Monday, June 6, 2011

Defend Libya Against Imperialist Attack

Defend Libya Against Imperialist Attack!
The International Communist League (Fourth Internationalist) calls on workers around the world to take a stand for military defense of semicolonial Libya against the attack begun yesterday by a coalition of rapacious imperialist governments. The French, British and U.S. rulers, in league with other imperialist governments and with the blessings of the sheiks, kings and military bonapartists of the Arab League, wasted not a moment in acting on the green light given by the United Nations Security Council on Thursday to slaughter countless innocent people in the name of “protecting civilians” and ensuring “democracy.” French air strikes were quickly followed by U.S. and British missile attacks, while Egypt’s military regime is providing arms to the Benghazi opposition forces. From Indochina and the Korean peninsula to the U.S.-led occupations of Iraq and Afghanistan today, the “democratic” imperialist rulers wade in the blood of millions upon millions of their victims. Recall that Britain and France historically carried out untold massacres in the Near East, Africa and the Indian subcontinent in order to pursue their colonial subjugation of those areas. Recall that Italy, now providing the use of its air bases for the attack, is responsible for the deaths of up to half the population of Cyrenaica in eastern Libya during its colonial rule prior to World War II.
Prior to the current attack, the conflict in Libya had taken the form of a low-intensity civil war, heavily overlaid by tribal and regional divisions, between the Tripoli-centered government of strongman Colonel Muammar el-Qaddafi and imperialist-backed opposition forces concentrated in the country’s eastern areas. Workers Vanguard No. 976 (18 March), newspaper of the U.S. section of the ICL, noted that “Marxists presently have no side in this conflict.” But as the article continued: “In the event of imperialist attack against neocolonial Libya, the proletariat internationally must stand for the military defense of that country while giving no political support to Qaddafi’s capitalist regime.” The civil war in Libya has now been subordinated to the fight of a neocolonial country against imperialism. Every step taken by the workers of the imperialist countries to halt the depredations and military adventures of their rulers is a step toward their own liberation from capitalist exploitation, impoverishment and oppression. Defend Libya against imperialist attack! U.S. Fifth Fleet and all imperialist military bases and troops out of North Africa and the Near East!
Recall that the slaughter of well over a million people in Iraq began with the imposition of a UN-sponsored starvation embargo and a “no fly zone” in the 1990s. The latest action by the Security Council, including the neo-apartheid South African regime led by the African National Congress, underscores yet again the character of the United Nations as a den of imperialist thieves and their lackeys and semicolonial victims. The abstention by the representative of China, a bureaucratically deformed workers state, gave tacit approval to imperialist depredation, emboldening the very forces which seek to overturn the 1949 Chinese Revolution.
The crocodile tears shed by the imperialist rulers and their media mouthpieces over the Libyans killed by the Qaddafi regime during the recent wave of protests stands in sharp contrast to their muted response to the continuing massacre of protesters in Yemen—whose dictatorship is a key component of Washington’s “war on terror”—and their ongoing support to the Bahraini kingdom, which hosts the headquarters of the U.S. Fifth Fleet. To aid in crushing mass protests, Bahrain last week invited in troops from the medievalist and theocratic Saudi monarchy, a key bulwark of U.S. imperialist interests in the region. In the eyes of the imperialist rulers, Bahrain’s Shi’ite majority and the Yemeni masses are less than human, with no rights they are bound to respect.
Numerous social-democratic leftists, typified by the United Secretariat (USec) and the British Cliffite Socialist Workers Party, have done their part to prepare the ground for imperialist massacres in Libya by cheering on the so-called “Libyan Revolution.” Having urged support for the cabal of pro-imperialist “democrats,” CIA stooges, monarchists and Islamists that comprise the Benghazi-based opposition, these reformists now feign to balk at imperialist military intervention in support of the opposition. The New Anti-Capitalist Party, constituted in 2009 by the USec’s French section, signed a call for a demonstration yesterday demanding that the Benghazi outfit be recognized as “the only legitimate representative of the Libyan people”—which French ruler Sarkozy had already done! At the same time, those left groups that have promoted illusions in Qaddafi’s “anti-imperialist” pretensions—such as the Workers World Party in the U.S.—seek everywhere and at all times to chain the working class to a mythical “progressive” wing of the bourgeoisie.
We pledge today, as we did at the time of the U.S. Reagan administration’s bombing of Libya in 1986, to “undertake every effort to propagandize the need for the world working class to take the side of Libya” against its imperialist enemies (“Under Reagan’s Guns in Libya,” WV No. 401, 11 April 1986). In the pursuit of profit and domination, the same capitalist ruling classes that brutally exploit the working class “at home,” only to throw workers on the scrap heap during periods of economic crisis, as today, carry out murderous imperialist attacks abroad. The struggle against imperialist war cannot be conducted separately and apart from the class struggle. Only socialist revolution can overthrow the system of capitalist imperialism which breeds war. Our path is that of the October Revolution of 1917, led by the Bolshevik Party of Lenin and Trotsky, which was a beacon of revolutionary internationalism for the proletariat everywhere. We struggle to reforge the Fourth International as an instrument that can lead the working masses, from the Near East to the imperialist centers, forward to new October Revolutions and a world socialist society.

MAPACHA WATATU MSIJE KUWA NDUMILA KUWILI KAMA WALIOWATUNGULIA KUZIKIMBIA BENDI ZAO

MAPACHA WATATU: Haturudi nyuma kamwe  Send to a friend
Saturday, 30 April 2011 20:37
0diggsdigg

Na Furaha Maugo
NI kundi linalofanya vizuri katika medani ya muziki wa dansi hapa nchini kwa sasa, linaundwa na vijana watatu ambao hawajazaliwa na baba wala mama mmoja, lakini bado wanajiita mapacha watatu.
Wakali hao ambao awali kabla ya kuunda kundi hilo, walikuwa katika bendi mbili tofauti za muziki wa dansi hapa nchini, hivi sasa wamekuwa gumzo katika anga la starehe na hasa muziki wa dansi.
Uwezo wao pia umedhihirika baada ya kujinyakulia tuzo ya wimbo bora wa Kiswahili wa mwaka katika tuzo za kili Music Awards 2010/11, ikiwa ni muda mfupi tu tangu kuanzishwa kwa kundi hilo na kuyabwaga makundi nguli wa muziki wa dansi kama Extra Bongo, Twanga Pepeta na Akudo Impact.
Awali kundi hili lilikuwa likiwatumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja; walikuwa wakiimba katika bendi zao na pia kulitumikia kundi lao ambapo Josee Mara alikuwa kundi la FM Academia, na Chokoraa na Kalala Jr walikuwa Twanga Pepeta.
Lakini ndoa hiyo iliwashinda na kuamua kuachana na bendi zao, ni hivi karibuni, Meneja wa wakali hao, Hamis Dakota amesema kuwa wanamuziki wake hawafikirii kurudi nyuma tena.
Dakota alisema kundi lake limejipanga vizuri kuhakikisha wanakabilia na soko la ushindani lililopo sasa na wanaamini watafanya vizuri kwa sababu imezungukwa na vichwa vikali katika tasnia ya muziki wa dansi.
“Kiukweli sasa hivi tunataka mabadiliko ikiwa ni pamoja na kuwa na  nyumba nzuri ya kuishi na maisha mazuri na haya yote yataletwa ikiwa tutafanya  kazi kwa juhudi na maarifa kila kukicha kwa ubunifu wa hali ya juu” anasema Dakota.
 “Mashabiki wakao mkao wa kula kwani tayari albamu ya pili yenye  jumla ya nyumba sita  imeshakamilika japokuwa hatujaipa jina rasmi ” anaongeza kusema Meneja Dakota.
Baadhi ya nyimbo zitakazokuwepo katika Albamu hiyo ni pamoja na Mjasiriamali iliyoimbwa na kutungwa na Chokoraa, Usia wa babu ya  Josee Mara, Mtoto wa Paka ya  Kalala junior, Sumu ya mapenzi remix ya Kalala Jr na Gari bovu ulioimbwa na kutungwa na mpiga vyombo Arosto Mashama .
Mapacha watatu walifikia uamuzi wa kuunda kundi lao mwaka 2010, vijana hao ambao wamekulia katika muziki na wamepitia bendi kubwa hapa nchini, haikuwapa shida kuwateka mashabiki wa muziki wa dansi kwani tayari walikuwa wakipendwa hata huko walipokuwa kabla ya kuunda kundi lao wenyewe.
Baada ya kuunda kundi la Mapacha Watatu, waliendelea kufanya shughuli zao kote kote, wakiimba na kufanya maonesho mbalimbali wakiwa na bendi zao (Twanga na FM Academia), huku pia wakilazimika kutumia nguvu zaidi kufanya maonyesho ya bendi yao.
Baada ya muda mfupi walifanikiwa kuachia Albamu yao ya kwanza iliyopewa jina la ‘Jasho la Mtu’ na ilikuwa na nyimbo kama ‘Shika ushikapo’, ‘Kipaji Changu’ na ‘Muhudumu’ wimbo ulio na mahadhi ya Afrika Magharibi (Gauo) ziliweza kufanya vizuri .
Ni kutokana na umahiri wao katika muziki wa dansi, wimbo wa ‘Shika Ishikapo’ uliweza kupendwa na hadi kuchaguliwa kuwa wimbo bora wa Kiswahili kwa mwaka 2010/11 katika tuzo za muziki za Kili, huku Khalid Chokoraa akishinda tuzo ya Rapa bora wa Kiume wa mwaka 2010/11 katika tuzo hizo.

KWANINI WATANZANIA WASINUFAIKE NA UTAJIRI WA MADINI WALIOPEWA NA MUNGU?

Hoja Binafsi ya kuunda kamati teule ya Bunge kuchunguza mkataba mpya wa madini ambao Waziri wa Nishati na Madini Karamagi ameusaini bila kuzingatia ma
Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe (Mb) Kigoma Kaskazini

MHESHIMIWA Spika, kwanza napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kunipatia fursa ya kuleta hoja hii hapa kwenye Bunge lako tukufu kwa mujibu wa kanuni zetu za Bunge. Kuletwa kwa hoja hii, bila kujali maamuzi ya kuhusu hoja yenyewe, ni ishara tosha ya ukomavu wa demokrasia yetu ambayo inakuzwa na mijadala ya Bunge lako tukufu. Nakupongeza kwa dhati kabisa kwa juhudi zako za kuliimarisha Bunge letu na kujenga muhimili imara wa ulinzi wa demokrasia ya vyama vingi nchini kwetu.
Mheshimiwa Spika, mnamo tarehe 16/7/2007 mara baada ya hoja ya Waziri wa Nishati na Madini kuamuliwa na Bunge lako tukufu, nilisimama mahala pangu na kutoa taarifa ya kukusudia kuleta hoja ya kuunda kamati teule ya Bunge. Nilisema kama ifuatavyo (kwa mujibu wa kumbukumbu sahihi za mijadala ya Bunge), ninanukuu ‘…naomba kutoa taarifa rasmi… kwamba nakusudia kuleta hoja ya kuunda kamati teule kuchunguza mkataba mpya wa madini ambao Waziri wa Nishati na Madini ameusaini bila kuzingatia maagizo ya rais (wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) ya kupitia mikataba ya madini aliyoyatoa mbele ya Bunge lako tukufu tarehe 30 Disemba, 2005.’ Mwisho wa kunukuu.
Mheshimiwa Spika, nimeshawasilisha hoja yangu hii kwa maandishi kwa Katibu wa Bunge na sasa nawasilisha rasmi katika kikao hiki cha Bunge kwa uamuzi. Nimezingatia kanuni 104 (2) katika kuwasilisha hoja yangu.
Mheshimiwa Spika, katika maelezo yangu niliyowasilisha bungeni wakati wa mjadala wa hotuba ya Waziri wa Nishati na Madini siku ya tarehe 16/7/2007, nilihitaji maelezo kutoka serikalini katika masuala makuu mawili yafuatayo:
  1. Kuondolewa kwa kipengele katika sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 1973 kuhusiana na asilimia 15% ya ‘capital allowance on unredeemed qualifying capital expenditure’ bila ya kibali cha Bunge lako tukufu.
  2. Kusainiwa kwa mkataba mpya wa madini wa mgodi (mradi) wa Buzwagi kati ya serikali na Kampuni ya Barrick na sababu za mkataba huo kusainiwa nje ya nchi, London, Uingereza, na vilevile kwa nini mkataba huo umesainiwa wakati bado serikali inafanya durusu (review) ya mikataba kufuatana na maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu Jakaya Mrisho Kikwete.
Mheshimiwa Spika, wakati akijibu hoja zangu Waziri wa Nishati na Madini alijenga hoja zake kama ifuatavyo:

A. Kuhusiana na asilimia 15% ya ‘capital allowance on unredeemed qualifying capital expenditure’

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini amenukuliwa na kumbukumbu za majadiliano ya Bunge akisema, ninanukuu: “…kwa hiyo pamoja na kwamba ninamheshimu sana Mheshimiwa Kabwe Zitto na sote tunamheshimu ni msomaji mzuri, lakini wakati mwingine lazima kuangalia vitu gani unasoma. Ni kwamba kipengele hiki cha sheria kililetwa hapa bungeni mwaka 2001 kwenye bajeti kikabadilishwa…” Mwisho wa kunukuu.
Mheshimiwa Spika, katika kuandaa hoja yangu hii, ilinibidi kupitia upya kumbukumbu za majadiliano ya Bunge ili kujiridhisha na maelezo ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini, maelezo ambayo mimi nililitaarifu Bunge lako tukufu tarehe 16/7/2007 kuwa sio sahihi.
Mheshimiwa Spika, Kumbukumbu hizo zinaonesha kwamba, sheria ya fedha ya mwaka 2001 (Finance Act. No.14 ya 2001) ilifanyiwa marekebisho kadhaa ikiwemo marekebisho ya sheria ya madini kifungu cha 87 ambapo kifungu kidogo cha (3) cha kifungu cha 87 kiliongezwa. Kifungu kidogo hicho kinasema, ninanukuu:
‘(3) The provisions of subsections (1) and (2) shall not apply to any person who, immediately before the first day of July, 2001 was not the holder of a mineral right granted under this Act.’
Mheshimiwa Spika, kifungu cha 87 cha Sheria ya Madini ya mwaka 1998 (No.5/1998) kinazungumzia mrahaba wa madini (Remission and deferment of royalties). Hivyo, kama sheria ya fedha ya mwaka 2001 haikubadili kipenge hiki, Mheshimiwa Waziri ametoa wapi jibu aliloliambia Bunge?
Mheshimiwa Spika, suala hili linahusu haki, kinga na madaraka ya Bunge kwa mujibu wa sheria namba 3 ya 1988.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo katika hotuba ya Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Basil Mramba, akiwasilisha hotuba ya Bajeti mwaka 2002, tarehe 13 mwezi Juni, alizungumzia kipengele hiki. Ninaomba kunukuu sehemu ya hotuba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Basili Mramba.
“Amendment to the Income Tax structure, (44) Mr. Speaker, in this area I propose to take the following measures:
(v) I propose to reinstate the additional 15 percent capital allowance on unredeemed qualifying capital expenditure as set out in the Mining Act. No. 5 of 1998.” Mwisho wa kunukuu.
Mheshimiwa Spika, nilipopitia sheria ya fedha ya mwaka 2002, nimekuta sehemu ya 8 inazungumzia mabadiliko katika kodi ya mapato ya 1973. Na hata katika ukurasa wa kwanza wa sheria hii (Arrangement of Contents), sheria ya madini haitajwi.
Mheshimiwa Spika, maelezo haya ya Waziri wa Fedha ya mwaka 2002 yanaonesha dhahiri utata wa kipengele hiki. Ni kwa vipi kifungu cha sheria ambacho hakijafutwa kirejeshwe?
Mheshimiwa Spika, tuchukulie kuwa maneno ya waziri ni ya kweli. Je, kwa nini makampuni ya madini ambayo yameingia mkataba na serikali kuanzia Julai mosi 2001 hayajaanza kulipa kodi ya mapato?
Mheshimiwa Spika, utata huu ambao umegubika sekta hii ya madini, unaweza kufafanuliwa na Bunge lako tukufu kupitia Kamati Teule. Kamati Teule ya Bunge ichunguze upitiaji wa mikataba hii na kuona kama kuna vitendo vyovyote vya uvunjifu wa sheria za nchi na kupotea kwa mapato ya serikali na ufisadi.

B. Kusainiwa kwa Mkataba wa Mgodi (Mradi) wa Buzwagi.

Mheshimiwa Spika, wakati akijibu hoja yangu kuhusiana na suala la mkataba mpya wa mgodi wa Buzwagi, Waziri wa Nishati na Madini amenukuliwa na kumbukumbu za majadiliano ya Bunge akisema kama ifuatavyo:
Mheshimiwa Spika, katika tathmini ya migodi, mgodi wa Buzwagi ni marginal mine ambao uhai wake si wa muda mrefu. Bila ya kutumia fursa ya sasa ya bei ya dhahabu, uwekezaji wake usingeweza kuwa wa faida. Hata hivyo, mkataba wa Buzwagi hauna mapungufu yaliyokuwamo kwenye mikataba ya zamani.’ Mwisho wa kunukuu.
Mheshimiwa Spika, mapitio ya mikataba ya madini ni mchakato ambao mwisho wake ni kuletwa kwa sheria ya madini hapa bungeni na kuifanyia marekebisho ili kuiboresha na kuondoa mapungufu. Hivyo, mpaka hapo sheria itakaporekebishwa, ndipo tutasema tumemaliza zoezi la kupitia mikataba ya madini na hivyo kusaini mikataba mipya na makampuni yote ya madini yaliyopo nchini na yatakayokuja kuwekeza.
Mheshimiwa Spika, suala ambalo linanipelekea kuomba kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza mkataba huu mpya, ni kuhusu uharaka uliopelekea Waziri wa Nishati na Madini kusaini mkataba huu. Sheria ya Madini bado haijarekebishwa, je, waziri anatumia vigezo gani kusema mkataba mpya wa Buzwagi aliousaini London hauna mapungufu?
Mheshimiwa Spika, Waziri wa Nishati na Madini aliliambia Bunge lako tukufu kuwa Buzwagi ni marginal mine. Vile vile waziri anasema kuwa Kampuni ya Barrick inamiliki migodi mitatu tu kupitia kampuni zake tanzu ambazo ni Bulyanhulu Gold Mine, North Mara Gold Mine na Pangea Minerals Limited Tulawaka. Kwa maelezo haya ya Waziri Karamagi, Buzwagi sio mgodi.
Mheshimiwa Spika, hoja hii ya kuwa Buzwagi sio mgodi inashabihiana kabisa na hoja ya Kampuni ya Barrick kwamba Buzwagi ni Project. Taarifa ya kampuni hii ya Barrick Gold Corporation-Global operations-Africa- Buzwagi, inaonesha kuwa Buzwagi ni mradi. Taarifa hii ninaiambatanisha katika hoja hii.
Mheshimiwa Spika, taarifa ya Barrick, Annual Review 2006 inasema ifuatavyo katika ukurasa wa 23, ninanukuu. ‘A major milestone was reached in February 2007 when we signed a mineral Development Agreement (MDA) with the Tanzanian government. In 2007, we expect to complete a detailed construction design and receive EIA approval.’
Mheshimiwa Spika, suala ambalo vile vile linanisukuma kuomba Bunge lako tukufu kuunda Kamati Teule ni kwamba, iwapo Buzwagi sio mgodi bali ni mradi, ni kwa nini tumesaini Mineral Development Agreement (MDA) mpya? Kwa kuwa Pangea Minerals Tulawaka ndio inaonekana kumiliki mradi huu, je, serikali imefanya marekebisho tu ya MDA na Kampuni ya Barrick? Naomba Kamati Teule ichunguze ni nini kilichosainiwa, marekebisho ya mkataba wa Tulawaka au MDA mpya ya Buzwagi?
Mheshimiwa Spika, Buzwagi inashika nafasi ya pili kwa uwekezaji wa Barrick katika migodi hapa nchini. Wakati kampuni hii inawekeza dola za Kimarekani 400 milioni katika Buzwagi, imewekeza dola za Kimarekani 600 katika Bulyanhulu. Je, ni kwa vipi Buzwagi iwe marginal mine wakati uwekezaji wake unashinda uwekezaji wa Tulawaka na North Mara?
Mheshimiwa Spika, chini ya kifungu cha 47 cha Sheria ya Madini ya Mwaka 1998 (Na.5/98), pamoja na mambo mengine kinataka leseni yoyote isitolewe mpaka taarifa ya mazingira iwe imetolewa na kuruhusu mgodi kuendelea na kazi.
Mheshimiwa Spika, wakati Waziri wa Nishati na Madini ameweka saini mkataba wa Buzwagi juma la mwisho la mwezi Februari 2007, Baraza la Mazingira nchini limetoa kibali (Environmental Impact Assessment- EIA approval) tarehe 11 mwezi Mei 2007. Ni kwa nini Waziri wa Nishati na Madini, Mheshimiwa Nazir Karamagi alisaini MDA ya Buzwagi na Kampuni ya Barrick kabla Baraza la Mazingira la Taifa (NEMC) halijatoa ruhusa?
Mheshimiwa Spika, sheria ya madini, niliyoitaja hapo awali, imeunda Kamati ya Ushauri ya Madini (Mining advisory Committee). Kabla ya waziri kusaini mkataba wowote ni lazima apate ushauri kutoka kamati hii. Kwa taratibu za kiserikali, kama kamati ikimshauri waziri na waziri akakataa ushauri huo, inampasa waziri atoe sababu ni kwa nini anakataa ushauri. Je, waziri alifuata ushauri wa Kamati ya Ushauri ya Madini kuhusiana na wakati mwafaka wa kusaini mkataba huu?
Mheshimiwa Spika, inawezekana kabisa MDA ya Buzwagi kusainiwa Uingereza sio tatizo. Kwa mfano, mwaka 2006 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilisaini mikataba kadhaa. Ni mingapi kati ya mikataba hii imesainiwa nje ya nchi? Nini madhara ya kisheria kwa mkataba kusaniwa Uingereza? Je, mkataba umeandikwa “signed in London...” au “signed in Dar es Salaam...? Kamati Teule ya Bunge ndio chombo pekee kitakachoweza kutoa majibu ya maswali haya.
Mheshimiwa Spika, suala hili ni suala la kitaifa. Halina hata chembe ya itikadi za kivyama. Ninaamini wabunge wataamua kwa maslahi ya taifa letu. Uundwaji wa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza mapitio ya mikataba ya madini na mazingira ya kusainiwa kwa mkataba mpya wa Buzwagi yatatoa msaada mkubwa kwa azma ya Rais wetu ndugu Jakaya Mrisho Kikwete ya kuona rasilimali za madini zinafaidisha nchi yetu.
Mheshimiwa Spika, ninaomba kutoa hoja

MIKOA MIPYA ITAANZISHWAJE BILA KUWEKWA KWENYE BAJETI,AU NI SIASA TUPU?

Bajeti ijayo haiitambui mikoa mipya  Send to a friend
Sunday, 05 June 2011 21:34
0diggsdigg
Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo
Boniface Meena
BAJETI inayotarajiwa kusomwa bungeni Juni 8, mwaka huu inaonyesha kuwa mikoa mipya iliyoanzishwa haijatengewa fedha za kuiendesha kwa mwaka wa fedha ujao.

Mikoa hiyo mipya ni Njombe, Simiyu na Geita ambayo kusudio la kuanzishwa kwake lilitangazwa bungeni mjini Dodoma mwaka jana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipokuwa akihitimisha Hotuba ya Makadirio ya Bajeti kwa ofisi yake.

Kwa mujibu wa mapendekezo yaliyowasilishwa katika Kamati ya Bunge ya Katiba Sheria na Utawala, mikoa iliyotajwa katika Bajeti ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), mikoa iliyotengewa mafungu ni 21 tu.

Kati ya mikoa hiyo, Dar es Salaam unaongoza kwa kuwa na bajeti kubwa ya Sh 213.8 bilioni huku Lindi ukishika mkia kwa kuwa na bajeti ndogo ya Sh 56.0 bilioni.Mbali ya Dar es Salaam mingine iliyotengewa fedha nyingi ni Mwanza (Sh175.6 bilioni), Mbeya (Sh163.4 bilioni), Shinyanga (Sh141.3 bilioni) na Kilimanjaro wenye Sh138.0 bilioni.

Mikoa inayoungana na Lindi kwa kutengewa bajeti ndogo ni Rukwa Sh63.9 bilioni, Singida Sh63.8 bilioni, Mtwara Sh78.2 bilioni na Kigoma Sh72.3 bilioni.

Bajeti kwa mikoa yote hiyo 21 ya Tanzania Bara ni kiasi cha Sh2.3 trilioni.

Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo alipoulizwa kuhusu suala la mikoa hiyo mipya kutotengewa bajeti alisema kuwa waziri anayeweza kuzungumzia suala hilo ni George Mkuchika wa (Tamisemi): "Mwulize Mkuchinka ndiye waziri ambaye ataweza kukueleza kuhusu hilo."

hata hivyo, jitihada za kumpata Mkuchika kutoa ufafanuzi zilikwama.Kamati ya Bunge ilipitisha mapendekezo ya bajeti hiyo ya Tamisemi na kuitaka kutoa kipaumbele katika miradi ya maendeleo kwenye halmashauri zote nchini.

Mkuchika aliiambia kamati hiyo kuwa kati ya fedha hizo, Sh2.3 trilioni zitatumika kwa ajili ya matumizi ya kawaida na zilizobaki zitatumika kulipa mishahara watumishi wake.Alisema kutokana na hali hiyo halmashauri nchini zitasimamia miradi yake na kuongeza mapato ambayo yatatumika kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo.

MIKOA MIPYA ILIYOANZISHWA

(i) Mkoa wa Njombe. Huu umezaliwa baada ya kumegwa na kuunganishwa kwa Wilaya za Njombe, Ludewa na Makete kutoka Mkoa wa Iringa. Mkoa huu utakuwa na wilaya mpya ya Wanging’ombe ambayo inatokana na kugawanywa kwa Wilaya ya Njombe.

(ii) Mkoa wa Geita. Huu unatokana na kumega na kuunganisha Wilaya za Geita kutoka Mkoa wa Mwanza, Bukombe kutoka Mkoa wa Shinyanga na Chato kutoka Mkoa wa Kagera. Mkoa huu utakuwa na Wilaya mpya ya Nyang’hwale ambayo inatokana na kugawanywa kwa Wilaya ya Geita.

(iii) Mkoa wa Simiyu. Unatokana na kumega na kuunganisha Wilaya za Bariadi kutoka Mkoa wa Shinyanga, Maswa kutoka Mkoa wa Shinyanga, Meatu kutoka Mkoa wa Shinyanga na Wilaya mpya ya Busega kutoka Mkoa wa Mwanza. Mkoa huu utakuwa na Wilaya nyingine mpya ya Itilima ambayo inatokana na kugawanywa kwa Wilaya ya Bariadi.

MADHUMUNI YA KUANZISHWA MIKOA MIPYA

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaelekeza kuwa, kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali, Rais anaweza kuigawa nchi katika mikoa au Wwlaya. Hivyo, madhumuni ya kuanzishwa kwa mikoa hiyo ni kuboresha utendaji wa serikali kuu kwa kupunguza ukubwa wa maeneo ya mikoa mama ili wananchi wapate huduma za kiutawala ngazi ya mikoa kwa karibu.

CALL FOR ACTION-CHADEMA

The Arrest of The Leader of Official Opposition in Tanzania, Hon. Freeman Mbowe (Mb) is infringement of freedom of Parliament and a threat to democracy in the country
CALL FOR ACTION
This is to bring to your urgent attention that the Leader of Official Opposition in Tanzania Parliament, Hon. Freeman Mbowe (Mp) who is also the National Party Leader (Chairman) of CHADEMA, the main opposition party in the country has been arrested today (4th June 2011) and is being held in custody at the Central Police Station in Dar es Salaam.
He has been arrested during the ongoing Parliamentary Committee sessions that he is attending as prelude to the fourth Parliamentary Session that is scheduled to commence on 7th June 2011.
He has been arrested by the Police by the order of Resident Magistrate's court which is tantamount to infringement of freedom of Parliament and a threat to democracy in the country. This is very unfortunate as the arrest comes against Court order which had exempted the MP’s from attending court sessions which are at mention stage at Arusha. The Court also made order to issue “notice to show cause” to sureties, but  court records do not indicate that the said notice to sureties had matterally  been issued. It is clear therefore that the said arrest is a result of a master plan of the rulling Party CCM whose Chairman is also the President of the United Republic of Tanzania. The arrest  clearly will destabilize the preparation of the Opposition Budget Speech.
The arrest is unlawful and unconstitutional as it contravenes the statutes in the Union Constitution and Commonwealth National Parliament customs and traditions, which accord lawmakers’ immunity whenever they are engaged in Parliamentary business.
Members of Parliament according To Parliamentary Immunities, Powers and Privilleges Act, 1988 may not be arrested during parliamentary sessions without Speaker’s authorization as per stipulations set forth in sections 5, 6 and 11 of the said Act.
Also article 100 of the Union Constitution of 1977 recognizes and defends freedom of expression, discussions, and parliamentary procedures and that such freedom will not be broken or questioned by any organ of the union government or in any court or anywhere outside the parliament.
We further call to your attention that there has been an ongoing trend of the police force in Tanzania arresting, beating and harassing opposition legislators . This is now becoming a pattern.
The list of CHADEMA Members of Parliament recently arrested and released on bail include Hon. Philemon Ndesamburo, Joseph Selasin, Godbless Lema, Hon. Meshack Opulukwa, Hon. Tundu Lissu (Chief Whip), Hon. Esther Matiko and a CUF legislator Hon. Magdalena Sakaya who is to date in custody. Hon Lissu was arrested, beaten and harassed while on official tour as Shadow Minister for Home Affairs.
However Incase of the ruling party, CCM MPs-some of whom with greater charges; Speaker’s permission is sought as evidenced by the Letter dated May 31 letter from Mwanza Special Police Investigator (SP) B.M. Wakulyamba asking the Speaker to authorise the questioning of CCM’s Busega MP, Titus Kamani in connection with an alleged plot to murder former Busega MP Dr Raphael Chegeni. The treatment of Opposition Parties is a double standard.
On 3rd June 2011 Mr Mbowe had told the press that he has been shocked by the arrest warrant issued in the pre text of court contempt since both him and the party has the record of respecting the court. Mr Mbowe explained that recognizing the role of the opposition in the budgetary proceedings that are ongoing the accused legislators agreed with the Resident Magistrate that they will appear in Court after the Budget sessions.
We ask for your support to call for his immediate release and condemn the actions of state machinery against the opposition legislators, leaders and democracy.
Issued by:

John Mnyika (Mp)
Secretary of Official Opposition
And Director of Foreign Affairs (CHADEMA)
+255-784-222 222

Sunday, June 5, 2011

NATUMAINI MAFANIKIO UNAYOYASEMA SIO KUPANGA CHUMBA KIMOJA USWAHILINI NA KUMILIKI BALOON 2ND HAND

ELIAS BARNABAS: THT imenifikisha hapa nilipo  Send to a friend
Saturday, 28 May 2011 18:05
0diggsdigg
Furaha Maugo
MAFANIKIO ya wasanii wanaopikwa ndani ya nyumba Nyumba ya Vipaji Tanzania (THT), tangu kuanzishwa kwake yanathibitisha  kazi nzuri inayofanywa na wasimamizi wa  nyumba hiyo.

Mmoja wa wasanii walitoka THT ni Elias Barnabas, maarufu kwa jina la Barnaba ambaye amefanikiwa kushinda tuzo ya Wimbo bora wa Zouk, katika tuzo za muziki za Kilimanjaro mwaka 2010/11.
Alijiunga na THT, mwaka 2006 kutokana na msukumo kutoka kwa rafiki yake waliyekuwa wanaimba, kupiga vyombo na kusali naye kanisani.

Tangu ameingia katika nyumba hiyo ya kuzalisha,  kutengeneza na kukuza vipaji, Barnaba ametawala sana midomoni mwa wapenzi wa muziki wa kizazi kipya.
Hii ni kutokana na baadhi ya nyimbo zake alizoimba na kufanya vizuri katika anga la muziki wa kizazi kipya hapa nchini.
Licha ya kuimba, Barnaba ana uwezo mkubwa wa kutumia ala mbalimbali za muziki kama vile gita na ‘keyboard’. Pia ana uwezo wa kupangilia sauti yake kwa ustadi na kutawala jukwaa vyema anapokuwa kukwaani.

Ni kutokana na uwezo wake huo, Barnaba amepewa jukumu la kufundisha wasanii wenzake katika kundi la THT.
Mafanikio ya baadhi ya nyimbo za kizazi kipya, zinazofanya vizuri hivi sasa zimetungwa na Barnaba, nyimbo hizo ni pamoja wimbo wa Mwasiti (Kisa Pombe), wimbo wa Ray C, (Watanionaje), ‘Kizunguzungu’ ulioimbwa na Rachel, ‘Najua’ ulioimbwa na Linah na ‘Shukurani’ ulioimbwa na Nakaaya.
Nyingine ni ‘Wrong number’ aliyoimbwa na Linah  na ‘Milele daima’, wimbo ambao unaofanya vizuri katika chati za vituo vingi vya redio na televisheni.


 “Ninashukuru Mungu sasa hivi  uwezo wangu ni mkubwa kwenye kuimba, kutumia vyombo na hata kuingiza sauti studio,” anasema Barnaba alipozungumza na Mwananchi Jumapili.
Kuonyesha kuwa anakipaji cha hali ya juu na anafanya kazi yake kwa umakini ilimchukua takribani miaka miwili (2008-2010)kukamilisha  albamu yake  ya  ‘Njia Panda’,  ambayo  alishirikiana na Amini iliyokuwa na jumla ya nyimbo 14.
Baadhi ya nyimbo zinazopatikana katika albamu hiyo ni ‘Njia panda’ aliyoimba na  Pipi, ‘Muongo’ , ‘ ‘Robo saa’,  na ‘Mbala mwezi’  zote ameimba akishirikiana na Amini, Wrong Number aliyoimba  na msanii bora wa kike mwaka 2011, Linah.
Nyingine ni ‘Kodi Mangasubi’ ,  ‘Nivumilie’, ‘Nimelimiss’,   ‘Baby I Love’, ‘mdomo’, ‘ Mwongo’, ‘Dukuduku’ na ‘Huruma’.
Barnaba anasema ingawa hakusoma sana,  mafunzo aliyopta THT  ndiyo yaliyomfikisha hapa alipo na kufafanua:  “Niliweka juhudi kubwa kwenye mafunzo nilipokuwa darasani na kuyafanyia kazi mambo yote niliyofundishwa na mwalimu wangu.
“Matunda ninayopata yametokana na heshima na uvumilivu niliokuwa nao kipindi chote cha mafunzo. Hivi sasa ninaweza kukidhi mahitaji yangu binafsi na nimehama nyumbani sasa nakaa kwangu na ninapata kila ninachohitaji,” anasema Barnaba.
Barnaba anasema  anavutiwa sana na kazi za wanamuziki wengine wa Afrika, kama vile Fally Ipupa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Barnaba anampamgo wa kurudi shule kujiendeleza.  “Kwa kuwa sikubahatika kumaliza elimu yangu vizuri nina mpango wa kurudi tena shule, nafikiria kuendelea na elimu ingwa sijajua nataka kusomea kitu gani,” anasema.
Wasifu
Alizaliwa Agosti 8, 1990 mkoani Morogoro, alipata Shule ya Msingi Kinondoni, Dar es Salaam mwaka1998 – 2004, alijiunga na Mikoji Sekondari na kuishia kidato cha tatu.
Ni mtoto wa kwanza katika familia ya watoto watatu. Kabla ya kuingia katika muziki alikuwa akifanya biashara ya kuuza genge nyumbani kwao na alikuwa akipiga vyombo mbalimbali vya mziki kanisani kwao.
Mbali na muziki Barnabas, anamiliki duka la kuuza nguo lililopo maeneo ya Kinondoni na siku za mwisho wa juma hupenda kutembelea ufukweni.

HATIMAYE EDWARD LOWASA NA ANDREW CHENGE WAWEKWA KITIMOTO

CCM yakiri kuwahoji na Rostam, Lowassa na Chenge  Send to a friend
Saturday, 04 June 2011 10:17
Mwandishi Wetu
CHAMA cha Mapinduzi (CCM), kimethibitisha kwamba kimewahoji Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge ikiwa ni moja ya hatua ya kutekeleza maazimio ya Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho uliofanyika Aprili 10 hadi 11 mjini Dodoma.

Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa CCM, Willison Mukama ilisema kuwa hiyo ni moja hatua za awali zilizochukuliwa na kuongeza kuwa nyingine zitafuata baadaye.

Alisema hatua hiyo ya awali, Makamu Mwenyekiti CCM (Bara), Pius Msekwa alikutana na wanaotajwa katika tuhuma hizo katika sura mbili, kwanza ya nafasi yake ndani ya chama na pia kama mzee wa CCM.

Mukama alisema Mei 26, mwaka huu Msekwa alikutana na Rostam ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na siku Iliyofuata alikutana na Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa.

Alisema siku hiyo hiyo ya Mei 27, mwaka huu alikutana na Mjumbe mwingine wa Halmashauri Kuu, Chenge."Kwa vile Msekwa alikutana kwa faragha na viongozi hao mmoja mmoja, hakuna anayejua kilichozungumzwa. Ni Mzee Msekwa na wao peke yao," alisema katika taarifa hiyo.

Alisema hatua itakayofuata baada ya hapo ni kufikisha kwenye vikao vya chama taarifa ya mambo yaliyojiri wakati wa mazungumzo baina ya Msekwa na viongozi hao."Endapo vikao husika vitaamua lolote kuhusiana na taarifa hiyo, umma utajulishwa," alisema.

Katika mkutano huo wa Halmashauri pamoja na mambo mengine, uliwataka viongozi wa CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi kutafakari, kujipima na kuchukua hatua wenyewe kwa maslahi ya chama na kwamba wasipofanya hivyo chama kitawawajibisha

POLISI WATENDEENI HAKI WBUNGE WA VYAMA VYOTE VYA SIASA,MBONA KAMATAKAMATA IPO KWA WAPINZANI PEKE YAO?

Mbowe, Zitto mbaroni  Send to a friend
Saturday, 04 June 2011 22:08
0diggsdigg
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe
Waandishi Wetu
MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe jana alitiwa mbaroni na Jeshi la Polisi baada ya kujisalimisha katika kituo Kikuu cha jijini Dar es Salaam.Katika hatua nyingine, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe, jana alikamatwa na polisi mjini Singida kwa kosa la kuzidisha muda wa kuhutubia mkutano wa hadhara.Habari zilizopatikana kutoka Singida na kuthibitishwa na Zitto mwenyewe, zinaeleza kuwa polisi walimkamata jana jioni kwa madai kuwa alihutubia mkutano wa hadhara mpaka zaidi ya saa 12:00. Muda wa mwisho kisheria kuhutubia mkutano wa hadhara ni saa 12:00 jioni."Mpaka sasa bado nipo polisi wanaendelea kunihoji," alisema Zitto kwa kifupi.

Hadi tunakwenda mitamboni, Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini alikuwa bado ameshikiliwa katika Kituo cha Polisi mjini Singida.Kukamatwa kwa Mbowe kunafuatia amri ya mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kuamuru akamatwe  popote alipo na kufikishwa mahakamani kwa kutotii amri ya kufika mahakamani katika kesi yake.

 Juni 2 mwaka huu, Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Charles Magesa,  alikubaliana na hoja ya wakili upande wa Serikali kuitaka mahakama kutoa amri ya kukamatwa kwa Mbowe kwa sababu ya kutotii amri ya kufika kortini au kumtuma mdhamini wake.Alisema sababu iliyotolewa mahakamani hapo kwamba mshtakiwa huyo ni mbunge na yupo kwenye vikao vya Kamati za Bunge haina uzito kwa kuwa hiyo ni moja ya shughuli zake kama ilivyo shughuli nyingine kwa watumishi wa Serikali.

Hakimu Magesa akitoa agizo hilo alisema kuwa inachokumbuka ni kwamba mahakama hiyo ilipokea maelezo ya kuwa washtakiwa hawatahudhuria mahakamani hapo Mei 27, mwaka huu na kwa sababu ya kuwapo vikao vya kamati za Bunge iliagiza wafike wadhamini wao kesi inapotajwa. Ndiyo maana Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini, alimpeleka mdhamini.Katika kesi hiyo iliyopangwa kuendelea kusikilizwa kesho, Mbowe na wenzake wanashtakiwa kwa kosa la  kufanya kusanyiko lisilo halali Januari 5, mwaka huu jijini Arusha.

Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwanasheria wa chama hicho, Mabere Marando alithibitisha jana kukamatwa kwa Mbowe saa 9:00 alasiri kutokana na amri ya mahakama."Ni kweli amekamatwa saa moja iliyopita kwa sababu ni amri ya mahakama na chama hakiwezi kumwombea dhamana itabidi apelekwe Arusha," alisema Marando.

 Pamoja na Marando kuthibitisha kukamatwa kwa Mbowe, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limesema halina taarifa zozote za kukamatwa kwa mwenyekiti huyo.Jeshi hilo limesema halina taarifa zozote juu ya mwenyekiti huyo kujisalimisha katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam. Mei 27, mwaka huu, mahakama hiyo ilitoa hati ya kukamatwa na kufikishwa mahakamani hapo kwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa na Mwenyekiti wake, Mbowe.

Pamoja na viongozi hao, mahakama hiyo pia iliamuru wabunge wawili wa chama hicho, Phillemon Ndesamburo (Moshi Mjini) na Godbless Lema (Arusha Mjini) wakamatwe na kufikishwa mahakamani baada ya kushindwa kuhudhuria mara kadhaa . Lakini, viongozi hao waliwasiliana na mahakama hiyo.
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, alipotafutwa ili kutoa ufafanuzi wa suala hilo hakupatikana kutokana na simu yake ya mkononi kuita bila ya kupokelewa.
Awali asubuhi, akizungumza na gazeti hili ofisini kwake, Kamanda Shilogile alisema kuwa hana taarifa zozote za Mbowe kukamatwa au kujisalimisha katika kituo hicho.

 “Sina taarifa zozote kuhusiana na kukamatwa kwa Mwenyekiti cha Chadema. Taarifa hizi ndiyo nazisikia kwenu waandishi wa habari. Mimi wala uongozi wangu hauna taarifa hizo,”alisema Shilogile na kuongeza;
“Angekuwa amekamatwa au amekuja kujisalimisha mkoa wangu ndiyo ungekuwa wa kwanza kupata taarifa hizo, labda mtafute Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, kama ana taarifa hiyo anaweza kukwambia.”Kova alipotafutwa kwa njia ya simu alisema yuko Zanzibar na kwamba hana taarifa zozote za kukamatwa kwa Mbowe.

Marando, Tundu Lissu
Mapema asubuhi Marando na  Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu walionekana wakiingia katika Ofisi ya Mpelelezi wa Mkoa wa Ilala (RCO),  Diwan Nyanda.Alipoulizwa ujio wake katika ofisi hizo, Marando alisema kuwa alikwenda katika ofisi hizo kwa shughuli zake binafsi na kwamba hana taarifa za kukamatwa kwa Mbowe.

Akizungumza na Mwananchi Alhamisi wiki hii baada kutolewa amri ya kukamatwa kwake, Mbowe alisema anatarajia kutoa tamko kuhusu suala hilo Ijumaa jijini Dar es Salaam.“Nitatoa tamko kesho, lakini nasikitishwa na tafsiri hii ya Mahakama kwamba mimi nimekaidi amri ya kufika katika vikao vya mahakama...,” alisema Mbowe

Mnyika
Katika hatua nyingine Mbunge wa  Ubungo, John Mnyika (Chadema) amesema chama hicho kitaandika barua rasmi katika Ofisi za Bunge kueleza jinsi wabunge wa vyama vya upinzani wanavyokamatwa bila kufuata kanuni na taratibu, wakati wana kinga ya kibunge inayowazuia kukamatwa bila kibali.

Alisema mpaka sasa wabunge wa upinzani ambao wamewahi kukamatwa bila kuombwa kwa kibali chochote kutoka kwa Spika wa Bunge ni pamoja na Godbless Lema (Arusha Mjini), Phillemon Ndesamburo (Moshi Mjini), Joseph Selasini (Rombo), Meshack Opulukwa (Meatu)Wengine ni Tundu Lissu (Singida Mashariki), Esther Matiko (Viti Maalumu-Chadema) na Magdalena Sakaya (Viti Maalumu-CUF) ambaye mpaka sasa yuko mahabusu mkoani Tabora huku kesi yake inatarajiwa kutajwa Juni 6 mwaka huu.

Imeandikwa na Hadija Jumnne, Fidelis Butahe na Edward Qorro

Tuesday, May 17, 2011

MAFISADI NI KAA LA MOTO?

RAIS Jakaya Kikwete ameonyesha kutokuwa na uwezo wa kufukuza wenzake ambao wametuhumiwa ufisadi kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), MwanaHALISI limeelezwa.
Uchambuzi wa hotuba yake wakati wa kufunga vikao vya chama – Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) mjini Dodoma wiki tatu zilizopita, ndio umedhihirisha udhaifu huo.
Badala ya kuwa wazi, thabiti na elekezi, mwenyekiti Kikwete aliongea kwa njia ya kubembeleza huku akijaribu kumtwisha mzigo kila mmoja ukumbini.
Katika hotuba yake ya kufunga, ambayo MwanaHALISI ina nakala yake, Kikwete anang’angania maneno mawili yanayoonyesha, ama woga au kutokuwa tayari kuchukua hatua.
Rais Kikwete alirudia neno “Kukubaliana” mara 18 na neno “Tufanye” mara saba, katika hotuba fupi ya karibu dakika 30. Maneno hayo yametumika pale ambako alitegemewa kutoa kauli inayouma.
“…tuliyokubaliana mnayajua…nikiyarudia nitakuwa nawasumbua kwa sababu tumekubaliana,” alisema bila kutaja kilichokubaliwa.
Tumekubaliana. Hakuna wa kumtumia meseji (sms) mwenyekiti, kwamba hawa jamaa wamekutukana na wewe jibu…Haya tumekubaliana wote. Tukafanye kama tulivyokubaliana” alisema Kikwete akionyesha kutwisha kila mmoja jukumu ambalo yeye angetekeleza mara moja – kufukuza mafisadi. 
Kikwete aliwaambia wajumbe wa NEC Dodoma, “Lakini ni matumaini yangu kwamba tuondoke hapa bila unyonge. Tukafanye kama tulivyokubaliana.
“Nafurahi tumefanya uchambuzi kwa kina na kwa kituo. Kila pendekezo moja baada ya jingine tumelijadili vizuri. Ni kwa sababu, tumejipa muda wa kutosha,” alisema.
Kikwete alisisitiza, “Hakuna atakayetoka hapa na kusema, nilitaka kusema, lakini mwenyekiti ameninyima nafasi. Yupo?” aliuliza Kikwete na sauti zikasikika zikisema, ‘Hakunaa…!’
“Kila aliyetaka kusema nimempa nafasi kwa sababu ya uzito wa jambo lenyewe (hataji jambo). Sisi ni chama cha siasa, kazi yetu ni kushinda uchaguzi; na tunapofanya tathmini ya uchaguzi uliopita, ndipo tunapojijengea nguvu ya kushinda uchaguzi mwingine.”
Kwa kauli hii, wachambuzi wanasema Kikwete alikuwa anawapiga kijembe akina Edward Lowassa, Andrew Chenge na Rostam Aziz ambao walituhumiwa lakini hawakuamsha mkono kujitetea; kwa maana kwamba sasa wanakubaliana na yaliyoamuliwa.
Tumefanya tathimini ya uchaguzi uliopita, ili tupate kujenga misingi ya kushinda uchaguzi mwingine. Tumezungumza kwa kina yote yenye udhaifu kwa upande wetu na tuliokubaliana tunayajua. Twende tukafanye yale tuliotaka tuyafanye sasa; yale ya muda wa kati na yale ya muda mrefu. Na tunapozungumzia muda mrefu hapa, tunakusudia kabla ya mwaka 2014.
Tufanye mageuzi. Tujenge upya chama chetu. Mkimaliza uchaguzi mnafanya tathimini na kwa muono wangu, chama chetu kinatakiwa kufanya mageuzi.
“Tumekuwa na mapendekezo mengi. Tumeletewa tabu (kitabu kikubwa) kubwa lenye kurasa 58. Tumechambua pendekezo moja baada ya jingine kwa utulivu, kwa kituo na kwa kina na tuliyokubaliana tunayajua sote.
“Na kwa kuwa mjadala ulikuwa mkali, safari hii watu walikuwa hawatoki nje, tofauti na vikao vingine. Tumekubaliana ya kuyafanya, twende tukayafanye.
Tumekubaliana mambo ya msingi ya tawi na shina; tumekubaliana kwenye muundao wa chama chetu; tuitishe mkutano mkuu wa taifa ili kurekebisha katiba ili sasa wajumbe wa NEC wapatikane kupitia wilaya ili kupanua uwakilishi.”
Kinachoonyesha kuwa Kikwete, ama anakwepa kusema hoja yenyewe anayojadili au hana dhamira ya kutenda, ni pale anapotaja waziwazi mabadiliko ya Katiba ili kupata wajumbe kutoka wilayani; lakini linalohusu kufukuza au kutenga watuhumiwa wa ufisadi, analizunguka kwa maneno “kukubaliana” na “kufanya” au “kutenda.”
Alisema, “Tumekubaliana kuchambua mazingira ya nchi yetu… Tumezungumza kwa ukali, kwa kina na kwa undani, suala la maadili kwa viongozi wetu. Tuliokubaliana mnayaelewa, lakini la msingi ni kwamba utovu wa maadili, miongoni mwa wanachama na viongozi ni mambo ambayo yamepunguza haiba ya chama chetu mbele ya wananchi.
Tumekubaliana, tusionekane kuwa lichama ambalo vitendo vya rushwa, hatuchukizwi navyo. Wanaofanya vitendo vya rushwa hatuwachukii. Tumekubaliana vizuri. Tumeanza kuchukua hatua na hizo hatua tulizoanza ni sehemu ya yale tuliokubaliana. Kwamba wenzetu tunaowatambua, tusiwaonee haya.
Tumekubaliana hatua mbili: Kwanza, kuwabana ili waamue wenyewe kuwajibika, lakini pili, wanapokataa, tusichelee kuwawajibisha. Maana kuendelea hivi, chama kinasemwa, lakini sisi tunakaa kimya kama vile hakuna kinachofanyika, kunakitokomeza chama chetu,” alieleza Kikwete.  
Ilipofikia CCM hivi sasa, hakuna uwezekano wa kusalimika. Kwa kufukuza watuhumiwa wa ufisadi au kwa kuwaacha katika chama, CCM haiwezi kurejesha hadhi yake.
“Imebakia njia moja tu: Chama chetu kijiandae kukaa pembeni na kujipanga upya; hatimaye kijitahidi kurejea madarakani,” ameeleza kiongozi mstaafu wa ngazi ya juu katika CCM.
Hata hivyo, katika kile kinachoonekana “kurejesha majeshi nyuma,” katibu mkuu mpya wa chama hicho, Wilson Mukama aliwaambia waandishi wa habari wiki iliyopita, “…hakuna mahali popote katika maazimio ya NEC panapotaja siku 90” za kufukuza mafisadi.
Mukama alisema, “Kama ni muda basi ni pale mwenyekiti wetu aliposema NEC ijayo. NEC hukutana kila baada ya miezi minne na kwa hiyo, kama ni siku, basi ni 120 na siyo 90.” Alikuwa akijibu swali la mmoja wa waandishi waliotaka kufahamu lini chama hicho kitaandika barua na kukabidhi watuhumiwa.
Katika mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari, Mukama alisema, “NEC ilitoka na maazimio 26. Azimio mojawapo linasema chama kiendelee na mapambano yake dhidi ya ufisadi na kwamba watuhumiwa wajitafakari, wajipime na kuchukua hatua.”
Taarifa zinanukuu mjumbe mmoja wa NEC ambaye hakupenda kutajwa gazetini akisema Kikwete alipitisha azimio la kuwafukuza Lowassa, Rostam na Chenge kwenye chama kwa staili ya kuviziana ili kuzuia kile alichoita, “hofu ya kujipanga na kurejesha mapigo.”

NDUGU YANGU NAPE JIPYA ULILONALO NI LIPI KAMA ULITAKA KUIASI CHAMA KWA UBABAISHAJI WAKE?

Vita ya Chadema, CCM sasa yafika patamu  Send to a friend
Sunday, 15 May 2011 11:01
0diggsdigg
Edwin Mjwahuzi, Ruvuma
VITA ya maneno kati ya Chadema na CCM jana imechukua sura mpya baada ya Fred Mpendazoe kumtaja Katibu Mwenezi na Itikati wa CCM, Nape Nauye kuwa miongoni mwa vigogo sita walioanzisha Chama cha Jamii (CCJ) .Mpendazoe alitoboa siri hiyo jana alipokuwa akituhubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Mbamba Bay kilichopo katika wilaya mpya ya Nyasa mkoani Ruvuma.

Mpendazoe alijitoa CCM Machi 30, mwaka jana akiwa Mbunge wa Kishapu na kujiunga na CCJ Aprili 16, mwaka huo kabla ya kuhamia Chadema, baada ya CCJ kukosa sifa na kufutwa na Msajili wa Vyama vya Siasa.Akihutubia mkutano wa hadhara katika mji wa Mbamba Bay, mkoani Ruvuma jana, Mpendazoe alisema ameamua kuliambia taifa ukweli kuhusu Nape, ili umma uepuke kudanganywa na propaganda za kijana huyo

.“Kelele zote anazopiga Nape kuitetea CCM ni za kinafiki kwani aliwahi kukigeuka chama hicho na kushiriki katika mipango yote ya kuanzisha CCJ”.Hata hivyo, Nape alipoulizwa na gazeti hili jana kuhusiana na madai hayo ya Mpendazoe, hakukataa wala kukubali kushiriki kuanzishwa CCJ, badala yake alisema, "Cha msingi waeleze (Chadema) CCJ ilikufaje, wasiseme ilizaliwaje, maana kuzaliwa ni sherehe na kufa ni kilio.” Nape ambaye hakusema lolote kama kombora la Mpendazoe ni la kweli aliwageuzia kibao Chadema akisema, "Pamoja na hayo yote, waache (Chadema) kubaka demokrasia."

Alifafanua akisema "Watanzania walipiga kura kuichagua CCM iwaongoze kwa miaka mitano ijayo, sasa wanaposema tutaandamana nchi nzima ili serikali iondoke kabla ya muda huo, huku ni kubaka demokrasia na ni uhaini."Mpendazoe alisisitiza kuwa Nape alishiriki katika kuandaa na kuandika katiba na miko ya uongozi ya CCJ, kutafuta fedha za kukuza chama na jengo la kuweka ofisi za chama hicho.

Alisema: “ Huyo Nape anayepiga kelele za kuitetea CCM ni mnafiki mkubwa pengine kuliko wanafiki wote hivi sasa. Mimi na yeye pamoja na wanaCCM wengine wanne, ndio tulioamua kuanzisha CCJ.“Nape ndiye aliyepewa jukumu la kutafuta nakala za katiba za vyama tawala vya nchini za Afrika, ili kupata katiba nzuri ya itakayoigwa katika kuandika katiba ya CCJ.”

Alisema Nape alilitekeleza vizuri jukumu hilo na kufanikiwa kuipata katiba ya chama tawala cha Afrika Kusini cha ANC, ambacho ndiyo kilitumika kwa kiasi kikubwa kuandaa katiba ya CCJ.Alisema yeye, Nape na vigogo wengine aliosema atawataja muda ukifika walifanya vikao vyote vya siri hadi wakaanzisha chama hicho cha CCJ.

“Tulifungua mtandao maalumu wa kuwasiliana kwa internet, ambao baadaye wenzangu waliufuta baada ya kubadili mawazo dakika za mwisho. Lilipotulazimu kukutana mimi na Nape tulipendelea kukutana katika eneo la vinywaji pale Mlimani City, jijini Dar es Salaam”.Alisema walifanya hivyo ili wasitiliwe shaka na maafisa usalama wa taifa waliopewa kazi ya kupeleleza wanaCCM waliohisiwa kutaka kuanzisha chama kipya.

“Nape alibadili mawazo ya kutaka kuihama CCM baada ya Rais Jakaya Kikwete kumteua kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi, kwa kuwa alikuwa na uchu wa madaraka ,” aliongeza. Alisema Nape aliisaidia CCJ kwa kukipa siri nyingi ikiwamo mambo yaliyokuwa yakijadiliwa kwenye mikutano ya Halmashauri Kuu ya CCM (Nec) na hata vikao vilivyokuwa vikifanyika katika Ofisi Ndogo ya CCM iliyopo Lumumba.“Nape pia alitupa siri kwamba baadhi ya walioanzisha CCJ walikuwa wanakaribia kufukuzwa kwani katika mkutano wa NEC, majina ya baadhi yao yalitajwa na kujadiliwa kwenye kikao hicho.'

Tuhuma za Chadema dhidi ya Nape na majibu ya Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM, ni mwendelezo wa siasa za jino kwa jino za kurushiana makombora yaliyobeba tuhuma nzito ndani yake.

Mei 12 mwaka huu Nape alimtaka Dk Slaa kuliomba radhi Bunge, huku Chadema nayo ikimtaja Nape kwamba ni mtuhumiwa wa ufisadi wa EPA uliofanyika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambapo Sh133 bilioni zilikwapuliwa. 
Tuhuma hizo kutoka kila upande, zimekuja baada ya Nape kutaja alichokiita unafiki wa Dk Slaa kwa kushinikiza kulipwa mshahara wa Sh7.5 milioni na Chadema, wakati alikataa mshahara wa Sh7 milioni alipokuwa mbunge akidai ni mkubwa na uliwanyonya Watanzania.

Katika mkutano wake wa hadhara siku hiyo Nape alimtaka Dk Slaa kuliomba radhi Bunge na wabunge kwa kile alichoeleza kuwa alipokuwa Mbunge wa Karatu, alichochea chuki kwa wananchi dhidi ya taasisi hiyo.
"Najua Chadema watakuwa wanajibu, lakini nasema msimamo wangu uko mbele zaidi kwamba Dk Slaa aliombe radhi Bunge na wabunge, kwani alichochea chuki kwa wananchi dhidi ya Bunge, halafu yeye anakuja kuchukua mshahara zaidi ya ule aliojidai kuukataa. Huu ni unafiki," alisisitiza Nape.

Nape alisema Dk Slaa ni Padre hivyo pia alipaswa kuungama kwa Mungu kwa kutokuwa mkweli ndani ya dhamira yake."Bahati nzuri Dk Slaa ni Padre, namshauri pia amwombe radhi Mungu, kwani amekuwa akipita mitaani kupandikiza chuki miongoni mwa Watanzania kumbe naye hana maadili yoyote," aliongeza Nape.

Wakati Nape akitoa shutuma hizo dhidi ya Dk Slaa, siku hiyo Mei 12, Chadema aliitisha mkutano na waandishi wa habari ambako licha ya kufafanua kuhusu mshahara wa Katibu Mkuu huyo na ununuzi wa magari, ilimwita Nape kuwa ni 'Vuvuzela' na kwamba hana sifa ya kuinyooshea kidole Chadema.

“Tuna ushahidi wa kutosha kuwa mmoja wa watu walionufaika na fedha za EPA kupitia kwa Jeetu Patel ambaye ameeleza vizuri jambo hili katika maelezo yake mbele ya kamati ya Rais,” alisema Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Chadema, Anthony Komu

AMAZING,WAS SITA THE FOUNDER OF CCJ?

Mpendazoe aanika walioanzisha CCJ  Send to a friend
Monday, 16 May 2011 21:39
0diggsdigg
Kada wa Chadema, Fred Mpendazoe akihutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa National Housing mjini Njombe.Picha na Edwin Mjwahuzi
Waandishi Wetu
KADA wa Chadema, Fred Mpendazoe amewataja mawaziri wawili wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, mbunge mmoja wa CCM na makada wengine wawili wa chama hicho tawala kuwa ni miongoni mwa watu waliokuwa katika harakati za kukihama na kujiunga na CCJ.Mpendazoe ambaye alikuwa kada wa kwanza wa CCM kuhamia CCJ wakati huo akiwa Mbunge wa Kishapu, aliwataja waanzilishi hao wa CCJ kuwa ni pamoja na Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta na Naibu Waziri mmoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye.

Kwa mujibu wa Mpendazoe, katika kundi hilo pia wamo kada wa Jumuia ya Umoja wa Vijana wa CCM na mbunge mmoja kutoka Mkoa wa Mbeya. Hatukuandika majina ya baadhi ya viongozi waliotajwa kwa sababu hatukufanikiwa kuwapata kujibu tuhuma hizo.Hata hivyo, Sitta alipipogiwa simu alisema asingeweza kuzungumza lolote kuhusu madai hayo akisema anasubiri kusoma alichosema Mpendazoe.

Mpendazoe aliwataja makada hao jana wakati akihutubia umati uliokusanyika kwenye Viwanja vya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Njombe Mjini katika mkutano wa hadhara wa Chadema."Nilipoondoka CCM mimi nilikuwa ni mmoja wa waanzilishi wa CCJ, lakini wengine walikuwa hawajulikani na leo nitawataja hao wengine kwa kuwa CCM inajidai kujivua gamba ili kuwadanganya wananchi," alisema Mpendazoe.Alisema hao aliowataja ndiyo waliotaka kukihama CCM, lakini walibaki si kwa ajili ya maslahi ya Taifa, bali ni kwa maslahi yao binafsi.

"Sitta na (makada wengine) wameingia katika Serikali ya Rais Jakaya Kikwete, lakini ni wasaliti na Serikali ya CCM ya sasa haiwezi kuwasaidia Watanzania," alisema na kuongeza:
"Wamevaa ngozi ya kondoo kwa kupinga ufisadi kwa maslahi yao, lakini leo bado wako pale."
Akizungumza katika mkutano huo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema viongozi wa CCM ni wanafiki na ndiyo maana, hawaelewi wanachokifanya zaidi ya kuwadanganya wananchi.

Aliitaka serikali kuacha ubabaishaji na kuchukua hatua zinazoweza kuwaletea wananchi maendeleo na kuliinua Taifa.
Dk Slaa alitumia nafasi hiyo kumshambulia Spika wa Bunge, Anne Makinda. Aliwahoji wakazi wa Njombe waliohudhuria mkutano huo kama uspika wake unawasaidia chochote na wao wakajibu kwa kupiga kilele: "Hakuna chochote."

"Nilipokuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa, niliwahi kukagua Njombe na miradi yenu nikagundua kuwa hakuna maendeleo yoyote ikiwamo kituo cha basi cha Njombe ambacho hakifai," alisema Dk Slaa.
Alisema kutokana na kuendelea kumpigia kura kwa muda mrefu, wananchi hao wataendelea kunyanyasika na familia ya mbunge wao itaendelea kuneemeka kwa kutumia mgongo wao.

Mukama: Chadema kiache ubabaishaji
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilson Mukama amekitaka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuacha kile alichodai kuwadanganya wananchi kwamba CCM kujivua gamba si kitu akisema hatua hiyo imefikiwa kukiimarisha chama baada ya kutambua kuwa bila hivyo nchi itayumba. Mukama alisema hayo kwa nyakati tofauti juzi na jana katika Kijiji cha Kibara, wilayani Bunda na katika Kijiji cha Kaburabura, wilayani Musoma katika mikutano ya hadhara, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku nane mkoani Mara.

Alisema CCM kimetumia dhana hiyo ya kujivua gamba ili kiweze kurudi kwenye misingi imara, ikiwa ni pamoja na kufanya mabadiliko makubwa, hali ambayo itakiweka kwenye mstari unaotakiwa ambao lengo lake ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata maendeleo na huduma zote muhimu.
Alisema anawashangaa wapinzani wanaotumia muda mrefu kujadili falsafa ya kujivua gamba na kuhoji uwezo wao katika kutekeleza miradi ya maendeleo.

Alisema amesikitishwa na kauli ya viongozi wa Chadema kwamba kuna uwezekano Rais Kikwete kuondoka madarakani kabla ya 2015 kwa kutolea mfano wa Waziri Mkuu wa Japan aliyeondolewa madarakani.
Alifafanua kuwa viongozi wa Chadema wanatakiwa kufanya uchunguzi kabla ya kutoa matamko kwa maelezo kuwa Waziri Mkuu wa Japan hawezi kufananishwa na Rais Jakaya Kikwete kwa vile aliwekwa madarakani na Bunge wakati Rais alichaguliwa na wananchi.

Alisema kuwa, hata Mwalimu Julius Nyerere enzi za uhai wake aliwahi kutamka kuwa, bila CCM ya kweli nchi itayumba na kwamba ndiyo maana chama hicho kimeamua kutumia dhana hiyo ya kujivua gamba ili kiweze kuwa imara na kinachoweza kusimamia maendeleo ya wananchi.

"Tunakiweka katika misingi ya kukiimarisha ili kiwe chombo imara ambacho kweli kinaweza kusimamia maendeleo katika maeneo yetu tunayoishi. Sasa hawa Chadema wameichukua dhana hiyo ya kujivua gamba visivyo kabisa," alisema.

Alisema hiyo inatokana na viongozi wa Chadema kuwa na tabia ya kurukia mambo bila kuyafanyia uchunguzi na kwamba wameichukua dhana hiyo visivyo na kuendelea kuwarubuni wananchi ili wakichukie CCM na serikali yao... "Hawa wanataka kwenda Ikulu kwa maneno ya udanganyifu kabisa na maandamano yasiyokuwa na msingi wowote."
Pia alisema kuwa CCM haiwezi kufa kama upinzani wanavyoendelea kuwaambia wananchi, kwani ni chama kikubwa, taasisi na si kampuni ya kibiashara.

Aidha, Mukama amekiponda Chadema ambacho kimekuwa kikidai kwamba CCM imekumbatia wafanyabiashara na kueleza kuwa Chadema ndicho kinayofanya hivyo."Sasa watu wanaokumbatia sera ambazo mwalimu alikuwa anazipinga, eti ndio wanakwenda kwenye kaburi pale wanasema tunakuomba leo utusikilize tuweze kutawala nchi hii kidogo," alisema.

Alisema CCM kina matajiri wachache ambao wanataka kukitumia kwa ajili ya kujinufaisha na kuonya kuwa wafanyabiashara ambao maadili yao hayaendani na chama chao wataondolewa na kuwekwa pembeni mara moja.

Amewataka wakuu wa wilaya nchini na viongozi wa CCM, kusimama imara na kuhakikisha fedha za miradi mbalimbali zinazoletwa na Serikali katika halmashauri husika, zinafanya kazi iliyokusudiwa na si kuishia kwenye mikono ya wajanja wachache.
Alisema kuwa ni lazima wakuu wa wilaya pamoja na viongozi wa chama hicho watekeleze wajibu wao ipasavyo wa kusimamia fedha za Serikali zinazopelekwa kwenye  halmashauri.Habari hii imeandaliwa na Boniface Meena, Njombe; Ahmed Makongo na Christopher Maregesi, Bunda na Beldina Nyakeke, Musoma Vijijini.

Monday, May 16, 2011

JE KUNA UHUSIANO KATI YA UFAULU WA WANAFUNZI NA UPATIKANAJI WA CHAKULA MASHULENI?

Weekend imeenda pouwa sana mtu mzima kwizera! kuhusu mada inayohusanisha chakula na ufaulu wa wanafunzi mashuleni,ni kweli kuna uhusiano mkubwa kati ya ufaulu wa wanafunzi na chakula,vijijini mara nyingi vyakula huwepo kwa wingi wakati wa mavuno lakini msimu wa mavuno ukishapita wanakijiji wengi hukubwa na tatizo la chakula kwa kuwa hawana elimu ya uhifadhi wa chakula,lakini pia mafuno wanakijiji wanayopata hayawawezeshi kufikia msimu mwingine wa mavuno. Hivyo,sehemu nyingi za vijijini wanafunzi wanafunzi hukubwa na njaa,mwanafunzi mwenye njaa hukosa hamasa ya kujifunza kwa bidii kwa kuwa muda mwingi watakuwa wanfikiria namna ya kukabili njaa inayowakumba badala ya kufuatilia yale wanayofundishwa na walimu mashuleni.Ndugu yangu Kwizera mimi mwenyewe ni mhanga wa kutokufaulu vizuri mitihani yangu ya primary school kwa tatizo la njaa,nakumbuka mimi na wenzangu tulikuwa tunakabiri njaa zetu kwa kwenda kuwasidia wafanya biashara kusukuma baiskeli zao zilizobeba mizigo kupanda mlima RUSUNWE wilayani KASULU kuelekea Burundi,na kisha kupatiwa fedha kiduchu ambazo tuliweza kunnua chakula, hali hiyo ilituathiri sana kitaaluma kwa kuwa kazi za kusukuma baiskeli kupanda mlima RUSUNWE tulikuwa tunaifanya wakati wa masomo. Hali hiyo ingeweza kuzuwilika kama tungekuwa tunapewa chakula mashuleni maana tungeelekeza mawazo yetu na fikira zetu katika masomo badala ya kuelekeza mawazo yetu na fikra zetu katika kusukuma baiskeli kupandisha mlima RUSUNWE ili kupata fedha za kununulia chakula.
Hivyo kama kutakuwapo mpango unaotekelezeka wa kuwapatia wanafunzi wa shule zetu za msingi chakula walau cha mchana,licha ya kuongeza ufaulu wa wanafunzi lakini pia mpango wa chakula mashuleni utaweza kuongeza mahudhurio ya wanafunzi mashuleni,kupunguza utoro reja reja wa wanafunzi mashuleni na kuongeza molari za wanafunzi kujifunza na kufuatilia kile wanachofundishwa madarasani.
Mimi ni LEONARD KILAMHAMA

JE NI KWELI NCHI HAITAWALIKI?


Dk. Slaa:
[Image] KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk.Willbrod Slaa, sasa ametamka rasmi kwamba nchi haitatawalika, kwani chama chake hakiko tayari kuona Watanzania wakiendelea kuwa katika hali ngumu ya maisha, huku Chama cha Mapinduzi (CCM) kikitekeleza mkakati wa siri wa kuwajaza matumaini hewa badala ya kutatua matatizo yao.
Dk. Slaa ameeleza kuunasa waraka wa siri wa CCM ambao ndani yake chama hicho kimekiri waziwazi kupoteza ladha kwa umma, huku mkakati pekee wa kujinusuru ukielezwa kuwa ni kubadili sura za viongozi wa chama hicho ili kuwajengea matumaini mapya Watanzania.
Kwa mujibu wa Dk.Slaa, waraka huo wenye mhuri mkubwa wa neno “siri” uliandaliwa na baadhi ya wataalam wa CCM waliofanya tathmini ya hali ya chama chao kisiasa na kuuwasilisha kwa viongozi wa juu wa chama hicho ambao tayari wameanza kuufanyia utekelezaji wa “kujivua gamba” kwa lengo la kuwapa matumaini hewa wananchi.
Dk. Slaa alifichua siri za waraka huo wakati akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika viwanja wa shule ya sekondari Msakila mjini Sumbawanga ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara ya chama hicho mkoani Rukwa, baada ya kuutikisa mkoa wa Mbeya kwa maandamano na mikutano ya hadhara kwa siku tatu mfululizo.
Alisema katika waraka huo CCM imekiri kuwa haikubaliki kwa Watanzania na kwamba iliporomoka sana katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana, lakini badala ya kurejesha tunu za taifa kama uadilifu, upendo, amani, umoja na uwajibikaji wa kuleta maendeleo yatakayoirejeshea imani toka kwa wananchi, chama hicho kimeamua kubadili tu sura za viongozi wake wa kitaifa.
“CHADEMA tunafanya mambo kwa utafiti. CCM wana waraka wa siri uliowafanya wajivue gamba lakini wanaume tayari tumeshaunasa, tena una mhuri mkubwa wa neno siri lakini tayari tunao. Katika waraka wao CCM wamekiri wenyewe kwamba hawakubaliki tena kwa Watanzania walio wengi, wamekiri wenyewe kwamba wamepoteza ladha kwa wananchi. Wamekiri wenyewe katika waraka huo, kwamba hawakubaliki kwa sababu wameacha siasa ya ujamaa na kujitegemea.
“Na ni kweli wameacha siasa ya ujamaa na kujitegemea. Mabilioni ya Kikwete sio ujamaa na kujitegemea. Mabilioni ya mtoto wake, anayeitwa Ridhawani nayo ni ushahidi tosha kuwa wameacha ujamaa na kujitegemea kama walivyokiri wenyewe kwenye waraka wao.
“Tatizo lao ni kwamba badala ya kuacha ufisadi na kurejesha tunu za taifa kama uadilifu, upendo, amani, umoja na uwajibikaji…badala ya kupunguza kodi kwenye mafuta, sukari, saruji, na bidhaa nyingine, ili wajijengee uhalali kwa umma, wao katika waraka wao wameamua wabadili sura za viongozi kwa kujivua gamba. Hawataji popote kwenye waraka wao jinsi watakavyoboresha maisha yenu,” alisema Dk.Slaa na kuongeza.
“CHADEMA hatuko tayari kuona Watanzania wakiteseka huku CCM yenye serikali badala ya kuchukua hatua za dharura kuwanusuru, inapanga kuendelea kuwadanganya kwa kubadili viongozi kwa kujivua gamba. Arusha nilitoa hotuba moja wakasema Dk. Slaa mchochezi…sasa leo nawatuma usalama wa taifa nendeni mkawaambie CCM kwamba nchi haitatawalika. Wasipochukua hatua CHADEMA itachukua hatua…kama Watanzania hawajui wanakula nini, wanavaa nini, watoto wao wanasoma vipi, wanatibiwa vipi, basi nchi hii haitatawalika.”
Alisisitiza kuwa nchi haitatawalika kwani kila kukicha ufisadi unakithiri badala ya kupungua huku akibainisha kuwa hata ripoti ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali ya hivi karibuni imeonyesha katika wizara moja pekee, wizara ya fedha na uchumi, jumla ya sh bilioni 365 ziliibiwa wakati zingeweza kutumika kunusuru maisha ya Watanzania.
Mwenyekiti wa chama hicho akihutubia wakazi hao wa Sumbawanga, alisema kupitia maandamano na mikutano ya hadhara inayofanywa na chama hicho nchi nzima, CHADEMA imedhamiria kuamsha nguvu ya umma katika kuishinikiza serikali kupunguza kodi kwenye bidhaa na huduma muhimu ili bei zishuke na maisha ya wananchi yawe nafuu.
Alisema kupanda kwa gharama za maisha kumesababishwa na ufisadi na sera mbovu za serikali ya CCM, ambayo inawatoza kodi kubwa wananchi maskini kupitia bidhaa na huduma mbalimbali huku serikali hiyo hiyo ikiwasemehe kodi wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa.
Katika hotuba yake hiyo iliyoonekana dhahiri kuwateka wakazi wa Sumbawanga, Mbowe alisema CHADEMA haipingi watu kulipa kodi, lakini haiko tayari kuona Watanzania maskini wakilipishwa kodi kubwa, huku serikali ikishindwa kuwapa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Akifafanua zaidi historia ya kodi na athari zake kwa wananchi, kiongozi huyo wa kambi ya upinzani bungeni alisema baada ya serikali ya Rais Benjamin Mkapa kuondoa kodi ya maendeleo, ilileta kodi nyingine ya Ongezeko la Thamani (VAT), ambayo wananchi wote sasa wanatozwa kila wanaponunua bidhaa dukani na kulipia huduma mbalimbali kama usafiri.
“Nyerere alikuwa akikusanya kodi bilioni saba kwa mwezi, mzee Mwinyi aliondoka akiwa anakusanya kodi ya bilioni 27, akaja Mkapa yeye hadi anaondoka alikuwa anakusanya bilioni 300 na ushei. Baada ya hapo akaja Kikwete, yeye anakusanya bilioni 420 kwa mwezi. Anakusanya fedha nyingi kwa sababu kuna kodi ya VAT iliyoongezwa katika bei za bidhaa na huduma mnazolipia. Mnalipa kodi bila kujua, mnalipa kodi kwenye mafuta, kwenye soda, usafiri, sukari, sanda, pipi...kila kitu kodi kodi kodi,” alisema Mbowe na kuongeza.
“Kwa sababu ya kodi ya VAT, leo katika nchi hii kila mwananchi analipa kodi, mtoto, mjane, kijana, mwanafunzi wote wanalipa kodi …hadi maiti nazo zinalipiwa kodi mnaponunua sanda kwa ajili ya kuzikia. ...lakini kodi hizo zinaishia kustawisha maisha ya vigogo wa serikali, wananchi wa Sumbawanga na Watanzania wengine wanazidi kuwa maskini, mmefikia mahali hamuwezi hata kununua kilo moja ya sukari kwa ajili ya chai au kilo ya mafuta mnaanza kupimiwa kwenye vifuko vya shilingi mia moja...hali ya hatari hii, taifa lina msiba wa umaskini, wananchi wanalia kila mahali sasa, kila kona ya nchi,” alisema.
Akitoa mfano wa jinsi kodi inavyofanya bei za vitu kuwa juu, Mbowe alisema katika kila Sh elfu moja anayotumia Mtanzania kununua bidhaa sokoni au dukani au kulipia huduma, serikali humkata kodi ya wastani wa sh 500 hadi 600, kodi ambayo kama ikiondolewa gharama za maisha zitakuwa nafuu.
“Soda moja inapotoka kiwandani inapaswa kuuzwa kwa Sh 150 lakini kwa sababu ya kodi iliyowekwa na CCM kuanzia viwandani soda moja mnauziwa kwa sh 500 hadi 600. Kila mnaponunua mfuko mmoja wa cement mnakatwa kodi ya Sh 7,500 ambayo kama ikiondolewa au kupunguzwa bei ya saruji itakuwa nafuu na wengi mtaweza kujenga.
“Kila chupa moja ya bia unayonunua unakatwa kodi ya sh 800. Ndiyo maana Kikwete kwa mwezi anakusanya bilioni 420 kutoka kwenu, lakini maendeleo hakuna. CHADEMA tutakomaa na suala la gharama za maisha ndani na nje ya bunge mpaka Watanzania maisha yao yawe nafuu,” alisema Mbowe na kushangiliwa.
Katika mkutano huo pia Mbowe aliwahamasisha wakazi wa Sumbawanga kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kupata Katiba mpya na kushinikiza katiba hiyo itokane na wananchi na sio itokane kwa utashi na maamuzi ya Rais Kikwete kama ilivyopendekezwa katika Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba.
Naye Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe akiwahutubia wananchi hao alisema kwa nafasi yake kama Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, ameagizwa na chama chake kuwasilisha bajeti mbadala katika bunge lijalo la bajeti ambayo pamoja na mambo mengine itashinikiza serikali kupunguza kodi kwenye mafuta ya petroli na dizeli kwa asilimia 50 ili yauzwe kwa angalau Shs 1665 kwa lita kutoka kwenye bei ya zaidi ya sh 2000 ya sasa.
“Gharama za maisha ziko juu kwa sababu ya mfumuko wa bei za mafuta ambao unasababisha na kodi. Bei ya mafuta ikishuka hadi 1,665 gharama za usafiri na bei za sukari na vyakula nazo zitakuwa angalau. Tutawataka waondoe kodi kwenye mafuta halafu wapunguze misahamaha ya kodi wanayoitoa kwa wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa … serikali inasemehe bilioni 635 za kodi zinazopaswa kulipwa na matajiri, sasa hizo zikafidie kwenye mafuta baada ya kupunguza kodi. Wakikataa watakiona cha moto, tutafanya maandamano ndani na nje ya bunge mpaka kieleweke,” alisema Zitto.

Friday, May 13, 2011

VIONGOZI WETU SI VYEMA KUINGILIA MAJUKUMU YA MAAFISA HABARI,HESHIMUNI WEREDI WA WANAHABARI

Ndimbo ajiuzuru Simba  Send to a friend
Thursday, 12 May 2011 21:05
Clara Alphonce
ALIYEKUWA Afisa Habari wa Simba, Clifford Ndimbo jana alitangaza kujiuzuru wadhifa wake kwa madai kuwa hashirikishwi kwa chochote na viongozi wake waliopo madarakani.

Ndimbo alijiriwa kuwa msemaji wa Simba ikiwa ni kigezo kimoja wapo cha kanuni za TFF na FIFA cha kuzitaka klabu zote za Ligi Kuu kuwa na vitengo vya Afisa Habari.

Akizungumza kwenye mkutano na wanahabri Ndimbo alisema ameamua kujiuzuru mwenyewe na wala hajashawishiwa na mtu yoyote ila ameamua hivyo kwa sababu viongozi wa Simba wamekuwa hawamthamini kwa kazi yake ya Afisa Habari wa klabu.

Alisema uongozi wa Simba hivi sasa chini ya Mwenyekiti Ismail Aden Rage umekuwa ukimbagua kwa kutokumshirikisha kwa kitu chochote ikiwemo safari za timu na kufanya mikutano bila kumshirikisha na mambo mengine mengi tofauti na mkataba wake unavyoeleza.

Alisema ameamua kukatisha mkataba wake wa miaka miwili alioingia na klabu hiyo toka wakina Rage waingie madarakani  japo kipindi cha miezi tisa amekuwa akifanya kazi kwa hali ngumu, lakini alipokuwa akiwahoji viongozi wake walikuwa wakimuahidi watamtekelezea.

Alisema barua hiyo aliyoiwakilisha jana kwa uongozi Simba itakuwa ni barua ya pili baada ya ile ya awali aliyoandika Aprili 5, 2011 kutokubaliwa baada ya kikao na baadhi ya wajumbe wa kamati ya utendaji na Katibu Mkuu wa klabu na kushauriana mambo kadhaa ambayo yalimrudisha kuendelea na kazi.

Alisema ameamua kujiuzuru baada ya kuona kuwa hakuna utekelezaji wowote wa yale waliyokubaliana katika kikao chao walichokaa Jumatatu Machi 28, 2011 na kamati ya utendaji na kamati ya fedha makao makuu ya klabu Simba kuanzia saa 7 mchana.

Alisema hata hivyo anashukuru kwa ushirikiano aliopewa na wanachama wa Simba, wafanyakazi na baadhi ya viongozi wa Simba kwa kipindi chote kwani amepata uzoefu mkubwa katika soka la Tanzania na klabu mbali mbali kupitia Simba ambalo kwa upande wake anaamini ni somo kubwa.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #6 Kifaru 2011-05-13 15:04
Niliota hili lingetokea na limetokea.
Quote
 
 
0 #5 LUGEYE 2011-05-13 13:02
Mh Rage kweli umezidi maana kila kwenye taarifa za habari za michezo we ndo msemaji hv uoni aibu sasa nini kazi afisa wa habari?mlimwajiri kwa kaz ipi?Samata kauzwa we ndo umetoa habari sijui nan mwingine kauzwa we ndo msemaji!hv hujui mipaka ya kaz yako mh?hv hamuwaoni wenzenu wa ulaya jaman?Abromovich wa chelsea mmiliki wa timu tangu mwaka uanze umemuona au kumsikia mara ngapi kwenye tv au press conference?yeye ni mtu wa kutoa order tu wako watendaji aliowaajiri sio kila kitu yeye hata kama ni boss,usilete siasa na mpira plz!jifunze kwa Berluscon wa Italia.
Quote
 
 
+1 #4 HAMAD SIMBA DAMU 2011-05-13 09:58
RAGE NI MWANASIASA, SAYANSI YAKE NDIYO HIYO YA KUMUONA KILA SIKU NA WAANDISHI WA HABARI WAKATI MSEMAJI WA KLABU YUPO NA ANALIPWA MSHAHARA HII NI AJABU,,,!!RAGE USITUHARIBIE KLABU YETU KAMA ULIVOVURUGA FAT, ENDELEA NA UBUNGE NA DHAMANA TULIYOKUPA SIYO YA KUMILIKI KILA KITU MWISHOWE TUTAAMBIWA HATA MINUTES ZA KIKAO UNATAKA UWE UNACHUKUA WEWE...SOKA LA SASA NI LA KISOMI HUENDESHWA KISOMI KWA KILA MMOJA KUSIMAMIA IDARA YAKE...
Quote
 
 
0 #3 Mosses 2011-05-13 08:25
Kaka Ndimbo ndio soka la bongo viongozi wetu wako kimaslahi zaidi.Nafikiri kungekuwa na chuo cha kuwapa mafunzo viongozi wote wanaotaka kuongoza vilabu,ama wangepata basi nafasi ya kwenda hata kwa chini hizi za bara la ulaya nakujifunza ni kwa namna gani watu wanafanya kazi kama team work
Quote
 
 
0 #2 Gulio 2011-05-13 08:22
Kwa kweli hiyo ni dalili mbaya wanasimba - tuliambiwa mambo yataendeshwa kisayansi - sayansi iko wapi hapa? - kwa nini mtumie waandishi wa habari badala ya kuyamaliza ndani kwa ndani? Acheni mambo ya siasa ndani ya klabu tutaambulia aibu badala ya mafanikio
Quote
 
 
0 #1 A 2011-05-13 05:50
Mbona hivo tena Simba au ndio mnataka kuwa maadui kicheko? Huu sio hata kidogo wakati wa malumbano bali ni wakati wakujipanga upya na kuirejesha Simba katika ahadi yake. Kwanini hamzitatui tafauti zenu kwa njia ya busara na ukimya na hivo nndivo wanavofanya waungwana. Simba inasifika kwa ustaarabu. Madhali kazi ipo na kila mmoja anataka kuona maendeleo, lazima kuwepo tafauti za maoni kwa lengo la kufikia mafanikio wala sio mtafaruki. Jamani jeepusheni na mambo ambayo yatayotupeleka kubaya. Chondeni hatutaki kusikia mijadala ya kubomowa tunataka mijadala ya kujenga. Tunapingia magazetini tunataka kufurahi na wala hatutaki kulia. Simba ina viongozi wenye ujuzi na waliosoma na msiwache mambo kufika hadi hiyo.
Quote
 
This little and beautiful girl was found 
uswahili,mburahati-dar es salaam

sometimes our reasoning and thinking
may be restricted by the environment
people we are enbraced as our friends

The failure of  previous set goal provides
an opportunities to plan for new goals

Net-working has power in recent world
only if u do it with a plan

Clean enviroment should be enhanced
for our health and proper thinking
because dirty environment results into
 unproper thinking

PENYE UKWELI,UONGO HUJITENGA! CCM KAMA HAINA JIPYA HIVI?

Marando, Nape ni jino kwa jino  Send to a friend
Thursday, 12 May 2011 22:06
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Nape Nnauye
Ramadhan Semtawa na Elias Msuya
CCM na Chadema, vimeendeleza siasa za jino kwa jino kufuatia viongozi wake kuzidi kurushiana makombora yaliyobeba tuhuma ndani yake.Jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alimtaka Dk Willibrod Slaa ambaye ni Katibu Mkuu wa Chadema aliombe radhi Bunge, huku Chadema nayo ikimtaja Nape kwamba ni mtuhumiwa wa ufisadi wa EPA uliofanyika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambapo Sh133 bilioni zilikwapuliwa. 

Tuhuma hizo kutoka kila upande, ambazo sawa na siasa za jino kwa jino, zimekuja baada ya Nape kutaja alichokiita unafiki wa Dk Slaa kwa kushinikiza kulipwa mshahara wa Sh7.5 milioni na Chadema, wakati alikataa mshahara wa Sh7 milioni alipokuwa mbunge akidai ni mkubwa na uliwanyonya Watanzania.Vyama hivyo jana kwa nyakati tofauti, kila kimoja kiliongeza mashambulizi dhidi ya kingine, ambapo Nape alikwenda mbali zaidi akimtaka Dk Slaa aliombe radhi Bunge na wabunge kwa alichoeleza kuwa Dk Slaa alipokuwa Mbunge wa Karatu, alichochea chuki kwa wananchi dhidi ya taasisi hiyo.

"Najua Chadema watakuwa wanajibu, lakini nasema msimamo wangu uko mbele zaidi kwamba Dk Slaa aliombe radhi Bunge na wabunge, kwani alichochea chuki kwa wananchi dhidi ya Bunge, halafu yeye anakuja kuchukua mshahara zaidi ya ule aliojidai kuukataa. Huu ni unafiki," alisisitiza Nape.Nape alisema Dk Slaa ni Padre hivyo pia alipaswa kuungama kwa Mungu kwa kutokuwa mkweli ndani ya dhamira yake."Bahati nzuri Dk Slaa ni Padre, namshauri pia amuombe radhi Mungu, kwani amekuwa akipita mitaani kupandikiza chuki miongoni mwa Watanzania kumbe naye hana maadili yoyote," aliongeza Nape.

Alifafanua kwamba mshahara anaolipwa Dk Slaa ni kodi ya wananchi inayotokana na ruzuku, hivyo ni matumizi mabaya kumpa mshahara mkubwa kama huo wakati aliukataa akiwa mbunge.Kama alivyofanya katika mkutano wa kwanza aliofanya Kata ya Ulugu jimboni Iramba, Nape alisema ataendeleza mashambulizi dhidi ya Dk Slaa katika mikutano yake yote itakayofanyika mkoani Singida ili kuweka wazi maovu ya kiongozi huyo kwa kile alichokiita uchonganishi.

"Hapa naelekea Iramba Mashariki, lakini ninachosema ni kwamba, nitaendelea kuwaeleza Watanzania unafiki wa Dk Slaa. Hatutaki viongozi wanaoeneza chuki wakati wao wenyewe hawana maadili yoyote,"aliongeza.
Alisema ndani ya Chadema wapo baadhi ya watu wanalipwa kiasi cha fedha ambacho ni kidogo na wanaishi kwa shida kubwa hivyo, kama Dk Slaa ni mwadilifu awaangalie hao.

MJumbe wa kamati kuu ya Chadema Mabere Marando akionyesha ripoti ya fedha ya chama hicho kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana
Chadema waja juu
Lakini mkutano na waandishi wa habari jana, licha ya kufafanua kuhusu mshahara wa Katibu Mkuu wake, Dk Slaa na ununuzi wa magari, Chadema jana  ilimuita Nape kuwa ni 'Vuvuzela' na kwamba hana sifa ya kuinyooshea kidole Chadema. “Tuna ushahidi wa kutosha kuwa mmoja wa watu walionufaika na fedha za EPA kupitia kwa Jeetu Patel ambaye ameeleza vizuri jambo hili katika maelezo yake mbele ya kamati ya Rais,” alisema Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Chadema, Anthony Komu.
Naye Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Mabere Marando alidai kuwa Nape aliwahi kuomba kugombea ubunge kupitia Chadema baada ya kushindwa kupata nafasi hiyo kupitia CCM, lakini wakamtosa kwa kuwa hakuwa na sifa.

“Nilikuwapo kwenye kikao cha kumjadili Nape, tukaona kuwa hana sifa kumzidi John Mnyika ambaye sasa ni mbunge” alisema Marando. Lakini akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu, Nape aliwataka Chadema kutoa ushahidi unaoonyesha kuwa alihusika na ufisadi wa EPA.

“Atoe ushahidi hadharani, unajua hawa watu ni waongo, hata Watanzania watawashangaa,” alisema Nape.
Kuhusu suala la kuhamia katika chama hicho, Nape alisema: “Tena uandike kabisa, mimi ndiyo ninao ushahidi wa wao kunitaka nikagombee kupitia chama chao nikakataa, kwa sababu siwezi kuhamia kwenye chama cha Wachagga, kile ni chama cha ukoo,” alisema Nape.

Mishahara ya Makatibu Wakuu
Akifafanua mshahara wa Dk Slaa, Komu alisema kuwa Katibu wake hawajawahi kuomba, kushinikiza wala kuchagiza kulipwa kiasi cha Sh 7.5 milioni kama inavyodaiwa bali analipwa Sh 1,725,000 milioni wakati mbunge analipwa Sh 2,305,000 kabla ya kukatwa kodi.
Alifafanua kuwa Dk Slaa pia hulipwa Sh900,000 za mafuta kwa ajili ya kwenda na kurudi ofisini. Vingine ni malipo ya nyumba, mawasiliano na uwajibikaji na hivyo kuufanya mshahara wake kufikia Sh7,174,000 kwa mwezi.

“Sekretarieti ya Kamati Kuu ilipeleka pendekezo hilo katika vikao vyake vya Kamati Kuu na Baraza Kuu na pendekezo hilo likapitishwa kwa njia ya uwazi na likaingizwa katika mpango kazi wa chama,”  alisema Komu.
Naye Mabere Marando alikituhumu CCM kuwa kinamlipa Katibu Mkuu wao Sh 11 milioni akisema:  “CCM wanapigia kelele mshahara wa Dk Slaa, mbona Mukama (Wilson) analipwa Sh11 milioni?. Mbona Rais Jakaya Kikwete analipwa posho nyingi tu? Ofisi yake iko Dodoma, lakini akienda huko analipwa posho, akirudi Dar es Salaam analipwa,” alisema Marando.

 Alipoulizwa na Mwananchi kuhusu madai ya Marando, Mukama alikataa kutaja mshahara wake akisema kuwa ni siri yake.
 “Mimi leo ndiyo natimiza mwezi mmoja tangu niingine ofisini, hata mshahara wenyewe sijauona. Mshahara ni siri yangu mwenyewe, nimeingia hapa baada ya kustaafu kwa hiyo ndiyo hivyo, naomba msiniingize kwenye hizo ‘debate’ (malumbano)” alisema Mukama.

Lakini akijibu hoja hiyo, Nape alisema kuwa Mukama analipwa mshahara kulingana na daraja la viongozi na hurekebishwa kama watendaji wengine serikalini.
“Katibu Mkuu wetu analipwa Sh1.5 milioni na hukatwa kodi. Vilevile hulipwa posho isiyokatwa kodi ya Sh300,000. Hayo mengine ya usafiri ni mambo ya kawaida tu. Usafiri anao na hulipiwa umeme wa LUKU na nyumba. Siyo suala la kificho hilo,” alisema Nape.

Mafuso ya Chadema
Wakijibu hoja ya Nape kuwa Chadema kimenunua magari chakavu, walikanusha wakisema kuwa magari hayo licha ya kutokuwa chakavu, siyo magari ya kawaida bali ni mitambo maalumu ya uenezi.

“Katika magari hayo kuna vipaza sauti (Public addressing system 3 sets) zenye thamani ya dola za Marekani 148,000 (Sh 222 milioni), jenereta tatu kila moja Sh15.5 milioni sawa na Sh47,000,000,” alifafanua Komu.

Naye Marando alisema kuwa chama ndiyo kilimwomba Mwenyekiti Freeman Mbowe awauzie magari hayo ndipo akakubali. “Mimi mwenyewe nilihusika kumwomba Mbowe atupe magari yale, akakubali. Baada ya hapo Kamati Kuu iliunda kamati ya watu wanne chini ya makamu mwenyekiti Zanzibar Mohamed Issa kumwomba mwenyekiti akiachie chama magari hayo.

Naye Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Profesa Abdallah Safari alisema kuwa CCM inatumia ujinga wa Watanzania kama mtaji wake na kuwataka Watanzania kutoyumbishwa na propaganda za CCM.