Wednesday, February 1, 2012

SERIKARI YA TANZANI IWEKEZA KWA SOKA LA WANAWAKE, ILI KUEPUKA AIBU KWA SOKA LA WANAUME

Twiga Stars yaichakaza Namibia
Timu ya Soka ya Taifa ya Wanawake, Twiga Stars, imewapa raha Watanzania, baada ya kuibanjua kibabe, Timu ya Wanawake ya Namibia.

Golikipa wa Namibia, alikabiliana na adhabu kali baada ya kutunguliwa mara tano katika ushindi wa jumla wa mabao 5-2 ambao Twiga imeupata leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwa matokeo hayo, Twiga inasogea hatua ya pili ya kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wanawake ikiwa na ushindi wa jumla ya mabao 7-2.
Katika mchezo wa kwanza uliofanyika Windhoek, Namibia, Twiga iliichakaza timu hiyo mabao 2-0.
Mchezo wa leo, Twiga ilianza kwa kusuasua lakini baadaye ilicharuka na kuipeleka puta Namibia, hivyo kuilazimisha mabao matatu ya haraka dakika za lala salama.
Kwa matokeo hayo, Twiga sasa itapambana kwenye mzunguko unaofuata na mshindi wa mechi ya Misri dhidi ya Ethio

SODOMA, SODOMA, SODOMA HIYOOOOOO INAKARIBIA

Mume wangu ananidandia ukuta, nimezoea, napenda, kuna athari kiafya?’
Mungu ni mkubwa sana. Tunakutana tena leo katika kona yetu. Karibu msomaji lakini nina kitu tofauti. Nimeamua nimsaidie dada yetu ambaye ana tatizo la kuzoea mchezo wa kwenda kinyume. Kudandia ukuta.

Ni msomaji wangu, hivyo naomba nisitaje jina lake. SMS yake inasomeka: “Nimeolewa lakini sijazaa. Mume wangu ananipenda na mimi kumridhisha nimekuwa nikimpa kila anachotaka.
“Moja ya vitu ambavyo aliniomba ni kuruka ukuta. Mwanzoni sikumuelewa lakini baadaye nilimkubalia. Tulipoanza nilisikia maumivu lakini sasa nimezoea, ninapenda. Wakati mwingine tukiwa faragha, sitaki amalizie kwa kawaida, akipita na ukutani angalau ndiyo natosheka.
“Kusema kweli nimezoea na sipendi kuacha, je, kuna athari kiafya baadaye?”
JIBU
Kutokana na unyeti wa swali la dada yangu, naomba jibu langu liwe refu ili mwisho aweze kuelewa. Hii ni mada nzima ambayo naamini itampa jibu linalotakiwa;
Binadamu ni watundu! Walipoona njia ya kawaida imezoeleka wakaamua kujaribu na nyingine ambayo hairuhusiwi. Lengo lao ni kupata utamu zaidi. Sodoma na Gomora iliangamizwa lakini haijasaidia, mapenzi ya kinyume na maumbile yameshika kasi ulimwengu wa sasa.
Utafiti uliofanywa na wanafunzi wa Chuo cha Marekani mwaka juzi, ulibaini kuwa mtu mmoja kati ya wanne anajihusisha na vitendo vya kudandia ukuta na tathimini ya jumla inaonesha kati ya 30% na 40% ya wakazi wote wa nchi hiyo wanashiriki ngono ya kinyume na maumbile.
Hiyo ni Marekani! Tanzania hali si shwari. Hakuna takwimu iliyotolewa na watafiti lakini muamko wa watu kuchangamkia mchezo wa kudandia ukuta ni mkubwa. Kinachowafanya wengi wageuke waumini wa ‘ibada’ hiyo haramu ni simulizi za utamu unaopatikana.
Kama Mwandishi wa Habari na Mshauri wa Saikolojia katika Masuala ya Kijinsia, najua ni kiasi gani hali ni mbaya. Ukiachana na msomaji huyo, pia nina malalamiko ya wanawake ambao wanadai kugeuzwa watumwa wa ngono ya mlango wa nyumba na waume zao au wapenzi wao.
Upo msemo kuwa wanaume wengi wanaathirika mno kisaikolojia kwa maneno ya vijiweni kuhusu mapenzi ya mlango wa nyuma. Kwamba stori za watu wakisifia uhondo ambao wanadai kuupata hujenga kitu tofauti kwa wale ambao hawajajaribu.
Watu hao ambao walikuwa hawajawahi kujaribu kabla, wakitoka kwenye vijiwe vyao, hubeba maneno hayo kwa umakini mkubwa, huku wakisumbuliwa na hisia za kutaka kujaribu. Matokeo yake, usiku ukiingia hutaka kulazimisha kwa wake zao.
Moja ya kesi ambazo nimewahi kukabiliana nazo ni kutoka kwa mwanamke mtu mzima ambaye ni mke mdogo wa mganga mmoja wa tiba za asili mwenye jina kubwa nchini (simtaji jina tafadhali). Mwanamke huyo nilikutana naye ofisini kwetu.
Mwanamke huyo alisema kuwa wakati anaanza mapenzi na mganga huyo ilikuwa kabla ya ndoa lakini baadaye mume alimbadilikia na kumtaka amruhusu awe anampitia kwa mlango wa nyuma. Eti, akamuahidi kwamba akimruhusu hilo, atampangia nyumba halafu atafunga naye ndoa.
Kwa kunasa maneno kutoka kwenye kinywa chake, mwanamke huyo baadaye alikubali baada ya kushawishiwa sana na kupewa ahadi nyingi. Alikuwa Mkristo, akabadili dini akawa Muislam, akapangiwa nyumba na akaolewa. Mapenzi yakawa matomoto.
Mambo yaliendelea mpaka akaathirika. Akawa hawezi hata kukaza misuli kuidhibiti haja! Wakati anakuja kunisimulia hayo, alikuwa yupo kwenye kipindi kigumu katika ndoa, yeye na mume wake walikuwa hawaelewani kabisa.
Huyo ni mmoja, mwingine ni mfanyakazi mmoja wa kampuni inayojihusisha na usambazaji wa vipodozi. Huyu ni mdada tu, alipokuja kuzungumza nami, kwa haraka nilimpa hongera za ndani ya moyo wangu kwa mafanikio niliyodhani anayo.
Alikuja na gari lake la kifahari, nikaamini ana mafanikio ya kimaisha na anafurahia mzunguko wake, kumbe sivyo! Alifunua kinywa chake kunisimulia alivyonavyo nilichoka! Dada huyo naye ni mmoja wa watumwa wa ngono ya kupitia mlango wa nyuma.
Alinieleza kuwa yeye kazi yake haiwezi kumfanya aishi maisha ya kifahari, akae kwenye nyumba nzuri na kumiliki gari la bei mbaya, ila katika mizunguko yake ya kimaisha, alipata kigogo mmoja ambaye alimua kumgharamia vitu hivyo.
Walianza kama wapenzi na akawa anamhudumia vizuri. Hakuwa na shida ya matumizi ya kawaida, kigogo huyo anayefanya kazi kwenye moja ya makampuni ya simu za mkononi alikuwa anakata. Baada ya miezi michache alimbadilikia.
Kigogo huyo akaanza kuomba njia haramu na kuahidi kumbadilishia maisha. Kwa kuanzia alimpangia nyumba ya kifahari mikocheni halafu akamtaka atekeleze ombi lake ili ampe gari. “Alianza kuniomba kama utani,” alisema dada huyo kisha akaongeza:
“Siku moja alikuja pale aliponipangia akiwa na gari mpya ambalo ndilo ninalotumia, akaendelea kunibembeleza halafu akaweka ufunguo wa gari mezani, kwamba nikikubali matakwa yake, litakuwa langu. Nilijifikiria sana lakini baadaye nilifumba macho nikakubali.
“Siku hiyo niliumia mpaka nikashindwa kukaa vizuri, nililia akanibembeleza, wiki nzima sikutoka ndani. Nilipoona anataka tena nikamkatalia lakini akasema ataninyang’anya gari, ikabidi nikubali. Gari amenipa lakini kadi anayo, kila nikikataa ananitishia kuninyang’anya, naendelea kuwa mtumwa mpaka najihisi kulegea.”
Yupo mwingine ambaye ni mhitimu wa Shahada ya Sheria, huyu aliingia kwenye matatizo makubwa na mfadhili wake, aliyekuwa anafanikisha ada yake ya chuo baada ya kukataa matakwa ya kigogo huyo ya kushiriki mapenzi ya mlango wa nyuma.
“Aliniambia eti njia ya kawaida wamepita wengi, kwa hiyo akataka nimruhusu afungue njia yake mwenyewe, yaani kinyume na maumbile, akaniahidi kuninunulia gari lakini nilipokataa, akagoma kuniunganisha na wafadhili ambao wangenilipa ada ya chuo,” alisema dada huyo.
Kauli hizo zinatoa picha kwamba wanaume wengi wanawageuza wanawake watumwa wa mchezo huo wa kudandia ukuta kwa jeuri ya pesa. Eti, wananogeshwa na stori kwamba ndiyo mlango mdogo na unaobana kuliko ule wa kawaida. Hawazingatii athari ambazo mwanamke anazipata.

Wednesday, December 14, 2011

WABUNGE MMECHAGULIWA KUWAWAKILISHA WANANCHI NA KUTATUA KERO ZAO, JE UGUMU WA MAISHA NI KWENU TU?

Nyongeza ya posho za wabunge yaibua mjadala mzito  Send to a friend
Wednesday, 14 December 2011 10:45
0digg
Na Joyce Mmasi
NYONGEZA ya posho za wabunge imekuwa gumzo na kuzua mijadala isiyo na kikomo katika jamii ya Tanzania.
Tofauti na mijadala ya awali ya kupinga ama kuiunga mkono, sasa kinachojadiliwa ni kauli tata za viongozi waandamizi wa bunge juu ya jambo hilo.
Kauli tata ni zile za Spika wa Bunge, Anne Makinda na Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashillilah ambazo zimeonekana kutofautiana kana kwamba zimetolewa na watu wasiofanya kazi katika taasisi moja.
Utata huu unatokana na ukweli kuwa viongozi hao wanatoa majibu yanayotofautiana kuhusiana na suala moja.
Viongozi hao ambao wanafanya kazi katika ofisi moja wamezua maswali kufuatia kutoa matamko tofauti kuhusiana na suala moja ambapo wakati mmoja anapinga habari ya kuwapo kwa nyongeza hiyo ya posho kwa wabunge mwingine anaibuka na kueleza kuwa nyongeza inayozungumzwa ipo na imefanywa kwa makubaliano baina ya ofisi, serikali na wabunge wenyewe.
Mparaganyiko huo wa mawazo unatokana na taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari kuhusu kuongezeka kwa posho za wabunge kutoka Sh70,000 hadi 200,000 kutwa hivyo kufanya bajeti ya posho hizo kwa mwaka kufikia Sh28 bilioni.

Kutokana na ongezeko hilo, kila mbunge atakuwa akilipwa Sh 80,000 kama posho ya kujikimu (per diem) anapokuwa nje ya jimbo lake, posho ya vikao,  Sh200,000 na mafuta ya gari Sh50,000 kila siku, sawa na Sh330,000 kwa siku huku mshahara jumla kabla ya makato ukielezwa kuwa ni sh 2.3 milioni.

Kauli tata za viongozi
Kwa mujibu wa Dk Kashillilah, mapendekezo ya kutaka posho za wabunge zipande, yaliibuka katika mkutano wa wabunge mjini Dodoma Novemba 8 mwaka huu, lakini hadi wakati anatoa tamko anasema yalikuwa hayajaanza kutekelezwa.
Siku kadhaa baadaye, Spika wa Bunge, Anne Makinda akaibika na kauli inayoonekana kupingana na ile ya katibu wake na akakiri kuwa ni kweli posho za wabunge zilikuwa zimeongezeka kutoka Sh 70,000 hadi Sh 200,000 kwa kikao na zilikuwa zimeanza kutumika.
Mbunge huyu alikuwa anapata Sh 70000 kwa hiyo tumemwongezea Sh130,000 na hupati 'unless' (isipokuwa) umefanya kazi ya Bunge na umesaini asubuhi na jioni hujafanya hivyo hupati hizo hela, anasema Makinda katika kauli inayokinzana na ile ya Dk Kashillilah ambaye wanafanya kazi katika ofisi moja.
Utata huu wa kauli toka kwa watendaji wakuu wa taasisi hii nyeti ya Bunge ndio ulioongeza kasi ya mjadala wa nyongeza za posho za wabunge. Waliopata fursa ya kuchangia wanahoji sababu ya kukinzana kwa majibu katika suala nyeti kama hilo.
Wengine wanaenda mbali zaidi kwa kusema utata huo unaonyesha ni jinsi gani suala hilo lilivyo tata na ambalo huenda likawa halikuwa na ‘baraka’ hata na baadhi ya watendaji hao na kwamba utekelezaji wake huenda umepelekwa haraka haraka bila kupata baraka za wahusika.
Utata huo unazungumziwaje?
Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila (NCCR- Mageuzi), anasema suala la kupishana kauli kwa viongozi wawili wa taasisi moja, ni udhaifu mkubwa kwa taasisi hiyo. 
Suala la posho linatakiwa litazamwe upya katika mihimili yote ya dola, panapokuwa hakuna kanuni ya kuweka uwiano miongoni mwa mihimili hii, kunasababisha manung’uniko na malalamiko kwa wananchi, inatakiwa itazamwe upya,  hili suala la posho lipatiwe ufumbuzi kabisa,” anasema Kafulila. 
Kwa upande wake, Profesa Ruth Meena ambaye ni mwanaharakati wa masuala ya kijamii na msomi aliyebobea anasema ni jambo la kusikitisha kuwa viongozi wa bunge wanapishana kauli juu ya suala hilo la posho.
Inasikitisha sana hawa wawakilishi wetu kujiongezea posho wakisema kuwa gharama za maisha zimepanda, kwenye hali kama hii ya sasa hakuna njia yeyote utakayo weza kutumia kuhalalisha ongezeka kama hili,  anasema.
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia anasema mfumo mzima wa utoaji wa posho nchini ni wa kifisadi.
Mbatia anasema ipo haja ya kuutizama upya mfumo huo ambao umeacha pengo kubwa kati ya mwenye nacho na asiyekua nacho.
Jambo hili halitendi haki kwa watanzania, linaweka tofauti kubwa kati ya wenye nacho na wasiokuwa nacho hii si sawa, mfumo mzima wa utoaji posho unatakiwa kutizamwa upya, anasema.
Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba Mkoani Kagera, Dk Methodius Kilani anasema ongezeko hilo la posho limekuja ghafla na kwamba kiwango hicho ni kikubwa na hakiendani na hali halisi ya uchumi wa nchi.
Watanzania wengi wanalalamika maisha magumu sasa Wabunge wanapoongezewa posho kwa kiwango kinachofikia Sh 200,000 watambue kwamba kuna wananchi wanaohitaji msaada, hizo nyongeza za posho zingeweza kuwasaidia kwa namna moja ama nyingine ambapo ongezeko la posho hizo zingeweza kuwasaidia anasema Askofu Kilaini.
Kwa upande wake, Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Alhad Mussa Salum  anasema kwamba haoni tatizo posho za wabunge kuongezeka na kwamba  kutokana na majukumu yao mazito ya kuwahudumia wananchi.
Ni jambo jema lakini wabunge watambue kwamba wananchi waliowachagua wana matatizo mengi ya kiuchumi sasa wanaposikia wabunge wameongezewa posho lazima nao watahoji lakini kinachotakiwa ni kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa kutatua matatizo ya wananchi wao”anasema Sheikh Alhad.
Lakini, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (Chadema)  anasema ongezeko hilo ni batili kwa sababu halina baraka za Rais Jakaya Kikwete.
Spika wa Bunge anajua kwamba posho zote hulipwa baada ya rais kuidhinisha. Anasema ongezeko la posho halikuidhinishwa kwakuwa uthibitisho wa kuidhinisha ni Masharti Mapya ya kazi kwa wabunge ambayo hayajatolewa na Ofisi ya Rais.
Anasema kitendo cha kuanza kulipa posho mpya bila masharti mapya ya kazi za wabunge ni kukiuka sheria ya utawala wa Bunge kifungu cha 19 na kwamba kutokana na hali hiyo, Tume ya Bunge inapaswa kuwajibika kwa kutumia vibaya mamlaka yake.
Anapendekeza posho mpya zifutwe na zilizolipwa zirejeshwe mara moja kwani zimelipwa kinyume na sheria. “Spika anapaswa kuheshimu sheria ambazo Bunge limepitisha na kwenda kinyume na sheria kwa makusudi ni kosa la kuvuliwa uspika, anaeleza.
Mbunge wa Jimbo la Ubungo,  John Mnyika (Chadema) anasema ongezeko hilo linatakiwa kusitishwa kwa kuwa mchakato wake umefanyika kinyume na taratibu.
Anasema kauli ya Spika Makinda kwamba nyongeza hiyo inatokana na kupanda kwa gharama za maisha mkoani Dodoma haina ukweli, wala mantiki na ina mwelekeo wa upendeleo

SERIKALI IKITAMBUA MCHANGO WA WALIMU,ITAWAJALI HATA KWA MASLAHI

CWT: Hakuna mwalimu aliyelipwa mpaka sasa  Send to a friend
Tuesday, 13 December 2011 19:45
0digg
Rais wa CWT, Gratian Mukoba
Pamela Chilongola
CHAMA Cha Walimu Tanzania (CWT), kimesema hakuna mwalimu yoyote aliyelipwa malimbikizo ya stahili mbalimbali na mishahara kama ilivyotangazwa  na baadhi ya vyombo vya habari.

Juzi Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Philip Mulugo alipozungumza na gazeti moja la kila siku siyo Mwananchi, alisema Novemba, mwaka huu, serikali ilikuwa imelipa Sh29 bilioni, kati ya Sh49.6 bilioni zinazodaiwa na walimu. Lakini jana Rais wa CWT, Gratian Mukoba alisema: “Hadi leo (jana) hakuna mwalimu yeyote ambaye alikuwa amelipwa malimbikizo ya stahili zao au mishahara yao.”

Alisema tangu Juni mwaka huu, CWT na Serikali wamekuwa na vikao kadhaa kuhusu madai hayo.

“Sisi tunadai mishahara yetu  tuliyodhulumiwa, tunakandamizwa sisi walimu tunashangaa badala ya kutulipa hela tunazodai, tunashangaa kusikia wabunge wameongezewa posho na vitu vingine ambavyo vimefikia Sh330,000 milioni.“Msimamo wetu wa kugoma Januari mwakani uko palepale, hivyo hakuna mtu ambaye atatulaumu,  imeshapita miezi mine, serikali haijafanya kitu chochote kuhusu sisi walimu,”alisema Mukoba.

Alisema madai hayo yanawahusu walimu zaidi ya 3,000 ambao hawajalipwa kuanzia mwaka 2008.Mukoba alisema kero nyingine ambayo itawafanya wagome ni walimu walioshushwa vyeo mwaka 2007 na kutopandishwa mpaka sasa.“Na hii imetokana na waraka kandamizi uliotolewa na serikali mwaka 2007 ambao uliwashusha vyeo baada ya kujiendeleza kielimu.

“Serikali ilikubali kuufuta waraka huo baada ya kuridhika kwamba ulikuwa unawakandamiza walimu, lakini hadi sasa unaendelea kutumika, haujafutwa,” alisema Mukoba.   
Alisema kuna walimu ambao wanapata mishahara inayolingana na kwamba haijarekebishwa. “Utakuta mwalimu anaanza kazi anakuwa sawa na yule mwalimu aliyeanza muda mrefu.“Utakuta mwalimu amepanda daraja, lakini mshahara wake haujarekebishwa huku akiendela kupokea mshahara wa zamani,”alisema Mukoba

NDANI YA CUF KWAFUKUTA, USHIKIANO WAO NA CCM BUNGENI NDIO CHANZO

Vita ya Seif, Hamad Rashid yavuta kasi  Send to a friend
Tuesday, 13 December 2011 20:39
0digg
Maalim Seif Shariff Hamad
KAMATI YA MAADILI YAINGILIA KATI, KUWASHUGHULIKIA WANAOKIUKA TARATIBU
Geofrey Nyang’oro
CHAMA Cha Wananchi (CUF), kimetoa tamko kuhusu vurugu zilizofanywa na wafuasi wake katika mikutano ya mbunge Wawi, Hamad Rashid Mohamed, huku kikipanga kumuita mbunge huyo mbele ya Kamati ya Maadili ili ajibu tuhuma za kukiuka taratibu za chama.Desemba 11 na 12 mwaka huu, wanachama wa CUF wamekuwa wakipambana kwa kutumia silaha za jadi yakiwamo mapanga katika mikutano iliyoitishwa na Hamad Rashid kwenye matawi ya chama hicho, Kata ya Manzese, huku tukio la juzi katika tawi la Chechinya, likisababisha umwagaji damu.

Jana akizungumzia vurugu hizo makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam,  Naibu katibu Mkuu wa CUF Bara, Julius Mtatiro alisema kitendo kilichofanywa na mbunge huyo ni kinyume na taratibu za chama.

Mtatiro alisema  Hamad Rashid  ameungana na baadhi ya wajumbe wa Baraza Kuu la chama hicho kuendesha mikutano hiyo kinyume na taratibu.

“Ifahamike kuwa haya yanayoendelea si sahihi. Chama chetu kina namna ya kipekee ya kutafuta uongozi. Hii ya Hamad Rashid  ni zaidi ya kutafuta ukatibu mkuu, ni njia ya kuua chama. Hatuwezi kutafuta ukatibu mkuu kwa njia ya umafia,”alisema Mtatiro.

Mtatiro alisema kutokana na vitendo hivyo, CUF inatarajia kumchukulia hatua mbunge huyo kwa mujibu wa taratibu zake. Katika hatua za awali, mbunge huyo pamoja na wenzake wanaomuunga mkono wataitwa kwenye Kamati ya Maadili na Nidhamu  wakati wowote kuanzaia sasa kwa ajili ya kuhojiwa.

Alisema baada ya mbunge huyo na washirika wake  kuhojiwa, taarifa zitapelekwa kwenye Halmashauri Kuu ya chama ambayo itaamua hatua za chukua  dhidi yao.
“Siwezi kusema ni hatua gani zitachukuliwa, sababu katika hili mimi sijui na wala Seif Shariff Hamad hajui, ila chama ndio kitakachotoa maamuzi kwa mujibu wa katiba,”alisema Mtatiro.

Alisema kwa mujibu wa taratibu za CUF, mikutano inayofanywa na Hamad siyo halali . Akasisitiza, “huwezi kufanya mikutano bila  kuwajulisha makao makuu ya chama, ofisi za mikoa na wilaya unakokwenda kufanya mkutano ua ziara”.

“Mimi Mtatiro pamoja na nafasi yangu siwezi kuondoka hapa na kwenda Wawi Pemba kufanya mikutano bila ya makao makuu ya CUF kujua na pia ofisi za mikoa na wilaya katika eneo husika. Ni lazima kutoa taarifa,”alisisitiza Mtatiro huku akitolea mfano ziara inayofanywa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif

“Ni kweli anataka ukatibu, kumekuwa na vitisho, lengo nini ni kuua chama! Lakini, Hamadi fedha anapata wapi? Uchaguzi tunafanya 2014, kwanini iwe sasa?,”alihoji Mtatiro.

Hamad Rashid akana
Gazeti hili lilipomtafuta Hamad Rashid kuzungumzia hatua hiyo ya chama chake, alisema "Mtatiro aeleze kwa nini alituma vijana kwenda kuvuruga mkutano wangu juzi badala ya kuleta bla bla."

Alisema awali mkutano wake ulitawaliwa na amani na alipokewa na viongozi wa chama katika tawi hilo na kupelekwa sehemu ya mkutano bila tatizo.

“Aulizwa kama ni haki kwa walinzi kuvamia mkutano wa wananchi, wakiwa na mapanga na sime kwa ajili ya kufanya vurugu ,“alisema.

Mbunge huyo alisisitiza kwamba  hajafanya kosa kwa kuamua kufanya ziara na mikutano ya hadhara bila kutoa taarifa kwa uongozi wa chama na kuongeza,   "Kama viongozi hao wa makao makuu wanaona taratibu zimevunjwa, walistahili kuniandikia barua ya kuniita na kunihoji. Sio kutuma vijana wa Blue guard  kwenda kuzuia mkutano."
Vurugu za juzi
Mtatiro alimtuhumu Mbunge huyo kuwa aliandaa vurugu kwa kukodi vijana zaidi ya 100, kutoka katika eneo la Nakos ambao ni wafuasi na wapenzi wa CCM.

Alisema vijana hao walipewa kazi ya kushambulia hata kwa kuua endapo wangewaona walinzi wa chama hicho maarufu blue guard.
Kuhusu walinzi kufika katika eneo hilo, Mtatiro alisema walikuwa wakitekeleza majukumu yao ya kila siku ya kufuatilia na kujua kila kinachoendelea katika chama hicho na pia moja ya kazi yao ni kuhoji jambo lolote linalofanywa kinyume na taratibu za chama.

“Hawa walinzi wa CUF walifika katika eneo hilo baada ya kusikia kuna mkutano unaofanyika kinyume na utaratibu wa chama. Hawa kazi yao ni kuhoji wahusika na kukusanya taarifa za kwanini watu wamekiuka taratibu kisha  kuziwasilisha kwenye ofisi za chama kwa ajili ya hatua zaidi,”alisema Mtatiro.

Alisema walipofika na kuanza kazi, ghafla walivamiwa na kundi la vijana zaidi ya 100 wakiwa na silaha za mapanga na marungu na kuanza kuwashambulia na kusababisha walinzi wanne na baadhi ya wanachama kujeruhiwa.
Ushuda wa majeruhi
Katika hatua nyingine, walinzi wawili walionusurika kifo katika mapambano hayo ya juzi;  Abdallah Kassim na Hamis Idd wakiwa na majeraha ya mapanga mmoja kichwani na mwingine  shingoni, walifika kwenye mkutano huo wa Mtatiro na waandishi wa habari na kueleza kilichotokea juzi.

Akizungumzia tukio hilo, Kassim ambaye alikuwa ameshikilia RB yenye namba MAG/RB/22150/2011 aliyoifungua katika kituo cha polisi Magomeni,  alisema ni Mungu tu ndiye aliyemuokoa.

“Sisi tulisikia kuna mkutano unafanyika kinyume na utaratibu wa chama eneo la Chechnya , tulikuwa walinzi 8, tulichukua gari na kwenda eneo la tukio. Tulipofika wenzetu waliingia ndani kwa lengo la kutaka kujua kinachoendelea ndipo tulipovamiwa,”alisema Kassim.

Alifafanua kwamba, kundi la vijana wakiwa na mapanga, Sime na marungu walianza kwa kutaka kutoa upepo gari walilokwenda nalo.

Kassim aliyekatwa panga shingoni, alisema wakati akifanyiwa unyama huo nyuma yake kulikuwa na kijana aliyetaka kumkata na panga kichwani lakiin mlinzi mwenzake akadaka mkono wa kijana huyo na kumuokoa.
“Panga hilo lingenikata sijui kama ningekuwa hai mimi, yaani ni Mungu tu alininusuru na kifo, ” alisimulia  Kassim kuhu akiwa na jereha  shingoni na kueleza kuwa anakabilia pia na maamivu mbavuni.
Naye Hamiss Idd aliliambia Mwananchi kuwa, tukio hilo na la hatari ambalo kamwe hakulitegemea na tayari ameshonwa nyuzi nne.

Alisema vijana hao waliowakata mapanga pia waliwapora  vitu vyote, walivyokuwa navyo pamoja na simu nane na kwamba yeye binafsi aliporwa  fedha tasilimi Sh 35,000.

Tuesday, November 22, 2011

Katiba: Chadema yataka kukutana na Kikwete


 Send to a friend
Monday, 21 November 2011 18:42
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Freeman Mbowe ,akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maamuzi ya kamati Kuu ya chama hicho juu ya Muswada wa Katiba mpya jijini Dar es Salaam jana.Kulia ni Katibu Mkuu wa Chama hicho Dk. Willibrod Slaa.Picha na Fidelis Felix
Geofrey Nyang’oro na Keneth Goliama
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeunda kamati ndogo ya watu sita kwa ajili ya kwenda kuonana na Rais Jakaya Kikwete kuwasilisha madai yake juu ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba wa mwaka 2011, uliopitishwa bungeni juma lililopita.

Kamati hiyo imeundwa katika mkutano wa dharura wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, uliofanyika Dar es Salaam juzi ili kukutana na Rais Kikwete kumjulisha kile walichoeleza kuwa upungufu wa muswada huo na kisha kumtaka atafakari kama ausaini kuwa sheria au la.

Akisoma tamko hilo kwa vyombo vya habari katika mkutano uliofanyika Makao Makuu ya Chadema jana, Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe alisema kamati hiyo ya watu sita, inafanya taratibu za kumuona Rais Kikwete wakati wowote kuanzia sasa.

Mbowe alisema kamati hiyo itaongozwa na yeye, Katibu Mkuu Dk Willbrod Slaa, Makamu Mwenyekiti (Bara) Said Arfi na Makamu Mwenyekiti (Zanzibar), Said Issa Mohamed. Wengine ni Mshauri wa Masuala ya Siasa wa chama hicho, Profesa Mwesiga Baregu, Profesa Abdallah Safari na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu ambaye pia atakuwa katibu wa kamati hiyo wakati wa mkutano huo.
“Hivi sasa taratibu za kumuona Rais zinaendelea, tutamuona wakati wowote kuanzia sasa na kumweleza mapendekezo yetu juu ya upungufu uliomo kwenye muswada wa sheria hiyo na kama atatusikiliza tutashirikiana naye akikataa tutawaeleza wananchi hatua za kuchukua,” alisema Mbowe.

Alisema ushiriki wa Chadema katika mchakato wa kuandika Katiba Mpya utategemea mazungumzo hayo akisema hiyo ndiyo fursa pekee inayoweza kutumika licha ya muswada huo kupitishwa ‘kibabe’.

“Bado kuna fursa za kisiasa na kijamii katika kujenga mwafaka wa kitaifa juu ya haja ya nia na mchakato na misingi ya Katiba Mpya, Kamati Kuu imesikitishwa na uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete badala ya kuzitumia fursa hizo amejiingiza kwenye upotoshaji uliofanywa na wabunge wa chama chake juu ya misingi na maudhui ya sheria hiyo,” alisema Mbowe na kuongeza,

“Kamati Kuu inaamini badala ya kuwaunganisha Watanzania na kujenga muafaka wa kitaifa unaohitajika katika kuandika Katiba Mpya, hotuba ya Rais Kikwete kwa wazee wa CCM wa Mkoa wa Dar es Salaam imezidi kuwagawa wa Tanzania kwa misingi ya ushabiki wa vyama vya siasa kitendo hiki ni hatari kwa Taifa.”

Alisema Katiba si mali ya viongozi wala wanasiasa, bali ni ya wananchi inayohitaji mchango mpana wa maoni yao juu ya kuunda sheria itakayokusanya maoni na hata kuundikwa kwake.

Alisema Chadema kitaendelea kuwaelimisha wananchi na wadau wote juu ya ubovu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na umuhimu wa kuwa na sheria bora itakayoratibu uundwaji wa tume ya kukusanya maoni.
Chama hicho kimewaagiza wabunge na viongozi wake kufanya mikutano ya ndani na ya hadhara yenye lengo la kuwaelimisha wananchi juu ya sheria hiyo na madhara yake.

Yalia na Polisi

Kamati Kuu ya Chadema pia imelaani kitendo cha Serikali kukizuia chama hicho kufanya mikutano na maandamano nchi nzima kwa kile ilichodai ni kukinyima haki ya kikatiba ya kufanya shughuli zake.

“Polisi kuzuia mikutano ya hadhara ya Chadema na maandamano ya amani ya wananchi wanaopinga mchakato uliopitishwa kuwa  sheria siyo tu kwenda kinyume na haki za msingi za kikatiba, bali pia unahatarisha amani na utulivu wa nchi,” alisema Mbowe.

Aliitaka Serikali kutoa tamko la kufuta amri hiyo huku akisisitiza kuwa Chadema kitaendelea kutumia njia zote za amani zilizopo ikiwemo mikutano ya hadhara na maandamano kama ilivyoainishwa katika Katiba ya sasa.

Kwa nini waligoma?
Awali, Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, alitaja sababu saba zilizowafanywa wasusie mjadala huo ikiwamo kukiukwa kwa Kanuni za Kudumu za Bunge wakati wa uwasilishwaji muswada huo.

Alisema Kamati ya Bunge iliingiliwa kazi zake kwa kuzuiliwa kukusanya maoni katika kanda 10 kama ilivyokuwa imepanga na badala yake maoni yakakusanywa kinyume na utaratibu na kuingizwa kwenye muswada huo.
Aliishutumu Serikali akidai kuwa iliingilia mchakato huo kwa kumtumia Spika wa Bunge, Anne Makinda.

Akizungumzia hatua ya wabunge hao kususa, Dk Slaa alisema kamati ilipongeza hatua hiyo akisema ulikuwa uamuzi wa kijasiri uliowafanywa wasiwe sehemu ya kupitishwa sheria mbovu.

“Kamati Kuu imewapongeza wabunge wa Chadema kwa kususia vikao vya kupitisha sheria hiyo kwani ushiriki wao ungeipa uhalali wa kisiasa na kijamii, sheria ambayo haikuzingatia nia ya haja ya dhati ya kuweka utaratibu wa kisheria utakaoiwezesha nchi yetu kupata Katiba Mpya,” alisema.

Wabunge wa Chadema na wenzao wa NCCR-Mageuzi, walisusia kikao cha Bunge kilichojadili na kupitisha Muswada wa Sheria mpya ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011.

HALI SI SHWARI NDANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI

CCM kwachafuka Send to a friend
Monday, 21 November 2011 18:54
Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein na Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Benjamin Mkapa, wakifurahia jambo kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu ya Chama hicho, mjini Dodoma jana. Picha na Edwin Mjwahuzi
UVCCM WAPANGA KUASI, NI HOFU YA KUFUTWA KWA UMOJA WAO
Neville Meena, Dodoma
HALI imezidi kuwa tete ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kundi kubwa la Umoja wa Vijana wa Chama hicho (UVCCM), linadaiwa kupanga mkakati wa kuasi, endapo mkakati unaodaiwa kuandaliwa wa kuuvunjwa umoja huo utafanikiwa.Hatua ya viongozi wa UVCCM kutoka karibu mikoa yote nchini kukusanyika mjini Dodoma kufanya kile walichokiita kuwa ni “kupigania umoja wao na chama chao,” imezidi kuchafua hali ya hewa.

Taharuki ndani ya chama hicho tawala imekuja kipindi ambacho vikao vikuu vya chama hicho ambavyo ni Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), vinakutana chini ya mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete.

Kamati Kuu ilianza jana saa 8:00 mchana pasipo Rais Kikwete kutoa maelezo yoyote ya ufunguzi. Kilitanguliwa na kikao cha Kamati ya Maadili kilichoanza juzi na kumalizika jana asubuhi, pia kikiongozwa na Kikwete.

Juzi usiku, wenyeviti wa UVCCM kutoka mikoa 18 nchini walikutana katika ukumbi wa baa moja maarufu iliyopo eneo la Area D mjini hapa kupanga mikakati jinsi ya kuuokoa umoja wao usivunjwe na hatua za kuchukua iwapo azma hiyo itatekelezwa.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na baadhi ya washiriki wa kikao hicho zinasema, moja ya maazimio ni kwamba ikiwa UVCCM utavunjwa, basi watahamia vyama vya upinzani, huku wakikitaja Chadema kuwa ni mahali panapowafaa kwa ajili ya kuendeleza harakati za ukombozi wa nchi.

Kikao hicho kilichohudhuriwa na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM na wale wa Baraza Kuu, kiliweka msimamo wa kutetea kuendelea kuwepo kwake kwa gharama yoyote, hata ikiwa ni kuwafungia ndani wajumbe NEC ya CCM iwapo wataridhia kufanya hivyo.

Kauli za viongozi
Hata hivyo, mmoja wa wajumbe wa Sekretarieti ya CCM ambaye hakupenda kuandikwa jina gazetini alisema hakuna mpango wa kufuta UVCCM na kuziita taarifa hizo kuwa ni za kupika.

Kauli yake iliungwa mkono na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye ambaye alisema: “Hakuna kitu kama hicho, mimi ni mshiriki wa vikao vyote vya Sekretarieti hakuna ajenda hiyo kwenye vikao vyetu hivi.”

“Ndiyo maana kwenye mkutano na waandishi wa habari nimesema kwamba watu waache kupandikiza vitu ambavyo kimsingi havipo, vikao hivi ni vya kawaida na ajenda zimewekwa wazi, sasa kama kuna watu wanaleta hizi hoja, basi wana malengo yao tu.”

Mapema Nape akizumgunza na waandishi wa habari alisema kumekuwapo na taarifa nyingi zinazowafanya Watanzania kutaharuki kana kwamba kuna vita inayotarajiwa kutokea mjini hapa.

“Naomba wanahabari wenzangu, nisaidieni maana haya yote yanatokana na taarifa zinazoandikwa kwenye magazeti na vyombo vingine vya habari, lakini ajenda zetu kama nilivyosema jana (juzi) zinafahamika, kubwa ni kupitia utekelezaji wa mabadiliko ndani ya chama chetu,” alisema Nape.

Naye Katibu Mkuu wa UVCCM, Martin Shigela alisema hana taarifa zozote kuhusu kuwepo kwa mpango wa kufutwa kwa umoja huo ambao yeye ni mtendaji wake mkuu na kwamba hata katika kikao cha sekretarieti ambacho yeye ni mjumbe hakukuwa na ajenda ya aina hiyo.

Hata hivyo, Shigela hakuwa tayari kuweka bayana iwapo alifahamu mkusanyiko wa viongozi wa UVCCM kutoka mikoani waliopo Dodoma, zaidi ya kusisitiza kwamba kipindi hiki ni cha kutulia kwa wana CCM kutokana na kuwepo kwa taarifa nyingine ambazo wakati mwingine vyanzo vyake si bayana.

Chimbuko la hisia
Chimbuko la hisia za kufutwa kwa UVCCM ni taarifa zisizo rasmi kutoka ndani ya vikao vya Kamati ya Maadili ambayo katika siku yake ya kwanza iliwahoji baadhi ya viongozi wake akiwamo Kaimu Mwenyekiti, Benno Malisa.

Wengi walihojiwa kuhusu utendaji wa kamati ya kutathmini upya uendeshaji wa UVCCM, ambayo tayari imefanya kazi yake katika mikoa 19 ya Tanzania Bara. Kamati hiyo inayoongozwa na Mjumbe wa Baraza Kuu ya UVCCM, Hussein Bashe, inatuhumiwa kuendesha mikutano iliyotumika kuwakashifu viongozi wa juu wa CCM wakiwamo Mwenyekiti Kikwete na Katibu Mkuu, Wilson Mukama.

“Kuna taarifa za uhakika kwamba ajenda hii haikupitia kwenye sekretarieti, inatoka kwenye kamati ya maadili kwa tuhuma kwamba eti sehemu kubwa ya UVCCM tuko nyuma ya kundi moja ndani ya chama,” alisema mmoja wa wenyeviti wa umoja huo na kuongeza:

“Sasa mpango wao ni kufuta viongozi wote wa kuchaguliwa na baada ya hapo waandae uchaguzi mwingine ili kuwaweka viongozi wanaowataka, sasa hili sisi tunasema hapana kama ni tatizo litatuliwe lakini wasituulie umoja.”

Mmoja wa maofisa wa CCM makao makuu alisema jana kuwa taarifa kwamba UVCCM inafutwa zimezagaa katika ofisi hizo lakini bado zilikuwa hazijathibitishwa kutokana uamuzi wa vikao vya Kamati ya Maadili kufanywa kwa siri kubwa.

Mkakati wa Kupinga
Taarifa za mpango huo ndizo zilizowatia wazimu UVCCM kiasi cha kuitana Dodoma kwa lengo la kukabiliana na NEC ikiwa ‘itathubutu’ kuubariki.

Habari kutoka ndani ya kikao cha juzi usiku zinasema wenyeviti hao walikubaliana kwa kauli moja kuwaita wenyeviti wa wilaya wa umoja huo wa vijana ili kuongeza nguvu za kuwakabili wakuu wa CCM.

Mmoja wa wenyeviti kutoka mikoa ya Kanda ya Mashariki alisema juzi usiku kwamba: “Katika hili tumejipanga, tunao vijana zaidi ya 300 wapo kambini, tutawaleta hapa, tutaungana nao kupinga uamuzi huu.”

Harakati za UVCCM zinakwenda sambamba na kupinga utekelezaji wa mpango wa kujivua gamba ambao wanasema unatekelezwa kwa upendeleo ukiwalenga baadhi tu ya watu.

Mmoja wa viongozi hao alinukuliwa na chanzo chetu akisema wanaopaswa kufukuzwa au kuchukuliwa kwa hatua na CCM ni makada ambako Rais Kikwete alipata kura chache wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka jana.

Kwa mantiki hiyo, vijana hao walisema mpango wa kujivua gamba hauna tija kwa sasa kwani unakigawa chama na kwamba CCM kina matatizo makubwa zaidi kinayopaswa kushughulikia badala na siyo kuchochea chuki miongoni mwa wanachama wake.

Maazimio ya NEC
NEC inakutana miezi minne tangu kilipokutana mara ya mwisho na kutoa maazimio ambayo yalisababisha mmoja wa makada wake, Rostam Aziz kujiuzulu ubunge katika Jimbo la Igunga pamoja na ujumbe wa NEC.

Rostam katika kujiuzulu huko aliitupia lawama sekretarieti ya chama hicho kwa kile alichokiita kuwa ni kuendesha siasa chafu dhidi yake na kuwataja kwa majina Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Tanzania Bara, John Chiligati na Nape kuwa wahusika.

Kujiuzulu kwa Rostam ni miongoni mwa mambo ambayo yanatarajiwa kuchukua nafasi katika mjadala wa CC na NEC.

Katika mazingira hayo, kuna kila uwezekano wa kutathmini jinsi falsafa ya kujivua gamba ilivyotekelezwa. Kuna madai kwamba Sekretarieti inayoongozwa na Mukama nayo imegawanyika katika suala la utekelezaji wa uamuzi wa NEC, hali inayoongeza sintofahamu ndani ya chama hicho.

HOTUBA YA RAISI KIKWETE KWA WAZEE WA CCM-DAR ES SALAAM


HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE,
KWA WANANCHI KUHUSU HALI YA UCHUMI NCHINI NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA, TAREHE 17 NOVEMBA, 2011

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa,
Mstahiki Meya,
Viongozi wa Serikali,
Wazee wangu,
Ndugu Wananchi,

Nakushukuru Mkuu wa Mkoa na viongozi wenzako wa Jiji la Dar es Salaam kwa kuniandalia fursa hii ya kukutana na Wazee wa Dar es Salaam.  Nawashukuru sana wazee wangu kwa kuitikia wito wangu huu wa kukutana nanyi.  Nimefarijika sana kwa mahudhurio yenu makubwa pamoja na taarifa kuwa ya muda mfupi.
Nimewaiteni wazee wangu nizungumze nanyi na kupitia kwenu nizungumze na wananchi wote wa Tanzania.  Mwisho wa mwezi uliopita sikuweza kufanya hivyo kupitia utaratibu wetu wa kawaida kwa sababu nilikuwa kwenye Mkutano wa Jumuiya ya Madola nchini Australia.  Mwisho wa Mwezi  huu nitakuwa Bujumbura kuhudhuria  Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, hivyo sitaweza kuongea na wananchi wakati huo. Lakini, yapo masuala kadhaa ambayo ni muhimu watu kupata ufafanuzi kutoka kwangu.  Kwa ajili hiyo nimeona nitumie fursa hii kuzungumza nanyi siku ya leo.   Leo nataka kuzungumzia hali ya uchumi na mchakato wa kupata Katiba Mpya.
Hali ya Uchumi
Ndugu Wananchi;
Katika kuelezea hali uchumi nchini, naomba nianze kwa kuelezea hali ya uchumi duniani kwani yanayotokea nchini yana uhusiano mkubwa na yanayotokea duniani.  Hali ya uchumi duniani siyo shwari.  Ukweli ni kwamba hali katika uchumi wa mataifa ya Marekani, Ulaya Magharibi na Japan haijatengemaa kufuatia machafuko ya masoko ya fedha na mdororo wa uchumi wa miaka miwili iliyopita.  Hivi sasa uchumi wa mataifa tajiri ya Ulaya , wanachama wa Umoja wa Ulaya na hasa wanachama wa Umoja wa Sarafu ya Euro unapita katika kipindi kigumu na mashaka.  Thamani ya sarafu hiyo inashuka na hata kuaminika kwake ni kwa mashaka. Mfumuko wa bei umepanda, ukosefu wa ajira umeongezeka na ipo hofu kubwa ya uchumi wa nchi hizo kudorora tena.  Lakini nchi hizi ndiyo masoko makubwa ya bidhaa zetu, watalii na bidhaa za viwandani.  Hivyo, athari zao zinatugusa na sisi.  Kuongezeka kwa mfumuko wa bei kunaongeza bei ya bidhaa tunazonunua kutoka kwao.  Aidha, kutetereka kwa uchumi wao nako kumepunguza masoko ya bidhaa zetu.
  Lakini kulegalega kwa sarafu ya Euro kumesaidia kuimarika kwa sarafu ya dola ambayo kabla ya hapo ilikuwa imepungua nguvu.  Kwa sababu hiyo thamani ya sarafu ya dola imepanda duniani ikilinganishwa karibu na sarafu nyingine zote pamoja na yetu.  Wakati huo huo bei ya mafuta imeendelea kupanda duniani kutoka dola 76.1 kwa pipa Septemba,, 2010 hadi dola 100.5 Septemba, 2011.  Jumla ya yote haya ni kuongezeka kwa mfumuko wa bei kutoka asilimia 4.2 Oktoba, 2010 hadi asilimia 17.9 Oktoba, 2011.
Ndugu Wananchi;
Serikali na vyombo husika vimekuwa vinachukua hatua mbalimbali kukabiliana na matatizo ya kushuka kwa thamani ya shilingi, bei ya mafuta, bei ya sukari na matatizo ya umeme.  Kuhusu kushuka kwa thamani ya shilingi Benki Kuu imeendelea kuchukua hatua zilizopo ndani ya mamlaka yake hususan kubana ulanguzi wa fedha za kigeni, kudhibiti matumizi ya fedha kigeni kufanyia malipo hapa nchini na kuongeza fedha za kigeni katika masoko ya fedha.  Kwa kweli uwezo wao una ukomo.  Jawabu la uhakika lipo kwenye uchumi wa mataifa makubwa kuchukua hatua thabiti kuimarisha uchumi wao ili thamani ya dola irejee mahali pake stahiki na bidhaa zetu zipate masoko ya uhakika na bei nzuri ili mapato yetu ya fedha za kigeni yaongezeke.
Kwa upande wa mfumuko wa bei, ni vyema tukatambua kuwa Asilimia 75 ya ongezeko hili imetokana na kupanda kwa bei ya chakula na mafuta.   Asilimia 25 iliyobaki imechangiwa na sera za fedha.  Kwa upande wa mafuta, tunaamini utaratibu wa kuagiza mafuta kwa pamoja utasaidia kudhibiti bei za ndani za bidhaa hiyo.  Aidha, itsaidia kupunguza makali ya athari ya bei za dunia zinazopanda.  Kwa upande wa bei za vyakula, tatizo kubwa ni uhaba wa chakula katika nchi jirani unaosababisha wote kututegema sisi na hivyo kupandisha bei nchini.  Tunaendelea kudhibiti magendo ya chakula na wakati huo kutengeneza taratibu rasmi za kuziuzia chakula nchi jirani.
Kwa upande wa sukari tumeamua kuruhusu tani 120,000 ziagizwe ili kupunguza uhaba wa bidhaa hiyo na kushusha bei yake.


Hatuko Peke Yetu

Ndugu Wananchi;
Ni vizuri tukafahamu kuwa, matatizo ya mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya fedha yetu siyo yetu peke yetu.  Nchi zote za Afrika Mashariki zinakabiliana na matatizo haya.  Kwa mfano, mfumuko  wa bei  kwetu ni asilimia 17.9, Kenya wako asilimia 18.9 na Uganda asilimia 30.5.  Wakati mwaka wa jana sote tulikuwa kwa watani karibu asilimia 5.  Kwa upande wa kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola sote tumeathirika.  Shilingi ya Tanzania imeshuka kwa asilimia 9.4, Kenya kwa asilimia 6.8 na Uganda kwa asilimia 17.4.  Randi ya Afrika Kusini kwa asilimia 18.7, Rupia ya India kwa asilimia 9.8, Pauni ya Uingereza kwa asilimia 6.6. na Euro kwa asilimia 9.7.
Ndugu Wananchi;
Katika kukabiliana na tatizo la umeme, Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa dharura wa kuongeza uzalishaji wa umeme.  Serikali imewawezesha TANESCO kukodi mitambo ya kuzalisha umeme kutoka kwenye makampuni ya Symbion (112 MW) na Aggreko (100 MW) na kununua mafuta ya kuendeshea mitambo ya IPTL (100 MW).  
Napenda niwahakikishie wananchi kuwa, ifikapo Desemba, 2011 hali ya upatikanaji wa umeme itakuwa nzuri na mgao utapungua sana baada ya kufunga mitambo mingine mipya ya kuzalisha umeme ya TANESCO (160 MW) na Symbion (60 MW).  Mikakati tuliyonayo ya muda mrefu ni kuongeza mitambo zaidi na kuongeza upatikanaji wa gesi ya kuendeshea mitambo kwa kujenga bomba kubwa la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam.
Mchakato wa Katiba
  Ndugu Wananchi;
Kama mtakavyokumbuka tarehe 31 Desemba 2010 katika hotuba yangu ya kuuaga mwaka 2010 na kuukaribisha mwaka 2011 nilizungumzia maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika ambayo sasa ni Tanzania Bara tarehe 9 Desemba, 2011.  Miongoni mwa mambo ambayo niliyataja kuwa tutayafanya katika kusherehekea siku hiyo adhimu ilikuwa ni kuanzisha mchakato wa kuitazama upya Katiba ya nchi yetu kwa nia ya kuihuisha ili hatimaye tuwe na Katiba mpya.
Nilifafanua siku ile kwamba tunataka kufanya hivyo si kwa sababu Katiba yetu ya sasa ni mbaya, la hasha!  Nilieleza kwamba Katiba yetu ya sasa ni nzuri na imelilea vyema taifa letu.  Tuna nchi yenye amani, utulivu na umoja pamoja na watu wake kuwa wa rangi, makabila, dini na itikadi mbalimbali za kisiasa.  Tunayo nchi ambayo imepiga hatua kubwa sana ya maendeleo ukilinganisha na ilivyokuwa miaka 50 iliyopita.  Pamoja na hayo tunataka kuihuisha Katiba yetu ili tuwe na Katiba inayoendana na Tanzania ya miaka 50 baada ya Uhuru wa Tanzania Bara, Tanzania ya miaka 47 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na Tanzania ya miaka 47 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Kwa ajili hiyo nilielezea dhamira  yangu ya kuunda Tume Maalum ya Katiba yaani Constitutional Review Commission itakayojumuisha Watanzania wa makundi mbalimbali katika jamii yetu na kutoka pande zetu mbili za Muungano.  Aidha, nilifafanua kuwa jukumu la msingi la Tume hiyo litakuwa ni kuongoza na kuratibu mchakato wa kupata maoni ya Watanzania kuhusu nini wanachokitaka kiwemo katika Katiba yao.
Tume itasikiliza maoni hayo na baadaye kutengeneza rasimu ya Katiba mpya ambayo baada ya kukubaliwa na Bunge itafikishwa kwa wananchi kutoa ridhaa yao kwa kupiga kura.  Nilisisitiza kuwa mchakato huo utawahusisha Watanzania wote wa ngazi zote na popote walipo mijini na vijijini.  Hapatakuwa na aina yoyote ya  kuwabagua watu kwa itikadi zao za siasa, shughuli wazifanyazo, dini zao, rangi zao au jinsia zao.
Ndugu Wananchi;
Nilifarijika sana na kauli za pongezi kwangu na kwa Serikali kwa uamuzi wa kuanzisha mchakato wa kupata Katiba mpya.  Miongoni mwa waliotoa pongezi alikuwa Ndugu Freeman Mbowe, Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa CHADEMA  ambaye wakati akichangia hotuba yangu ya kufungua Bunge Jipya, tarehe 11 Februari, 2011; nanukuu Hansad ya Bunge aliposema “Mheshimiwa Spika, ninapenda kwenye hili, nimpongeze Rais kwa kuwa msikivu, na Rais anapofanya jema tutampongeza, Serikali yake inapofanya jema tutaipongeza na Chama chochote kitakapofanya jambo jema kwa Taifa letu, tutakipongeza.  Napenda kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa sababu moja ya msingi sana, kuridhia mabadiliko au kuitafuta upya Katiba ya nchi yetu.”  mwisho wa kunukuu.    Lakini siku chache baadaye Chama chake kikaja na msimamo tofauti, wakawa wanalalamikia kunyang’anywa hoja yao na kukataa Rais asiunde Tume ya Katiba na wala asihusike kabisa na mchakato huu.  Tangu wakati huo wameendesha kampeni kubwa ya kutaka Rais asihusishwe kwenye mchakato wa kubadili Katiba
 Kwa kweli watu wengi wanaoitakia mema nchi yetu walishangazwa na madai hayo na vitendo vya ndugu zetu hao.  Hii si mara ya kwanza kwa nchi yetu kufanya zoezi la marekebisho ya Katiba au hata kuandika upya Katiba tangu Uhuru na Muungano.  Mara zote hizo iliundwa Tume ya kukusanya maoni ya wananchi ambayo iliundwa na Rais.  Ndivyo ilivyokuwa wakati wa Rais wa Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere,  Rais wa Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi na Rais wa tatu Mzee Benjamin Mkapa.  Mwalimu Julius Nyerere alifanya hivyo mara tatu.  Mara ya kwanza mwaka 1963 wakati wa kubadilisha mfumo wa vyama vingi kwenda Chama kimoja, Rais aliunda Tume ya Mheshimiwa Rashid Kawawa, Amon Nsekela.  Mara ya pili wakati wa kutengeneza  Katiba ya Kudumu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 aliunda Tume ya Mzee Sheikh Thabit Kombo.  
Mwaka 1984 Mabadiliko ya Katiba ya 1977 yaliyoweka ukomo wa Urais na kuingiza katika Katiba Haki za Binadamu, yaliyotokana na mchakato uliokuwa ni wa Kichama, ambapo CCM ilikusanya maoni kupitia mtandao wa kichama kuanzia Matawi hadi kufikia Makao Makuu.  Wakati wa Rais Ali Hassan Mwinyi wa Awamu ya Pili, kulikuwa na Tume ya Jaji Mkuu Francis Nyalali iliyotuletea mabadiliko  ya nane ya Katiba yaliyoruhusu vyama vingi vya siasa.  Wakati wa Rais wa Awamu ya Tatu, mzee Benjamin Mkapa kuliundwa Tume ya Jaji Kisanga iliyoleta mabadiliko ya 13 na 14 ya Katiba ya nchi.
Hivyo la ajabu lipi kwa Rais wa sasa kuunda Tume ya Katiba?  Amepungukiwa nini Kikatiba na Kisheria ambacho Marais wenzake walikuwa nacho katika madaraka yao?  Hakipo hata kimoja!  Madaraka waliyokuwa nayo Marais waliomtangulia ndiyo aliyonayo Rais wa sasa.  Hajapungukiwa chochote kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi.  Kwa kweli hakuna hoja yoyote ya msingi ya kumuengua Rais katika mchakato wa kutengeneza Katiba ya nchi.  Haipo hoja ya Kikatiba wala ya Kisheria.  Hivi Rais asipounda Tume, nani aiunde Tume hiyo?  Na huyo atakayeunda atapatikanaje?
Juzi Bungeni msemaji wa kambi ya upinzani, katika mjadala wa Muswada wa Kuunda Tume ya Kukusanya Maoni alisema Rais ni dikteta.  Ama kweli “akutukanae hakuchagulii tusi” kama ulivyo msemo wa Kiswahili.  Hivi mimi kweli ni dikteta?  Kwa jambo lipi?  Hivi ndugu zangu Rais dikteta anatoa uhuru mkubwa kama uliopo sasa wa vyombo vya habari na wa watu kutoa maoni yao?  Kama mimi ningekuwa dikteta kweli nina hakika hata yeye asingethubutu kusema hivyo na kama angethubutu basi mpaka sasa asingekuwa anatembea kwa uhuru.  Mimi ninachofahamu ni kuwa nasemwa kwa kuwapa watu, vyama vya siasa na vyombo vya habari uhuru mkubwa mno ambao watu wanaona unatumika vibaya kusema maneno yasiyokuwa na staha au hata matusi, fitina na kupandikiza chuki katika jamii.  Labda, nijaribu kuwa dikteta kidogo watu waone tofauti yake.  Naamini kungekuwa na malalamiko makubwa zaidi ya haya.
Ndugu Wananchi;
Mimi na wenzangu Serikalini tumefanya yote ambayo Katiba ya nchi na Sheria vinaruhusu.  Ndivyo Marais walionitangulia na Serikali zao walivyofanya tena sisi tumefanya zaidi ya wao.  Wote waliunda Tume za kukusanya maoni ya Katiba na wakati wa Mwalimu Julius Nyerere liliundwa Bunge Maalum la Katiba lililojumuisha Wabunge na wananchi wengine kama tulivyoamua kufanya sisi.  Ilifanyika hivyo wakati wa kutengeneza Katiba ya Tanganyika kuwa Jamhuri na Katiba ya Kudumu ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977.  Sisi tulichofanya cha ziada ni kulihusisha Bunge kutunga Sheria ya Kuunda Tume ya kusimamia mchakato wa Katiba mpya na vile vile kuwapa wananchi wote ridhaa ya kuamua kwa kuipigia kura Katiba inayopendekezwa.  Ni kutokana na nyongeza hii ndipo tukaona busara ya kuwepo kwa Sheria maalum ya kuongoza mchakato wa kupata Katiba mpya.  Tumepanua demokrasia na kuwahusisha wananchi wenyewe siyo tu katika kutoa maoni bali pia kutoa uamuzi wa mwisho kuhusu Katiba ya nchi yao, badala ya kuwaachia Wabunge na viongozi wengine Serikalini peke yao.  Kwa kweli tunastahili pongezi badala ya shutuma na lawama zisizokuwa na msingi.
Pia inasikitisha kuona au kuwasikia watu wanaojua wakijifanya ukweli huu hawaoni au  hawajui.  Baya zaidi ni pale wanapojihusisha na kupotosha ukweli na kuipaka sura isiyokuwa ya kweli kuhusu kinachofanywa na Serikali.  Mimi hujiuliza kwa nini wanafanya hivi.  Kwa nini wanafanya hiyana ya upotoshaji wote huu?  Kwa kweli sipati majibu ya uhakika.  Labda ndiyo ile dhamira ya kutaka nchi isitawalike.  Au ndiyo pengine ni ile nia ya kutaka kwenda Ikulu kwa njia ya mkato.  Ati kwa kutumia nguvu ya umma.  Basi hata hiyo nguvu unaitumia bila ya kuwa na hoja za kweli?
Ndugu Wananchi;
Nayasema haya kwa sababu kumekuwepo na upotoshaji mkubwa wa jambo hili tangu baada ya hotuba yangu ya tarehe 31 Desemba, 2010 mpaka wakati wa kuwasilishwa kwa Muswada wa Sheria wa Kuunda Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliomalizika leo Bungeni.  Upotoshaji wa kwanza ulikuwa ni ule wa kujenga dhana kana kwamba Serikali imewasilisha Muswada wenyewe wa Katiba mpya.  Wapo watu wamefanywa waamini hivyo wakati si kweli hata kidogo.  Huu ni Muswada ambao ukipitishwa, itaundwa Tume ya kukusanya maoni ya wananchi kuhusu nini wanachokitaka kijumuishwe katika Katiba yao mpya.  Kwa maneno mengine, maoni yenu mtakayoyatoa wananchi kwa Tume ndiyo yatakayotumika kutengeneza Katiba mpya.

Ndugu Wananchi;
Katika Muswada huu kuna mambo tuliyotaja kuwa ni ya msingi ambayo yamewekewa wigo wa kuhakikisha yanalindwa.  Mambo hayo ni yale ambayo yanalitambulisha taifa letu na tunu zake kuu.  Mambo yenyewe ni haya yafuatayo:  Kuwepo kwa nchi yetu na mipaka yake; kuwepo kwa Serikali, Bunge na Mahakama; kuwepo kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; kuwepo kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar; umoja wetu, mshikamano wetu na usalama wetu; Mfumo wa uchaguzi kwa kura unaotoa fursa kwa wote; Hifadhi ya haki za Binadamu; Haki za watu; Usawa mbele ya sheria na haki; Uhuru wa kuabudu na kuvumiliana kwa imani zetu.
Kumekuwepo na upotoshaji ati huko ni kuwaziba watu midomo.  Siyo hivyo hata kidogo.  Mambo hayo yanajadiliwa, lakini siyo kwa nia ya kuyaondoa bali kuboresha.  Kwa mfano, kuhusu Muungano,  tunachosema ni kwamba hatujadili kuwepo au kutokuwepo kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bali namna bora ya kuendesha shughuli za Muungano wetu.  Lakini, tulichokifanya siyo kitu kigeni, hata Rais wa kwanza alifanya hivyo mwaka 1963 alipounda Tume ya Mfumo wa Chama Kimoja cha Siasa iliyoongozwa na Mheshimiwa Rashid Kawawa.  Alitoa mwongozo na aliyataja mambo ya kulinda.  Sisi tulichokifanya ni kuyataja kwenye sheria badala ya kuwa Mwongozo wa Rais.
Ndugu Zangu, Watanzania Wenzangu;
Kwani Katiba ya Nchi ni kitu gani.  Katiba hutaja nchi na mipaka yake.  Kwetu sisi nchi yenyewe ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotokana na kuungana kwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika.  Pili, Katiba inaelezea jinsi nchi hiyo itakavyoendeshwa kwa maana ya mihimili mikuu mitatu ya dola ya Utawala/Serikali, Bunge na Mahakama.  Katiba inafafanua jinsi Serikali inavyopatikana, muundo wake na inavyofanya kazi.
Aidha, inaeleza jinsi Bunge linavyopatikana, jinsi linavyofanya kazi ya kutunga sheria na mahusiano yake na mihimili mingine.  Vile vile, Katiba inaeleza jinsi Mahakama inavyofanya kazi ya kutoa haki, muundo wake na jinsi Majaji na Mahakimu wanavyofanya kazi.  Kwa kweli mchakato wote huu unahusu hayo.  Tunatakiwa kutoa maoni juu ya namna gani bora zaidi na ikiwezekana namna mpya ya kuendesha shughuli za Muungano wetu na jinsi mihimili yetu inavyopatikana na kufanya shughuli zake.
Ndugu Wananchi;
Jambo lingine lililopotoshwa ni dhana ya muswada kusomwa mara ya kwanza.  Kwa mujibu wa utaratibu wa kutunga sheria, Miswada, husomwa mara tatu Bungeni.  Muswada kusomwa mara ya kwanza ni pale unapogawiwa kwa Wabunge baada ya kuchapishwa katika gazeti la Serikali siku 21 kabla ya kuwasilishwa Bungeni.  Baada ya kuchapishwa, hugawiwa kwa Wabunge.  Muswada husomwa mara ya kwanza Bungeni ili kutoa fursa kwa Mheshimiwa Spika kuwasilisha Muswada huo kwenye Kamati iuchunguze na kuutolea maoni.  Mheshimiwa Spika anaweza pia kuielekeza Kamati kutafuta maoni ya wananchi.
Baada ya Kamati kukamilisha kazi yake, Muswada husomwa mara ya pilli ambapo Muwasilishaji atatoa hoja kwamba Bunge liujadili Muswada pamoja na kutoa maelezo ya Muswada.  Mjadala huanza kwa Kamati ya   Bunge kutoa maoni yake ikifuatiwa na maoni ya Kambi ya Upinzani.  Wakati Kamati ya Bunge inapojadili Muswada, Waziri mhusika huwepo na mara nyingi maoni ya Kamati ya Wabunge na wadau hujumuishwa wakati Waziri anapowasilisha hoja Bungeni ya Muswada unaposomwa mara ya pili.  Baada ya mjadala, Bunge hukaa kama Kamati ya Bunge zima ambapo hupitia Muswada kifungu kwa kifungu.
Katika hatua hii Wabunge huweza kupendekeza mabadiliko mahsusi kwenye kila kifungu.  Aidha, Waziri nae anaweza kutetea marekebisho ya Muswada.  Baadaye Bunge hurejea, taarifa ya Kamati ya Bunge zima hutolewa kwamba Muswada umepitiwa kifungu kwa kifungu na kukubaliwa.  Kisha Muswada husomwa mara ya tatu kuashiria kwamba Muswada umepitishwa.  Mara nyingi Muswada hutokana na majadiliano katika hatua hizi zote, mabadiliko hufanywa na wakati mwingine mabadiliko  huwa makubwa kiasi kwamba kufanya  Muswada uliochapishwa na kusomwa mara ya kwanza na ule uliokubaliwa mwishoni uwe tofauti kabisa.
Ndugu Wananchi;
Muswada huu ulisomwa mara ya kwanza mwezi Aprili na kupelekwa kwenye Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala mwezi Aprili, 2011.  Tangu wakati huo Kamati imekuwa ikiufanyia uchunguzi Muswada huo na kukusanya maoni ya wadau.  Walisikiliza wadau Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar pamoja na kufuatilia maoni ya makongamano, magazetini na kwenye mitandao.  Kisha Kamati ikayajadili na kutoa mapendekezo yake ambayo Serikali iliyasikiliza na kuyajumuisha wakati uliposomwa mara ya pili.  Muswada huu haukuwahi kuondolewa Bungeni.  Kwa sababu hiyo, hakuna sababu ya kurudia kusomwa mara ya kwanza kwa mujibu wa taratibu za kuendesha Bunge.  
Tukumbuke kwamba baadhi yao waliahidi kwamba wangetoa Katiba Mpya katika siku mia moja tu.  Serikali imechukua miezi kumi na mmoja na wanalaumu kwamba eti inawahisha mchakato!!  Hiyo Katiba ya siku mia moja sijui wangeipataje bila kuwashirikisha wananchi?
Ndugu Wananchi;
  Ni kutokana na hoja hizo Spika akaamua Muswada uendelee kujadiliwa na Bunge na leo Bunge limeupitisha Muswada huo.  Baadae Muswada utaletwa kwangu kwa ajili ya kutiwa saini uwe Sheria.  Baada ya hapo itabakia kazi yangu na Rais wa Zanzibar kuunda hiyo Tume ili mapema mwakani kazi ya kukusanya maoni ya wananchi ianze.  Lengo letu ni kuwa ifikapo mwaka 2014 zoezi zima liwe limekamilika ili mwaka 2015 tufanye uchaguzi tukiwa na Katiba mpya.  Itapendeza tukisherehekea miaka 50 ya Muungano na Katiba mpya.  Ni matumaini yangu kwamba wananchi wote watashiriki kwa ukamilifu kutoa maoni yao kwa Tume hiyo.

Ndugu Wananchi;
Nimechukua muda wenu mwingi kuyafafanua masuala haya kwa umuhimu wake.  Nia ni kutaka watu waelewe maoni ya upande wa Serikali.  Matatizo ya kiuchumi yanayotukabili tunaendelea kuyashughulikia.  Yale yaliyo kwenye uwezo wetu tutayamaliza na yale yaliyo nje ya uwezo wetu tutaendelea kuchukua hatua za kupunguza makali.  Aidha, tutaendelea kutoa wito kwa mataifa husika kuchukua hatua thabiti kutatua matatizo yao kwani tunaoumia ni wengi.
Ndugu Wananchi;
Kwa upande wa mchakato wa kupata Katiba mpya nawasihi Watanzania tujiandae kwa maoni ya kutoa kwenye Tume ya Katiba mara itakapoanza kazi.  Kwa wale ambao hawatapata walichokitaka nawaomba warudi kundini, sote tuungane kwa hatua inayofuata.  Najua wanayo maoni mengi mazuri wayatayarishe na kuyawasilisha kwa Tume itakayoundwa.  Njia ya maandamano na vurugu si ya busara kufuata.  Haijengi bali inabomoa, haina faida bali hasara nyingi, haina faraja bali machungu kwa pande zote.  Busara ituongoze sote kuchagua njia inayojenga, yenye faida, furaha na faraja kwa wote.  Tutofautiane bila kupigana.  Serikali itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa nchi ya amani na utulivu.  
Mwisho
Ndugu Wananchi,
Naomba nimalizie kwa kuwashukuru wananchi kwa kuwa na subira kwa kipindi chote hiki toka tutangaze nia yetu ya kuanza mchakato wa kupata Katiba mpya.  Kwa mara nyingine tena nawaomba mjiandae kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kupata Katiba mpya mara utakapoanza ili tuendelee kuijenga na kuiendeleza nchi yetu na vile vile tuendelee kuithamini na kuitunza amani ya nchi yetu.

Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki Tanzania!
Asanteni sana kwa kunisikiliza!

Monday, October 10, 2011

RAISI MSAAFU WA CAPE VERDE ATWAA MABILIONI YA MO IBRAHIMU KWA UONGOZI ULIOTUKUKA

The former president of Cape Verde, Pedro Pires, has been awarded an African leadership prize of U.S. $5 million for transforming his country "into a model of democracy, stability and increased prosperity."

Pires is the recipient of the 2011 Ibrahim Prize for Achievement in African Leadership, established by the Sudanese business pioneer, Mo Ibrahim. The award is paid over 10 years, and is accompanied by an additional annual payment of U.S. $200,000 for life.



Salim Ahmed Salim, former secretary-general of the Organization of African Unity and chairman of the prize committee, said Cape Verde had won international recognition for its record on human rights and good governance. It was also the second African country to improve its position and rise above the United Nations category of the world's least developed countries.

Gabonews

Cape Verde President Pedro Pires, left, with Gabon President Ali Bongo. (file photo)

Salim said Pires enhanced his credentials when he stepped down at the end of his second term. "Dismissing outright suggestions that the constitution could be altered to allow him to stand again, he said: 'This is a simple matter of faithfulness to the documents that guide a state of law.' Throughout his long career President Pires has been dedicated to the service of his people, including those in the diaspora, while retaining his humility and personal integrity."

The prize is open to democratically-elected former heads of government who have observed term limits and left office within the last three years.

The prize has been awarded only twice: to Joaquim Chissano of Mozambique in 2007 and Festus Mogae of Botswana in 2008. In 2009 and 2010 the prize committee said it could not find a worthy recipient among Africa's recently-retired leaders.

Saturday, September 10, 2011

FAINALI ZA MASHINDANO YA MISS TANZANIA NI LEO JUMAPILI TAREHE 11, 2011


KITENDAWILI cha nani ataibuka kuwa Vodacom Miss Tanzania 2011 kitateguliwa leo usiku ambapo warembo 30 kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania wakichuana kuwania taji hilo.

Ni ukweli usiofichika kuwa mashindano ya mwaka huu ambayo ni ya 18 tokea kuanzishwa kwake mwaka 1994 ni ya kihistoria kutokana na sababu mbali mbali. Mbili kubwa ni mashindano ambayo yatakuwa moja ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru na pili ni mshindi wa mwaka huu atazawadiwa zawadi nono tokea kunzishwa kwa mashindano hayo.

Mwaka huu mrembo atapewa zawadi ya Jeep Patriot model ya mwaka huu yenye thamani ya shs. Milioni 72 huku akipewa fedha taslimu sh. Milioni 8. Hii ni zawadi ya kihistoria kwani imevunja rekodi ya mwaka 2003 ya Sylvia Bahame ambaye alizawadiwa gari aina ya Nissan Hardbody yenye thamani ya shs milioni 55 na fedha taslimu shs. 7 million.

Ikumbukwe mwaka jana ambapo mrembo anayemaliza muda wake, Geneieve Mpangala alipewa gari maarufu kwa jina la Mkoko na fedha taslim shs milioni 10 na kufanya jumla ya zawadi zote kufikia milioni 20.

Hii ni hatua kubwa kwani tofauti ya shs milioni 60 si haba na zawadi ya kwanza imewafanya warembo wengi kupagawa kwani hawakuamini macho yao kile walichokuwa wanakiona.

Zawadi nyingine za washindi ni sh. Milioni 6.2 kwa mshindi wa pili, sh. 4 millioni kwa mshindi wa tatu na sh. Milioni 3 kwa mshindi wane. Mshindi wa tano atapewa sh. Milioni 2.4.

Warembo watakaoshika nafasi ya sita mpaka 15 watapewa sh. Milioni 1.2 na waliobaki (16-30) watapewa kifuta jasho cha sh. 700,000.

ìTunatarajia kuwa mashindano magumu sana, hii inatokana na zawadi ya mshindi wa kwanza ambayo warembo wengi wameelekeza nguvu zao huko kwa sababu ya ukubwa wake na vile vile kiu ya kuiwakilisha nchi katika mashindano ya Dunia (Miss world) mjini London,î alisema meneja masoko wa kampuni ya kuuza magari ya CFAO zamani DT Dobie, Alfred Minja.

Minja alisema kuwa wametambua na kuamua kurudisha hadhi ya mashindano hayo ili kuleta mvuto wake wa awali kwani mwaka 2005, Nancy Sumari alizawadiwa nyumba iliyojengwa kule Tabata.

Tofauti na miaka ya nyuma, mashindano ya mwaka huu ni yana ugumu wa aina yake kutokana na ukweli kuwa imekuwa vigumu kujua nani ataibuka mshindi tofauti na mwaka jana, juzi na miaka ya nyuma.

Genevieve Mpangala ambaye atalivua taji lake alionekana wazi wazi kuwa hana mpinzani na hata wakati wa Miriam Gerald na Nasreem Karim. Ukali wa warembo hao ulikuwa wa aina yake na kupewa nafasi hata kabla ya kupanda jukwaani.

Ni vigumu kutabiri nani mshindi, nimefuatilia maonyesho mbali mbali ya televisheni wakiwa kwenye nyumba na mengine, ushindani ni mkubwa sana, lakini mshindi ni mmoja tu,alisema Rodrick Mwambene ambaye kupitia duka la Mama Tike aliwahi kudhamini mashindano mbali mbali ya vituo.


WALIOINGIA TOP 15:
Mwajabu Juma (Temeke, Miss Top Model), Rose Hurbert (Kaskazini, Vipaji), Alexia Williams (Ilala, Miss Personality), Tracy Mabula (Kanda ya Ziwa, Miss Photogenic), Loveness Flavian (Kanda ya Mashariki, Mrembo bora wa michezo).


WANAOWANIA TOP 15:
Weirungu David, Neema Mtitu (Chuo Kikuu Huria), Cynthia Kinasha (Temeke), Zerulia Manoko, Christina Mwenegoha (Kanda ya Kati), Jeniffer Kakolaki, Salha Israel (Ilala), Dalila Ghribu, Maua Kimambo (Kanda ya Kati), Blessing Ngowi, Glory Lory (Elimu ya Juu), Stacey Alfred, Zubeda Seif (Kanda Kaskazini), Stella Mbuge, Husna Maulid, Hamisa Hussein (Kinondoni), Princess Chiaro Masonobo (Udsm), Atu Daniel, Leila Juma, Christine William (Nyanda za Juu Kusini) , Mariaclara Mathayo, Asha Saleh (Mashariki), Irene Karugaba, Glory Samwel (Kanda ya Ziwa).


Warembo wanaoiwakilisha Dar es Salaam:

Weirungu David, Neema Mtitu (Open University), Mwajabu, Cynthia Kinasha, Husna Twalib (Temeke), Alexia Williams, Jeniffer Kakolaki, Salha Israel (Ilala), Blessing Ngowi (Institute of Social work), Glory Lory (IFM), Stella Mbuge, Husna Maulid, Hamisa Hussein (Kinondoni), Princess Chiaro Masonobo (Udsm).


KIINGILIO: SHS. 100,000

BURUDANI
Diamond, kidumu, Juliana, Akili the Brains, Bob Junior maarufu kama Rais w Sharobaro,

MAJAJI WA MWAKA HUU:
Prashant Patel, Crescentius Magori, Victoria Lukindo, Cynthia Masaki, John Njoroge, Benard Mlunya , Javier Diz Rio, Martin Ngadada, Pratma Shah.

WAREMBO WA MIAKA YA NYUMA:
1994 -Aina Maeda,
1995- Emily Adolf
1996- Shose Sinare
1997 - Saida Kessy
1998- Basila Mwanakuzi
1999- Hoyce Temu
2000 - Jacqueline Ntuyabaliwe
2001- Happiness Magese
2002- Angela Damas
2003- Sylvia Bahame
2004- Faraja Kotta
2005 - Nancy Sumari alishinda taji la Miss World Africa
2006- Wema Sepetu
2007- Richa Adhia
2008- Nasreen Karim
2009- Miriam Gerald
2010 - Genevieve Emmanuel

TALAKA SI SURUHISHO LA MATATIZO YA UHUSIANO, SURUHISHO NI KUONGEA NA MWENZA WAKO

Watu bwana, wakikwaruzana ‘Nenda kwenu mbwa wee’…wengine ‘Nipe talaka hunifai!”
“MBWA wewe, najuta sijui kwanini nilikuoa, yaani kati ya wanawake, wewe si lolote, pumbavu kabisa….” Ni kati ya kauli ambazo wanawake wamekuwa wakikumbana nazo kwenye ndoa.

Kama wewe mwanamke uko kwenye ndoa ambayo haina majuto na kero, ni suala la kumshukuru Mungu. Ukweli ni kwamba kuna wanawake wengi wanateswa na wanaume.

Usione wanaume mitaani, usifikiri mwanaume ambaye unakwenda naye gesti na kuachana, ndivyo anavyokuwa kwenye ndoa, wengi ni kero. Si wengi ambao wanawaheshimu wake zao.

Baadhi ya wanaume ni wasomi, ni watu maarufu, lakini kwenye nyumba zao ni takataka. Hawana heshima kwa familia, ndio unaweza kuona kwa mfano baba mtu mzima, anakataa kutoa huduma kwa watoto, eti kisa kagombana na mkewe. Akili iko wapi ndugu yangu kama sio upumbavu?

Kuna wanaume, eti mkewe haruhisiwi kupanda kwenye gari, anapandisha machangudoa…huu ni upumbavu. Dalili kwamba huna akili ni kuendekeza vitu ambavyo haina maana katika maisha. Kuna wanaume wengi hawana akili. Wanachojua wao ni kutembea kwenye nyumba nzuri za starehe na makahaba.

“Mke wangu amekuwa kero, dawa yake naona ni ndogo tu kumchukua nyumba ndogo” ndivyo wengi wanavyojidanganya. Wanafikiri kwamba nyumba ndogo ni mali, lakini nyumba ndogo hawa ni wafanyabiashara, wanachokifanya ni kwamba anakusikiliza eeeh mke wangu hana maana, hanipi raha, eeeh ooh na ujinga mwingine mwingi unamwambia.
Yeye yuko kibiashara zaidi, kwamba anaangalia matatizo uliyonayo kisha anajitahidi kufanya kila linalowezekana kuhakikisha unapata raha, hasa kwa sababu anaamini yuko kibiashara kwa maana kuwa utampa fedha na mambo mengine kama haya.
Nyumba ndogo ni wezi, ni majambazi, na ni wafanyabiashara, baadhi yao huwa wanakuwa bize kujifunza namna ya kuwanasa wanaume. Kuna wengine wanasoma vitabu mbalimbali vya mahaba, ili kumnasa mwanaume asikumbuke kwao.
Kwa wanaume wasio na akili, wanafikiri wanayofanyiwa ni kwa upendo, kumbe hakuna lolote la maana. Bali kinachofanywa na nyumba ndogo ni kusaka njia za kuishi kupitia migongo ya hao wanaume.
Mwanaume mwenye akili timamu ataangalia namna ya kuondoa kasoro zilizoko kwenye nyumba yake. Ndugu zangu tunapokuwa na shamba kama kwa mfano umepanda mahindi na kumeota magugu, kinachofanyika sio kwamba huwa tunang’oa mahindi na kwenda kuyapanda kwenye shamba jingine, bali tunasaka dawa ya kuua magugu ili mahindi yaweze kuota vizuri.

Kuna wanawake pia wana kauli za ujeuri, eeeh kuna wengine kama ulimgusa jana, ukimwambia na leo tena nataka ‘tupigane’ anaanza kulalamika “aaah bwana eeeh nataka kupumzika, aaah jana umetaka na leo unataka kwani mimi ng’ombe, hata ng’ombe huwa wanapumzika’.

Kauli chafu hazitakiwi katika suala zima la ndoa. Kama kweli unaumwa au una jambo linakusumbua, ni suala la msingi kuzungumza taratibu. Acha kuwa mwenye kauli chafu kwa mkeo, acha kuwa na kauli chafu kwa mumeo.
Kuna watu wengeine, wakikwaruzana kidogo ‘Nenda kwenu mbwa wee’…wengine utawasikia wanasema ‘Nipe talaka hunifai!” Ndoa nzuri huwa inajengwa kwa maneno na fikra za kila mtu kuamini kuwa hata kama kunatokea migogoro, cha msingi ni kuangalia chanzo cha mgogoro na kuumaliza. Utaachana na wangapi?
Kuringa kwenye ndoa kwa sababu eti una mwanamke mwingine nje ya ndoa ni upumbavu…kuringa labda una mwanaume mwingine nje ya ndoa ni ujinga.Mtu mwenye akili sahihi na iliyo timamu, baada ya ndoa anachokiangalia ni namna ya kuboresha maisha yake.

Kuna wanaume wanawapiga sana wake zao, wanasema maneno mabaya. Lakini mwanaume kama kichwa cha familia, anapaswa kuwa na akili nzuri, anapaswa kuwa mfano wa kuigwa, kwa kuwa na kauli nzuri, sio ndio jamani?

Sasa kwabahati mbaya kuna watu ni vichwa, lakini matendo yao ni sawa na unyayo sijui maana hata nikisema ni sawa na kiuno bado hawafai. Je wewe mwanaume unaishije na mkeo au watoto kwenye familia yako? Eti kuna wanaume wanaamini nyumba ndogo ni kila kitu katika maisha…eti akigombana na mkewe ndio atakwenda kupata faraja!!!

Ndugu yangu mbona unakuwa huna akili kiasi hiki. Unapotoka nje, kwanza ni kwamba uniaibisha mwenyewe, yule ambaye uko naye kwa asilimia kubwa hata kama anakuchekea, kwanza anajua yuko kibiashara, lakini katika nafsi yake anaamini wewe ni mwanaume usiyefaa, kama uliyeweza kumdharau mkeo na watoto, utashindwa nini kumdharau yeye ambaye hauna naye mikataba yoyote?

Kama ni suala ni migogoro ndio inakumbikiza nyumbani, kwani unafikiri ni mtu gani ambaye unaweza kuishi naye bila kukwaruzana? Wewe umeishi kwenye tumbo la mama yako kwa miezi sijui tisa au chini ya hapo, na bado kuna wakati mnakwaruzana, iwe mtu tu mmekutana mitaani?

Migogoro ni jambo la kawaida katika uhusiano wa kimapenzi au ndoa. Cha msingi ni kufungua milango ya kujadiliana. Tatizo kubwa kuna watu wana kiburi kichafu kabisa, kwamba hawezi kusema nimekosa nisamehe….hata kama kweli amekosa. Ndoa haiwezi kwenda kokote kama watu wake hawako tayari kusameheana au kuomba msamaha

MELI YAZAMA ZANZIBAR, WATU ZAIDI YA 190 WAFA


WATU 160 wamefariki dunia na wengine 521 kujeruhiwa baada ya meli ya abiria LCT Spice Islanders, iliyokuwa ikisafiri kutoka Unguja kwenda Pemba, kupinduka na kuzama baharini.

Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa meli hiyo iliyokuwa imebeba abiria zaidi ya 600, ilizama usiku wa kuamkia jana kwenye Bahari ya Hindi kati ya Nungwi na Pemba, kilomita 20 kutoka Bandari ya Zanzibar.

Kwa mujibu wa habari hizo, meli hiyo iliyotokea Unguja kwenye Bandari ya Malindi, ilipata hitilafu ikiwa njiani, kisha ikapinduka na kuanza kuzama taratibu. Ilikuwa na makoti ya uokoaji 200 tu.

Mwandishi Mkongwe nchini, Salim Salim, aliambia gazeti hili kwamba juhudi za kuoka zilianza kufanyika mapema kwa ushirikiana wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), KMKM, Jeshi la Polisi na wananchi kutoka eneo la Nungwi.

Salim alisema saa tata baada ya ajali hiyo kutokea jeshi la polisi lilifika katika eneo la polisi pamoja na wananchi walitoka sehemu mbalimbali. Polisi walitumia helikopta mbili na wananchi asilimia kubwa akiwa wavuvi walitumia mashua.

Pia boti za uokoaji za Azam na Express Zakhir zilifika katika eneo la tukio mapema na kuifanya kazi kubwa ya uokoaji.


Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP, Said Mwema alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo jana na kwamba chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana.

Alisema mpaka kufikia jana mchana watu waliokolewa katika ajali hiyo wakiwa hai walikuwa 525 na waliofariki 62.

Mwema alisema imeunda kamati maalum ya kufuatilia tukio hilo ambayo pia itahusisha Usalama wa Taifa.

“Hivi sasa Jeshi la Polisi, JWTZ, Usalama wa Taifa, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na KMKM ndio wanashughulikia suala zima la upelelezi ili kujua chanzo cha ajali hiyo,” alisema Mwema

Aliongeza: “ Eneo la Usimamizi wa mawasiliano na uratibu itakuwa chini ya Kamishna wa Polisi Zanzibar, pia kuna kikosi kazi cha uokoaji na kikosi cha kukusanya taarifa na upelelezi wa tukio hilo,”.

Alipoulizwa idadi kamili ya watu waliofariki katika ajali hiyo pamoja na uwezo wa meli hiyo kubeba abiria na mizigo Mwema alisema: “Hivi sasa ndio tunaendelea na uchunguzi ili kubaini idadi kamili ya waliofariki, ila kwa sasa kinachofanyika ni uokoaji”.

Rais Shein

Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein, alifika kwenye eneo la tukio na kushiriki kikamilifu kutoa huduma ya kwanza kwa walinusurika katika ajali hiyo.

Akizungumza katika kijiji cha Nungwe, Dk Shein aliwataka Wazanzibari kuwa wavumilivu katika kipindi hiki wakitiana moyo kwa yote yaliyotokea.

"Huu ni mtihani wa Mwenyezi Mungu. Wazanzibari tuwe wavumilivu, Serikali itakayogharimia shughuli zote za mazishi," alisema Dk Shein.

Dk Shein alisema maiti waliotambuliwa watachukuliwa na ndugu zao kwa ajili ya mazishi ila wale ambao ndugu hawataonekana watazikwa na Serikali kwa utaratibu maalumu.



Shuhuda
Mwandishi Mkongwe wa habari Zanzibar, Salim Salim, amelieleza gazeti hili kuwa meli hiyo ilizama katikati ya Kisiwa cha Pemba na Unguja eneo ambalo ndilo lenye mkondo mkuu bahari kuliko mikondo yote ya bahari barani Afrika.

Mikondo mingine mikuu ya bahari inayoufuatia mkondo wa Bahari wa Nungwi ni Pemba Channel ulioko nchini Msumbiji na Affond ulioko Somalia

Alisema ajali hiyo ilisababisha maduka yote kisiwani Pemba kufungwa kutokana na wakazi wengi wa pemba kwenda kutambua miili ya marehemu, iliyofanyika katika Viwanja vya Maisara vilivyoko kiwani humo.

"Wananchi walianza kutambua miili ya marehemu saa 8:30 mchana wakiwamo viongozi wote wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar walioongozwa na Rais Shein na Makamu wake wa Kwanza, Maalim Seif Sharif Hamad.

"Maduka yote yamefungwa na misikitini kunafanyika sala maalumu. Pia vituo vyote vya radio na televisheni visiwani hapa, vimeacha kupiga muziki na pia kutakuwa na maombolezo maalumu ya ajali," alisema Salim.

Salim alisema katika viwanja hivyo vya Maisara walikusanyika madaktari kutoka maeneo mbalimbali ya Zanzibar ambao kwa pamoja wanatoa huduma ya kwanza katika mahema maalum kwa majeruhi.

"Sanda zinashonwa hapohapo uwanjani na Serikali imesema itagharimia shughuli zote za mazishi," alisema Salim.

Salim alisema maiti zote zilizokuwa zikitolewa, zilikuwa zimepewa namba na mpaka anaondoka uwanjani hapo jana mchana, maiti 160 zilikuwa zimeopolewa.

"Kazi ya uokoaji inaendelea ila mpaka mimi naondoka eneo la tukio, kulikuwa na maiti 160. Niseme tu kwamba, Serikali safari hii imeonyesha kuwajali wananchi wake, kwa kuharakisha kuanza uokoaji," alisema.


Dk Shein ashiriki kutoa
huduma ya kwanza

Katika hatua nyingine, jana Rais Shein alikuwa miongoni mwa madaktari waliokuwa wakitoa huduma ya kwanza kwa majeruhi wa ajali hiyo ya meli.

Dk Shein ambaye siku nzima alikuwa katika eneo la tukio, akishirikiana na madaktari kuwapokea wagonjwa katika mahema maalumu na kuwapa huduma ya kwanza.

Watu wengi walionusurika katika hali hiyo walionekana kupata mshituko mkubwa, ingawa hawakuwa na majeraha makubwa.
Kazi hiyo ya uokoaji ilikuwa ikiongozwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na KMKM.
Wakati Dk Shein akiwa anashiriki kutoa huduma ya kwanza kwa majeruhi, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad alionekana muda wote akiwa sambamba na vikosi vya uokoaji akisimamia kwa karibu zoezi hilo.

"Maalim Seif alionekana akisimamia upatikanaji wa vifaa na vitu vingine muhimu vya uokoaji," kilisema chanzo cha habari kutoka Pemba

Kichanga aokoka kifo

Katika hali isiyokuwa ya kawaida mtoto mchanga anayekadiriwa kuwa na umri wa miezi minne hadi mitano, aliokolewa katika ajali hiyo.

Televisheni ya Channel Ten, ilieleza kuwa mtoto huyo alikutwa akielea juu ya maji licha ya kutovalishwa kifaa chochote maalumu vya kuogolea. Kwa mujibu wa Kituo hicho cha Televisheni, mtoto huyo anaendelea vizuri.

Sumatra wazungumza

Akizungumza na Mwananchi Jumapili Meneja Mawasiliano kwa Umma wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), David Mziray.
Alisema taarifa walizonazo zinaeleza kuwa meli hiyo iliondoka Unguja kwenda Pemba saa 4:20 usiku jana.

“Mpaka sasa meli ya Mv Jitihada imeelekea eneo la tukio kwa ajili ya kuokoa watu, meli ilikuwa na abiria 500 na wafanyakazi 12,” alisema Mziray.

Aliongeza: “Meli hii imesajiliwa Zanzibar na taarifa za kuzama kwake zilifika saa 9:10 usiku wa kuamkia leo(jana),”.

Kikosi cha wanamaji Dar
Awali gazeti hili lilifika katika ofisi za kikosi cha wanamaji jijini Dar es Salaam na kuelezwa kuwa meli hiyo iliondoka jana (juzi) jioni ikiwa na abiria 229.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili kwa njia ya simu akiwa njiani kuelekea ilipozamia meli hiyo Kamanda wa Kikosi hicho, Mboje Kanga, alisema meli hiyo ilizama ikiwa na zaidi ya watu 500.

“Mpaka sasa sijui kinachoendelea ndio niko njiani naelekea eneo la tukio, nipigie baadaye nitakuwa nimetapa kila kitu,” alisema Kanga.

Wafanyakazi Bandarini
Baadhi ya wafanyakazi wa bandarini pamoja na wabeba mizigo walilieleza gazeti hili kuwa huenda meli hiyo ilizama kutokana kubeba mizigo mingi.
Wafanyakazi hao ambao walikuwepo katika bandari hiyo wakati ikiondoka katika bandari ya Zanzibar wanasema kuwa jinsi ambavyo ilipakia abiria na mizigo huenda itakuwa ndiyo sababu ya kuzama kwake.
Mmoja wa wafanyakazi hao ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema wakati meli hiyo ikiondoka Unguja alikuwepo na kwamba ilikuwa imeelemewa upande mmoja.
“Meli iliruhusiwa kuondoka bandarini Unguja kwa nguvu kwa kuwa watu waliokuwa wakitaka kupanda licha ya kuwa kuambiwa imejaa na walikuwa wengi. Meli ilipakiwa idadi kubwa ya nondo, madirisha, magunia ya unga wa ngano na mahindi,” alisema.
Mfanyakazi mwingine aliyejitambulisha kwa jina moja la Shadrack alisema meli nyingi zinazotoka Unguja kwenda Pemba huwa zinajaza mizigo na watu wengi na kusisitiza kuwa, eneo la Nungwi ni baya hasa kama meli ina mzigo mkubwa kwa kuwa eneo hilo lina mkondo mkubwa wa maji.
“Nakwambia wazi meli hii ilikuwa na watu zaidi ya 600 maana wanasema waliookolewa tu ni 500…,” alisema Shadrack.

Hekaheka Bandarini Dar
Mwananchi Jumapili lilifika asubuhi bandarini jijini Dar es Salaam na kuta idadi kubwa ya watu wakitafuta usafiri wa meli kuelekea Zanzibar kwenda kutambua ndugu zao waliokuwa katika meli hiyo.
Ally Hamisi alilieleza gazeti hili kwamba, katika meli hiyo kulikuwa na ndugu zake saba ambao hajui kama wako hai ama wamekufa.
“Walikuwa wametoka katika harusi…, kwa kweli nimechanganyikiwa kabisa, pia alikuwemo jirani yangu ambaye nilikabidhiwa ili nimpeleke Zanzibar na mpaka sasa hajaonekana,” alisema Hamis.
Alisema meli hiyo ilipofika Unguja walipanda ndugu zake wengine watatu.
“Ni jambo la kusikitisha sana, usiku nilipigiwa simu na mmoja wa ndugu zangu akanieleza kuwa tumuombee kwa kuwa meli ilikuwa ikizama, baadaye simu yake haikupatikana tena na sijui kama yupo salama au la,”.
Naye Khamisi Abdallah alisema kwa masikitiko kuwa katika meli hiyo alikuwa na ndugu 10.
“Nimekata tiketi ili niende kushuhudia mwenyewe…, mpaka sasa siamini na sijui nani kapona nani kafariki, inaniuma sana,” alisema Abdallah kwa masikitiko.
Mwantumu Suleiman ambaye ni mkazi wa Zanzibar, alisema alikuja jijini Dar es Salaam na mume wake na mdogo ambao waliondoka na meli hiyo.
“Wao walikwenda ila mimi nilibaki hapa Dar es Salaam nilikuwa naumwa tumbo, niliposikia habari hizi nimechanganyikiwa kweli, bado sijapona, lakini acha niende nikashuhudiwa kilichotokea,” alisema Mwantumu kwa masikitiko.

Hii ni mara ya pili meli kuzama katika bahari ya Malindi katika kipindi cha miaka miwili iliyopita. Mei 29, 2009, meli ya mizigo inayomilikiwa na Kampuni ya Seagul, MV Fatih, ilipinduka na kuzama katika Bandari ya Malindi, Zanzibar na kuua watu watatu na kujeruhi wengine 27.

Meli hiyo ilipinduka na kuzama ghafla ikiwa tayari imeshafunga gati katika Bandari ya Malindi majira ya saa 4.00 usiku na abiria waliokuwemo walikuwa wanataka kushuka.

Akisimulia mkasa wa ajali hiyo kepteni aliyekuwa akiendesha meli hiyo, Ussi Ali Ussi, alisema wakati akiingia bandarini ghafla aliona meli hiyo ikijaa maji na kulala upande wa kushoto.

Habari hii imeandaliwa na Talib Hamad, Fidelis Butahe, Claud Mshana, Elias Msuya na Geofrey Nyang’oro, Igunga

Wednesday, August 17, 2011

JOSE CHAMELEONE ABADILI DINI

Msanii wa mziki kutokea pande za uganda ameamua rasimi kubadili dhehebu lake la dini, msanii huyo ambaye alikuwa muumini wa roman catholic ameingia rasimi dini la kiislamu

Friday, June 10, 2011

CHADEMA WAIKOSOA BAJETI YA TANZANIA 2011-2012

Thursday, 09 June 2011 23:
Neville Meena, Dodoma
KAMBI ya Upinzani Bungeni imedai kwamba kuna upotoshaji mkubwa katika Bajeti ya S 200erikali iliyowasilishwa bungeni juzi na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, huku ikidai kwamba bajeti hiyo ni ya kulipa posho na madeni.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Kambi hiyo mjini Dodoma na kusainiwa na Waziri Kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe inabainisha kuwa upembuzi uliofanywa umebaini kuwapo kwa upotoshaji mkubwa wa kitakwimu na kimaudhui uliofanywa kwalengo la kuwajengea matumaini wananchi.
"Kambi ya Upinzani Bungeni imeshtushwa na kushangazwa na hatua ya Serikali kutenga zaidi ya robo ya bajeti kulipa madeni na kulipana posho (asilimia 27), asilimia 14 kulipa madeni na asilimia 13 kulipa posho mbalimbali," ilisema taarifa hiyo.
Miongoni mwa maeneo ambayo yanadaiwa kuwa na upotoshaji ni kiasi cha fedha zilizotengwa kwa ajili ya kukabiliana na tatizo la umeme, ongezeko la jumla la Bajeti ya Serikali ikilinganishwa na ile ya mwaka 2010/11, posho mbalimbali, faini kwa madereva wazembe na ulipaji wa madeni ya Serikali.

Hakuna mradi mpya wa umeme
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, tamko la Serikali kwamba imetenga kiasi cha Sh537 bilioni kwa ajili ya kutatua tatizo la umeme, si kweli kwani kwa jumla Wizara ya Nishati na Madini, imetengewa Sh402.071 bilioni na kwamba hakuna mradi mpya wa umeme hata mmoja utakaoanzishwa.

"Fedha hizo zimegawanywa katika mafungu ya matumizi ya kawaida Sh76,953,934,000  na  kwa upande wa bajeti ya maendeleo zimetengwa Sh325,448,137,000. Sh325 bilioni zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo ya Wizara ya Nishati na Madini zinatosha kwa mradi mmoja tu wa umeme wa 160 MW, 100 Dar es Salaam na 60 Mwanza,"inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Zitto ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, alisema katika taarifa hiyo kuwa, kutokana na hali hiyo hakuna mradi mpya wa umeme unaoonekana katika bajeti hiyo na kwamba kauli ya Mkulo ililenga zaidi kuwajengea wananchi matumaini hewa na si hatua za kweli kumaliza matatizo ya umeme nchini.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hakuna ongezeko lolote halisia la fedha katika bajeti ya mwaka huu, kwani kati ya Sh13.525 trilioni zilizotengwa, Sh1.901 trilioni, sawa na asilimia 14.06 ya bajeti yote ni kwa ajili ya kulipa madeni ya Taifa.
"Kwa mantiki hiyo, mtaona kuwa fedha kwa ajili ya kuendesha Serikali pamoja na kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo zitabaki Sh11.624 trilioni ambazoni ni sawa na fedha za bajeti ya mwaka unaomalizika wa 2010/2011," alisema Zitto katika taarifa yake hiyo na kuongeza: "Kwa kuzingatia kwamba thamani ya shilingi imekuwa ikishuka, bajeti iliyotangazwa ni ya kulipa madeni".
Bajeti ya posho sasa Sh987 bilioni
Kuhusu hatua za kupunguza posho, kiongozi huyo alisema hakuna ukweli wa kauli hiyo kwani Serikali imetenga kiasi cha Sh987 bilioni kwa ajili ya kulipa posho mbalimbali, fedha ambazo ni sawa na asilimia 13 ya bajeti nzima.

 Taarifa hiyo ilibainisha kuwa kutokuwapo kwa nia ya dhati ya kupunguza posho, inaonekana katika hatua za kufanya marekebisho katika sheria ya kodi sura ya 332 ili kusamehe kodi ya mapato katika posho wanazolipwa wafanyakazi wa Serikali na wanaofanya kazi katika taasisi zinazopata ruzuku kutoka kwenye Bajeti ya Serikali.
"Hii inaonyesha kuwa kauli ya kufuta au kupunguza posho ilitolewa na Serikali ili kupumbaza wananchi, lakini haina udhati,"alisema.

 Taarifa hiyo ilieleza kuwa bajeti imeongeza mzigo mkubwa kwa wananchi kutokana na hatua yake ya kuongeza kiwango cha faini kwa madereva wazembe kutoka Sh20,000 hadi Sh300,000, na kwamba kiasi cha Sh50,000 kilichotangazwa na Waziri Mkulo juzi kinatofautia na maelezo kwenye vitabu vya bajeti.
Alisema hatua hiyo itawaathiri wananchi hasa vijana walioajiriwa ama kujiajiri katika huduma za usafiri na usafirishaji na kwamba kipengele hicho pia kinalenga kuuhadaa umma.
Serikali juzi ilitangaza hatua kadhaa za kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima katika mwaka wa fedha wa 2011/2012, lakini fedha za matumizi mengineyo, maarufu kama Other Charges (OC), zimeongezwa kwa asilimia 8.62 ikilinganishwa na Bajeti ya Serikali inayofikia ukomo tarehe 30 mwezi huu.
 Fedha za OC katika bajeti mwaka ujao wa fedha ni Sh3.089 trilioni ikilinganishwa na kiasi cha Sh2.823 kilichotengwa katika mwaka wa fedha wa 2010/2011, likiwa ni ongezeko la Sh266.599 bilioni.
Fungu la fedha za OC ndilo hutumika kugharimia posho mbalimbali kwa watumishi wa umma na uendeshaji wa semina, warsha na makongamano pamoja na kugharimia safari za viongozi ndani na nje ya nchi.
 Kafulila adai bajeti haijazingatia  vigezo vya uchumi
Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila aliliambia Mwananchi katika viwanja vya Bunge kuwa, hali hiyo inadhihirisha kwamba bajeti iliyowasilishwa na Mkulo ililenga zaidi kutafuta kuungwa mkono kuliko kuzingatia vigezo vya kiuchumi.

"Kama mwaka wa fedha unaoishia mwishoni mwa mwezi huu fedha za OC ni kidogo kuliko zile ambazo zimetengwa mwaka ujao wa fedha, basi ni dhahiri kwamba hatuwezi kusema posho zitapunguzwa, hapa nadhani kuna tatizo,"alisema Kafulila.
 Alisema fungu la fedha za OC lazima lipitiwe upya kwani fedha zilizotengwa ni zaidi ya kiasi cha fedha ambazo Serikali imeomba kutoka kwa nchi wahisani kwa ajili ya kutekeleza miradi  ya maendeleo.
"Iwapo fedha za OC ni Sh3 trilioni na fedha za miradi ya maendeleo tunazoomba kutoka kwa wafadhili ni kiasi hicho hicho, utaona kwamba ni jambo la kushangaza, hapa kuna mambo mengi ya kuweka sawa,"alisema Kafulila, huku akibainisha kuwa bajeti hiyo ya Serikali si mbaya sana kwani imekumbuka umuhimu wa miundombinu ya usafirishaji.
Akiwasilisha bungeni juzi Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/12, Waziri Mkulo alibainisha hatua kadhaa za Serikali kudhibiti matumizi yasiyokuwa ya lazima akiahidi kupunguza posho zisizo na tija, safari za ndani na nje za viongozi na ukubwa wa misafara ya viongozi hao ili fedha husika ziweze kutumika kugharimia shughuli nyingine za maendeleo.
"...........Serikali itasitisha ununuzi wa samani za ofisi, hususan zile zinazoagizwa kutoka nje ya nchi, kupunguza malipo ya posho mbalimbali yasiyokuwa na tija, kupunguza matumizi ya mafuta kwa magari ya Serikali, kupunguza safari za ndani na nje ya nchi, ikiwa ni pamoja na ukubwa wa misafara na kuendelea kupunguza semina na warsha, isipokuwa pale inapobidi na kwa kibali cha Ofisi ya Waziri Mkuu..," alisema Mkulo.
Sh3 trilioni kutoka nchi wahisani
Kadhalika majedwali ya ufupisho wa hesabu za bajeti ya Serikali kwa mwaka 2011/12 yanabainisha kuwa fedha za maendeleo zinazotarajiwa kutoka kwa nchi wahisani ni kiasi cha Sh3.054 trilioni. Kiasi hicho kinazidiwa kwa asilimia 18.9 sawa na Sh5.853 bilioni kikilinganishwa na fedha za OC ambazo ni Sh3.089 trilioni.

 Katika bajeti hiyo, fedha zote zilizotengwa na Serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo ni Sh4.925 trilioni, ambapo fedha za ndani ni Sh1.871 trilioni.
 Mchanganuo mzima wa bajeti hiyo unaonyesha kuwa fedha za miradi ya maendeleo zilizotengwa ni sawa na asilimia 31 ya bajeti nzima, wakati fedha za matumizi mengineyo (OC) ni sawa na asilimia 32, mishahara asilimia 23, malipo ya madeni asilimia 8, madeni mengine asilimia 3 na riba ya madeni ya ndani na nje asilimia 3.