vitendo hivyo vimechangia kwa kiasi kikubwa kuwafanya viongozi wa serikali nchini kujiona kuwa ni miungu kwa sababu wanatukuzwa.

Waliopewa siku 90 CCM wataaibika karibuni
Katika hatua nyingine, Nape alisema kuwa viongozi walioombwa na chama wajipime wenyewe na kuchukua uamuzi wa kuachia nyadhifa zao mapema kutokana na kutuhumiwa na wananchi juu ya tabia zao za kifisadi, kwamba sasa siku zao za kuja kuaibishwa, zinahesabika.

"Watu sasa wameanza kusema kuwa Nape hana nguvu tena za kupambana na ufisadi nchini, nawaambia kuwa si kweli. Sijalala wala sijaishiwa nguvu za kutokomeza ufisadi. Hawa wanaotuhumiwa kwa ufisadi wanakipa chama machungu na kuanza kukikosesha imani kwa wananchi, wanapaswa kujiondoa wenyewe na wasisubiri kuja kuapishwa kwa kufukuzwa kwa nguvu," alisema.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), John Chilingati aliwataka viongozi na wanachama wa chama hicho ngazi ya wilaya na mikoa kusaidia kukirudisha kwenye misingi yake ya awali ili wananchi waendelee kukiamini.
Chiligati ambaye pia ni Mbunge wa Manyoni Mashariki, alitoa wito huo juzi alipozungumza na wananchi wa Kata ya Ikungi, Singida.
Alisema vikao vya Halmashauri Kuu vilivyofanyika hivi karibuni mjini Dodoma, vilibaini kuwa CCM imefika mahali pabaya kwa kuanza kuacha misingi yake na kusababisha baadhi ya wanachama wake na wananchi kwa ujumla, kuanza kukosa imani nacho.

Tuesday, May 10, 2011

MAPUMZIKO NI MUHIMU KWA WANAFUNZI

Je, wanafunzi huhitaji kupumzika?  Send to a friend
Monday, 09 May 2011 21:30
0diggsdigg
Na Minael Msuya
NIMEWAHI kusikia baadhi ya wanafunzi wakilumbana kuhusu suala la mapumziko pindi wanapomaliza masomo na kurudi majumbani mwao.Malumbano yao yalinifanya nitafakari kwa kina kuhusu elimu husika na mapumziko hayo ndipo nilipojaribu kuwauliza wadau wa elimu.

Wadau hao walinifafanulia kuwa hakuna kazi isiyokuwa na mapimziko, hivyo masomo yanahitaji mapumziko ili mwanafunzi aweze kurejesha akili mpya na kufanya kazi kwa umakini zaidi.

Wanafunzi hao waliokuwa wakilumbana kuhusu mapumziko, baadhi walisema baada ya kutoka shuleni mwanafunzi anapaswa kupata muda mfupi wa kupumzika ili aweze kupata nguvu na akili yake iweze kutulia.

Walisisitiza kuwa mtu anaposoma wakati wote anachoka akili na mwili wake unashindwa kumudu kufanya hata kazi za kawaida mbali na masomo hivyo kila kitu kina faida zake katika kuimarisha mwili na akili ya mtu.
Lakini, wengine walisema baada ya kutoka shule mwanafunzi anapaswa kufanya kazi za nyumbani ili asipoteze muda wake wa kujisomea suala ambalo kimsingi halikuwa na nguvu kwa kuwa tayari wadau wa mambo hayo walisema kila kazi inahitaji mapumziko.

Katika  udadisi  wangu niligundua kuwa wapo wanafunzi wanaojitengea muda mzuri wa kusoma na kufanya kazi pindi wanapotoka shuleni lakini wanasahau kuwa wanapaswa kupata muda wa kupumzisha akili zao japo kwa robo saa.
Hata hivyo fikra zangu zilifika mbali na kujikuta nikiwamulika wazazi kuhusu kuwapangia watoto wao muda wa kazi na kusoma, hapo nilitambua kuwa wazazi wanaweza kuwa chanzo cha kuwafanyisha watoto kazi pindi wanapotoka shuleni kuliko kuwapa muda wa kupumzika na kujisomea.

Katika hili wadau wa elimu wanasema mwanafunzi anapojisomea bila mpangilio wowote ukiwemo muda wa kupumzika anaweza asifikie malengo yake kwa kuwa atakuwa anajichosha kwa kudhani kuwa atafanikiwa kumbe anapotea.

Ni vyema kila mwanafunzi akatambua wajibu wake kimasomo, kupumzika na kusaidia kazi za nyumbani ili aweze kuimarisha afya na kutengeneza msingi mzuri utakaomfanya afaulu vizuri kwa kuzingatia mambo hayo matatu.

Wazazi nao wanatakiwa kuwapangia watoto wao muda wa kupumzika, kujisomea  na kufanya kazi za nyumbani na si kuwapangia watoto kazi  wanapotoka shuleni bila kuwapa muda wa kupumzika.

Wapo baadhi ya wazazi wanawapangia watoto wao kazi nyingi pale wanapotoka shuleni bila kufahamu kuwa watoto wamechoka kwa kiwango gani walipokuwa shuleni.

Kufanya hivyo kutamsaidia mwanafunzi yeyote yule kuweza kumudu masomo yake vizuri kwa kuwa atakuwa na uwezo wa kusoma na kufanya kazi kwa wakati na hata kuweza kupumzisha akili yake pale inapokuwa imechoka.
 

MAISHA NI MAGUMU MNO,

JK: Pato litaongezeka muhula huu  Send to a friend
Monday, 09 May 2011 21:44
0diggsdigg
Habel Chidawali,Dodoma
Rais Jakaya Kikwete, amesema kasi ya kukua kwa pato la Mtanzania ni ndogo na kwamba  juhudi za makusudi lazima zifanyike ili kuongeza pato hilo.Rais Kikwete alitoa kauli hiyo jana mjini Dodoma, alipokuwa akifungua semina elekezi kwa viongozi na watendaji wakuu kwa serikali.

Hata hivyo alitamba kuwa pato la Mtanzania litaongezeka katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia sasa na kwamba hiyo inatokana na baadhi ya nchi wahisani, kuahidi kuongeza misaada kwa Tanzania.

Alisema katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake, umasikini umepungua kwa asilimia mbili tu, lakini alisisitiza kuwa hiyo itabadilika kwa kiwango kikubwa katika muhula wa pili na mwisho wa uongozi wake.

Alisema mkakati uliopo  sasa serikalini ni kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2025, Tanzania inakuwa nchi yenye uchumi wa kati na pato la Mtanzania wa kawaida linatarajia kufikia kati ya Dola 2,500 na 3,000 za Marekani, ikilinganishwa na Dola 600 za sasa.

Kuhusu kipindi cha miaka mitatu alisema kama mipango ya wahisani na Benki ya Dunia, itakuwa mizuri na kukubali kuisaidia Tanzania Dola 2.8 milioni za Marekani, taifa litakuwa katika nafasi mzuri ya kutengeneza ajira na kupambana na umaskini.

Katika hatua nyingine, kiongozi huyo wa nchi alisema hali ya nchi ni salama na itaendelea kuwa salama kama Watanzania, watashikamana na kuwa wamoja.Semina hiyo ilihudhuriwa na Waziri mkuu, Jaji mkuu, Mwanasheria mkuu mawaziri, manaibu mawaziri,makatibu na manaibu makatibu wakuu na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Pius Msekwa na Waziri Mkuu mstaafu Cleopa Msuya.Mada zinazotarajia kutolewa katika semina hiyo itakayodumu kwa ipindi cha siku nne ni pamoja na masuala ya uongozi itakayowasilishwa na Msekwa.

Mada nyingi ni ushirikiano wa viongozi wa serikali na vyama vya siasa itakayowasilishwa Msuya, Masuala ya Uchumi (Mwakilishi wa Benki ya Dunia),Ulinzi (Wakuu wa vyombo vya Ulinzi)  na masuala ya Muungano ambayo yatazungumzwa na viongozi wahusika.

Katika semina hiyo serikali inapanga mipango ya muda mfupi na muda wa kati itakayoitekeleza katika kipindi cha miaka mitano.

Semina hiyo imefadhiliwa kwa ushirikiano na Taasisi ya Uongozi, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (Tanapa) Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Benki ya NMB.

KIKWETE MAWAZIRI WAKO UMEWAPA MAJUKUMU MENGI MNO,MAWAZIRI WKO NDIO WABUNGE,WAKUU WA MIKOA,WAJUMBE WA NEC! JE NI MUDA UPI WATAFUATILIA KERO ZA WANANCHI?

Kikwete alia na mawaziri mizigo  Send to a friend
Monday, 09 May 2011 21:54
0diggsdigg
Rais Jakaya Kikwete
Habel Chidawali, Dodoma
RAIS Jakaya Kikwete amewataka mawaziri na makatibu wakuu kujiamini katika utendaji wao wa kazi badala ya kutegemea maelekezo ya mamlaka zilizo juu yao.Alisema hayo jana alipokuwa akifungua semina elekezi kwa viongozi na watendaji wakuu wa Serikali iliyofanyika katika Ukumbi wa St Gasper nje kidogo ya Manispaa ya Dodoma.“Hadi leo sijui kwa nini hasa watu (mawaziri) wanashindwa kuzungumza mambo yaliyofanywa na Serikali na kuwapa uwanja mpana wenzetu wa upande wa pili (wapinzani) ambao wanajua kweli kuvitumia vyombo vya habari. Sisi tunaendelea kulalamika kila siku kwamba hatuandikwi, nani atakuandika wakati hutoi taarifa,” alisema Kikwete.


“Kuna wakati waziri mmoja aliwahi kunipigia simu na kusema 'Mheshimiwa Rais habari hii tuikanushe?' Nilichokifanya nilimwambia pima wewe baada ya hapo nikakata simu,” alisema
Rais Kikwete alisema kitendo cha mawaziri kukataa kutoa habari na kuwafanya maofisa habari wa wizara kuwa kama waandishi wa habari ni hatari kwa serikali.


Katika hotuba yake, Rais Kikwete aliwataka watendaji hao kufanya kazi kwa kufuata misingi ya Katiba, sheria, kanuni na taratibu ili kukwepa hasara inayoweza kutokana na uamuzi usiofuata kanuni na kuiaibisha Serikali.
"Ni muhimu kwenu kama viongozi mkajielimisha juu ya Katiba, sheria, kanuni na taratibu mbalimbali zinazoongoza utendaji kazi katika sehemu zenu za kazi. Uhalali wa maamuzi mtakaoyafanya hupimwa na sheria," alisema Kikwete na kuongeza:
"Ukifanya uamuzi unaokinzana na sheria utahojiwa wewe binafsi lakini pia utaibebesha Serikali mzigo wa hasara na fedheha itakayotokana na uamuzi huo. Uamuzi usiofuata sheria unaweza kuwa na madhara kwa wananchi.
"Heshimuni Katiba na fuateni sheria, kanuni na taratibu zilizopo katika utekelezaji wa majukumu yenu. Katika semina hii masuala hayo yatafafanuliwa na kuzungumzwa. Kadhalika, uhusiano wa Serikali na mihimili mingine ya dola yaani, Bunge na Mahakama utafafanuliwa."


Rais Kikwete pia aliwataka watendaji hao kuepuka kauli na vitendo vinavyoweza kuwafarakanisha na kuleta mgawanyiko katika Serikali ili kulinda dhana ya uwajibikaji wa pamoja.
"Viongozi na watendaji wakuu wa wizara hamna budi kujenga uhusiano mzuri na uwajibikaji wa pamoja. Haifurahishi kuona waziri na katibu mkuu au waziri na naibu waziri; naibu waziri na katibu mkuu au katibu mkuu na naibu katibu mkuu hawaelewani."


"Wanasemana na hata wanapingana hadharani, yaani mbele ya wafanyakazi. Baya zaidi ni pale wanapopingana katika vyombo vya habari kuhusu uamuzi au utendaji wa wizara au serikali kwa jumla. Hayo si maadili mema katika taasisi yoyote.


"Kama unaona vigumu kuuafiki ni bora kutoka. Hairuhusiwi kupinga taasisi ambayo wewe umo ndani kama mmoja wa viongozi wake. Ni vyema hili likaeleweka. Msitupe tabu ya kuulizana maswali na kuwasemea."
Rais Kikwete pia aliwataka watendaji hao kuwa mstari wa mbele kuzungumzia mafanikio ya Serikali ili kuziba midomo ya wapinzani wanaopita kila kona nchini na kuwaeleza wananchi kuwa haijafanya chochote.


"Sijui kwa nini hatuwi wepesi kuyasemea mafanikio mengi tuliyoyapata tukaacha wasiotutakia heri wanaosema hatukufanya kitu wasikike mpaka waonekane wanasema kweli," alisema.


Alisema hajui na hana majibu mazuri ya kwa nini Serikali imekuwa ikishindwa kuzungumza mambo mazuri yaliyofanywa katika kipindi cha miaka mitano na hata wakati mwingine kushindwa kuzungumza jambo hadi wampigie simu, kitu ambacho ni aibu.


Alisema kuna udhaifu katika kujipanga kwa wasemaji kutokana na kuchelewa kutoa taarifa au kukanusha habari ambazo zimekuwa zikitolewa na upinzani, jambo linalowafanya wananchi waamini kuwa ni kweli, kwani uongo ukizungumzwa mara nyingi hugeuka na kuwa ukweli.


“Unajua mimi sijui hadi leo ni kwa nini hasa watu wanashindwa kuzungumza mambo yaliyofanywa na serikali na kuwapa uwanja mpana wenzetu wa upande wa pili ambao wanajua kweli kuvitumia vyombo vya habari huku sisi tunaendelea kulalamika kila siku kwamba hatuandikwi, nani atakuandika wakati hutoi taarifa,” aliuliza Kikwete.


Alikanusha madai kuwa baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika habari za upinzani na kuacha habari nzuri za serikali na badala yake akasema woga na urasimu uliowajaa wasemaji katika serikali, ndilo tatizo hasa kwa kuwa hawajui kuwa vyombo vya habari vinatafuta habari na kama wao hawatoi habari ni lazima waandike zile zinazotolewa na upande wa pili.


Katika hatua nyingine, Kikwete alisema kuwa anategemea kuona Serikali yake ikifanya kazi kwa umoja na ushirikiano mkubwa katika kipindi hiki cha miaka mitano na kwamba kushirikishana na kupeana habari iwe ndiyo dira ya maendeleo yao.


Sikuteua mawaziri wa kusoma mafaili ofisini
Aliwataka viongozi hao kuacha umangimeza, badala yake watoke ofisini kujionea matatizo ya wananchi.
"Mawaziri na makatibu wakuu lazima mtoke. Hiyo ndiyo njia bora zaidi ya kujua mambo yahusuyo wizara zenu na ndiyo njia bora ya kuongoza: kuona wenyewe na kutenda," alisema Rais Kikwete na kuongeza: "Hii itawafanya mjiamini kuelekeza na pia mnaposimama mbele za watu na kusema. Msiwe mamangimeza. Tokeni, tembeeni kuona shughuli zenu. Tembeleeni wananchi muwafahamu, wawafahamu, mjue shida zao muwatatulie."


Alikemea tabia ya viongozi hao kushinda kwenye mitandao kila siku na kusoma ujumbe badala ya kwenda kuwatumikia wananchi vijijini.Alisema tabia hiyo haipaswi kuvumiliwa hata kidogo na akaonya viongozi wa namna hiyo wataishia kuwa wababaishaji na hatakwenda nao katika kipindi chake cha uongozi.


“Mimi sikuteua mawaziri wa kusoma mafaili ofisini, bali niliteua watu wanaoweza kukimbizana kwa kasi zaidi, ari zaidi pamoja na nguvu zaidi, kwani nataka kuwasikia mkichakarika huko kwenye miradi mlikopeleka fedha, siyo kupokea taarifa ofisini bila ya kujua fedha za walipa kodi zinatumikaje huko.”


Dawa ya mawaziri hawa ipo jikoni
Rais Kikwete pia aliwatahadharisha mawaziri ambao wamekuwa wakipinga kauli na miswada ya mawaziri wenzao, huku wengine wakiwa wanatoa siri za Serikali.Alisema kuwa watu wa namna hiyo dawa yao iko jikoni kwa kuwa kitendo wanachokifanya si kizuri ndani ya Serikali.


Alisema anayo mamlaka ya kuchagua na ya kumwondoa waziri wakati wowote akiamua, hasa kama haoni umuhimu wa kuendelea na mtu wa aina hiyo.


“Katika hili nawaambia mapema kabisa kuwa waziri anayeishi kwa kupinga miswaada ya Serikali ajue kuwa anaipinga Serikali na hivyo sitakuwa tayari kufanya kazi na mtu wa aina hiyo. Sehemu kubwa ya kazi zenu mawaziri nataka ziwe za Serikali na zile za jimbo mtajua namna mtakavyojipanga bila ya kuharibu kazi za Serikali,” alisema.


Pato la Mtanzania litakua miaka mitatu ijayo
Rais Kikwete alisema kasi ya kukua kwa pato la Mtanzania ni ndogo na kwamba kunahitajika juhudi za makusudi katika kuongeza pato hilo. Hata hivyo, alitamba kuwa pato la Mtanzania litaongezeka katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia sasa kutokana na baadhi ya nchi wahisani kuahidi kuongeza misaada kwa Tanzania.


Alisema katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake, umaskini umepungua kwa asilimia mbili tu hivyo, akaahidi kuwa katika kipindi cha miaka mitano ya awamu ya pili ya uongozi wake, umaskini utapungua kwa kiasi kikubwa.


Alisema mkakati uliopo hivi sasa serikalini ni kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2025, Tanzania inakuwa nchi yenye uchumi wa kati pato la Mtanzania wa kawaida likitarajiwa kufikia Dola za Marekani 2,500 hadi 3,000. Sasa ni Dola 600. Kuhusu kipindi cha miaka mitatu, alisema kuwa, ipo mipango mizuri kutoka kwa wahisani, ikiwamo Benki ya Dunia ambayo imekubali kuisaidia Tanzania kiasi cha Dola 2.8 milioni ambazo zinaweza kusaidia katika kutengeneza ajira na kupambana na umaskini.


Semina hiyo ilihudhuriwa na watendaji wote wa Serikali wakiwamo Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, mawaziri na manaibu waziri, makatibu na naibu makatibu wakuu, Mwanasheria Mkuu na naibu wake, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na viongozi wastaafu, akiwamo Spika wa zamani na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa Msuya.

Wednesday, May 4, 2011

HATIMAYE AROBAINI YA OSAMA BIN LADEN YATIMIA


World 'safer' without Bin Laden, says barack obama

Map showing location of compound where Bin Laden was killed
Bin Laden killed: How it happened
More details are emerging of how al-Qaeda leader Osama Bin Laden was found and killed at a fortified compound on the outskirts of Abbottabad in north-west Pakistan.
The compound is a few hundred metres from the Pakistan Military Academy, an elite military training centre, which is being described as Pakistan's equivalent to Britain's Sandhurst or the West Point academny in the US.
There were conflicting reports about the compound's distance from the academy, with Pakistan's military saying they are as much as 4km (2.4 miles) apart.
In any case the compound lies well within Abbottabad's military cantonment, and it is likely the area would have had a constant and significant military presence and checkpoints.
Pakistan's army chief is a regular visitor to the academy, where he attends graduation parades.
The operation against Osama Bin Laden began at about 2230 (1730 GMT) and lasted about 45 minutes, military sources told BBC Urdu. Two or three helicopters were seen flying low over the area. Witnesses say they caused panic among local residents.
One report of the operation emerged in real-time: Sohaib Athar, an IT consultant living in Abbottabad, posted on Twitter at about 0100 (2100 GMT) that a helicopter was hoveringabove the city.
He continued tweeting as the operation unfolded before eventually realising: "Uh oh, now I'm the guy who liveblogged the Osama raid without knowing it.
Barbed wire and cameras The target of the operation was the compound, which had at its centre a large three-storey building.

Abbottabad

  • Abbottabad - known as "city of pines"- is a small town nestled in the beautiful lush, green hills of north-west Pakistan.
  • It is an agricultural community, but with a population of about 120,000, it provides a centre for many of the neighbouring villages
  • It is a military garrison town and has one of Pakistan's most prestigious training academies
  • It takes its name from British Major James Abbott who founded it in 1853 after he annexed the Punjab area
When the helicopters landed outside, men emerged from the aircraft. The raid was conducted by a special team of US Navy Seals.
People living in the area, known as Thanda Choha, told BBC Urdu that they were commanded in Pashto to switch off their lights and not to leave their homes.
Shortly afterwards residents said they heard shots being fired and the sound of heavy firearms.
At some point in the operation one of the helicopters crashed, either from technical failure or having been hit by gunfire from the ground.
The compound was about 3,000 sq yds in size but people from the area told the BBC that it was surrounded by 14ft-high walls, so not much could be seen of what was happening inside.
The walls were topped by barbed wire and contained cameras.
There were two security gates at the house and no phone or internet lines running into the compound.
'Waziristan Mansion'
After the operation witnesses said all they could see was fire snaking up from inside the house.
Osama Bin Laden did resist the assault and was killed in battle, US officials told White House reporters.
Footage from inside Bin Laden's compound
The officials described the operation as a "surgical raid" and said three adult males, including Bin Laden's adult son, were killed. But, they added, a woman who was being used as a shield was also killed.
According to local residents speaking to BBC Urdu the forces conducting the operation later emerged from the compound, possibly with somebody who had been inside.
They said that women and children were also living in the compound.
One local resident told the BBC Urdu that the house had been built by a Pashtun man about 10 or 12 years ago. The resident said that none of the locals were aware of who was really living there. However, the New York Times said US officials believed that the house was specially built in 2005.
According to one local journalist, the house was known in the area as Waziristani Haveli - or Waziristan Mansion.
The journalist said it was owned by people from Waziristan, the mountainous and inhospitable semi-autonomous tribal area close to the Afghan border, which until now most observers believed to be Bin Laden's hiding place.
This house was in a residential district of Abbottabad's suburbs called Bilal Town and known to be home to a number of retired military officers from the area.
Intelligence officials in the US are quoted by AP as saying that the house was custom-built to harbour a major "terrorist" figure.
'Trusted' courier
Compound in Abbottabad Police walk past the compound where the battle took place
As details of the raid emerged it became clear that the operation had been long in the planning. US officials said they received intelligence that Osama Bin Laden might be in that compound as long ago as last summer.
CIA experts analysed whether the "high value target" living at the compound could be anyone else but they decided in the end that it was almost certainly Bin Laden.
US intelligence agents focussed in particular on one of Bin Laden's couriers - a man identified as a protege of captured al-Qaeda commander Khalid Sheikh Mohammed.
He appeared to be one of the few couriers completely trusted by Osama Bin Laden, who helped keep the al-Qaeda figurehead in touch with the rest of the world.
For years US intelligence had been unable to name the courier. But four years ago they worked out who he was and two years later they discovered where he operated.
It was only in August 2010 that they located him in Abbottabad, Pakistan.
US officials described as "extraordinary" the security measures in the Abbottabad compound - among them high walls and barricades, very few windows, and a 7ft high privacy wall on the second floor.
After the US attack Pakistani troops arrived at the scene and began securing the area.

More on This Story


Saturday, April 30, 2011

ADHABU DHIDI YA VIGOGO AMBAO HAWAKUSAIDIA CAMPAIGN ZA CHAMA ZAANZA,


Tido Mhando afungua ukurasa wa adhabu hizo:
Ninampango wa kurudi kijijini kwangu Tanzania,na kushirikiana na wanakijiji wenzangu katika shughuri za maendeleo” hiyo ilikuwa ni kauri yake Tido baada ya kuulizwa na mtangazaji wa shirika la utangazaji la uingereza(BBC) anatarajia kufanya nini baada ya kustaafu kazi yake ya utangazaji (BBC). Binafsi namuona Tido kama muungwana aliyekuwa tayari kushirikiana na watanzania wenzake katika kuleta maendeleo na ndio maana pamoja na pesa nyingi alizopata mara baada ya kustaafu BBC lakini alikubari kutoa mchango wake wa uzoefu katika nchi yake, nasema Tido ni muungwana na mzalendo kwa kuwa hakutaka kubaki ughaibuni ambapo angepata kazi za mkataba na kupata mapesa mengi lakini akakubali kurudi Tanzania.
Mchango wa Tido unaonekana katika kulibadirisha television ya taifa(TVT) na kuwa Shirika la utangazaji la tanzania(TBC) ambayo imejiongezea watazamaji wengi si Tanzania tu bali hata nje ya nchi, TBC imeweza  kuondoa mtazamo wa watanzania wengi ambo awali walikiona chombo hicho kama cha chama kinachoongoza dola, TBC chini ya uongozi wake Tido hakika imekuwa kama chombo cha umma na si chombo cha ccm,hii imechangiwa na msimamo thabiti wa mkurugenzi wake ndugu Tido ambaye aliruhusu habari kurushwa pasipo upendeleo wa chama chochote cha siasa, dini, kabila na mahali.
Enzi za TVT mchakato majimboni uliosusiwa na wanaccm na ambao umekigharimu sana chama hicho na kupoteza viti vingi vya ubunge, usingeweza kuoneshwa  kama ulivyooneshwa na TBC, huo ni mfano tosha kwamba ndugu Tido alikuwa jasiri ambaye hakumugwaya hata bosi wake aliyempa ukurugenzi.
Leo kumekuwa ni mijadara mbalimbali mara baada kuona kichwa cha habari katika gazeti moja la kila siku likinadi kuwa Tido mhando ametimuliwa, mtangazaji wa leo wa  jambo Tanzania Raheli MHANDO wa  TBC hakuweza kusoma habari hiyo pamoja na mesaji nying tulizo mtumia kumtaka atufafanulie kuhusu habari hiyo! Wengi tunajiuliza je, mchango wa Tido katika TBC ulikuwa unapingwa hata na wafanyakazi wenzake wa TBC? Je mwajiri wa Tido ameona Tido hajafanya lolote katika kukiendeleza chombo hicho cha umma? Je Tido amekamatwa mchawi kwa CCM kupoteza viti vya ubunge na udiwani? Je Tido ni kigogo wa kwanza aliyefungua ukurasa wa adhabu dhidi ya waliochangia ccm kupoteza viti vya ubunge kwa kuruhusu mchakato majimboni? Maswali hayo tumekosa majibu yake kabisa kwa kuwa Tido kwetu sisi watazamaji wa TBC na wapenda habari zisizoegemea upande wowote, amekuwa ni shujaa wa kipekee ambaye hana hudi kupongezwa kwa kukuza democrasia hapa Tanzania na nchi za jilani kupitia TBC!
Hivi mcango wa Tido hauonekani mpaka kufikia hatua ya kufukuzwa kama mbwa ambaye hana uwezo wa kubweka au ubwa mla kuku wa kufugwa? Ugumu ulikuwa wapi kumuongezea muda wa miaka miwili ndugu Tido mhando ili kukamilisha mipango yake aliyokuwa nayo katika kukiendeleza chombo hicho cha umma wakati huu ambapo chombo hicho kinafanya mabadiriko ya kitechnolojia? Ndugu yangu Tido, je ulikuwa huelewani hata na wafanyakazi waliokuwa chini yako, mbona wanakwepa kuhabarisha umma habari zozote zinazokuhusu ili kuweka udharimu huo uliofanyiwa hadharani?udharimu huo uliofanyiwa ndugu yangu Tido, naufanisha na ule aliofanyiwa mhadhili wa chuo kikuu cha dar es salaam Prof. Baregu ambaye naye alifukuzwa kama mbwa baada ya mkataba wake kuisha,  walau yeye alipedwa na jumuia nzima ya chuo kikuu ambao walifikia hata hatua ya kugoma ili kushinikiza Proffesa huyo masuala ya siasa arudishwe chuoni hapo.
Tukifuata ule usemi unaosema ukiona mwenzako anyoa wewe tia zako maji, basi vigogo wote ambao hawakuchangia katika kufanikisha kampeni za chama dola wajiandae kwa adhabu za kufukuzwa kama mbwa pasipo kujali mchango wenu katika taifa letu! Vigogo wa TANESCO ambao umeme ulikatika wakati wenye dola wakifanya kampeni, wakuu wa wilaya na mikoa ampapo wenye dola walizomewa na kusodolewa wakati wakifanya kampeni, na viongozi wa chama ambao hawakufanya maandalizi mazuri kuwapokea wenye dola wakati wa kampeni ikiwa ni pamoja na kukodi piki piki na tex, nyote mjiandae kwa kuwa kigogo mwenzenu Tido wa TBC tayari amefungua ukurasa wa adhabu zichukuliwazo.
naitwa Leonard, nipo Rukwa.    

MUUNGANO NIUTAKAO MIMI MWANANCHI WA KAWAIDA

Kumekuwa na hoja nyingi kuhusu muungano viswa vya Zanzibar na Tanganyika,ambavyo vyot kwa pamoja viliiunda Tanzania,waasisi wa muungano huo marehemu mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Shehe Abeid Karume walilenga kukuza na kudumisha undungu baina ya watanganyika na wazanzibara. Muungano ambao juzi umetimiza miaka 47 umepoteza malengo ya awali ya kujenga na kudumisha undugu,nionavyo mimi ubinafsi wa viongozi wa kisiasa walioshika dola baada ya waasisi Nyerere na karume ndio chanzo cha chokochoko za muungano.Nionavyo mimi waasisi wa muungano walifikia hatua ya kwanza ambayo ilizaa serikari ndogo ya Zanzibar na Serikari ya muungano wa Tanzania, hivyo ingekuwa jukumu la viongozi wa sasa kuendelea kujenga na kudumisha undugu kwa kendeleza hatua ya pili kwa kufanya serikari mbili kuwa serikari moja ya Tanzania yenye raisi mmoja tu badala ya serikari tatu au mbili ambazo zimekuwa zikipigiwa upato. Sioni kwanini viongozi wa kisiasa wanaendeleza kuweka vitu ambavyo kwa namna moja au nyingine ndio vyanzo vya chokochoko za muungano wetu? kulikuwa na na haja ipi kwa zanzibar sehemu ya Tanzania kuwa na Bendera yake,wimbo wake wa taifa,majeshi yake na serikari yake? viongozi wa kisiasa tuache ubinafsi, sisi wananchi wa kawaida tungependa kuona muungano wa zanzibar na Tanganyika unazaa serikari moja chini ya raisi mmoja ili kuwa na nguvu za kuharakisha maendeleo ya Tanzania kwa ujumla wake! Kuna ugumu upi zanzibar ambayo wakazi wake ni takribani millioni moja sawa na idadi ya watu katika mikoa mingine tanzania,kuongozwa na wakuu wa mikoa kama ilivyo kwa mikoa mingine?hakika kero za muungano zitakoma pale ambapo tanzania itakuwa na serikari moja tu.

Monday, April 18, 2011

VYAMA VYA SIASA TOENI MAHESABU YENU BANA

Vita ya ufisadi yageukia vyama vya siasa  Send to a friend
Tuesday, 19 April 2011 08:13
0diggsdigg
Ramadhan Semtawa
VYAMA sita vya siasa vyenye wawakilishi bungeni, vinadaiwa kuwa vimeshindwa kuwasilisha taarifa za hesabu kuhusu matumizi ya ruzuku ya jumla ya Sh17.14bilioni kwa mujibu wa sheria.Vyama hivyo ambavyo vinapata ruzuku inayotolewa na Serikali ni pamoja na Chama Cha Mapinduzi (CCM), Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chama cha Wananchi (CUF), Chama cha Tanzania Labour (TLP), NCCR-Mageuzi na UDP.
Tuhuma hizo zimo kwenye Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), inayoishia Juni 30, 2010.

CAG ametoa ripoti hiyo baada ya sheria, kwa mara ya kwanza kumpa mamlaka ya kuvikagua vyama vya siasa ambavyo mahesabu yao, yanapaswa kuwasilishwa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa Tanzania.

"Taarifa za fedha kwa malipo ya ruzuku ya Sh17,146,819,904 kwa vyama vya siasa mbalimbali hazikuwasilishwa na vyama husika katika Ofisi ya Msajili," ilisema Ripoti ya CAG katika fungu la 27 kuhusu Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na matumizi ya ruzuku.

Takwimu kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa zinaonyesha kuwa CCM kinapata ruzuku ya asilimia 70, CUF asilimia 20, Chadema asilimia nane na NCCR-Mageuzi, UDP na TLP vinagawana asilimia mbili.

Katika mahesabu ya kawaida, kati ya fedha hizo Sh 17.14 bilioni, CCM itakuwa imepata mgawo wa Sh12bilioni, CUF Sh 3.43bilioni, Chadema Sh1.37bilioni na vyama hivyo vitatu kwa asilimia mbili yao vikipata Sh343milioni.

Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa alipoulizwa na gazeti dada la The Citizen kwa simu alisema asingeweza kuzungumzia jambo hilo nyeti kwa mawasiliano ya simu kwani anahitaji kukaa na kulifanyia kazi kwa kina.

Hata hivyo, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovic Utouh katika ripoti hiyo alisema kitendo hicho ni kinyume cha kifungu 14 (1) na (3) cha Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992.


Sehemu ya kifungu hicho inasema, "Chama chochote cha siasa ambacho kina usajili wa kudumu, kinapaswa kutunza hesabu zake vizuri za ruzuku na kuwasilisha kwa Msajili."

Kifungu hicho kinaendelea: "Kwa kutumia taarifa ya mwaka ya ukaguzi wa hesabu uliofanywa na mkaguzi anayetambulika kwa mujibu wa Sheria ya Ukaguzi wa Hesabu, huku ikiwa na tamko la mali zote zinazomilikiwa na chama hicho."

 Utouh alisema pia kwamba Sh56.9milioni zilitumika na msajili huyo wakati hazikuhusiana na shughuli za vyama vya siasa.

"Jumla ya Sh56,180.44milioni zilitumika na Msajili wa Vyama vya Siasa wakati hazikuhusiana na shughuli za vyama vya siasa," alisema Utouh katika taarifa hiyo.

Mbali na tuhuma hizo, Utouh alisema kwamba kiasi cha Sh272.8milioni zilitumika kulipa deni la miaka ya nyuma la Bodi ya Udhamini ya chama cha UDP bila kuonyeshwa katika taarifa za fedha na kusema: "Malipo haya yanaathiri utendaji wa ofisi kwa mwaka wa sasa wa fedha."

UDP kinaongozwa na John Cheyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

Alipoulizwa kuhusu fedha hizo, Cheyo alisema hajaisoma vyema ripoti hiyo na kuongeza kwamba atakuwa kwenye nafasi nzuri kuzungumzia hilo baada ya kuipitia kwa kina.

"Kwa sasa hivi itakuwa ni vigumu kuzungumzia ripoti hiyo wakati sijaisoma vizuri. Nitakuwa siko sahihi kama nitazungumza bila kuisoma. Nipe muda nisome kisha nitaweza kuizungumza," alisema.


Saturday, April 16, 2011

PAMBAMOTO KUWANYIMA ULAJI WAMILIKI WA MAGAZETI HURU

RAIS Jakaya Kikwete ameombwa kuminya kiuchumi vyombo vya habari binafsi ili kuimarisha vijarida vitakavyoanzishwa na umoja wa vijana wa chama chake (UV-CCM), MwanaHALISI limegundua.
Mawasiliano kati ya viongozi wa umoja huo yanaonyesha kumwomba rais Kikwete  kumuagiza katibu mkuu kiongozi (Philemon Luhanjo), kuelekeza taasisi na mashirika ya umma, kutoa kipaumbele cha matangazo kwa vijarida vya CCM na umoja wake.
Aidha, mawasiliano hayo yanataka Luhanjo, kwa ushirikiano na mkurugenzi wa mawasiliano (ikulu), kuelekeza makatibu wakuu wa wizara zote za serikali na wasemaji wote wa wizara/maafisa uhusiano kuhakikisha wanafanikisha mradi huo wa kunyonga vyombo huru vya habari.
Kwa mujibu wa mawasiliano kati ya Kaimu Mwenyekiti wa UV-CCM, Benno Malisa na katibu msaidi wa chama hicho, wilayani Iringa, Charles Charles, njama hizo zitadhoofisha vyombo huru vya habari na kuimarisha vijarida vya CCM ili “kufanya propaganda zenye maslahi kwa CCM.”
Katika mawasiliano hayo ya imeili ya 30 Machi 2011, saa 9:14 asubuhi, Charles anasema vyombo vingi vya habari nchini maandishi yake yanakwenda kinyume na malengo ya CCM.
Anasema, ”…magazeti ya Uhuru na Mzalendo yamefikia mahali hayana tena mvuto kwa wasomaji na yamekosa utaalamu wa kuyaboresha kutoka pale yalipo hivi sasa na kubadilika; naamini kwamba hatimaye sasa kuna umuhimu wa lazima wa kuwa na gazeti na, au magazeti mbadala…kama sehemu ya mkakati wa kuelekea mwaka 2014 na 2015.”
Charles anashauri gazeti hilo kuchapishwa haraka kutokana na kile alichoita, “hali mbaya ya kihabari dhidi ya CCM na serikali yake inayofanywa na vyombo vingi vya habari hivi sasa na hasa televisheni na magazeti binafasi.”
“Kwa muda mrefu sasa, magazeti ya watu binafsi nchini yameungana kufanya mashambulizi makubwa dhidi ya CCM, jumuiya zake na serikali,” anasema Charles na kuongeza, “Kadri muda unavyokwenda ndivyo hali inavyozidi kuwa mbaya maradufu.”
Waraka wa Charles unamshawishi Malisa kutoa Sh. 11.3 milioni kila mwezi ili kuendesha gazeti la PAMBAMOTO linalomilikiwa na UV-CCM.
Malisa alipoulizwa kuhusu mawasiliano na Charles alisema umoja wake haujafanya “uamuzi wowote kuhusu ufufuaji gazeti la Pambamoto kutokana na hali ya uchumi kutokuwa nzuri.”
Amesema, hata hivyo, akiwa kiongozi, anapokea ushauri na maoni yoyote kutoka kwa wanaotakia mema UV-CCM.
Charles anasema, “Kwa kuwa asimia 75 ya mapato ya vyombo vya habari duniani hutegemea matangazo na mauzo huingiza asilimia 25 tu, nashauri kwamba pindi gazeti hili likianza basi ufanyike utaratibu wa makusudi wa kulipatia matangazo kutoka wizara na taasisi zote za serikali yakiwamo mashirika ya umma kama TTCL (kampuni ya simu) na TANESCO (shirika la umeme la taifa).”
Mashirika mengine ambayo anataka yatoe matangazo kwa gazeti hilo, ni Sumatra, Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Shirika la Viwango la Taifa (TBS), Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), Mamlaka ya Bandari (THA), Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
“Hili lifanyike kwa kuiomba serikali kupitia kwa mwenyekiti wa taifa wa CCM, Rais Kikwete,” ameeleza katika ujumbe wenye sauti ya kulialia.
Lengo la mkakati huo ambao Charles anasema atasimamia mwenyewe, ni kulipa uwezo gazeti kwa kupunguza utegemezi wa ruzuku kutoka vyanzo vingine ambavyo vitakuwa vinatoa fedha.
Gazeti ambalo wahusika wamepanga kumhusisha Rais Kikwete kama “meneja wa matangazo,” kwa mujibu wa waraka, litatoka kila wiki chini ya usimamizi wa Charles anayesema ana “uzoefu… wa muda mrefu wa shughuli hizi.” Litachapwa nakala 5,000 kila wiki.
Charles ambaye yuko Iringa, anamuomba Malisa kusaidia kumrejesha Dar es Salaam ili aweze kufanya kazi yake hiyo kwa urahisi. Hata hivyo amesema atafanya uhariri wa gazeti kutokea nje ya chumba cha habari. 
Ofisa huyo wa CCM anasema wimbi kubwa la vijana, akina mama na makundi mengine limeunga mkono kwa nguvu nyingi “upande wa washindani wetu kisiasa na kuzidi kuimarika, hali ambayo kwangu naamini kwamba itaendelea kuwa mbaya zaidi katika siku zijazo.”
Akiandika kama anayesisitiza kupewa kazi, Charles anasema, “ …ni lazima nilisimamie kuliko kazi hiyo kufanywa na mtu mwingine kwa sababu anaweza kuingiza matakwa yake, kinyume na kazi maalum tunayopanga kuifanya.”
Charles amepanga kujilipa Sh. 440,000 kama mhariri mkuu na mhariri wa habari. Naye mwenyekiti wa bodi ya uhariri atapewa Sh. 300,000. 
Charles anaambatanisha “gharama halisi” za uendeshaji wa gazeti hilo, “fedha ambazo naamini kuwa zitapatikana bila tatizo kama utakuwapo utashi wa kufanya hivyo,” anaeleza.
Katika waraka huo, pamoja na fedha, anaomba vitendea kazi kama kompyuta aina ya laptop. Anasema fedha ambazo zitatumika kuendesha gazeti hilo “ambalo tayari limesajiliwa na serikali, zitatokana na mradi mkubwa wa jengo la kitegauchumi cha UV-CCM.”
Katibu huyo wa CCM aliyewahi kuandikia gazeti la Tazama anamweleza Malisa kuwa “gazeti la kila wiki la Tazama Tanzania ndilo pekee ambalo ni pro-CCM na serikali yake kwa asilimia 100. Lakini yaliyobaki yote yakiwemo hata ya makada wenzetu hayana msimamo wowote,” anaeleza.
Viongozi na makada wa CCM wanaomiliki vyombo vya habari ambao Charles anadai hawaisadii CCM, ni pamoja na wamiliki wa magazeti ya Rai, Mtanzania, The African, Bingwa na Dimba. Vyombo hivi humilikiwa na Rostam Aziz, mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya CCM.
Wamiliki wengine wa vyombo vya habari ambavyo Charles anawagombanisha na Kikwete kuwa wanahujumu serikali yake, ni Anthony Diallo anayemiliki Radio Free Afrika na Star TV na magazeti ya serikali ya Habari Leo na Daily News.
Nalo gazeti la Tazama ambalo Charles anasema linafanya kazi za CCM kwa asilimia 100, limewahi kutuhumiwa na mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela kwa kutumikia “genge la watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini.”
“Kama gazeti anasema hilo linatumikia CCM, basi labda si hii CCM ninayoijua mimi. Huyo Charles Charles ninayemfamu, amekuwa akiwaandika vibaya wajumbe wa Kamati Kuu (CC) wa chama chetu. Sasa hao CCM anaosema wanatetewa na gazeti la Tazama ni wepi,” anasema Christopher ole Sendeka, mbunge wa Simajiro CCM.
Anasema, “Mimi mwenyewe na makada wenzangu, akiwamo ndugu yangu Nape Nnauye, tumeandamwa na gazeti hilo mara kadhaa. Hata mheshimiwa Sitta amelalamikia Tazama mara kadhaa,” anaeleza Sendeka alipoulizwa anavyolifahamu Tazama.
MwanaHALISI lilipowasiliana na Charles kwa njia ya simu ili kupata maoni yake kuhusu kile alichoandika kwa Malisa, alijibu haraka, “Mimi sijui.

Wednesday, April 13, 2011

KATIBU MPYA WA CCM BAADA YA KUVUA GAMBA LA KALE

Mrithi wa Makamba aingia na moto  Send to a friend
Tuesday, 12 April 2011 22:20
0diggsdigg
Katibu Mkuu mpya wa CCM Wilson Mukama
Waandishi Wetu, Dar na Dodoma
UPEPO wa kisiasa ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), unazidi kuvuma kwa kasi baada ya Katibu Mkuu mpya wa chama hicho, Wilson Mukama, kutangaza kiama kwa mafisadi akitaka wajiuzulu mapema, huku Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Chama hicho, Makongoro Nyerere akitajwa kuchochea maamuzi magumu dhidi ya genge hilo.Kauli hizo nzito za vigogo hao dhidi ya genge la mafisadi ambalo lina nguvu za fedha ndani na nje ya chama hicho tawala, ni sehemu ya mpango mkakati wa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, wa kukivua magamba.Mukama ambaye ndiye Mtendaji Mkuu wa chama hicho aliyetangazwa mjini Dodoma usiku wa kuamkia jana, alisema ili chama hicho kiweze kurudisha heshima yake kinatakiwa kuwa na watu safi wasiotiliwa mashaka kabisa katika jamii. Akizungumza na Mwananchi ofisini kwake muda mfupi baada ya kumaliza kikao na watendaji wa mikoa wa chama hicho, Katibu huyo alisema hana jipya atakalopeleka CCM isipokuwa yeye atasimamia weledi na misingi iliyokuwapo tangu kuanzishwa kwa CCM.
“CCM inatakiwa kujengwa upya kabisa na ili hayo yaweze kufanikiwa, kuna kila sababu za kuwa na watu safi, hivyo mimi nawataka ndugu zangu wasimame katika misingi ya zamani tuliyokuwa nayo katika chama chetu,” alisema Mukama na kuongeza:
“Nawataka wote wenye tuhuma za rushwa na ufisadi ndani ya chama waanze kujiuzulu mapema ili kulinda heshima yao, kwani tunaingia kujenga chama sio kukibomoa.”
Katibu Mkuu huyo ambaye ana kibarua kigumu cha kusafisha chama na kukirejesha katika misingi ya waasisi wake  tangu enzi TANU na CCM ya mwaka 1977, alisema mwelekeo wa CCM pamoja na sera zake bado unakubalika kwa wananchi na kuongeza: "Kinachotakiwa sasa ni kuwa na usimamizi na maamuzi magumu kwa kila mtu atakayekabidhiwa dhamana hiyo".
Akizungumzia juu ya chama kujengwa upya alisema: "Ili tuweze kufanikiwa katika hilo mimi nitasimamia maamuzi ya Kamati Kuu ya CCM ya kukirudisha chama kwa wanachama ngazi ya chini ili wao ndio wakafanye maamuzi.”
Mukama ambaye alikuwa akizungumza kwa kujiamini alisema atasimamia kikamilifu itikadi ya Ujamaa na Kujitegemea, kwa kuwa ndio sera kubwa ya CCM tangu kuanzishwa kwake.
Jambo lingine alilosisitiza kiongozi huyo ni pamoja na kukiongoza chama katika kupata ushindi ambao hautakuwa ukitiliwa mashaka na watu wengine.“Jambo kubwa na la msingi hapa ni kukiongoza chama katika kufikia malengo makubwa ya kupata ushindi usiokuwa na manung’uniko, kwani mbinu za kivita hupatikana katika medani sio uwanja wa vita,” alitamba Mukama. Hata hivyo, alisifia hatua ambayo imechukuliwa na chama ambayo imesaidia kukijenga hadi sasa.
Aliyataja mafanikio ya hatua hiyo kuwa ni pamoja na kuwa viti vingi bungeni, kwani zaidi ya asilimia 78 ya wabunge wanatoka CCM.

Abeza nguvu ya upinzani
Akizungumzia nguvu za upinzani, Mukama alibeza na kusema hilo haliwezi kumsumbua yeye wala kumfanya asilale usingizi, kwani anatambua ni wapi panatakiwa kusimamiwa na ni wapi panatakiwa kutolewa maelekezo yake.
“Kwenye siasa hata siku moja ni kubwa sana huwezi kuidharau. Leo tutazungumzia miaka minne ili tuingie katika Uchaguzi Mkuu mwingine, hivyo bado kuna muda mzuri na wa kutosha kufanya maandalizi, ndio maana siwezi kutaja moja kwa moja chama kinachonipa tabu bali kitajulikana mbele ya safari,” alitamba Mukama

Ofisini siku ya kwanza
Kutwa nzima jana, Mukama akiwa na wasaidizi wake John Chiligati (Bara), Vuai Alli Vuai (Zanzibar) pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, walifanya vikao na makatibu wa mikoa na watumishi wa CCM Makao Makuu.Awali, Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Kikwete, alizungumza na watumishi makao makuu na baadhi ya makada wa chama kwa lengo la kuitambulisha Sekretarieti mpya na kuweka mikakati.

Makamba ataka aachwe
Kwa upande wake Katibu Mkuu aliyeachia ngazi, Yusuph Makamba, alisema huu ni wakati wake wa kupumzika kwani amechoka.Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana kuhusu uamuzi mgumu wa kujiuzulu aliouchukua mjini Dodoma hivi karibuni alisema, "Naomba mniache nipumzike... Nimechoka."
Alifafanua kwamba ametumikia nchi kwa zaidi ya miaka 50, hivyo huu ni wakati wake kupumzika na watu wengine kufanya kazi na yeye aachwe apumzike.
"Nimetumikia nchi hii kwa miaka mingi, nimekuwa mkuu wa wilaya, mkoa na baadaye chama, sasa ni wakati wangu wa kupumzika kwani kazi niliyofanya ni kubwa," alisisitiza.
Katibu Mkuu huyo mstaafu aliyetuhumiwa kukigawa chama, alisema kama ni chama kimepata uongozi mpya ambao anaamini utaweza kusimamia ajenda zake kwa ufanisi.
Makongoro Nyerere amchochea JK
Mtoto wa Baba wa Taifa ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara, Makongoro Nyerere, amemshauri Mwenyekiti wake Rais Kikwete, kuwabwaga wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi hata kama ni maswahiba wake kisiasa.
Habari kutoka ndani ya kikao cha Nec, zilidokeza gazeti hili kwamba Makongoro alimweleza Rais Kikwete wakati wa kikao kuwa hana budi kuchukua uamuzi utakaowaumiza marafiki zake, ili kukinusuru chama.
“Vitabu vitakatifu vinatueleza kuwa awali Mungu alikuwa akishirikiana kwa karibu na shetani, lakini shetani alipoanza ushetani wake, Mungu akamtimua na kumtupa uwanjani. Mungu hakai na shetani,” mpasha habari wetu alimnukuu Makongoro.
Makongoro anadaiwa kumweleza Rais Kikwete kwamba, watu wa Dar es Salaam walipokwenda kuhiji katika kaburi la baba yake, walipata jibu la kuwa Kikwete ndiye anayefaa, hivyo asivurugwe na watu wachache.
Makongoro alimtahadharisha rais kuwa kama atachukua uamuzi wa kuilipa Kampuni ya Dowans Sh94 bilioni, hakuna Mtanzania atakayemwelewa.
Katika hatua nyingine, uamuzi wa kuvunjwa kwa Sekretarieti na Kamati Kuu ya CCM, kumechochea wanachama kudai mabadiliko yafanyike haraka katika ngazi ya mikoa.
Mbunge wa Kinondoni (CCM), Iddi Azzan, alisema mabadiliko yaliyofanywa ndani ya chama hicho ni mazuri.
Hata hivyo, Azzan alisema mabadiliko hayo yanatakiwa kufanyika katika ngazi za mikoa na wilaya ambako alidai kuwa kumeoza.
Aliitaka Sekretarieti ya Mkoa wa Dar es Salaam kujiuzulu kama walivyofanya wa Sekretarieti ya Taifa.
Sekretarieti ya CCM, Mkoa wa Dar es Salaam inaundwa na Katibu wa CCM Mkoa, Kilumbe Ng'enda, Katibu Mwenezi, Juma Simba, Katibu wa Uchumi, Abbas Tarimba, Katibu wa Wazazi, Mustafa Yakub, Katibu wa UWT, Tatu Mariaga na Katibu wa UVCCM, Omar Mwanag’alu.

January  ajiuzuluKamati ya Bunge
Katika tukio lingine, Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa wa CCM, Januari Makamba, anatakiwa kujiuzulu nafasi yake ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, John Chiligati, alisema Makamba anatakiwa kupima uzito wa kazi aliyopewa na ile ya Bunge. Anatakiwa kubaki na ubunge kwa sababu sio kazi ya kuwajibika kila siku.
Katika mkutano wake Nec iliamua kuwa watumishi wa chama wanatakiwa kuwapo kila siku kwa ajili ya utendaji na kwamba wanatakiwa kutenganisha viongozi wa Serikali na chama.
Habari hii imeandikwa na Habel Chidawali na Midraj Ibrahim, Dodoma, Ramadhan Semtawa, Dar

Thursday, April 7, 2011

UTAFITI KUHUSU ELIMU TANZANIA

Hakielimu watangaza utafiti kuhusu elimu  Send to a friend
Wednesday, 06 April 2011 21:54
0diggsdigg
Fidelis Butahe na Hussein Issa
TAASISI ya Hakielimu, imetoa ripoti ya utafiti kuhusu uhusiano wa ubora wa mitaala na utoaji wa elimu bora, unaonyesha kuwa mtaala wa elimu wa Tanzania, hauna uwezo wa kutoa wahitimu mahiri, katika nyanja mbalimbali.

Utafiti huo unasema asilimia 79.9 ya walimu walipendekeza kutumika kwa kitabu cha aina moja cha kiada katika kufundishia wanafunzi wa shule zote nchini.Ripoti hiyo inasema ni   asilimia 20 tu walimu, ndio waliopendekeza kuendelea kwa sera ya sasa ya kutumika kwa vitabu vya kiada vya aina mbalimbali.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya utafiti,  vitabu vingi vya kiada, haviendani na muhtasari rasmi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, jambo linalochangia katika kuwapotosha wanafunzi.

Utafiti huo ulifanyika Agosti mwaka jana katika wilaya sita nchini na kuhusisha maofisa elimu wa wilaya, walimu, wanafunzi na wazazi.Unaonyesha kuwa baadhi ya vitabu vina makosa makubwa ya kimaudhui na lugha na hivyo kuwafanya wanafunzi, washinwe kuunganisha kinachofundishwa na kile wanachotarajia kupata.

Akizungumza wakati wa kuwasilisha ripoti hiyo, Mchambuzi wa Sera wa taasisi hiyo, Mtemi Zombwe, alisema ni asilimia 35 tu ya walimu na asilimia 26 ya wanafunzi, ndio walioripoti kuwa mitaala unafaa katika kuandaa wahitimu mahiri wenye kujiamini

Alizitaja wilaya ambazo utafiti huo umefanyika na mikoa ya wilaya hiyo katika mabano kuwa ni Monduli (Arusha), Mafinga (Iringa), Pangani (Tanga), Misungwi (Mwanza), Uyui (Tabora) na Bukombe (Shinyanga).

"Katika utafiti huu walimu, wazazi na wanafunzi, walibainisha kuwa elimu iliyokuwa ikitolewa kati ya miaka ya 1980-1990 ilikuwa ikimwezesha mhitimu kuwa na mawazo ya kujitegemea katika ngazi yoyote ya elimu aliyofikia," alisema Zombwe."Wengi wa watu waliohojiwa walisema kwamba elimu ya sasa inamfanya mhitimu ategemee zaidi kuajiriwa na kufanya kazi za ofisi," alisisitiza mchambuzi huyo.

Alisema katika utafiti huo. walimu waliikosoa serikali kwa kuanzisha mtaala ambao hauendani na mahitaji ya watu.

"Pia wameilalamikia serikali kwa kufanya mabadiliko ya mtaala bila kuwahusisha walimu na wanafunzi, jambo ambalo walidai linawafanya wawe nyuma katika utekelezaji wa mitaala," alisema Zombwe.Alisema wazazi wengi waliohojiwa, walionyesha kutokuwa na uelewa mkubwa kuhusu mitaala na sera  ya elimu nchini, jambo ambalo limewafanya wawe nyuma katika kufundisha na kujifunza.

Mapendekezo
Kufuatia utafiti huo wadau wa elimu walitoa mapendekezo kwamba matumizi ya vitabu vya aina tofauti, hayana tija kwa sababu yanawafanya wanafunzi wajifunze dhana zinazotofautiana wakati wanatarajiwa kufanya mtihani wa aina moja.

Alisema pia walitaka kuwe na udhibiti wa ubora wa vitabu, kuwapo kwa nyenzo na vifaa vya kufundishia na walimu kufahamishwa kuhusu sera za elimu

Friday, April 1, 2011

BABU KAMA KAWA AENDELEA KUGAWA DOZI YA KIKOMBE

Mawaziri wengine wapata kikombe  Send to a friend
Sunday, 27 March 2011 05:59
0diggsdigg
Neville Meena  na Mussa Juma, Loliondo
Mchungaji akimimina dawa tayari kwa kuwanywesha wateja wake
NI kama mbio za kupokezana vijiti kwa mawaziri wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete ambao wanaendelea kumiminika katika Kijiji cha Samunge, Loliondo kwa ajili ya kunywa dawa ya kutibu magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Ambilikile Mwasapile.

Jana ilikuwa ni zamu ya mawaziri wawili ambao ni Ezekiel Maige wa Maliasili na Utalii pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk Terezya Hovisya, ambao walifika Samunge na kila mmoja kupata kikombe cha babu.

Mawaziri hao walifika Loliondo asubuhi kwa ndege ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (Tanapa) kisha kwenda Samunge na jioni waliondoka kwenda mkoani Manyara.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili katika Uwanja wa Ndege wa Loliondo mara baada ya kurejea kutoka Samunge, Maige alisema: "Nimekunywa dawa mimi binafsi, si kwa niaba
ya Serikali wala kitu kingine chochote…".

Maige ambaye pamoja na Hovisa walionekana kuwa na haraka kutokana na kubanwa na sheria za uwanja wa ndege kutotumika zaidi ya saa 12.00 jioni, pia alizungumzia mazingira ya utoaji wa dawa hiyo akisema lazima zichukuliwe hatua za haraka kubadili mfumo wa sasa wa utoaji.

Alisema hivi sasa taratibu za utoaji wa dawa hiyo  si nzuri kwani zinawalazimisha baadhi ya wagonjwa kukaa kwenye foleni kwa siku saba wakisubiri zamu zao hali ambayo alisema ingeweza kuepukwa.

Kauli ya Maige imekuja wakati ambao Serikali inasubiriwa kutoa tamko rasmi kuhusu kuendelea ama kusitishwa kwa tiba hiyo baada ya kujadili hali ilivyo katika vikao vilivyokuwa vikiongozwa na Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi.

MTOTO WA MKULIMA HALI YA MAISHA YA WATANZANIA WENGI NI MBAYA HAKUNA HAJA YA UTAFITI

Kweli Waziri Mkuu hajui hali ngumu inasababishwa na nini!  Send to a friend
Thursday, 31 March 2011 21:21
0diggsdigg
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
JUZI Waziri  Mkuu, Mizengo Pinda,  aliitaka Taasisi ya Kuondoa Umaskini  nchini (Repoa) kufanya utafiti wa kina kujua ni kwa nini wananchi wa kawaida wanalalamikia hali ngumu ya maisha wakati kitaifa uchumi unakua. Kwa maana nyingine ni kwamba, Pinda kama Waziri Mkuu na msimamizi wa shughuli za Serikali hajui kwa nini Watanzania wanaendelea kuwa maskini wakati mazingira ya kiuchumi yanatoa fursa ya watu kuondokana na tatizo hilo, ambalo kadiri siku zinavyozidi kwenda ndivyo linavyozidi kukua.

Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa 16 wa  Repoa, Pinda alieleza kuwa Serikali inatumia tafiti zinazofanywa na taasisi hiyo kupata ufumbuzi wa tatizo hilo na mengine yanayolikabili taifa.

Hii ni changamoto nzuri kwa Repoa ambayo imethaminiwa na kwamba inafanya kazi nzuri inayoweza kuisaidia Serikali kupata ufumbuzi wa matatizo yanayoihangaisha nchi yetu katika nyanja za uchumi na maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Kwa maana hiyo basi, Repoa inatakiwa kufanya kazi ya ziada kuvumbua tatizo la umaskini uliotopea unaoendelea kuongezeka miongoni mwa wananchi wa kawaida ili Serikali ichukue hatua, kwa kuwa mpaka sasa inaamini kuwa uchumi wa nchi unakua hata kama bei za bidhaa zinaendelea kupaa kila wakati.

Hata hivyo, tunadhani jukumu kubwa liko mikononi mwa Serikali kwa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa taarifa na ripoti za tafiti zilizofanyika kitaalamu na kuwasilishwa kwake.

Tunasema hivyo kwa sababu, kama hakuna dhamira ya dhati katika kutekeleza na kusimamia hakuna kitakachobadilika, hata kama Repoa watafanya kazi nzuri na kuandaa ripoti inayotoa mwongozo na njia ya kukabiliana na umaskini  hakuna kitakachofanyika.

Tuna kila sababu ya kusema hivyo, kwa vile hatuamini kama kweli Serikali yenye vyanzo vingi vya kupata taarifa, ikiwamo kukua na kuanguka kwa uchumi haijui kwa nini wananchi wanalalamikia hali ngumu ya maisha.

Lakini, je ni kweli Serikali haijui sababu ya watu wa kawaida kukabiliwa na umaskini? Je, ni kweli Waziri Mkuu hajui kuwa kuna mfumuko wa bei kwa bidhaa zote? Kama anajua kuwa bei za vyakula na bidhaa nyingine muhimu ziko juu yakiwamo mafuta ya petroli, inakuwaje ashangae wananchi kulalamikia hali ngumu ya maisha pamoja na umaskini unaowaandama?

Inashangaza kusikia kwamba wakati wananchi wa kawaida ambao ndiyo wengi wanalalamika,  Serikali inasema uchumi wa nchi unakua na haijui kwa nini imekuwa hivyo! Katika hali  halisi, uchumi wa nchi unakuwaje na nguvu wakati wananchi wa kawaida ambao ndiyo wengi wana hali ngumu?

Hoja yetu inasimama katika msingi kwamba, pato la taifa la ndani linagawanywa na idadi ya watu.  Sasa kama watu wengi ni maskini, uchumi unakuaje?  Unakuwaje imara na bei zikiwa juu ambazo wananchi hawawezi kuzimudu?

Tunachojua ni kwamba kama kweli uchumi wa nchi unakua, kwa tafsiri ya uwiano wa mapato na wananchi wake maana yake hivi sasa utajiri uko mikononi mwa watu wachache wanaomiliki njia zote za uchumi.

Pia inamaanisha utajiri wa nchi hii unashikiliwa na watu wachache, jambo ambalo ni hatari kwa ustawi wa jamii na taifa letu kwa ujumla.  Maana yake ni kwamba, ikiwa uchumi wa taifa uko mikononi mwa watu wachache ubepari umekomaa na ni hatari kwa taifa kwa sababu kwa kawaida bepari huangalia mazingira ya kibiashara kama yanaruhusu yeye kuendelea kuwepo, vinginevyo anaweza kuhamisha biashara zake  na kila kitu alichowekeza na kupata hapa nchini.

Mambo mengi yanayoweza kutokea katika hali hii ni kushamiri kwa rushwa na ufisadi, ukwepaji wa kodi ambalo pia limekuwa tatizo kubwa hapa nchini.  Haiwezekani uchumi wa taifa ukue wakati Mamlaka ya Mapato (TRA) inashindwa kuvuka malengo ya kukusanya kodi na wakati huohuo Serikali ikishindwa kutekeleza miradi ya maendeleo ya jamii  kwa kukosa fedha, mpaka zitoke kwa wafadhili.Tunamshauri Waziri Mkuu na Serikali kusema ukweli juu ya mambo yanayochangia hali ngumu ya maisha inayowakabili wananchi wake.

MMH NI ZAMU YA WAZIRI MAGUFURI KUNYA KIKOMBE CHA BABU WA LOLIONDO

Magufuli apeleka Sh1bn Loliondo  Send to a friend
Thursday, 31 March 2011 21:56
0diggsdigg
Neville Meena na Mussa Juma, Samunge
WAZIRI wa Ujenzi, Dk John Magufuli, jana aliingia katika Kijijini Samunge kwa mchungaji Ambilikile Masapila na kupata kikombe cha dawa, kisha kutangaza neema ya kujengwa kwa barabara kuu inayoingia kijijini hapo.

Magufuli aliuambia umati wa watu uliokuwa ukisubiri zamu yao kunywa dawa kuwa, Serikali itatumia Sh1.05 bilioni kwa ajili kutengenenza barabara hiyo ili iweze kupitika wakati wote kwa lengo la kuwarahisishia usafiri wanaokwenda kunywa dawa kwa Babu Masapila.

Barabara inayoingia katika kijiji hicho ambacho kimeshuhudia maelfu ya magari yakiingia kila siku tofauti na ilivyokuwa awali, ipo katika hali mbaya kiasi cha baadhi ya maneo kutoruhusu magari kupishana.

Kwa mujibu wa Magufuli, Serikali ilikwishatoa Sh500/-milioni kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kuanzia Mto wa Mbu eneo la Kigongoni, Ngaresero, Samunge hadi kuungana na barabara ya kutoka mkoani Mara.

Dk Magufuli alisema jana ndio aliuagiza uongozi wa Wakala wa Barabara nchini (Tanroads) Makao Makuu kutuma Sh500 milioni ili kuharakisha ujenzi huo.

"Tayari fedha hizo zimeshatumwa Tanroads mkoani Arusha na Meneja wa Mkoa, Kakoko (Deodatus), niko naye hapa hivyo kazi itakwenda haraka ili watu wanaokuja kwa mchungaji kunywa dawa wasiendelee kuteseka," alisema Dk Magufuli huku akishangiliwa na mamia ya watu waliokuwa wakimsikiliza.

Waziri pia huyo alisema kwa mamlaka aliyonayo, atawasiliana na uongozi wa Mfuko wa Barabara ili utume fedha za dharura kiasi cha Sh50 milioni kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorogoro kwa ajili ya kufanya matenegenezo mengine ya barabara, wilayani humo.

Alisema fedha zilizotengwa kwa ajilii ya barabara za nchi nzima kupitia mfuko huo zinafikia Sh286 bilioni katika bajeti ya mwaka 2010/11, na kwamba upo uwezekano mkubwa wa fedha za dharura kupatikana kwa ajili ya matenegenezo ya barabara ya Samunge.

Matengenezo
Kwa mujibu wa Magufuli, matengenezo ya barabara hiyo ni muhimu sana kwani awali barabara hiyo kuanzia Mto wa Mbu ilikuwa ikipitisha magari kati ya 20 na 25 kwa siku lakini, sasa yameongezeka hadi 3,500 kwa siku.

"Nasema barabara hii ni muhimu sana hivyo nakuagiza Meneja wa Tanroads mkoa wa Arusha kuhakikisha mkandarasi aliyepewa kazi ya kutengeneza barabara hii anafanya kazi usiku na mchana ili ikamilike, akizembea fukuza," alisema Magufuli na kuongeza:

"Sheria namba 17 ya mwaka 1997 na vifungu vyake inatoa mamlaka ya kuondolewa kwa mkadarasi anayezembea. Pia sheria inaelekeza kufikishwa mahakamani kwa wakandarasi wa aina hiyo, na
akitiwa hatiani na anaweza kufungwa miaka mitano. Hivyo basi sheria ipo na pale tutakapolazimika tutaitumia".

Magufuli aliuagiza uongozi wa Halmashauri ya Ngorogoro kuwasilisha maombi ya dharura ya fedha za matengenezo ya barabara katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) ili kuwezesha matengenezo ya barabara nyingine kufanyika.

"Tukiacha barabara ya kuja huku, nimetembelea barabara zenu katika wilaya ya Ngorongoro, kwa kweli ni mbaya sana hivyo zinahitaji matengenezo,"alisisitiza.

Juzi Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Eliasi Ngorisa, aliliambia Mwananchi kwamba halmashauri yake ilikuwa imeomba kiasi cha Sh400 milioni kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya kuifanyia matengenezo ya dharura barabara zinazoingia kijijini Samunge.

Dk Magufuli pia alimwelekeza Meneja wa Tanroads mkoani Arusha kuandaa mpango wa matengenezo ya barabara za Ngorongoro na kuwasilisha mapendelezo yake serikalini kwa ajili ya utekelezaji wake.

"Kaandike mpango huo sasa na ulete ili tuone jinsi ya kufanya, kama hujui kuandika tafuta watu wakusaidie," alisema Magufuli na kusababisha umati wa watu
kuagua kicheko.

Waomba msaada
Tofauti na viongozi wengine waliowahi kufika kwa mchungaji Mwasapila, Waziri Magufuli aliruhusu maswali kutoka kwa wananchi waliokuwa wakimsikiliza.

Wengi wao walilalamikia hali mbaya ya mazingira. "...pamoja na kwamba wewe si Waziri wa Afya, lakini tunajua unatoka Serikalini, tunaomba utusadie maana afya zetu zipo hatarini. Huwezi kuamini kwani huko barabarani unakuta mtu anajisaidia haja kubwa hapo,na mtu mwingine anakula chakula, kwa kweli hali ni mbaya tunaomba msaada,"alisema Nicholas Mwangoka.

Akijibu hoja hiyo, Waziri Magufuli alisema atawasilisha taarifa yake kwa Waziri Mkuu ambaye yupo mkoani Arusha na kwamba anaamini kupitia njia hiyo waziri wa sekta ya afya atafikishiwa ujumbe ili hatua za haraka ziweze kuchukuliwa.

Mapema mchungaji Mwasapila kupitia kwa msaidizi wake, aliomba Serikali ijenge daraja katika mto wa Samunge ambao umekuwa kikwazo cha magari kuingia kijijini hapo kwani hufurika kila mvua zinaponyesha.

Pia mchungaji huyo alimshukuru Waziri huyo kwa ahadi aliyoitoa akisema kuwa hatua hiyo inamtia moyo kuendelea kutoa tiba kwa wagonjwa wanaofika nyumbani kwake.

"Nakushukuru sana kwa ujio wako na yale uliyoyasema, unatupa matumaini,unatupa moyo, asante tunashukuru sana," alisema Masapila.

Foleni yapungua Samunge
Katika hatua nyingine, foleni ya magari ambayo ilikuwa zaidi ya kilometa 30 kutoka eneo analotolea tiba mchungaji Masapila sasa imepungua.

Kupungua kwa foleni hiyo kumetokana na utaratibu mpya wa kuingiza magari katika kijiji cha Samunge ambao unatarajiwa kuanza leo, pia kutokana na kasi ya mchungaji huyo katika kugawa dawa.
  

Tacaids yawaasa wagonjwa
Ellen Manyangu anaripoti kutoka Dar es Salaam kuwa, Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (Tacaids), imewataka wagonjwa waliokunywa dawa ya Mchungaji Masapila kutoacha kuendelea na dozi walizopewa hospitalini kwa kuwa dawa hiyo haijathibitika kutibu Ukimwi.

Mratibu wa  tume hiyo Dk Bwijo Bwijo alisema jana kuwa utafiti bado unaendelea kujua endapo kikombe hicho cha babu, kinaweza kutibu magoonjwa yanayoelezwa.

Alisema hayo jana alipokuwa akizungumza katika mjadala ulioandaliwa na Kituo cha Radio Clouds FM na kufanyika katika hoteli ya Kempisky jijini Dar es Salaam jana asubuhi.

Akizungumza katika mjadala huo, Dk Bwijo alisema dawa ya Mchungaji Masapila bado inafanyiwa utafiti ili kuthibitisha kama inatibu, hivyo wananchi hawapaswi kuacha kutumia dawa za kitabibu ghafla.

Kwa mujibu wa Bwijo, jitihada za kuthibitisha ubora wa dawa hiyo bado zinaendelea kwa ufadhili wa Shirika la Afya Duniani (WHO) na Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kudhibiti Ukimwi (UNAIDS).

“Wagojwa wote walioko kwenye matibabu ya dawa za kitaalamu na wamekunywa kikombe cha dawa ya babu wasiache kutumia dawa zao mpaka itakapothibitishwa kuwa dawa hiyo ni halali na inatibu,” alisema Dk Bwijo.

 Mwenyekiti Mstaafu wa Mtandao wa Wanaoishi na Ukimwi Afrika (TANEPHA), Alex Margery, alisema suala la Loliondo limejaa sura ya Ukimwi na kutahadharisha kuwa watu wasiache kutumia dawa za kitaalamu kwa kuwa dawa ya babu bado haijathibitishwa.

Alisema walishajitokeza watu mbalimbali katika nchi za Kenya na Afrika Kusini na kutoa dawa zilizoaminika kuwa zinatibu maradhi sugu ikiwemo ukimwi, lakini baadaye zilisababisha watu wengi kufa kutokana na kuacha kutumia dawa za kitaalamu kwa imani kuwa wamepona.

“Hili ni jambo la hatari sana hasa kwa jamii yetu kwani wagonjwa wanaacha kutumia dawa za kisayansi zilizothibitishwa kutibu, au kupunguza makali ya maradhi waliyonayo kwa imani kikombe cha dawa wanachopewa Loliondo  kinawaponyesha…, "alitahadharisha Margery.

Aliongeza dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi ARV zilikuwa katika dozi kubwa ya vidonge 14 kwa siku moja, lakini kadri siku zinavyoongezeka dozi hiyo inapungua na hivi sasa ni kidonge kimoja kwa siku.
Mtaalam wa Afya ya Jamii na Ukimwi, Dk Bennect Fimbo, alisema awali ugonjwa wa Ukimwi ulikuwa tishio kwa jamii kwa vile hawakuwa na uhakika wa mtu kuishi nao muda mrefu lakini, hivi sasa mtu anaweza kuishi nao kwa muda wa miaka 20.

Aliongeza kuwa mti wa Mugariga unaotumiwa na babu kama dawa umefanyiwa utafiti kwa muda mrefu, hivyo inapaswa uchunguzi wa ziada ufanyike ili kubaini mti huo unatibu magonjwa yapi na dozi yake.

Kandoro aweka udhibiti
Kutoka Mwanza Frederick Katulanda na Sheila Sezy wanaripoti kuwa, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro, amewaagiza wasafirishaji wa watu wanaokwenda kutibiwa kwa Mchungaji Masapila kuwaorodhesha watu wote ili kuweka kumbukumbu.

Akizungumza jana katika kikao chake na wamiliki a mabasi, Kandoro alisema Serikali imepanga utaratibu maalum ikiwa ni pamoja na kuweka vizuizi kwa lengo la kupunguza msongamano na kuwezesha wagonjwa kumfikia babu haraka zaidi.

Alisema Serikali imetambua kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa la watu wanaoenda Loliondo kwa ajili ya matibabu hayo hivyo utaratibu huo mpya utasaidia kupunguza msongamano.

Alifahamisha kuwa kuanzia sasa magari yote yanayotoka Mwanza na Kagera na wageni kutoka nchi za Rwanda, Uganda na Burundi kwenda Loliondo, wanapaswa kujiandikisha jijini Mwanza na kuacha majini yao katika kizuizi cha Magu.

Magari yatakayoruhusiwa kuondoka na kupita katika vizuizi ni yale yenye nguvu maalumu (four wheel drive) na mbasi. Malori ya aina yote hayaruhusiwi kwenda huko, alisema.

Akizungumzia suala la nauli kuwa juu, Kandro alisema serikali haitaingilia utozaji wa nauli bali kuhakikisha inaboresha mazingira ya Loliondo na kwamba nauli zitashuka zenyewe.

MI9CHONGO YA KUSOMA HIYOOOO


Fri, April 1, 2011 9:35:48 AM
New Zealand Open Development Scholarships | 8 Fully Funded PhD Scholarships | Apply Today
...
From:
Scholarship-Positions.com <admin@scholarship-positions.com>
...
Add to Contacts
To:leonardkilamhama@yahoo.com

New Scholarships from Scholarship-Positions.com April 1, 2011
Home   Search in Universities   Post a Job Free   Subscribe  
Subscribe in Reader


Please forward this email to your friends if they are also interested in scholarships.

2011 New Zealand Open Development Scholarships for Applicants from Selected Developing Countries, New Zealand
New Zealand Open Development Scholarships for Students from Bolivia, Ecuador, Honduras, Kenya, Mongolia, Nepal, Nicaragua, South Africa, Tanzania, Zambia, China,.. [Read Full Scholarship Detail]


8 Fully Funded PhD Scholarships at the University of Salzburg, Austria
2011- Doctorate Programme in the field of Imaging the Mind Consciousness, Higher Mental and Social Processes at University of Salzburg.. [Read Full Scholarship Detail]

2011 China Postgraduate Scholarship by Tan Kah Kee Foundation 
Tan Kah Kee Foundation Announce Tan Kah Kee Postgraduate Scholarship 2011 Study Subject: Courses  offered by Tan Kah Kee Foundation.. [Read Full Scholarship Detail]


10 ESRC Doctoral Training Studentships at University of London, UK
Ten ESRC-funded studentships in the social sciences are available as part of the Goldsmiths and Queen Mary ESRC Doctoral Training.. [Read Full Scholarship Detail]


2011 Project Assistant and JRF Positions in CSIR-Central Mechanical Engineering Research Institute, India
CSIR-Central Mechanical Engineering Research Institute offers Project Assistant and JRF Positions 2011 Study Subject: Robotics & Mechatronics, Microsystem Technology, Rapid.. [Read Full Scholarship Detail]

Overseas Scholarships for Computer Science Postgraduate Programmes at Heriot Watt University, UK
Funding for Postgraduate  Scholarships in Computer Science for International Applicants 2011 - 2012, UK Study Subject: Computer Science or Information.. [Read Full Scholarship Detail]


Achievement Scholarship and Foundation Scholarship in Swiss German University, Indonesia
Scholarships in Undergraduate programme in the field of Information Technology, Accounting, Pharmaceutical Engineering and Biomedical Engineering at Swiss German University.. [Read Full Scholarship Detail]


2011 Emerging Leaders in the Americas Program, Canada
Undergraduate and Graduate Scholarships for the applicants of Caribbean,Central America,North America,South America by Government of Canada in Canada-2011 Study Subject:Study.. [Read Full Scholarship Detail]


2012 Canada-CARICOM Leadership Scholarships Program in Canada
Undergraduate and Graduate Scholarships Program in the field of Good Governance, Prosperity, Rule of Law, Democratic Development, Pure and applied.. [Read Full Scholarship Detail]


2011 Canadian Commonwealth Scholarship Program
Graduate Canadian Commonwealth Scholarship Program for the applicants of Asia-Pacific and Africa by Government of Canada-2011 Study Subject:Open to all.. [Read Full Scholarship Detail]


2011 ECBA Scholarships Positions in Law, Pennsylvania
The Erie County Bar Association Scholarships  Positions in Law2011, Pennsylvania Study Subject: Law Employer: The Erie County Bar Foundation Level:.. [Read Full Scholarship Detail]


Maria Pia Gratton International Award at University of Illinois, USA
2011 -International Award for female graduate at University of Illinois in USA Study Subject:Academic and cultural experience Employer: University of.. [Read Full Scholarship Detail]


Kurdish Studies PhD Studentship at University of Exeter, UK
2011-Doctorate studentship in the field of Kurdish Studies of at University of Exeter in UK Study Subject:study of the Kurds.. [Read Full Scholarship Detail]


2011 PhD Studentship: fMRI Decoding of Mental State at Radboud University, Netherlands
Doctorate studentship in the field of fMRI Decoding of Mental State at Radboud University,Nertherlands -2011 Study Subject:fMRI Decoding of Mental.. [Read Full Scholarship Detail]


SCIBE PhD Position at Oslo School of Architecture and Design, Norway
Doctorate Positions in the field of Scarcity and Creativity in the Built Environment in Oslo School of Architecture and Design.. [Read Full Scholarship Detail]


2011-PhD Position in Philosophy of Law, Radboud University, Netherlands
Doctorate positions in the field of Philosophy of Law at Radboud University in Netherlands-2011 Study Subject:Philosophy of Law Employer:Radboud University.. [Read Full Scholarship Detail]


Adam Smith Fellowship and College Lectureship in Political Economy, UK
Pembroke College Announce Adam Smith Fellowship and College Lectureship in Political Economy, UK Study Subject: Political  Economy Employer: Pembroke College.. [Read Full Scholarship Detail]


Dean’s Award for Outstanding Scholarship Nomination at Michigan Tech, USA
Michigan Tech – Houghton, MI Announce Dean’s Award for Outstanding Scholarship, USA Study Subject: Courses offered by Michigan Tech –.. [Read Full Scholarship Detail]


Last Minute Deadline: World Bank Scholarship Program 2011-March 31 2011
Are you a national of a World Bank member country? Then you might be eligible for Japan/World Bank Graduate Scholarship.. [Read Full Scholarship Detail]


India Study Abroad Fellowships by Inlaks Foundation 2011
2011 Inlaks Shivdasani Foundation Announce Ravi Sankaran Fellowships,  India Study Subject: Sport Employer: Inlaks Shivdasani Foundation Level: Master Scholarship Description:.. [Read Full Scholarship Detail]


Fellowships for International Students in USA- 2011

This section includes the fellowships of 2011 for those students who want to study in USA. These fellowships are open for those also who want to work with their studies in USA. So these scholarships provide them a great opportunity to buildup a bright future. The eligibility criterion may vary accordingly. Let’s have a look [...]


[Read More..]

Media Education: An Emerging Field

With the stupendous growth of the media industry, Media education has witnessed a dramatic change over the last decade. Due to this phenomenal growth demand for well trained, professional journalists is very much on the higher side. Face of Media Education has entirely changed today. Big Media Houses have opened up private journalism colleges which [...]


[Read More..]

Scholarships for International Students in UK-2011

This section of the scholarships bolg includes the Scholarship for those students who want to study in UK. These scholarships provide them a great opportunity to buildup a bright future. The eligibility criterion may vary accordingly. Let’s have a look on these scholarships. 2011 International Postgraduate Scholarship at University of Strathclyde, UK Organization: University of [...]


[Read More..]

Clinical Research: A Viable Option for Science Graduates

Clinical research a viable and a lucrative option for science graduates. With the discovery and introduction of biotechnological drugs, the pharmaceutical and biotechnology industry is booming and expanding. Companies like Amgen, Genentech, UCB etc have given new and prominent dimensions to this field. Companies like Pfizer, Johnson and Johnson, Novartis are some well known Pharmaceutical [...]


[Read More..]


Applying for GRE? Join LearnWordlist.com for Free!


Scholarship-Positions.com Question Answer Forum
http://scholarship-positions.com/forum/
Scholarship-Positions.com on Twitter
http://twitter.com/newscholarships
Help Others
Forward this Newsletter.
 
 
 
Scholarship tags
2008 2009 Assistant Assistantship Australia Available Biology College Denmark DOCTORAL Fellow Fellowship Foundation France Germany Graduate IndiaInstituteInternational Molecular National Norway PhD PhD Position Position Postdoc Positions Postdoctoral Postgraduate Program ProgrammeResearch Scholarship ScholarshipsSchool Science Student Students Studentship Switzerland Technology UK University USA
 
Links
Home
Scholarship Forum
Search in Worldwide Universities
Post a Job Free
IndiaJobs.co.in
Scholarship-Positions.com
Scholarship Positions: Scholarships Financial Aid Fellowships, PhD, Postdoctoral, Graduate College Scholarships Find College University Scholarships and Financial Aid Positions Free
Scholarship-Positions.com
International Scholarships and Financial Aid Information Services
Office: 106 Civil Lines, Church Road, Bareilly, India, 243005
Forward This Email: Do you know some one who would benefit from this email, please forward it to them.


To unsubscribe or change subscriber options visit:
http://www.aweber.com/z/r/?7AzMDCxMtCwcHOysbMwctEa0nCwcTGxsLA==