Saturday, March 19, 2011

KANISA KATORIKI HAIFUSIANI NA CHADEMA

KANISA KATORIKI HAIFUSIANI NA CHADEMA  Send to a friend
Saturday, 19 March 2011 09:37
0diggsdigg
Israel Mgussi, Dodoma
RAIS wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Mkuu Yuda Thadeus Ruwa'ichi amewaponda wanasiasa wanaotaka kuwafumba mdomo viongozi wa dini nchini wanaokemea rushwa, ufisadi na ukiukwaji wa maadili unaofanywa na baadhi ya viongozi waandamizi wa Serikali na vyama vya siasa.Ruwai'chi ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki, Mwanza pia amewajia juu wanaolihusisha kanisa hilo na ustawi wa Chadema akisema kuwa huo ni uzushi na kuwanyooshea kidole baadhi ya wanaCCM na baadhi ya waandishi wa habari aliosema hawapendi kuchanganua mambo na kuwa na uhakika nayo.

Askofu Ruwai`chi (pichani) alisema Kanisa Katoliki halikiteulii chama chochote cha siasa mgombea na akakipa angalizo CCM akitaka kijidodose juu ya sababu zilizomfanya Dk Willbrod Slaa kukihama na sasa kuonekana kama ni mtu anayekichanganya akili na kutaka iache alichokiita propaganda zenye malengo ya kuwagawa watu katika misingi ya dini.

“Kama Slaa (Dk Willbroad Slaa) alikuwa mwanaCCM akaikimbia. Sasa jifunzeni na kukumbuka historia, CCM wana mchango gani katika hilo la Dk Slaa kuikimbia, wakijibu swali hilo itakuwa vizuri sana," alisema akisisitiza.Askofu Ruwai'chi alisema hayo juzi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Parokia ya Kibaigwa, Dodoma muda mfupi baada ya kumpokea Askofu mteule wa Jimbo Katoliki la Dodoma, Mhashamu Gervas Nyaisonga ambaye atasimikwa rasmi leo mjini Dodoma.

Kuhusu Kanisa Katoliki kudaiwa kuwa limekuwa likikiunga mkono Chadema, Askofu Ruwai'chi alisema kuwa hakuna ukweli wowote kuhusu uvumi huo na kwamba kauli hizo zimekuzwa na baadhi ya wanaCCM ambao wamekosa sera na kukurupuka kutoa kauli zisizo za msingi.

“Hizo ni kauli danganya toto, Kanisa halina chama, ila likibidi kuzungumza litazungumza kama lilivyokuwa likifanya kwa maslahi ya watu wote. Viongozi wa dini wasipozungumza watakuwa hawalitendei haki taifa, wanapaswa kusimamia haki pale inapoonekana kupotoshwa, kanisa halina chama," alisema Askofu huyo.Alisema Chadema ni chama chenye mkusanyiko wa watu wa dini na madhehebu yote, hivyo watu watumie akili zao kutafuta ukweli wa uvumi huo aliosema ni wa kupotosha.

Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki nchini alisema kila mtu ana wajibu wa kuhakikisha kwamba Tanzania inakuwa njema. Akaeleza kushangazwa kwake na wachache wanaotaka kupandikiza mbegu ya udini ambayo alisema kimsingi haipo nchini.

Alisema kauli kama hizo alizoziita za kichochezi pia zinajenga swali kuwa, huenda CCM ni chama cha watu fulani, lakini akasema kuwa wao viongozi wa dini na kanisa kwa ujumla kazi yao ni kuhakikisha maslahi ya taifa hayachezewi wala hayaendi kiholela, akisisitiza kuwa ni haki ya kila mtu kuwa na mtazamo tofauti wa kisiasa muhimu asivunje sheria.
Huku akisisitiza kuwa Tanzania haiendeshwi katika misingi ya falsafa za kidini wala madhehebu, Askofu Ruwai'chi alisema kuwa viongozi wa dini zote nchini wanapaswa kuzungumza na kukemea dosari za kiutendaji na kiuwajibikaji zinazofanywa na baadhi ya viongozi na watumishi wa umma na kwamba bila hivyo itakuwa ni kutowatendea haki Watanzania.

Alisema viongozi wa dini wanapaswa kuzungumzia matatizo yaliopo nchini, kuhamasisha haki, ukweli, amani na kushughulikia maendeleo ya watu wote bila kuogopa wanaowabeza na kutaka kuwaziba midomo kwa kisingizio kuwa wanaingilia Serikali.

“Kuzungumza siyo kuingilia, viongozi wa dini wana wajibu wa kutoa kauli na kuwashuhudia watu mambo mbalimbali yanayotokea katika nchi, wasipoongea watakuwa hawalitendei haki Taifa,” alisema Askofu Mkuu Ruwai'chi.
Askofu Ruwaichi alisema kuwa viongozi wa dini mbali na kutunza dini, lakini wana wajibu mkubwa wa kusimamia mustakabali wa taifa kwa kuhakikisha wanakemea na kusemea mienendo ya kiovu ambayo kwa namna moja au nyingine, inaweza kuvuruga amani na umoja wa kitaifa.

Askofu mteule Nyaisonga atasimikwa leo katika Kanisa Kuu la Paulo wa Msalaba Mjini Dodoma na Rais Jakaya Kikwete pamoja na Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa na viongozi wengine wa dini na madhehebu mbalimbali wanatarajiwa kuhudhuria.
Juzi, mamia waumini wa Kanisa katoliki walijitokeza na kuandamana kwa ajili ya mapokezi ya askofu huyo mteule aliyewasili majira ya saa 7:00 mchana Kibaigwa, Dodoma akitokea Mbeya ambako alikuwa akitumika katika shughuli za kitume akiwa Padri Daraja la Pili.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Saturday, 19 March 2011 09:46
 

Comments 

 
0 #7 elibariki yerald 2011-03-19 11:01
umenena baba askofu..nawapenda viongozi wa dini kama ninyi mnaochana ukweli bila kumung'unya,,na akija leo mhuyo jamaa.mumwambie kwa msisitizo zaidiiiiiiiiiii iii
Quote
 
 
+1 #6 yamasoft 2011-03-19 11:01
Naam, askofu umesema kweli, nafikiri umefika wakati wananchi kutanzua kwa akili zetu bila kuyumbishwa na wanaopandikiza mbegu ya udini katika mambo mbalimbali. Kwa mtazamo wangu CCM wanapaswa kutambua ndani ya vyama vya siasa kikiwamo chenyewe kuna watu wana imani zao tofauti lakini hoja ni kutenganisha shughuli za dini na siasa! Shughuli za siasa zikifanya na mtu mwenye imani furani ni wajibu wao kutambua anasimama pale kama mwanasiasa na si mwana dini furani! Tukumbuke ikiwa tutasahau hili na nje ya hapo hata CCM nayo itakuwa na udini! Watanzania wenzangu akili za kuambiwa tuchanganye na za kwetu! Haipaswi kuliruhusu swala la udini liwe chanzo cha watu wachache kuficha uozo wao wakitutaadhalis ha tukisema tutakuwa na udini! Maendeleo ni matam kwa watu wa dini zote, hivyo pale yanapoitaji kuyapigania ni wajibu wetu sote tukemee hata kama wanaofanya uozo ni wafuasi wa dini zetu!
Quote
 
 
+1 #5 J.G.Z 2011-03-19 10:55
tutafika tu tunapotaka kwenda, lakini sharti la kwanza lazima tumalize hizi changamoto zilizopo mbele yetu.
Quote
 
 
0 #4 Katiba TANGANYIKA 2011-03-19 10:45
Angalau tutapumua sasa!

Tulichoka na mambo ya loliondo. Haya ndio mambo yenyewe, tuendelee na ujenzi wa taifa tuwabane MAFISADI
Quote
 
 
+3 #3 itondo 2011-03-19 10:26
Yangu ni machache tu: Kwa hii hoja ya udini iliyopandikizwa na CCM dhidi ya CHADEMA wakitegemea support ya wananchi kiukweli itawamaliza wao CCM; ni suala la muda tu. CCM hawakujua unaposema CHADEMA (au chama kingine chochote) kina udini, unamaanisha wewe (CCM) pia una-suuport ya hao wa dini nyingine. Hii inaonesha jinsi viongozi wa CCM wanavyokurupuka na kutoa kauli bila kupima athari za kauli hizo. Wao ni ku-focus short term political success. Hii ni hatari.
Quote
 
 
+3 #2 mtanzania hai 2011-03-19 09:59
Hapo ni ukweli Padri anachosema; CCM waache kumtafuta mchawi kwa kuingiza udini kama kimbilio la kukiandama CHADEMA; sera zao za kubebana, undugu, ufamilia, ufisadi, kujuana, urafiki etc katika kuendesha serikali ndio unaowafanya washindwe kufurukuta kwa CHADEMA. Watanzania wa sasa sio wale wa mwaka 1977 wana upeo tofauti sana, wanataka kuona na sio kusimuliwa; MKAPA alionyesha na kuboresha nchi mbona haya mambo hayakuwepo yamekuwa tata hivyo? Maisha yamezidi kuwa ghali na hakuna chochote huku mfumuko wa bei na ufisadi vikizidi kushika chati; Tunaelekea wapi Watanzania? Tuchape kazi na serikali iwajibishwe!
Quote
 
 
+5 #1 mabuwe 2011-03-19 09:58
Mhashamu Askofu Yuda , hapo umenena, rudia tena kuwapasha hayohayo kwenye sherehe maana huko cream yote ya viongozi wenye propaganda chafu itakuwepo.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!

BURIANI DR. REMMY

BURIANI DR. REMMY



Image
Remmy Ongala

Habari Zaidi:

  • Simba ichangamkie mabilioni ya CAF

  • Dede kuhama Mlimani kwenda Msondo ni manufaa kwa bendi hizo

  • Chipukizi wanane Vijana Stars wanaweza kucheza nje

  • (NYUZ BIN NYUZ):Dk. Remmy aliwahi kuihama Super Matimila

  • Ngulungu:Coastal Tuliwaduwaza Simba mwaka 1990

  • Rose Muhando,Mukabwa kuwashika Dar es Salaam

  • Usiri unavyotawala uchimbaji wa tanzanite

  • Mabadiliko ya tabianchi yaanza kuathiri Tanga

  • KISWAHILI SANIFU:Neno ‘hadi’ linatumiwa tofauti na maudhui yake

  • CCM na Chadema Shinyanga ni ‘watani wa jadi’

  • Mvua zakwamisha Kilimo Shinyanga

  • Ulinzi kwa albino sasa umeijengea sifa serikali

  • Shinyanga wadhibiti mauaji ya vikongwe

  • Utafiti wainua kilimo cha ndizi Kagera

  • Mabaki ya katani yazalisha umeme Hale

  • Mbinu mpya za ufugaji kuku wa kienyeji

  • Wilaya ya Mpwapwa yajikongoja kielimu

  • RASHID WARIOBA:Kutoka kuuza maji hadi kumiliki mgodi

  • Sekretarieti ya Ajira na changamoto ya walio pembezoni

  • Mzizi wa fitina kukatwa biashara za vileo Zanzibar


  • Habari zinazosomwa zaidi:

  • Balaa lingine kwa Chenge

  • Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi

  • Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa

  • ‘Housigeli’ anataka kuniharibia ndoa

  • Kikwete achekecha wakuu wa wilaya

  • Vatican yamvua jimbo Askofu

  • Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%

  • Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa

  • Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu

  • JK apigilia msumari wa mwisho Dowans

  • RAHA ya kona hii kwanza ni kuwatakia kheri wasomaji, nami mwandishi kuwajulisha hali
    yangu, kwa hakika mimi ni mzima na naendelea vizuri kuwapasha mengi yanayohusu muziki wetu wa zamani.

    Leo nianze na kushukuru wa wasomaji wengi kunitumia ujumbe ukiwa na hili au lile, ilimradi wenye dira ya kuberesha safu yetu hii. Kwa walioshiriki kunitumia ujumbe na hata kunipigia simu nawashukuru kwa dhati kabisa kutoka moyoni.

    Lakini kati yetu leo nimalize kiu ya msomaji wetu Ibrahim Vuai, aliyejitambulisha kwamba anaishi Vuoni kisiwani Zanzibar. Yeye alituma ujumbe akilaani tabia ya wanamuziki kuhamahapa kutoka bendi moja kwenda nyingine, akisema kwamba hiyo ni moja ya vigezo vilivyodumaza muziki wa Tanzania.

    Kwa kweli akawataja wengi tangu miaka ile ya 1960 mpaka akaja hivi karibuni akalikumbushia tukio la bendi mbili za African Stars ‘Twanga Pepeta’ na Extra Bongo Next Level kuchukuliana wanamuziki.

    Huko sikutaka kuingia sana, ila kubwa jingine ni pale alipowataka wanamuziki waige mfano wa
    aliyekuwa kiongozi wa bendi ya Super Matimila Dk Remmy Ongala ambaye alimtaja kuwa ni mwanamuzikji aliyetulia, kwani alipotoka Makassy na kujiunga Orchestra Matimila basi hakutoka hadi umauti ulivyompata mwishoni mwa mwaka jana.

    Hapa kidogo ndipo kwenye masahihisho yaliyonifanya niandike makala hii, kwa vile zipo kumbukumbu za kimuziki zinazoonesha kwamba licha ya uvumilivu wa muda mrefu Dk Remmy akiwa na bendi ya Super Matimila lakini aliwahi kuhama.

    Ikumbukwe mwaka 1985 mwimbaji huyo alitangazwa kuikimbia bendi ya Matimila, na alipohojiwa na vyombovya habari alikiri kuiacha bendi hiyo na kurejea bendi ya Orchestra
    Makassy.

    Ndicho kipindi hicho alichotunga wimbo Narudi Nyumbani, lakini ndani yake kulikuwa na maneno siyo yale yaliyorekodiwa baadaye Wimbo huo ulikuwa ukisema "Narudi kwa mjomba" ikiwa na maana anarejea kwenye bendi ya mjomba wake Mzee Makassy ambaye ilielezwa miaka hiyo kuwa wana undugu fulani.

    Hata katika msiba wa mwanamuziki huyo mtu aliyeitwa Kiteguru Makassy ndiye huo aliyekuwa mmiliki wa bendi ya Makassy na ndiye aliyekuwa msmemaji wa familia. Kilitokea nini wakati huo?

    Labda watu wengi na hasa wale wasiojua historia hii watakuwa wakijiuliza kilichojitokeza kwenye bendi ya Matimila ambayo yeye alikwa akiiongoza tangu alipoachiwa kijiti na aliyekuwa mpiga solo hatari wa bendi hiyo Mosese Fanfan ambaye naye alitokea Orchestra Makassy.

    Baada ya kuwa kiongozi wa muda refu na pia kuweza kutunga nyimbo nyingi ndani ya kundi hilo ilitokea wakati umuliki wa bendi hiyo ulihitaji kuiweka bendi kwenye utawala kwa idara maalum.

    Kama vile idara ya fedha na masuala mengine yawe nje ya kiongozi mkuu Dk Remmy ili kumpa nafasi yeye afanye vizuri kazi yake ya muziki.

    Labda tukio hilo na mengine ambayo hayakufahamika kirahisi yalimfanya mwimbaji huyo kutangaza kuikimbia bendi hiyo na kweli alipokewa kwa shangwe kwenye bendi yake ya zamani aliyopata kutamba nayo na nyimbo kama Siku ya Kufa, Harusi ya Mwanza, Namolema, Athumani Valuvalu, Sisca na Mosese.

    Hatimaye mzee mwenyewe Makassy akasimma jukwaani na kuimba pamoja na Dk Remmy na pia walifanikiwa kurekodi wimbo mmoja uitwao Shida za Dunia.

    Baadhi ya mashairi ya wimbo wa Dk Remmy alioimba na Mzee Makassy baada ya kurejea bendi ni haya:- Kweli nasikitika mtoto anapozaliwa anakuta shida nyingi za duniani, njaa kali, magonjwa mengi,shurua kuhara homa kali"

    Hata hivyo katika bendi ya Matimila ilikohesabiwa na wapenzi wa muziki kwamba kutakuwa na pengo, nako kulichangamka kiasi chake. wanza kitu kilichowashangaza wapenzi wengi ni kuwepo kwa sauti ya Dk Remmy licha ya yeye mwenyewe kutokuwepo kwenye bendi hiyo.

    Sauti hiyo ilikuwa na mwimbaji anayeitwa Bink Wabinsalunjivu, ambaye pia uvaaji wake wa kofia alishabihiana na Dk Remmy licha ya kumudu sauti yake. Vilevile alikuwepo mwimbaji
    mwingine Nkhulu Wabangoie aliyejiunga na bendi hiyo akitokea Orchestra Marquiz Du Zaire.

    Kipindi hicho Binki aliibuka na kibao kiitwacho Roda Binti Rashid, na Talakaka Changamka, ambapo Wabangoie alikuja na wimbo wa Sifa za Mage.

    Kwa kuwepo na 'vichwa' hivyo na vilevile kuimarika kwa ukumbi wa Wami Bar iliwawezesha wapenzi wa Matimila kuendelea kuingia kwenye kumbi wanazofanya maonesho kwa vile kulikuwa na mabadiliko fulani ya muziki.

    Kwani licha ya waimbaji hao kubuni mbinu mpya lakini pia aliyekuwa mpiga solo wa bendi
    hiyo Batii Osenga Lipopolipo aliweza kuchangamsha mkono na hivyo kujikuta wakipiga mtindo
    mpya wa Talakaka Changamka.

    Hata hivyo Dk Remmy alikuwa yari amejawa na mapenzi ya bendi ya Orchestra Matimila kwani hata kabla ya miezi mitatu akatangaza kurejea Matimila na safari hii akiubadilisha wimbo uliokuwa ukiimbwa Narudi kwa Mjomba sasa ukawa Narudi Nyumbani Matimila.

    Aliporejea mwimbaji Binki aliacha bendi hiyo na kwenda kuanzisha bendi ya Salna Brothers
    akiwa na mwimbaji mwingine Kapelembe Kokoo ambao waliisuka bendi hiyo hadi kunyakuwa ubingwa wa pili wimbo wa taifa kufuatia kibao chao kiitwacho Ufitina, wakati washindi wa kwanza walikuwa ni Mk Group kufuatia wimbo wao Utakuja Kuanguka Kwenye Matope.

    Dk Remmy naye aliifanyia ukarabati mkubwa bendi ya Matimila kwa kuwakaribisha wanamuziki wengine kama vile wapiga solo wengine Christopher Kasongo aliyepiga wimbo wa Mariam Wangu na Cobra Wabilumbu.

    Hapo ndipo alipoibuka na vibao kama Mariam wangu, Mwanza Mji Mzuri na nyimbo nyingine kadhaa, Kwa hiyo zipo kumbukumbu kuwa Dk Remmy alitoka Matimila wakati fulani na kurejea Makassy lakini baadaye akarejea kwenye bendi hiyo hadi alipofariki.

    WAZARI MAGUFURI BADO TUNAKUHITAJI, DONT EVER THINK OF KUJIUZULU

    Waziri Magufuli hajajiuzulu
    Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 18th March 2011 @ 23:50 Imesomwa na watu: 426; Jumla ya maoni: 0



    Habari Zaidi:

  • Anaswa akiuza kichwa cha mkewe, matiti

  • Kikwete acharuka, amtaka Ngeleja awe makini

  • Waziri Magufuli hajajiuzulu

  • Wanaochakachua mafuta kufungiwa maisha

  • Wabunifu majengo hawataki kuingiliwa

  • Sekondari 'ya kitapeli' yafungwa

  • Waliouawa baada ya kuua polisi wafikia sita

  • Kikwete amteua Kamishina Magereza

  • Moto watekekeza nyumba, duka la vipuri Dar

  • Tanzania ina uhaba wa Wafamasia 14,000

  • Askofu awafunda vijana

  • Maliasili Mpanda waelemewa

  • Waliokuwa wamekosa madarasa kuanza masomo

  • Nahodha awaponda wanasiasa

  • Babu wa Loliondo ageuzwa mradi

  • Watuhumiwa walioua Polisi 2 wauawa

  • Wanafunzi wanaofeli wamkera Kikwete

  • Mkulo ataja vipaumbele 12 vya bajeti ijayo

  • Chadema, vyombo vya habari walaumiwa

  • 'Wananchi waruhusiwe kuwawajibisha wabunge'


  • Habari zinazosomwa zaidi:

  • Balaa lingine kwa Chenge

  • Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi

  • Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa

  • ‘Housigeli’ anataka kuniharibia ndoa

  • Kikwete achekecha wakuu wa wilaya

  • Vatican yamvua jimbo Askofu

  • Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%

  • Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa

  • Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu

  • JK apigilia msumari wa mwisho Dowans

  • SERIKALI imetamka kwamba, habari za kujiuzulu kwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli hazina ukweli wowote, na ni uzushi wa baadhi ya vyombo vya habari.

    Baadhi ya magazeti ya kila siku nchini (si HABARILEO), leo yaliandika taarifa kuhusu kujiuzulu kwa Magufuli.

    Magazeti hayo yalidai kuwa Magufuli kajiuzulu kwa kuwa hakufurahia katika kile kinachodaiwa kuwa ni kuingiliwa kiutendaji na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

    Serikali iimekanusha taarifa hizo na kusisitiza kuwa, Magufuli anaendelea na kazi , hajajiuluzu, hajawahi kuwa na wazo la kujiuzulu na pia hana sababu za kujiuzulu.

    Taarifa hiyo ya serikali imo katika taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Marango.

    “Tunataka kuchukua nafasi hii kuwaarifu na kuwahakikishia kwamba, taarifa hizi si za kweli. Mheshimiwa Waziri anaendelea na kazi zake vizuri, amekuwepo ofisini jana na leo na anaendelea na programu zake za kazi kama kawaida.

    “Tunaomba kuwahakikishia wananchi kwamba, Mheshimiwia Waziri Magufuli hajajiuzulu, hajawahi kuwa na wazo la kujiuzulu na hana sababu za kujiuzulu,” imesema sehemu ya taarifa hiyo iliyokuwa imepewa baraka zote na Waziri Magufuli.

    Amesisitiza kuwa, kutokana na ufafanuzi huo, Waziri Magufuli ambaye ni mmoja wa mawaziri wachapakazi hodari katika serikali ya Rais Kikwete, anaendelea na jukumu alilopewa na Rais la kuiongoza Wizara ya Ujenzi.

    Tangu kuchapishwa kwa habari hizo jana, chumba cha habari cha gazeti hili kilipokea simu nyingi zikiuliza ukweli wa kujiuzulu kwa Waziri Magufuli kama ilivyokuwa imeandikwa, ingawa `kiujanjaujanja’.

    Uvumi juu ya kujiuzulu kwa Magufuli ulianzia kwenye mitandao na ujumbe mfupi wa simu ikidaiwa kuwa, waziri huyo alifikia uamuzi huo baada ya kushindwa kuvumilia kitendo cha Waziri Mkuu kumtaka apunguze kasi ya bomoabomoa ya nyumba na mabanda yaliyojengwa katika hifadhi za barabara kote nchini.

    Pinda, akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Kagera hivi karibuni, alisema ameonesha kasi kubwa katika kushughulikia suala hilo.

    UGUMU WA MAISHA USITUFANYE TUTUMIE NJIA AMBAZO NI KINYUME NA SHERIA,MILA NA TAMADUNI

    ANASWA NA MZIGO WA KICHWA NA MATITI YA MKWEWE
     
    Imeandikwa na Raymond Mihayo, Kahama; Tarehe: 18th March 2011 @ 23:58 Imesomwa na watu: 423; Jumla ya maoni: 0



    Habari Zaidi:

  • Anaswa akiuza kichwa cha mkewe, matiti

  • Kikwete acharuka, amtaka Ngeleja awe makini

  • Waziri Magufuli hajajiuzulu

  • Wanaochakachua mafuta kufungiwa maisha

  • Wabunifu majengo hawataki kuingiliwa

  • Sekondari 'ya kitapeli' yafungwa

  • Waliouawa baada ya kuua polisi wafikia sita

  • Kikwete amteua Kamishina Magereza

  • Moto watekekeza nyumba, duka la vipuri Dar

  • Tanzania ina uhaba wa Wafamasia 14,000

  • Askofu awafunda vijana

  • Maliasili Mpanda waelemewa

  • Waliokuwa wamekosa madarasa kuanza masomo

  • Nahodha awaponda wanasiasa

  • Babu wa Loliondo ageuzwa mradi

  • Watuhumiwa walioua Polisi 2 wauawa

  • Wanafunzi wanaofeli wamkera Kikwete

  • Mkulo ataja vipaumbele 12 vya bajeti ijayo

  • Chadema, vyombo vya habari walaumiwa

  • 'Wananchi waruhusiwe kuwawajibisha wabunge'


  • Habari zinazosomwa zaidi:

  • Balaa lingine kwa Chenge

  • Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi

  • Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa

  • ‘Housigeli’ anataka kuniharibia ndoa

  • Kikwete achekecha wakuu wa wilaya

  • Vatican yamvua jimbo Askofu

  • Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%

  • Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa

  • Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu

  • JK apigilia msumari wa mwisho Dowans

  • POLISI wamemkamata mkazi wa Kijiji cha Mwamala wilayani Nzega katika mkoa wa Tabora, Tano Katinda, akiwa katika harakati za kuuza kichwa cha mtu anayesadikiwa kuwa ni mkewe na viungo vingine vya mwili wa mwanamke.

    Katinda alikamatwa Ijumaa asubuhi wakati alipokwenda kuuza 'bidhaa' hizo kwa Polisi waliokuwa lindoni benki.

    Mtuhumiwa huyo pia amekutwa na sehemu nyingine za viungo vya mwili yakiwemo matiti na sehemu za siri za kike.

    Alikuwa akizunguka na viungo hivyo vikiwa katika mfuko wa plastiki maarufu kama Rambo kwa lengo la kusaka wateja katika mitaa ya mjini wa Kahama mkoani Shinyanga.

    Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Diwani Athumani, amethibitisha kukamatwa kwa mwananchi huyo, na kwamba, mtuhumiwa alikamatwa jana saa 3 asubuhi baada ya kufika katika benki ya CRDB, tawi la Kahama.

    Alisema , baada ya kuzunguka kutafuta soko la viungo hivyo vya binadamu hadi katika Stendi Kuu ya mjini Kahama, akidai anauza nyama ya nguruwe maarufu kama Kitimoto, baadhi ya watu walimwelekeza akawauzie watu waliopo eneo na benki.

    Katinda alisonga mbele hadi tawi la NMB akawakuta askari aliowatangazia kuwa anauza kitimoto, walimjibu kuwa wao ni Waislamu, labda akajaribu kwa askari waliokuwa lindo katika benki ya CRDB iliyopo jirani na NMB.

    Anasema, mtuhumiwa alitii ushauri huo na kusonga mbele hadi CRDB alikoinadi nyama aliyokuwa anaiuza.

    Lakini mmoja wa askari hao baada ya kuchungulia alibaini kuna kichwa cha binadamu na viungo vingine, walimweka chini ya ulinzi na kumfikisha katika kituo cha polisi cha wilaya, mjini Kahama.

    “Awali kijana huyo alionekana kwenye eneo la stendi mabasi maeneo ya CCM Kahama akiuza viungo, hivyo ndipo alipoelekezwa kwenda kuuza kwa askari waliokuwa katika malindo ya benki za CRDB na NMB huku watu hao wasijue kijana huyo ni nini amebeka katika furushi lake,” alisema Kamanda Athumani.

    Kwa mujibu wa kamanda huyo wa polisi, kijana huyo baada ya kukamatwa alikiri kuwa viungo hivyo vilikuwa vya mke wake aliyetajwa kwa jina la Kabula Luziga (18), mkazi wa Itobo, Nzega.

    Alisema, kijana huyo baada ya kuulizwa alisema alimuua mkewe usiku kwa kutumia panga baada ya kumvizia akiwa amelala.

    Mtuhumiwa huyo aliwaeleza Polisi kuwa, kiwiliwili cha mwili wa marehemu Luziga alikiacha katika chumba chake nyumbani kwa babu yake aliyemtaja kwa jina moja la Mwanandilila huko katika Kijiji cha Mwamala, Nzega.

    Hata hivyo, kamanda huyo alisema baada ya kumhoji kijana huyo alidai kuwa alisikia matangazo kwenye kituo kimoja cha Redio cha mjini Kahama kuwa, viungo hivyo ni mali na tayari kuna wateja wanaovihitajika, ndipo alipoamua kumuua mkewe
    ingawa wakati akiuza alidai ni nyama ya kitimoto.

    Kamanda Athumani amesema, jeshi la Polisi linaendelea na upelelezi ikiwa ni pamoja na kuchunguza akili ya kijana huyo.

    Kikosi cha askari polisi mjini hapa kiliondoka jana mchana kwenda kijijini Mwamala kuona kama kweli kuna kiwiliwili cha marehemu Luziga.

    Thursday, March 17, 2011

    How much will I earn with AdSense?

    How much will I earn with AdSense?

    HOJA ZA ZITTO KABWE KUHUSU UGUMU WA MAISHA TANZANIA

    Zitto airarua serikali
    •  Abeza Rais kulalamikia matatizo badala ya kuyatatua

    na Bakari Kimwanga

    MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Zitto Kabwe, ameitaka serikali ichukue maamuzi ya haraka ya kulinusuru taifa na tatizo la umeme nchini, kwani uzoefu unaonyesha ndiyo imekuwa ikichelewesha na wakati mwingine kukwamisha uwekezaji wa miradi mikubwa ambayo ingeweza kulipatia taifa umeme wa uhakika.
    Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (CHADEMA), aliyasema hayo wakati akisoma ripoti ya mapendekezo ya kamati yake kuhusu tatizo la umeme, ambayo kwa kiasi kikubwa imeonyesha kuwa uzembe na urasimu ndani ya serikali umechangia kwa kiasi kikubwa taifa kukosa umeme wa uhakika na kujikuta likiingia gizani mara kwa mara.
    Akisoma maazimio hayo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, alilitaka Baraza la Mawaziri chini ya Rais Jakaya Kikwete kufanya maamuzi ya haraka ili kukamilisha miradi ya umeme wa makaa ya mawe ya Liganga na Mchuchuma, aliyosema ina uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha na wa uhakika.
    Alisema wakiwa katika ziara ya siku tano ya kukagua mradi wa Liganga na Mchuchuma, walibaini kuwa ipo haja ya haraka kwa serikali kutimiza wajibu wake kufanikisha utekelezwaji wa haraka wa miradi hiyo na kwamba wanaunga mkono hatua zilizofanywa na Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) kwa kukamilisha hatua za kumpata mbia kutoka nchini China.
    Alisema kukamilika kwa miradi hiyo kutaifanya nchi inufaike kwa kupata umeme wa Megawati 1500 KV ndani ya kipindi cha miaka mitano na kuendelea, ambao unaweza kuzalishwa kwa takriban miaka 150 kabla ya makaa ya mawe kwisha.
    “Hatuwezi kuwa na taifa la walalamikaji kila mara…. rais, wabunge na wananchi wote sasa tumekuwa walalamikaji lakini muhimu ni kwa baraza la mawaziri kufanya uamuzi wa haraka ili kuinusuru nchi na tatizo la umeme.
    “Hata kampuni tanzu itakayoundwa ili kuendesha miradi hii ifuate taratibu zote za uchimbaji ikiwamo kusainiwa kwa mkataba wa uendelezaji wa mgodi kwa madhumuni ya kulinda masilahi ya taifa na watu wa Ludewa,” alisema Zitto.
    Alisema NDC wameingia ubia na Kampuni ya Atomic Resources ya Australia na kuunda Kampuni tanzu ya TANCOAL Energy wilayani Mbinga kwa lengo la kuzalisha umeme wa megawati 450, ambapo shirika hilo litakuwa na hisa ya asilimia 30 na uwekezaji wake utakuwa ni dola za Marekani milioni 350.
    “Mkataba wa ubia kati ya NDC na Kampuni ya Sichuan Honga kutoka nchini China ili kuendeleza mradi wa Mchuchuma na Liganga ni vema ukasainiwa haraka na serikali,” alisisitiza Zitto.
    Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), alisema Wizara ya Nishati na Madini inatakiwa kuharakisha utoaji wa leseni ya uchimbaji wa makaa ya mawe kama ilivyokuwa imeombwa na Kampuni ya TANCOAL ambayo inamilikiwa kwa ubia na NDC ili uchimbaji huo uanze na umeme uzalishwe.
    Kwamba, umefika wakati kwa TANESCO kuanza kuwekeza katika msongo wa kusafirisha umeme kuelekea kwenye miradi hii ili iwe ya maana, ikiwa ni pamoja na suala la msongo wa umeme kuwa chini ya TANESCO.
    Akifafanua kuhusu mradi wa umeme wa makaa ya mawe wa Kiwira, alisema kamati yake inaunga mkono hatua ya mashirika ya umma kuwekeza katika sekta ya uzalishaji wa umeme na Shirika la Hifadhi ya Jamii nchini (NSSF), kujitokeza kuendesha mgodi huo.
    “Kamati yetu mwaka 2009 ilikwenda nchini Malaysia na kukuta mashirika ya mifuko ya hifadhi za jamii yamewekeza na kuzalisha umeme megawati 27,000 huku wakiwa na akiba ya megawati 12,000 ya umeme katika nchi yao, je, Tanzania tunasubiri nini?” alihoji Zitto.
    Alisema kamati hiyo itakuwa na mkutano na wadau wa kujadili miradi ya umeme ambapo mkutano huo utawakutanisha NDC, STAMICO, TANESCO,NSSF na CHC pamoja na makatibu wakuu wa wizara na wenyeviti wa kamati za Bunge za Viwanda, Biashara, Nishati na Madini ili kujadiliana kwa pamoja na kupata njia mbadala zaidi.
    Akijibu maswali, Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Deo Filikunjombe, alisema kamati yao imefuatilia na kubaini kuwa mchakato wa kurejesha umiliki wa mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira na kubaini kuwa mchakato huo bado haujakalimika kama ilivyokuwa imeelezwa awali.

    KILIO CHA WASANII WOTE NCHINI TANZANIA NIA HAKI ZA KAZI YA MIKONO YAO,

    KILIO CHA WASANII WOTE NCHINI TANZANIA NIA HAKI ZA KAZI YA MIKONO YAO,  Send to a friend
    Thursday, 17 March 2011 08:56
    0diggsdigg
    Kituo cha wasanii wachoraji Mwenge jijini Dar es Salaam
    Na Charles Kayoka
    Jicho la Msafiri kwa leo liko Dar-es-Salaam, Mwenge, kijiji cha wachongaji. Lengo mahsusi ni kuzua mjadala juu ya namna ya kulinda au kuanzisha haki miliki kwa wabunifu wa sanaa za uchongaji. Ninaamini kuwa mfumo wa kibiashara wa sasa hauwapatii faida kubwa wabunifu, na hata taifa kwa ujumla.

    Nilivutiwa kwenda Mwenge baada ya kufika duka moja hapa jijini na kukuta bidhaa za uchongaji zikiuzwa kwa bei ya juu, kama mara tatu ya ile inayouzwa pale Mwenge kijijini. Nikajiuliza kama tofauti hii kubwa ya bei kama inampatia msanii faida au kuwa msanii akishaiuza bidhaa yake anakosa udhibiti kabisa wa biashara ya bidhaa hiyo na hivyo hawezi kupata faida inayoweza kumuinua kimaisha.

    Majadiliano na wafanyabiashara na wasanii yamenionyesha kuwa kuna changamoto kadhaa zinazofaa kufanyiwa kazi. Changamoto ya kwanza ni kukosekana kwa wanunuzi wengi wa Kitanzania ambao wangewezesha biashara hii kuneemeka. Nikaambiwa wengi wa Watanzania huja pale kununua bidhaa za mavazi- T-shirts, vikoi na vitambaa vya magauni na kwa kiwngo kidogo hereni  na bangili.

    Watanzania hawana utamaduni wa kununua vinyago kwa ajili ya kupamba majumbani mwao. Sababu hasa nini? Ili kuwafanya watanzania kupenda kupamba kazi za sanaa katika nyumba zao kunahitajika msukumo wa kibiashara na mtazamo mpya utakaojenga hamasa ya kupenda vitu vyetu hasa kazi za sanaa.

    Hapo awali niliwahi kupata malalamiko kuwa bidhaa zinapobuniwa Tanzania na kwenda nchi za jirani huko huweza kutolewa nakala nyingi na kuuzwa nje ya Afrika Mashariki kwa bei ya juu. “Sio hivyo tu ndugu mwandishi, sisi tunatambua kuwa bidhaa zetu za usanii zikinunuliwa na wageni kutoka nchi jirani zikifika huko zinagongwa mihuri kuwa zimetengenezwa huko na sio kuwa zimetoka Tanzania kama chanzo asilia,” aliniambia msanii mmoja.

    Licha ya kuwa hakuna juhudi wanazofanya kuweka mfumo wa kudhibiti haki miliki na kuweka haki za ubunifu- intellectual property rights, wasanii hawa hawajui soko la bidhaa zao na wengi hutegemea walanguzi wa kati kununua na hao ndio wanaowatafuta wanunuzi nje ya nchi. Kwa kukosa maarifa ya kibiashara wasanii wabunifu hawawezi kujua kama wananyonywa  na kuwa wana haki ya kulinda rasilimali zao na pia kufaidika kutokana  na ubunifu wao.

    Lakini wao wenyewe nilipoongea nao walisema kuwa hawaoni shida. Tangu mababu ubunifu umekuwa ni mali ya umma. Ukibuni sanaa ni sawa mwenzio akikuiga na kuuza na kufaidika kutokana na ubunifu wako. Wenzetu ulaya wanaweza kuzuia kuigiza kwa sababu wameanza vizuri kwa kulinda haki za wabunifu. Sisi hatukuanza hivyo, kwa maelezo yao, basi tuendelee kwa mtindo huuhuu.

    Aidha wafanyabiashara wanaonunua bidhaa toka kwa wasanii wanasema msanii hana haki ya kudai kuwa usanii wake unaigizwa au kurudufiwa kwa sababu akishauza kazi haki ya kumiliki ubunifu wake anaiuza pia.  Sijui watu wa COSOTA na wizara ya viwanda na wanasheria wanaojihusisha na haki hizi za ubunifu wanaweza kusema nini kuhusu hili.

    Sidhani kama Ulaya unaweza kufanyia mzaha kiasi hiki haki za ubunifu wa msanii. Kuwa unabuni sanaa yako kwa mtindo wako wa pekee, inavutia wanunuzi, halafu wanunuzi wanaamua kuirudufu kwa kadri wanavyoweza na msanii (mbunifu) asilia akabaki tu akiona upujufu huu ukitendeka na akanyamaza.

    Wasanii wetu, nilipowauliza kama wanasajili kazi zao za ubunifu, wakasema kuwa hawajui kama wanaweza kufanya hivyo na kuwa wameona waishi kadri walivyozoea kwani hata wao huletewa kazi za ubunfi kutoka nje na kuzirudufu na kujipatia fedha kwa njia hiyo. Waakala wa usajili wa kampuni, hataza na alama za biashara – BRELA inapaswa kufanya kazi zaidi ili kulinda haki za kundi hili.

    Mmoja wa wachuuzi wa sanaa mwanamama alisema kuwa tatizo liko pia upande wa serikali. Anaamini kuwa Mashirika kama HANDICO kama ilivyokuwa zamani yangeweza kuratibu ulinzi wa haki za wabunifu wa sanaa; aidha aliamini kuwa Shirika linalohusiana na Utalii, SIDO, au wizara ya viwanda wanatambua kabisa kuwa usanii unaweza kuleta pato kwa Watanzania na taifa, lakini wanaona kinachotendeka wao wananyamaza.

    “Kama leo hii watu wa nchi jirani wanauuza Mlima Kilimanjaro kama wao na sisi tunashindwa kuzuia hilo iweje tuweze kudhibiti uharamia wa bidhaa za sanaa unaofanywa na wageni?” Aliuliza mfanyabiashara huyo. Hivi ukifika Afrika Kusini ukaona kazi ya Kimasai imewekwa mhuri kuwa imetengenezwa Zambia hapana shaka utashituka hasa kama nchi itakuwa na utaratibu wa kusajili bidhaa zake. Mara moja utajua kuwa kuna uharamia na wasanii wan chi yako wananyonywa na unaweza kuchukua hatua.

    Mfanyabiashara mwingine alisema kuwa yeye anatambua kuwa biashara ya sanaa ina fursa kubwa ya kuajiri watu wengi na kama ikiimarishwa ingeweza kuwa sekta madhubuti ya kutoa ajira kwa Watanzania wengi kuanzia huko kunakokatwa miti, wachongaji na  wauzaji wa ndani. Alisema kumekuwa na tabia ya kutojali kazi za kijadi wakati inaonekana wazi kuwa wageni wanakuja kwa makundi kununua bidhaa na kwenda nazo  nje.

    Kama mpingo unapatika Tanzania kwa wingi zaidi kuliko sehemu nyingine Afrika, inakuwaje serikali haioni kuwa hii ni hazina ya taifa na inayoweza kulipatia taifa kipato.  Nadhani hii ndio changamoto kubwa ya wafanyabiashara wa kazi za ubunifu.

    Wakati wasanii wa nyimbo, vitabu na picha wanaweza kulinda haki zao za ubunifu, hawa wa kazi za uchongazi hawaoni kuwa inawezekana, na kuwa hakuna baba mlezi wa kuwasaidia kutambua haki hizo. Mtu anaweza kutambua ugumu wa kuanzisha mchakato wa kulinda ubunifu katika kazi za sanaa, lakini kwa nia na makusudi, hakuna lisilowezekana kufanyika.
    Kama serikali inatambua kuwa hili ni swala la uhai wa taifa na kuondolea umasikini wananchi, ni lazima ianzishe mchakato utakaowahusisha wataalamu na wadau mbalimbali kufikia mahali ambapo hatimaye sekta hii inatambulika na haki za wasanii zinalindwa.

    Hizi sio changamoto rahisi kwa sekta hii, lakini zikifanyiwa kazi na tukafanikiwa

    utaliiupdate@gmail.com This e-mail address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it , 0766959349

    Wednesday, March 16, 2011

    MOJA YA MAHAFALI YA F6 NILIYOHUDHURIA

    WASICHANA WALOICHANA PAPER WAPATA NAFASI SHULE ZA A-LEVEL

    WASICHANA WALOICHANA PAPER WAPATA NAFASI SHULE ZA A-LEVEL  Send to a friend
    Thursday, 17 March 2011 07:52
    0diggsdigg
    Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa
    Fredy Azzah
    WASICHANA wote waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2010 na kufaulu kwa kupata daraja la I mpaka la III (Division One mpaka Three), wamepata nafasi za kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya Serikali, huku wavulana waliopata nafasi hiyo wakiwa ni asilimia 97. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa alisema wanafunzi wote hao wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangiwa Aprili tatu mwaka huu kuanza masomo.
    Kwa mujibu wa Dk Kawambwa, wanafunzi waliokuwa
    na sifa za kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano pamoja na vyuo vya ufundi ni 36,990 wakiwamo wasichana 11,210 na wavulana 25,780.
    “Wanafunzi 36,366 ambao ni asilimia 98.31 ya waliokuwa na sifa stahili wamepangwa kidato cha tano na vyuo vya ufundi, kati yao wasichana ni 11,210 sawa na asilimia 100 ya wenye sifa na wavulana ni 25,156 ambao ni asilimia 97.58 ya wanafunzi wenye sifa,” alisema Dk Kawambwa.
    Wanafunzi wa kike waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano pamoja na vyuo vya ufundi ni asilimia 30.83 ya wanafunzi wote 36,366 waliopangwa.
    Mwaka 2010 wanafunzi wa kike 12,638 walichaguliwa kuendelea na masomo, ikiwa ni asilimia 42.33 ya wanafunzi wote.
    Kutokana na hali hiyo, idadi ya wanafunzi wa kike waliochaguliwa kuendelea na kidato cha tano na vyuo vya ufundi mwaka huu, ni pungufu ya wanafunzi 1,428 ukilinganisha na ile ya mwaka jana.
    Kwa ujumla, wanafunzi waliopangiwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi mwaka jana, walikuwa 33,662. Wasichana walikuwa 12,638 na wavulana 21,024.
    Hata hivyo, Dk Kawambwa alisema mwaka 2010 wanafunzi waliochaguliwa walikuwa asilimia 83.52 ya wenye sifa, hivyo mwaka huu kuna ongezeko la asilimia 12.63, kwa awamu ya kwanza.Alisema wavulana 624 sawa na asilimia 2.42, hawakuchaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya ufundi kutokana na sababu mbalimbali.
    Alizitaja sababu hizo kuwa ni kutokuwa na uwiano wa alama za masomo (credits), alama kutotimia na baadhi kuwa na umri wa zaidi ya miaka 25.
    Alisema wanafunzi 29 walikuwa na umri uliozidi miaka 25 ambao kisheria hauwaruhusu kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano kwa shule za Serikali.
    Wanafunzi wengi wa kike wamepangwa kusoma masomo ya Historia, Jiografia na Kiingereza (HGL), kati ya wote waliochaguliwa wanafunzi 1,610 sawa na asilimia 14.4 walichagua masomo hayo.
    Alisema wanafunzi 1,593, watasoma CBG; 1,574 watasoma HKL, 1,472 watasoma PCB, 1,108 watasoma HGK na wanafunzi 1,035 watasoma HGE.
    Kwa upande wa wavulana, wanafunzi wengi wamechaguliwa kusoma masomo ya sayansi. 4,307 sawa na asilimia 17.1 watasoma PCM; 4,177 sawa na asilimia 16.6 wakichaguliwa kusoma PCB, 3,079 HGL, 2,722 HGK, 2,504 HKL na wanafunzi 2,249 wakichaguliwa kusoma CBG.
    Wanafunzi 916, wasichana wakiwa 55 na wavulana 861 wamechaguliwa kujiunga na mafunzo ya vyeti katika vyuo vya ufundi vya Mbeya (MIST), Dar es Salaam (DIT), Arusha (ATC) na Chuo Maji Dar es Salaam.
    Kutokana na hali hiyo, wanafunzi wa kike waliochaguliwa kusoma masomo ya sayansi na vyuo vya ufundi mwaka huu ni  4,357 ikiwa ni ongezeko la wanafunzi 195, ikilinganishwa na wanafunzi 4,162 waliochaguliwa kusoma masomo hayo mwaka jana.
    Kwa upande wa wavulana, idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kusoma masomo hayo mwaka huu imeongezeka kwa asilimia 25.9, kutoka wanafunzi 12,664 waliopangiwa kusoma masomo ya sayansi ikilinganishwa na mwaka jana ambapo wanafunzi 10,057 ndio waliochaguliwa kusoma masomo hayo.
    Pia idadi ya wanafunzi hao waliopangiwa kusoma sayansi ni asilimia 50.3 ya wanafunzi wote wa kiume waliochaguliwa kuendelea na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.
    Katika hatua nyingine, Waziri Kawambwa alisema wanafunzi 624 wenye sifa ambao hawakuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano au vyuo vya ufundi, bado wana nafasi za kuendelea na masomo hayo kwa kujiunga na shule za sekta binafsi.
    Dk Kawambwa pia alieleza kuwa wanafunzi ambao bado Baraza la Taifa Mitihani (Necta), halijatangaza matokeo yao, pindi yatakapotoka na kama watakuwa na sifa zinazotakiwa, watachaguliwa kujiunga na shule au vyuo vya ufundi.
    Dk Kawambwa aliwataka wakuu wa shule zisizokuwa za Serikali kuwasilisha majina ya wanafunzi wa kidato cha tano waliojiunga na shule zao ili kuiwezesha  wizara yake kuwa na kumbukumbu sahihi.
    Waziri huyo alitoa angalizo kuwa mtindo wa wazazi kuomba uhamisho wa watoto wao kabla ya kuripoti katika shule walizopangwa, safari hii hautakubaliwa kwa kuwa wizara hiyo imewapanga wanafunzi katika shule walizoomba.

    Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
    Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
    Last Updated on Thursday, 17 March 2011 08:05
     

    Comments 

     
    0 #1 ANOLD MADANDI 2011-03-17 08:42
    ushauri toeni nafasi kwa wavulana na wasichana wafanye mitihani tena ili waweze kuongezwa ktk vyuo vya ufundi vilivyoko hapa inchini kwani wanahitajika sana nchini iwe na wataalam wengi ahsante
    Quote
     

    Add comment

    Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!

    ELIMU KUHUSU KATIBA KWA WATANZANIA



    Katiba iweke misingi ya usawa na fikra za utaifa  Send to a friend
    Wednesday, 16 March 2011 00:00
    0diggsdigg
    Na Charles Kayoka
    HIVI karibuni, hasa wakati na baada ya uchaguzi, gumzo juu ya udini katika siasa limeibuka na limekuwa moja ya mada katika mikutano ya CHADEMA. Niliona bango moja katika maandamano likisomeka, “Udini ni ghilba za Wanasiasa.” Nami nakubaliana na maelezo hayo ya kuwa wanasiasa wanapoona wanashindwa kupata uhalali wa kutawala wanakimbilia makundi yao ya kiimani kuomba msaada kwa kisingizio kuwa watu wa imani ingine- imani pinzani, hawamtaki kwa sababu ya kuwa wa imani tofauti.

    Hili huweza kupata mashiko kama watu wa dini husika hawana uwezo wa kufanya upembuzi yakinifu. Ndio maana udini unaweza kuwa ni ghilba tu ya wanasiasa kuomba msaada wa kundi.

    Lakini kwa Tanzania udini katika siasa hauwezi kuelezeka kwa kauli rahisi namna hii! Udini ni matokeo ya matumizi ya makusudi ya nguvu za kundi ili kujijengea uhalali wa kuendelea kuwepo madarakani na pia kutumika kama ajenti wa kuwasaida watu wa kundi lako kwa sababu wamekutuma ufanya hivyo, au unahisa una wajibu wa kufanya hivyo.

    Kumekuwa na madai ya namna hiyo dhidi ya uongozi tangu wakati wa Nyerere. Na hakuna Rais Tanzania aliyekwepa tuhuma za kuwa anatumiwa na dini yake. Lakini wakati huu pia tuhuma hizi aidha zinasema uongozi uliopo unatumiwa kidini au unawatuhumu wapinzani kuwa wawakilishi wa dini.

    Hizi ni dalili kuwa Tanzania kama nchi imekosa itikadi unganishi ambayo ingewatambulisha viongozi kwa itikadi hiyo na tungetambuana hivyo kama raia na uongozi ungepimwa kwa utekelezaji wa itikadi husika.

    Nchi inapoendeshwa kwa msingi wa fedha na mashindano katika kupata fedha na mali, ni wazi umoja utajengwa kwa msingi wa fedha na mali. Lakini kwa sababu binadamu lazima tuishi katika makundi, dini na kabila huweza kuwa moja ya makimbilio ya kujengeana umoja na kujitambua.

    Lakini ufisadi unapozidi na kuwa kupata ajira, kwa mfano,kunategemea unajuana na nani, ukoo, kabila au dini, ni lazima watu watadhani kuwa ili ufanikiwe ni lazima uwe na uhusiano wa kiitikadi na anayekusadia kufanikiwa.

    Udini unaweza kutokana na kukosa fikra yakinifu ya vyanzo, na katika kutatua matatizo, hasa ya umasikini. Watu wanaweza kudhani wamekuwa masikini kwa sababu tu watu wa dini fulani wanatawala badala ya kuuchungunza mfumo mzima wa uchumi unavyowafanya watu wote masikini na wachache matajiri.

    Kwa kawaida huwa ni rahisi hao matajiri wachache kuwaghilibu mlio wengi kwa lugha za kuwafanya msione ukweli wa jinsi wanavyowanyonya. Na mkadhani hata ni matajiri kwa kudra ya Mwenyezi Mungu.

    Lakini kutokukubali kufanya mkutano wa katiba ambako ndiko kutakapo patikana majadiliano ya namna siasa itakavyoendeshwa kunaweza kuwa moja ya chachu ya udini.

    Katiba ni chombo muhimu sana katika kujenga itikadi ya umoja wa kitaifa. Wanaohofu isitengenezwe kwa mkutano wa pamoja wanaogopa kuwa ile misingi wanayoitumia sasa ya udini na ukabila itaondolewa na watawajibika kwa misingi ya usawa na fikra za utaifa. Wananchi tusidanganyike.

    mohamedmusta@gmail.com This e-mail address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it , 0766959349

    EDWARD LOWASA IS ONE OF THE FORMER PRIME MINISTER IN TANZANIA

    Lowassa apata kikombe Loliondo  Send to a friend
    Tuesday, 15 March 2011 23:47
    0diggsdigg
    Waandishi Wetu
    WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa juzi alipata tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapile katika Kijiji cha Samunge, Tarafa ya Sale, Loliondo, mkoani Arusha.Lowassa alifika katika eneo hilo mchana akiwa na viongozi kadhaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na Serikali kisha kupata kikombe kimoja chenye dawa kinachotolewa na mchungaji huyo kwa ajili ya tiba.
    Tofauti na viongozi wengine, Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), Jimbo linalopakana na Kijiji cha Samunge, alikwenda huko akiwa na viongozi mbalimbali wakiwamo viongozi wa dini na baadhi ya wapigakura wake.
    Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Lowassa alithibitisha kwenda Loliondo na kuwataja viongozi wa dini alioambatana nao katika msafara wake kuwa ni Askofu Msaidizi wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini, Dk Frederick Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Dayosisi ya Kaskazini Kati (Arusha), Mchungaji John Nangole.
    Katika ramani ya utendaji kazi ya KKKT, Jimbo la Masai Kaskazini ndipo kilipo Kijiji cha Samunge ambako ni makazi ya Mchungaji Mwasapile.“Ni kweli, nimekwenda pale na wapigakura wangu pamoja na viongozi wa dini, Msaidizi wa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Dk Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Mchungaji Nangole,” alisema Lowassa na kuuliza: “Kwani hiyo nayo ni habari jamani?”
    Baada ya Lowassa kufika katika kijiji hicho akiwa na ujumbe wake, aliongoza moja kwa moja hadi kwa Mchungaji Mwasapile na kuzungumza naye kisha akapata kikombe cha tiba na kuondoka.

    Kabla ya Lowassa kwenda kupata tiba, amekuwa akitoa msaada wa nauli kwa wagonjwa mbalimbali wa jimbo lake kwenda kwa mchungaji huyo ambaye dawa yake inadaiwa kutibu magonjwa ya saratani, kisukari, pumu, shinikizo la damu na Ukimwi.Lowassa ni miongoni mwa wanasiasa maarufu nchini ambao wameshafika kwa mchungaji huyo kupata tiba hiyo wakiwamo mawaziri, naibu mawaziri, wabunge, wakuu wa mikoa na wilaya.


    Katika jitihada za kudhibiti usalama na kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma kwa mchungaji huyo bila matatizo, Serikali imeimarisha ulinzi kwa kuweka askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), katika kijiji hicho na kusimamia magari. Pia imepeleka wauguzi kusaidia wagonjwa mahututi kabla ya kumfikia mchungaji na imetoa pia jenereta kwa ajili ya kufua umemeKaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Raymond Mushi alisema jana kuwa, sasa walau hali ni nzuri kwani msongamano umepungua.

    "Ni kweli sasa hali inaridhisha na jana watu wamekwenda kupata tiba na kurejea makwao mapema hili ndilo serikali inalolitaka. Tunaomba watu wanaopeleka wagonjwa wawe wanauliza kwanza hali ya msongamano," alisema Mushi.Mushi alisema inawezekana watu wanaokwenda katika kijiji hicho kusubiriana katika Mji wa Mto wa Mbu ambako kuna huduma nyingi muhimu kuliko wote kwenda huko kwa wakati mmoja.

    Alitoa wito kwa watu wenye wagonjwa mahututi kuacha kuwapeleka moja kwa moja kwa mchungaji huyo kabla ya kupata ushauri wa kitaalamu kuhusu afya zao.Katika hatua nyingine, wagonjwa kadhaa waliolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili wameanza kutoroka wodini na kwenda Loliondo kupata matibabu ya magonjwa sugu yanayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwaisapile, Mwananchi imeelezwa.
    Habari zilizopatikana hospitalini hapo jana zimeeleza kuwa wagonjwa hao walianza kuondoka Muhimbili juma lililopita baada ya Serikali kubariki matibabu hayo. Ofisa mmoja mwandamizi wa hospitali hiyo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe gazetini, amesema kuwa wakati baadhi ya wagonjwa hao wakiwa wanatoroka wodini, wengine wamekuwa jasiri kwa kuwaaga madaktari wao.
    “Wagonjwa wameanza kuondoka na wengine bila hata ya kuaga, hivyo hatujui hatima yao kama watafika salama huko Loliondo,” alisema.Ofisa huyo alisema juma lililopita, mgonjwa mmoja aliyekuwa amelazwa chumba namba 15 katika Wodi ya Kibasila, aliondoka baada ya kusikia taarifa kuhusu huduma hiyo.
    “Kuna mgonjwa mmoja aliyekuwa amelazwa Kibasila Wodi namba 15 aliondoka aliposikia kuwa Babu ameanza tena kutoa matibabu hayo ambayo awali yalisitishwa,” alisema.Hata hivyo, Ofisa Habari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Aligaisha alisema hana taarifa za kutoroka wodini kwa wagonjwa hao na kwenda kufuata tiba huko Loliondo... “Sina taarifa zozote za kuondoka kwa wagonjwa hapa hospitalini.”

    Matibabu Loliondo yapandisha nauli Ubungo
    NAULI za kwenda Arusha kutoka Ubungo, Dar es Salaam zimepanda kwa kasi katika siku za hivi karibuni kutokana na wingi wa wasafiri wanaoelekea Loliondo kupata tiba hiyo ya magonjwa sugu.Habari zilizolifikia gazeti hili jana kutoka kituoni hapo zimeeleza kuwa, nauli hizo zimepanda kutoka Sh18,000 hadi Sh30,000 tangu juma lililopita.
    Mmoja wa mawakala wa mabasi ya abiria katika kituo hicho ambaye hakutaka kutajwa gazetini alisema ongezeko hilo la nauli limetokana na baadhi ya mawakala kukodi mabasi na kuwasafirisha abiria.“Nikupe siri moja tu ambayo inatufanya tupandishe nauli. Lengo letu ni kupata faida, ujue sisi tunakodi basi zima kisha tunakatisha tiketi kwa bei yetu ili na sisi tupate faida,” alisema.

    Mmoja wa abiria aliyekuwa akisafiri kuelekea Arusha, Charles Manyama alisema mabasi yaendayo huko yamegawanyika katika madaraja matatu yale ya bei ya juu, bei ya kati na bei ya chini lakini kwa sasa bei imekuwa ni moja kwa mabasi yote.
    Kwa mujibu wa abiria huyo, zamani nauli za Arusha zilikuwa Sh25,000 kwa basi la daraja la juu, Sh18,000 kwa mabasi ya daraja la kati na Sh15,000 kwa daraja la chini, lakini sasa mabasi yote yanatoza kati ya Sh25,000 hadi Sh30,000.“Mawakala hawa wanadhani kila mtu anayepanda magari haya anakwenda Loliondo lakini siyo kweli, wengine tuna safari nyingine kabisa," alisema Manyama na kuongeza:

    "Unakuta bei zinashangaza na kupanda sana. Hata hivyo, inashangaza kuona wanadamu tunakosa utu. Watu wanakwenda kupata matibabu wanapandishiwa nauli, walipaswa kuwaonea huruma wagonjwa hawa,” alisema Manyama.Jitihada za kumtafuta Meneja wa kituo cha mabasi Ubungo ziligonga mwamba baada ya taarifa kutoka ofisi kwake kueleza kuwa alikuwa nje kikazi.

    Polisi Arusha wadhibiti usafiri wa Loliondo
    Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limeitaka Halmashauri ya Jiji la Arusha kuweka vituo vinavyotambulika kwa ajili ya wagonjwa wanaokwenda kupata matibabu kwa Mchungaji Mwasapile ili kuepuka utapeli.

    Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa alisema jana kuwa kutokana na idadi kubwa ya watu kutaka kwenda Loliondo, kumezuka vituo vingi ambavyo vinaweza kuwa chanzo cha utapeli kwa watu wanaotoka mikoani."Nafahamu hili ni jambo ambalo manispaa wanahusika nalo, wahakikishe kuwa hakuna vituo visivyo rasmi ili wananchi wasije kudanganywa na watu wabaya," alisema.

    Katika kituo kilichoibuka ghafla baada tiba ya magonjwa sugu kuanza kutolewa cha Chini ya Mti, kulizuka vurugu za madereva na madalali waliokuwa wakibishania kiwango cha nauli, hatua iliyosababisha polisi wenye silaha kupelekwa katika eneo hilo.
    Hatua ya polisi kuonekana katika kituo hicho, ilisababisha wasiwasi kwa wananchi kuwa huenda Serikali imesimamisha utaratibu wa wananchi kwenda Loliondo, jambo ambalo kaimu kamanda huyo alilikanusha.

    "Tunachokifanya ni kuweka utaratibu mzuri, polisi wanasimamia sheria. Magari mengine yanazidisha idadi ya watu na kutoza pesa nyingi zaidi. Sumatra wakisema nauli sahihi ni kiwango fulani na madereva wakizidisha basi tunawakamata," alisema.
    Wananchi waliozungumza na gazeti hili bila kutaja majina yao walisema kuwa wanashangazwa na bei ya nauli kuwa juu hata baada ya Serikali na KKKT, Dayosisi ya Kaskazini Kati kuboresha mazingira ya kuwahi kupata tiba na kuondoka kijijini Samunge.

    "Mwanzoni walikuwa wanasema magari yanakaa sana huko, kwa hiyo wanafidia hizo siku za kungoja wagonjwa lakini sasa hivi ukienda leo unarudi kesho na nauli bado iko juu," alisema mmoja wa wananchi hao.Nauli ya kutoka Mjini Arusha hadi Samunge, Loliondo ni Sh100,000 kwenda na kurudi kwa magari aina ya Land Cruser ,huku nauli ya mabasi ikiwa pungufu zaidi.
    Habari hii imeandaliwa na Nevile Meena, Ibrahim Yamola, Dotto Kahindi Dar na Mussa Juma, Filbert Rweyemamu, Arusha

    Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
    Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
     

    KUMEKUCHA LOLIONDO NCHINI TANZANIA

    Tusherehekee dawa ya Loliondo kwa hadhari kubwa  Send to a friend
    Tuesday, 15 March 2011 21:19
    0diggsdigg
    Mchungaji Ambilikile Mwasapile
    KAMA kuna tukio ambalo liliwahi kugusa hisia na maisha ya  wananchi wengi katika historia ya nchi yetu, basi tukio hilo ni kupatikana kwa dawa inayosemekana inatibu magonjwa sugu na yaliyoshindikana, yakiwamo Kisukari, Kansa na Ukimwi. Hakika, tunashindwa kupata maneno stahiki ya kuelezea jinsi Watanzania walivyopokea habari za kupatikana kwa tiba hiyo iliyoelezwa kupatikana katika Kijiji cha Samunge, wilayani Loliondo, mkoani Arusha.

    Ni tukio lililoitikisa na linaloendelea kuitikisa nchi yetu wakati maelfu kwa maelfu ya wananchi, wazee kwa vijana, wanaume kwa wanawake wa itikadi na imani zote wakielekea kijijini Samunge kumuona Mchungaji Ambilikile Mwasapile ili awapatie tiba ya magonjwa hayo sugu. Ndio maana tunasema kuwa hilo ni tukio kubwa na la kihistoria, na ukubwa wa tukio hilo hasa unatokana na ukweli kwamba ni tukio la kiimani. Kwamba Mchungaji huyo alioteshwa katika ndoto mwaka 1991 kuwa kuna dawa itakayoshushwa kwake ili aitumie kutibu  magonjwa ambayo yameshindikana kutibiwa na binadamu. Mashuhuda wengi wanasema walitibiwa na dawa ya mchungaji huyo tangu alipoanza kutoa huduma hiyo mwaka 2009. Baadhi wamejitokeza hivi karibuni na kusema kuwa wamepona maradhi hayo sugu.

    Na kama hiyo haitoshi, watu waliopata dawa ya Mchungaji Mwasapile tangu habari za tiba yake zilipochapishwa na gazeti hili kwa mara ya kwanza wiki iliyopita, wamesema dawa hiyo imewatibu na sasa wanaona wako fiti. Baadhi ya madaktari wamethibitisha kuwa wateja wao ambao awali walikuwa wanasumbuliwa na magonjwa hayo wamethibitika kupona baada ya kutumia dawa hiyo inayojulikana kwa jina la Mugariga.
     
    Hicho hasa ndicho kielelezo cha sababu ya maelfu kwa maelfu ya wananchi kumiminika Loliondo wakitokea kila pembe ya nchi yetu wakifuata dawa hiyo inayosemekana ni ya ajabu. Pia hicho ndicho kielelezo cha akili, mawazo, macho na masikio ya Watanzania wote kuelekezwa katika Kijiji cha Samunge na kutekwa na nguvu anayosemekana kuwa nayo Mchungaji Mwasapile.
     
    Na hasa hiyo ndio sababu ya Serikali kujikuta njia panda pasipo kujua la kufanya. Katika kuonyesha hali ya kuchanganyikiwa, Serikali kwanza ilitangaza kupiga marufuku shughuli za Mchungaji  Mwasapile na baada ya wananchi kupaza sauti wakitaka huduma hiyo iendelee, Serikali ilisalimu amri mara moja hasa baada ya kutambua kuwa sauti za wananchi zilikuwa za kiimani zaidi.
     
    Ni kwa sababu hiyo tunaipongeza Serikali kwa kutambua kuwa badala ya kuweka vizuizi ili maelfu kwa maelfu ya watu wasifuate tiba hiyo kijijini Samunge, ilikuwa busara kuwawezesha watu wapate tiba hiyo. Serikali ilifanya vyema kugundua kuwa maelfu ya watu waliokuwa wanafuata tiba hiyo wasingeogopa vizuizi au vitisho vyake, kwani baadhi yao walikuwa wamekata tamaa kutokana na maradhi sugu yaliyokuwa yanawasumbua, hivyo walikuwa tayari kwa lolote, hata kufa.
     
    Vilevile, Serikali iligundua kuwa isingekuwa na askari wa kutosha kusimamia amri zake kwa sababu askari wengi walikuwa njiani kuelekea kijijini Samunge na wengine tayari walikuwa wamewasili huko kupata dawa hiyo. Pia, baadhi ya  mawaziri, wabunge na watendaji wakuu serikalini walikuwa miongoni mwa wananchi waliokuwa wanafuata dawa hiyo.Ndio sababu tangazo la Serikali kuruhusu shughuli hizo za tiba kuendelea ziliwapa watu wengi faraja na matumaini makubwa.
     
    Sisi tunawahadhalisha wananchi na Serikali kuwa, pamoja na tiba hiyo kuwa suala la kiimani, tusifanye makosa kuanza kufanya sherehe. Tunawashauri wananchi wote kwanza waipe dawa hiyo muda wa kutosha ili itoe matokeo na baadaye wataalamu wa afya wayathibitishe pasipo shaka.
     
    Kwa upande mwingine, tunawashauri wale wanaohisi wameponywa au hawajaponywa na dawa hiyo wajitokeze kutoa ushuhuda ili mamlaka husika ziweze kufanya tathmini na kuwapa wananchi maelekezo stahiki. Ni imani yetu kuwa watakaoponyeshwa na dawa hiyo hawatafanya vitendo hasi, bali watamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwaletea nuru mpya