Monday, December 17, 2012

UKAHABA UDOM NI AIBU KWA TAIFA LA TANZANIA

by Alex Nicholaus Thomas Mushi .


Kwa dhati ya moyo wangu nimesikitishwa sana na taarifa zilizozagaa kwenye vyombo vya habari kuhusu kujiuza kwa dada zetu wa UDOM. Wasomi ambao wana Dodoma na watanzania kwa ujumla walitegemea kujifunza kutoka kwao. Taarifa hizi zimenichochea kukaa chini na kuandika waraka huu huku nikizingatia ukweli kwamba UDOM ndipo nilikosomea masomo yangu ya shahada ya kwanza; mbali na matatizo yote yaliyonikumba katika safari hiyo ya kukamilisha shahada hiyo lakini nalazimika kusema kitu kwa faida yetu wote.

Ikumbukwa moja ya mategemeo ya jamii ya wana Dodoma kutoka kwenye chuo cha UDOM kilipo anzishwa mwaka 2007 ilikuwa ni kujionea jamii staarabu iliyoelimika na yenye kila sifa ya kuigwa, na pia jamii ya Dodoma ilitegemea watoto wao wangejionea namna wasomi hawa wanavyoishi kwa kusadifu kwa vitendo elimu, maadili na mila za nchi yao. Zaidi waliamini mambo hayo yangekuwa chachu ya kuwachochea vijana wao kuzingatia masomo ili na wao siku moja wafikie elimu hiyo ya Chuo lakini hali imekuwa tofauti kabisa. Leo jamii hii ya wana Dodoma wanashuhudia wasomi wanaoshinda mitaani wakiranda randa na nguo za kuogelea na za kulalia kana kwamba walikotoka hakuna wazazi, wanashuhudia wasomi wanaojiuza kama njugu.

Kiukweli siwezi hata siku moja kuruhusu kulea au kuipamba tabia hizo hata kama kuna sababu za msingi ambazo zinaweza zikawa zimesababisha tatizo hili kutokea. Kinachofanywa na dada zetu hawa ni kitendo ambacho kila mungwana anapaswa kukikemea kwa nguvu, na zaidi ya yote ni wajibu wetu wote kama vijana kurudia maadili yetu kama watanzania na kulaani kwa nguvu haya. Kama tutaruhusu tabia hii ikaota mizizi tutaandaa wasomi wasio waadilifu na wasio jiamini, tutandaa wasomi wenye shahada za kwenye chupi (nisamehewe kwa hiyo lugha lakini nimekosa neon linalokidhi ninachomaanisha),tutandaa wasomi walioathirika hivyo kupoteza nguvu kazi ya taifa, tutaandaa taifa la wavivu na wasifikiri kwa ufanisi.

Tukumbuke kuruhusu tabia hii kubobea ni kuruhusu kuporomoka kwa elimu ambayo ni msingi wa taifa lolote duniani. Na sidhani kama ni busara kuangalia umauti wa taifa letu kwa kuruhusu tabia hii kuota mizizi, kwani dhambi hiyo haitaishia chuoni tu, itaingia makazini na hapatakuwa na kazi zaidi ya uzinzi tu, baada ya hapo dhambi hii itasambaaa hadi kwa watoto na wajukuu wetu na hatimaye itakuwa ndio mfumo wetu wa maisha. Lakini mbali na yote niliyoeleza hapo juu ninayo yangu kwa serikali yangu, vijana hawa wa UDOM ni watoto wenu na wengine wameingia pale wakiwa hawana hata elimu ya kimaisha au ya kujitegemea, wengine wanakutana na kila aina ya tabia pale.

Mimi nilisha kuwa kiongozi wa mikopo UDOM-HSS kwa karibu miaka yote ya masomo yangu ya shahada ya kwanza, naelewa kiasi sababu na wakati dada zetu hawa wanapojiuza. Kipindi ambacho dada zetu hawa hujiuza huwa ni pale Bodi ya mikopo inapochelewesha mikopo ya wanafunzi, hali huwa mbaya kiasi dada zetu hawa ufika mahali wanalazimika kujidhalilisha ilimradi wapate chochote cha kujikimu. Na ukizingatia majumbani kwao hawa msaada wowote wanaoupata.

Mfano mzuri wa ucheleweshaji wa mikopo kwa wanafunzi wa kozi ya Uhusiano wa Kimataifa (BA IR) hawajapewa mikopo yao mpaka leo, na wanatakiwa kula, kunywa, kuwasiliana na kununua vitini vya masomo ili hali familia walizotoka ni masikini wa kutupwa. Haya yote ni mazingira hatarishi kwa dada zetu hawa. Serikali kama mzazi nakuomba mliangalie kwa umakini sana suala hili ili tuwaepushie wale wanajihusisha na tabia hii ya kuuza miili yao kutokana na kuishiwa au kukosa fedha za kujikimu Muda mwingine unaweza kusema serikali inafanya makusudi kuwacheleweshea mikopo yao wa sababu wanaonufaika sana na tabia hiyo ya dada zetu kujiuza ni wabunge wanapokuja kwenye vikao vyao vya bunge.

Kujiuza kwa dada zetu hawa ni dhahiri ni matokeo ya mambo kadhaa ambayo serikali haina budi kuyafuatilia kwa kina na hatimaye kutatua kwa ustawi wa tafa letu la Tanzania. Hatupaswi kufurahia tabia hii hata kidogo kwan kufanya hivyo kunaweza liathiri taifa letu kwa ujumla wake siku za usoni.

……………“ukiona panafuka moshi ujue kuna moto”…………

MTOTO KUMKOSOA BABA HARDHARANI INA MAANA GANI?WATENDAJI WA SERIKALI WAMEWEKWA NA CCM, HIVYO KUSHIDWA KWAO NDIO KUSHIDWA KWA CCM





Viongozi wa CCM mkoa Njombe wakishirikiana na makamu mwenyekiti wa CCM Taifa Phili Mangula ( wa pili kulia ) kuwaongoza wanachama wapya wa CCM zaidi ya 600 waliojiunga na CCM jana wakati wa mapokezi ya makamu huyo wa kwanza kulia ni mbunge wa jimbo la Njombe kusini na spika wa bunge Anne Makinda wa tatu kutoka kulia ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Njombe Deo Sanga ambae ni mbunge wa jimbo la Njombe kasikazin na anayefuatia ni katibu wa CCM mkoa wa Njombe Hosea Mpangike




Deo Filikunjombe miongoni mwa wananchi









Msafara wa pikipiki kwenye mapokezi ya Mangula Njombe

Picha na Said Ng'amilo wa Mjengwablog







Habari na Francis Godwin


MBUNGE wa jimbo la Ludewa mkoani Njombe Deo Filikunjombe awakuna wapiga kura wa jimbo la Njombe Kaskazini Linaloongozwa na mbunge wake Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Njombe Deo Sanga Kwa kuwalipua watendaji wabovu serikalini ,mbele ya makamu mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi ( CCM) Tanzania bara Philip Mangula.


Filikunjombe ambea alipewa nafasi ya kusalimia katika mkutano huo mkubwa wa mapokezi ya Mangula mkoani Njombe alisema kuwa masikitiko ya wananchi juu ya serikali ya CCM yanatokana na baadhi ya viongozi wabovu ndani ya Chama na serikalini ambao wamekuwa wakifanya kazi chini ya kiwango na kupelekea wananchi kukichafua Chama tawala.


" Ndugu zangu wananchi wa Makambako na mkoa wa Njombe Chama chetu CCM ni Chama kizuri sana na safu hii ya sasa chini ya Rais Kikwete ,Kinana na Mangula ni safu ya uhakika na itakiwezesha Chama chetu kuendelea kuaminiwa zaidi na watanzania ...ila tatizo ni viongozi wachache wa serikali wasiowajibika katika nafasi zao"kauli iliyowakuna wananchi na kushindwa kujizuia kushangilia huku wakiimba wewe ni Jembe .


Hata hivyo Filikunjombe alisema kuwa ili Chama kuendelea kupendwa na akina Mangula na Kinana wanapaswa kusaidiwa na watanzania wote kwa kuombewa zaidi ili kuendelea kuifanya kazi hiyo bila woga ndani ya chama.


Kwa Upande wake Mangula mbali ya kusifu mapokezi makubwa ya kihistoria Katika mji wa Makambako na Njombe mkoani Njombe aliweza kutoa ya Moyoni kuhusu Kati yake na Rais Jakaya Kikwete kwa Madai kuwa yeye alikuwa hajui chochote juu ya uteuzi wake na kuwa alisitaajabu kupokea simu ya Kikwete kuhusu kusudio la uteuzi wake.


" Kweli Mimi nilikwenda Dodoma katika mkutano mkuu wa CCM Kama mualikwa ila Nikiwa Hotelini nilipokea simu ya mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Kikwete akiomba kuniteua kuwa makamu mwenyekiti na baada ya kwenda Ukumbini wajumbe wote walinipa kura zote za ndio...kweli namshukuru sana mwenyekiti wangu na wanachama wote na sasa ni kazi zaidi na sitawaangusha"


Hata hivyo aliwataka wana CCM kufanya vikao bila kuchota na kuwa wasizingizie kukosa ajenda kwani hata kukosa ajenda ndani ya CCM ni ajenda Kukosa agenda pia ni agenda ndani ya CCM pia yaweza kuwa ajenda.


Aidha amehimiza nidhamu na taratibu ndani ya CCM kuendelea kuzingatiwa ili kukiwezesha Chama kuwa na amani na kuwa iwapo taratibu ndani ya Chama hazitazingatiwa upo uwezekano wa Amani ndani ya nchi kutoweka.


Alisema kuwa haitapendeza kuona Tanzania inafika mahali inaendeshwa bila Chama iwapo tutaruhusu wasiopenda Amani kuendelea kuvuruga Amani yetu iliyopo...

Tuesday, December 11, 2012

KUMEKUCHA CCM NA CHADEMA VITANI TENA


“Lengo la kutoa mafunzo kwa wenyeviti na makatibu wa ni kuwajengea uwezo wa uwajibikaji, kudai haki zao ili kuleta hamasa kwa Watanzania kushiriki kikamilifu kwenye mchakato wa mabadiliko,” anasema Kigaila"

KUMALIZIKA kwa chaguzi za ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM kumeamsha joto la kisiasa nchini.
CCM na Chadema ndio hasa vyama vinavyoonekana kutolala. Kila kimoja kimeanzisha mbinu mpya ya kujijenga na kujiongezea wafuasi wanaokiunga mkono.
Nia ya vyama hivi ni moja, kujiongezea mtaji wa kukivusha katika uchaguzi mkuu wa 2015 na kushika dola.
Wakati CCM ‘mpya’ ikitajwa kuanza harakati za kupita mikoani na kutangaza mikakati ya kurejesha imani yake kwa wananchi, Chadema imeingia kambini kwa mbinu mpya za mashambulizi, hasa ngazi ya vijijini ili kuikaba koo CCM.
Safu mpya ya CCM
Katika kile walichokiita kurejesha imani ya wananchi kwa chama hicho, viongozi wa Sekretarieti wamefanya ziara ya kutathmini utekelezwaji wa ahadi zake kama zilivyoelekezwa katika ilani yake ya uchaguzi.
Wakiongozwa na Katibu wake, Abdulrahman Kinana, Makamu mwenyekiti, Philip Mangula wameanza mkakati huo kwa nia ya kuwaeleza wananchi kile kilichofanywa na Serikali yao inayoongoza.
Katika hatua ya kwanza ziara ilianzia Mtwara, ikihusisha mikoa minne, mingine ikiwa ni  Rukwa, Geita, kumalizia Arusha.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, anasema lengo la ziara hiyo katika maeneo hayo yenye fursa nyingi za maendeleo ni kuhakikisha wananchi wanapata majibu ya jinsi utekelezwaji wa ahadi za chama hicho tawala ulivyofanyika.
Anasema ziara hiyo inawahusisha mawaziri wa Serikali ambao wanatoa ufafanuzi wa masuala kadhaa, yakiwemo utekelezaji wa ahadi zikiwemo zilizotolewa mwaka 2010 wakati wa kampeni.
Harakati hizo za CCM zinakuja muda mfupi baada ya kupata viongozi wapya, ambao kwa nyakati tofauti, wameahidi kupambana na rushwa iliyokithiri nchini na ndani ya chama hicho.
Wakiwa mkoani Mtwara, kete ya viongozi hao ilichezwa kwenye matatizo ya wakulima wa korosho, zao ambalo ndilo tegemeo kwa wananchi wa mkoa huo. Pia waligusia bandari na miundombinu mingine ambapo waliahidi kuyafanyia kazi maeneo yote yaliyoonekana kusababisha kero kwa wananchi hao.
Mtindo huo wa CCM kutembea na mawaziri wa Serikali unaelezwa kuwa na manufaa kwani hutakiwa kutolea ufafanuzi utekelezaji uliofanywa na chama hicho, na pale ambapo kuna tatizo, hukumbushwa ili kuhakikisha kasoro hizo zinaondolewa haraka.
Katika baadhi ya maeneo katika mkoa huo viongozi hao wapya wamembana na changamoto ikiwemo kuzomewa kwa mawaziri, ambapo Kinana na Nape waliweza kutuliza hali hiyo kwa kukubali kasoro zilizoainishwa na wananchi na kuahidi kuzirekebisha.
Mawaziri waliokumbana na zomea zomea mni Hawa Ghasia (Serikali za Mitaa na tawala za Mikoa), Naibu wake, Aggrey Mwanri na Waziri Kilimo na Uahirika, Christopher Chiza.
Wananchi walieza kukerwa na hatua ya Serikali kuipeleka gesi inayochimbwa Dar es Salaam huku wananchi wa Mtwara wakikosa kunufaika na rasilimali hiyo.

MATAJIRI WA TANZANIA WANAOTAMBULIKA AFRIKA NZIMA



"Anayeongoza katika orodha hiyo ni Bakhressa anayemiliki mali na fedha zenye thamani ya Dola za Marekani 620 milioni sawa na Sh992 bilioni (Dola moja Sh1,600) akifuatiwa na Dewji ambaye utajiri wake ni Dola 560 milioni (Sh896 bilioni). Wengine na kiasi cha mali na fedha wanazomiliki kwenye mabano ni Rostam (Sh672 bilioni- Dola 420 milioni) Mengi (Sh448bilioni- Dola 280 milioni) na Mufuruki (Sh176 bilioni - Dola 110 milioni)".

WAFANYABIASHARA watano, Said Bakhressa Gulam Dewji, Rostam Aziz, Reginald Mengi na Ali Mufuruki, wametajwa na Jarida la Ventures Africa linalozungumzia masuala mbalimbali ya uchumi wa Afrika kuwa ndiyo matajiri zaidi nchini.

Anayeongoza katika orodha hiyo ni Bakhressa anayemiliki mali na fedha zenye thamani ya Dola za Marekani 620 milioni sawa na Sh992 bilioni (Dola moja Sh1,600) akifuatiwa na Dewji ambaye utajiri wake ni Dola 560 milioni (Sh896 bilioni). Wengine na kiasi cha mali na fedha wanazomiliki kwenye mabano ni Rostam (Sh672 bilioni- Dola 420 milioni) Mengi (Sh448bilioni- Dola 280 milioni) na Mufuruki (Sh176 bilioni - Dola 110 milioni).

Matajiri hao wamepatikana baada ya kuangalia nafasi zao kifedha, ufanisi wa kampuni zao katika soko la hisa, mfumo wa wanahisa katika soko la hisa na mtiririko mzima wa fedha katika akaunti zao kwenye benki mbalimbali.

Jarida hilo linalotoka mara moja kwa mwezi kutoka Afrika Magharibi, limesema matajiri hao wa Tanzania ni kati ya Waafrika wenye utajiri ambao ni mabilionea 4,800 kutoka mataifa 17.
Asilimia kubwa ya watu 1,523 ni mamilionea na wamo katika ripoti ya watu matajiri Afrika.
Jarida hilo linataja jinsi matajiri hao walivyokuwa wajasiriamali wadogo kabla ya kuibuka na kuwa mabilionea.

Said Salim Bakhresa
Jarida hilo limesema chanzo cha utajiri wa Bakhressa ni mapato yanayotokanana uzalishaji wa bidhaa mbalimbali kwenye viwanda vyake.

Mfanyabiashara huyo aliacha shule akiwa na umri wa miaka 14 na kuanzisha biashara zake. Alianza kuuza urojo Zanzibar na baadaye alifungua mgahawa miaka ya 1970.

Mgahawa huo ulipanuka na alitumia faida yake kufungua mashine ya kusaga pamoja kiwanda za usindikaji vyakula, huku akiunda Kundi la Makampuni ya Bakhressa.
Aliendelea kusindika vyakula mbalimbali na kutengeneza unga wa mahindi na baadaye kuanzisha kiwanda cha kuoka mikate na baadaye kutengeneza chocolate, ice cream, vinywaji na makasha ya kufungashia bidhaa. Kutokana na shughuli hizo, kwa mwaka huingiza Sh800 milioni.
Kampuni zake kwa sasa zinafanya biashara mbalimbail katika nchi za Tanzania, Uganda, Malawi, Rwanda na Msumbiji na ameajiri zaidi ya wafanyakazi 2,000.

Gulam Dewji
Mfanyabiashara huyo ana utajiri unaokadiriwa kufikia Dola 560 milioni kutokana na kuzalisha bidhaa na kutoa huduma mbalimbali.
Ni mmoja wa mataikuni wa Tanzania tangu miaka ya 1970 na kazi yake kubwa ilikuwa kuingiza bidhaa mbalimbali kutoka nje.

Alianza na kampuni ndogo aliyoiita Mohammed Enterprises Tanzania, ambayo kwa sasa ni kati ya kampuni kubwa Afrika Mashariki na Kati.
Miongoni mwa mali zake ni Kiwanda cha 21st Century Textiles, moja ya viwanda vikubwa vya nguo Kusini mwa Jangwa la Sahara. Kampuni yake ina viwanda vinne, Tanzania na Msumbiji huku ikizalisha Dola 100 milioni kwa mwaka. Pia kampuni hiyo husindika juisi kwa matunda ya Tanzania, mafuta ya kula, sabuni na tishu.

Kampuni hiyo pia inamiliki kampuni ya bima, makontena, kampuni za kuuza mafuta ya petroli na maduka ya kuuza bidhaa mbalimbali zaidi ya 100 Tanzania nzima.
Hata hivyo, Gulam alisema jana kwamba takwimu zilizotolewa zimekosewa. Alisema kwa sasa yuko nje ya Dar es Salaam na atatoa taarifa sahihi atakaporejea.
“Kuna baadhi ya tarakimu zimekosewa niko Morogoro kuangalia biashara zangu nikirudi Dar es Salaam nitazungumza,” alisema Dewji.

Rostam Aziz
Ameelezwa kuwa utajiri wake umetokana na kuendesha shughuli zake mbalimbali ikiwamo kampuni za mawasiliano ya simu, madini na biashara za usafiri wa meli.
Mwanasiasa huyo mwenye asili ya Asia, alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuwa Mbunge wa Igunga mwaka 1993 na alishinda kwa vipindi viwili.

Aliachana na ulingo wa siasa mwaka 2011. Anamiliki asilimia 19 ya Hisa za Kampuni ya Vodacom ambayo ina wateja zaidi ya milioni nane.

Ameelezwa pia kuwa anamiliki Kampuni ya Ujenzi ya Caspian na sehemu ya Bandari ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Kampuni ya Hutchison Whampoa ya Hong Kong.
Akizungumzia utafiti huo, alisema: “Umefanyika kwa umakini isipokuwa tu kwa upande wangu wanasemas ninamiliki asilimia 19 ya Kampuni ya Vodacom kitu ambacho si sawa kwani ninamiliki asilimia 35.”

Reginald Mengi
Mengi anakimiliki kampuni mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari, viwanda vinavyozalisha vinywaji baridi vya Coca-Cola na ana mgodi wa dhahabu.

Mfanyabiashara huyo baada ya kufanya kazi ya uhasibu ambayo ndiyo taaluma yake, alifanya biashara ya kutengeneza kalamu za wino zilizopata soko kubwa Afrika Mashariki.
Leo hii, IPP Group ambayo Mengi ni mwenyekiti wake, inamiliki magazeti mbalimbali ikiwemo Financial Times, ThisDay na The Guardian, televisheni mbili kubwa Afrika Mashariki na Kati EATV na ITV na vituo vya redio. Anamiliki Kampuni za IPP Gold na Handeni Gold.

Ali Mufuruki
Utajiri wake unatokana na biashara mbalimbali za rejareja na za ushirika.
Ni mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa Tanzania Infotech Investment Group.
Kampuni hiyo inajumuisha Watanzania na Waganda kwa ajili ya kuuza bidhaa za Afrika Kusini za Woolworth.

Infotech hufanya kazi ya uendelezaji makazi na ukodishaji, matangazo na shughuli za mawasiliano.

Thursday, November 15, 2012

POLISI WASIINGILIWE NA CHAMA DOLA KATIKA UTENDAJI KAZI ZAO


RAIS Jakaya Kikwete juzi aliwaonya wanachama wa CCM akiwataka waache kubweteka kwa kuwategemea askari polisi katika masuala ya kisiasa, kwani kufanya hivyo watakuwa wanajidanganya.

Kikwete alitoa kauli hiyo wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Nane wa CCM uliofanyika kwa siku tatu mfululizo katika Ukumbi wa Kizota mjini Dodoma.

Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, alisema kitendo cha wanaCCM kuishi katika siasa kwa kutegemea Jeshi la Polisi hakipaswi kukubaliwa kwani kimepitwa na wakati.

“Mnaishia kulalamika tu kila siku, eti wanatukana halafu mnaishia kusema ndiyo kawaida yao…au utasikia mtu anasema eti Serikali haipo! Kazi ya Serikali siyo hiyo, hiyo ni kazi ya kisiasa maana hao ndio wenzenu,”alisema Kikwete na kuongeza:

“Sasa mnataka wakisema Serikali ya CCM haijafanya kitu polisi wawafuate, au wakisema Kikwete nchi imemshinda, polisi wakawakamate? Kama wakisema hatujafanya kitu ni kazi yenu kusema kwamba tumefanya kitu, waonyesheni barabara, shule na mambo mengine.”

Licha ya kwamba hakuwataja moja kwa moja, kauli za Rais Kikwete zilikuwa zikielekezwa kwa uogozi wa Chadema ambao kimsingi kinaonekana kuwaumiza vichwa CCM.

Huku akirudia mara kadhaa maneno hayo alisema, “Nataka mfahamu ndugu zangu kuwa tukiishi kwa kutegemea Jeshi la Polisi kufanikisha mambo yetu, tutakwisha na tutakwisha kweli.”

Kikwete aliwatuhumu viongozi wa upinzani kwamba ni waongo na kwamba wakati mwingine wamekuwa wakizusha mambo ambayo hayapo, huku wakijifanya kuwa na ushahidi wa kimaandishi.

Alimtaja Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa kwamba kuna wakati aliwahi kuzusha kwamba yeye (Kikwete), na makada kadhaa wa chama hicho wakiwamo Rostam Aziz walikuwa jijini Mwanza usiku, wakati si kweli kwani siku waliyodai alikuwa Nachingwea mkoani Lindi kwenye mikutano ya kampeni za urais.

Katika mazingira hayo, aliwataka wanaCCM kila mahali kujibu hoja za wapinzani kwa kauli na vitendo na wasikubali kuburutwa kwani uongo ukiachwa kwa muda mrefu unageuka kuwa ni ukweli.

Aliwaeleza kuwa ukimya wao katika kujibu hoja za wapinzani ni sumu kwao na kwamba wenzao wameanza kuaminika zaidi yao licha ya kuwa CCM ndio wenye majibu yote.

“Mkijibu kwa hoja wanatulia, sio Polisi. Nakumbuka Mwigulu aliwajibu pale bungeni kuhusu bajeti yao mbadala. Walipoitoa kijana wetu akasimama na kupiga msumari kweli wakachanganyikiwa sasa hizo ndio kazi zinazotakiwa jamani,” alisisitiza Kikwete.

Mbali na hilo aliwaonya kuacha malumbano ya mara kwa mara akieleza kuwa hali hiyo inakibomoa chama.

Alisema baadhi ya wanaCCM wamekuwa wakitumia muda mwingi kukosoana wao kwa wao, huku wakitoa nafasi kwa adui zao.

Mwenyekiti huyo alisema hakuna mtu kutoka nje ya chama anayeweza kukidhoofisha CCM kwa hoja isipokuwa chama hicho kinaumizwa na wanachama wake ambao wamekuwa wakilumbana bila sababu.

Akizungumzia suala la wagombea urais aliwataka wanachama wenye nia kufuata taratibu zote za chama pamoja na kuvumiliana ili ifikapo Mei 2015, mkutano utafanya uamuzi wa nani anasimama kupeperusha bendera ya chama hicho.

“Kwa wale mnaotaka kugombea, andikeni hiyo tarehe tutakuja hapa kuteua, lakini msituvuruge lazima mfuate utaratibu. Utaratibu huo utatangazwa, maana mkianza kupita huko na huko ndiko tunakopata matatizo,” alisema Kikwete.

Kikwete juzi alichaguliwa kwa mara nyingine kuwa Mwenyekiti wa CCM baada ya kupata asilimia 99.92 ya kura zilizopigwa, huku kura mbili zikimkataa. Kadhalika mkutano huo uliwachagua Dk Ali Mohamed Shein kuwa Makamu Mwenyekiti (Tanzania – Zanzibar) na Phillip Mangula kuwa Makamu Mwenyekiti (Tanzania Bara).

VURUGU ZA KIKUNDI CHA UAMSHO Z'BAR, KARUME ATUSHWA ZIGO


RAIS Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Aman Karume juzi usiku alizomewa na baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku wakimwita kwamba ni mmoja wa wanakundi la Uamsho.

Uamsho ni kundi ambalo katika siku za hivi karibuni limekuwa likihusishwa na vurugu ambazo zimekuwa zikitokea Tanzania Visiwani, ambazo zimesababisha watu kadhaa kukamatwa na kufikishwa mahakamani.

Rais Karume alikutana na zahama hiyo wakati akitoa hotuba ya kuwaaga wanaCCM baada ya kumaliza ngwe yake ya utumishi ndani ya chama hicho akiwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar.

Dalili za Rais Karume kuzomewa zilianza baada ya baadhi ya wajumbe kutoka Mkoa wa Mjini Magharibi kuanza kutaja neno ‘Uamsho’ kila alipokuwa akizungumzia matatizo yaliyopo Zanzibar.

Hali ilikuwa mbaya zaidi pale alipokuwa akizungumzia vurugu za kidini ambazo ziliikumba Zanzibar hivi karibuni zikiongozwa na kikundi cha Uamsho.

Karume alisema kuwa kikundi cha Uamsho kina haki ya kutoa maoni yake kuhusu muungano, lakini hakipaswi kufanya vurugu kama ambavyo kimekuwa kikifanya.

Wakati akiendelea kuzungumzia suala hilo, kelele nyingi zilienea katoka kwa wajumbe wa mikoa ya Zanzibar ambao walikuwa wakipaza sauti, “ Uamsho huyo….Uamsho huyo… Uamsho huyo….”

Hali hiyo ilimfanya wakati mwingine kukatiza hotuba yake na kulazimisha kuwatuliza watu hao kwa kusema “CCM oyeee….CCM…..oyeee…Mapinduziii….”
Hata hivyo, baada ya kelele hizo kuendelea Karume alionekana kuhamaki na kuwaambia wajumbe hao kwamba amechoka kusikia akiitwa jina hilo la Uamsho.

“Nimechoka kusikia naitwa jina hilo ati,” alisema Karume na kuongeza:
“Hivi wengine wana vichwa vya samaki kwa nini mnapiga kelele wakati mimi ninapozungumza, si mniache nizungumze mambo ambayo ni muhimu zaidi kwa masilahi ya chama chetu.”

Hata hivyo, licha ya kutafuta namna ya kuwatuliza wanachama hao kwa maneno mengi na historia ya maisha yake tangu alipojiunga na Chama cha ASP mwaka 1970, bado hakukuwa na utulivu na safari hii kelele zilianza kwa pande zote za wajumbe.

Kwa upande wa wajumbe wa Bara, baadhi yao walikuwa wakipiga kelele za kumtaka kumaliza hotuba yake ambayo walisema ilishachukua muda mrefu huku wakisema hakuna cha ajabu alichokuwa akizungumza.

Mara baada ya kumaliza hotuba yake, Karume alihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya Redio Deutche Welle ya Ujerumani, na alisisitiza kuwa Uamsho wana haki ya kutoa maoni yao kuhusu muungano, lakini hawaruhusiwi kuvunja sheria.

Aliwataka wanachama wa kikundi hicho kujenga hoja, kwani alisema wengine wana hoja za msingi, lakini wasitumie vitisho.

Karume alistaafu uongozi wa CCM katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti (Tanzania Visiwani) na nafasi yake ilichukuliwa na Rais wa sasa wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein.

Tofauti na utamaduni ambao CCM kimeujenga kwa viongozi wake wakuu, Karume aliendelea kuwa makamu mwenyekiti hata baada ya kustaafu urais wa Zanzibar, hivyo kumlazimisha Dk Shein kusubiri hadi juzi kuchukua nafasi hiyo.

Kwa kawaida, viongozi wa ngazi ya Rais wa Muungano na Zanzibar, baada ya kuondoka katika nafasi zao za uongozi wa nchi, pia huachia madaraka ndani ya chama na kumwachia Rais mpya.

Saturday, November 10, 2012

Serikali kitanzini hoja binafsi ya Zitto, watanzania wafuatia kwa jicho la tatu


Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (kushoto) akimwonyesha Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk David Mathayo baadhi ya ushaidi aliokuwa nao wa hoja yake binafsi inayoitaka serikali kuchukua hatua dhidi ya watanzania walioficha fedha haramu nje ya nchi, mjini Dodoma. Picha na Edwin Mjwahuzi 

 NGUVU za Serikali za kutaka kuifuta hoja binafsi ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Kabwe Zitto ya kuitaka Serikali kuchukua hatua dhidi ya Watanzania walioficha fedha haramu nje ya nchi, jana zilishindwa baada ya wabunge kadhaa kumgomea Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema kufanya hivyo.
Dalili za Serikali kutaka kuzima hoja hiyo zilianza baada ya Jaji Werema kusimama na kutoa mapendekezo ya kufuta vipengele muhimu.
Hatua hiyo ilizusha mvutano mkali, huku baadhi ya wabunge wakisema Serikali inataka kuifuta hoja hiyo muhimu kwa mustakabali wa taifa.

Mapendekezo ya Werema
Katika mapendekezo yake, Jaji Werema alipendekeza kufanyika kwa marekebisho kwenye kipengele katika hoja hiyo ya Zitto ambacho kiliitaka Serikali iwasiliane na Benki ya Dunia ili kupitia Kitengo cha Assets Recovery Unit irejeshe nchini mabilioni ya fedha yanayomilikiwa na Watanzania katika benki za Uswisi na maeneo mengine yote ambayo hufichwa fedha ili kukwepa kodi.
Jaji Werema alitaka pendekezo hilo liondolewe kwa maelezo kuwa mamlaka za uchunguzi ikiwamo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Usalama wa Taifa zinalifanyia kazi suala hilo.
Eneo jingine katika hoja ya Zitto ambalo Jaji Werema alipendekeza lifanyiwe marekebisho ni kuwapiga marufuku viongozi wa Serikali na watoto wao pamoja na Watanzania wengine kufungua akaunti nje akisema suala hilo litashughulikiwa kwa mujibu wa sheria ya fedha za kigeni.
Pia alitaka pendekezo lililomo katika hoja ya Zitto cha kutaja akaunti za watu wenye fedha benki za nje na kuzichapisha katika vyombo vya habari lifanyiwe marekebisho kwa kuondolewa.
Alisema suala hilo ni gumu na linakwenda kinyume na sheria za benki zinazotaka kutunza siri za wateja wao.
Kuhusu pendekezo la kuitaka Serikali katika Bajeti ya mwaka wa fedha wa 2013/13 kuanzisha kodi maalumu ‘Financial Transaction Tax’ ya angalau asilimia 0.5 ya thamani ya ‘transaction’ ili kuweza kuwa na rekodi za uhakika fedha za ndani na zinazotoka nje ya nchi, Werema alitaka lifutwe akisema hiyo inahitaji utafiti wa kutosha.
Alisema ofisi yake imechukua siku nyingi kufanya uchunguzi kuhusu fedha hizo ikiwemo kwenda Uswisi na kwingineko na kwamba itashirikiana na vyombo binafsi vya uchunguzi kufanya kazi hiyo.
Pendekezo jingine lililopingwa na Jaji Werema lilikuwa ni kuitaka Serikali kuwabana Watanzania wenye fedha nje ya nchi waeleze walikozipata akisema kazi hiyo inaweza kufanywa na Takukuru.

Wabunge wamshukia
Baada ya kutoa mapendekezo hayo, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu alisema anamshangaa Mwanasheria Mkuu kwa kufanya marekebisho ambayo yanaizima hoja ya Zitto.
Huku akinukuu vifungu vya Kanuni za Bunge, alisema Mwanasheria Mkuu anataka kuua hoja hiyo na kwamba mapendekezo yake yanakwenda kinyume na kanuni ambazo zinataka kila badiliko katika hoja liwiane na jambo linalojadiliwa.
“Hoja ya mabadiliko ya Mwanasheria Mkuu kuondoa mapendekezo hayo, kwa maoni yangu yanakinzana na Kifungu 53 (3) (4) cha Kanuni za Bunge, kinachopendekeza kuwapo kwa mabadiliko na siyo kufuta hoja.
Alisema hatua ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya kupendekeza mabadiliko hayo ni kufuta hoja jambo ambalo alisema ni kinyume cha kanuni. Kwa mujibu wa kanuni za Bunge, mtu ambaye anaweza kuiondoa hoja ni mtoa hoja na si mtu mwingine yeyote.
Alimtaka Spika kutumia busara yake kumzuia Mwanasheria Mkuu kufuta hoja hiyo muhimu kwa mustakabali wa nchi.
Baada ya maelezo hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi alisimama na kuunga mkono mapendekezo ya Mwanasheria Mkuu, huku akielekeza ‘makombora’ kwa Lissu kuwa anachokisema kinapingana na mtoa hoja Zitto, ambaye anakubaliana na Mwanasheria Mkuu.
Hata hivyo, Zitto alisimama na kutoa ufafanuzi kuwa hakubaliani na mapendekezo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa sababu yanazima hoja yake.
Baadaye Lukuvi alisema anaunga mkono pendekezo moja katika hoja ya Zitto la Serikali kuwasilisha bungeni ripoti ya uchunguzi katika Bunge la 11 na kwamba ili kasi hiyo iende vizuri yashirikishwe pia kampuni binafsi ya uchunguzi.
Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM), alipinga pendekezo la kuiondoa hoja hiyo na kuunga mkono azimio kwamba Bunge liiagize Serikali kufanya uchunguzi huo na ripoti yake iwasilishwe katika Bunge la 11 na ikishindwa, Bunge liunde kamati ndogo ya kufanya kazi hiyo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Tamisemi), Hawa Ghasia, aliuanga mkono mapendekezo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali akisema vyombo vya uchunguzi viachiwe kuchunguza mabilioni ya fedha yaliyopo nje ya nchi.
Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka (CCM), alipinga akisema mapendekezo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali yalikuwa na lengo la kuua hoja hiyo akisema wabunge watafanya dhambi kubwa kuiondoa hoja hiyo ya msingi.
Sendeka alitaka hoja hiyo iboreshwe kwa kumtaka Zitto awataje hadharani watu ambao wameficha fedha nje ya nchi ili Watanzania wawafahamu... “Ukiwataja hawa hoja yako itakuwa na mashiko, tusaidiane na wala siyo fedheha kuwataja.”
Alitaka kamati iundwe kuchunguza jambo hilo ili ukweli ujulikane.
Baada ya kubanwa na wabunge, ndipo Jaji Werema alisimama na kulegeza msimamo wake kwa kurejesha pendekezo la Serikali kushirikiana na vyombo vingine vya uchunguzi vya nje pamoja na wachunguzi binafsi kufanya kazi hiyo.
Alikubali pia pendekezo la kuitaka Serikali kuja na mkakati wa kueleza nini imekifanya katika Bunge la 11.
Aliwataka wabunge wote wenye majina ya watu walioficha fedha nje ya nchi kuyapeleka Takukuru au wamkabidhi yeye.
Baada ya hapo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alisimama na kusema hoja ya Zitto haikuwa mbaya na kusema Mwanasheria Mkuu pia alikuwa na nia njema.
Alisema Serikali haiwezi kumficha mhalifu akisema kama mtu ameiba atachukuliwa hatua bila ya kumwonea haya. Aliungana na Mwanasheria Mkuu kutaka Serikali iachiwe jambo hilo ilifanyie kazi.
Akihitimisha mjadala huo, Spika wa Bunge, Anne Makinda alisema hoja ya Zitto haijatupwa bali, inaingia kwenye utaratibu wa Serikali wa kuyatekeleza maazimio hayo.
Alisema Serikali itapaswa kutoa taarifa ya utekelezaji wa hoja ya Zitto katika Bunge la 11 la Aprili) mwakani na kama ikishindwa, Bunge litaunda kamati kufanyia uchunguzi maazimio hayo.

Msimamo wa Zitto
Akizungumza baada ya uamuzi huo wa Bunge, Zitto alisema ameridhishwa na hatua hiyo akiamini kwamba itafanyiwa kazi.
Alisema amefurahi pia kwa kuwa hiyo ni mara yake ya kwanza kwa hoja yake kufanyiwa kazi na Bunge.

Sunday, October 28, 2012

TAFAKARI KISHA MWAMBIE ACHUKUE HATUA

JE TANZANIA INAHITAJI VIONGOZI WA NAMNA HII KATIKA ULIMWENGU HUU WA SAYANSI NA TECHNOLOJIA?

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Augustino Mulugo wakati akitoa hotuba yake katika mkutano wa wataalam wa elimu huko Afrika Kusini. (Picha na Youtube)
Na Walusanga Ndaki
JANA mtandao huu uliandika makala iliyokuwa na kichwa cha habari ‘MAKOSA’ YA WAZIRI MULUGO NI YA BAHATI MBAYA AU UFAHAMU MDOGO?…
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Augustino Mulugo wakati akitoa hotuba yake katika mkutano wa wataalam wa elimu huko Afrika Kusini. (Picha na Youtube)
Na Walusanga Ndaki
JANA mtandao huu uliandika makala iliyokuwa na kichwa cha habari ‘MAKOSA’ YA WAZIRI MULUGO NI YA BAHATI MBAYA AU UFAHAMU MDOGO?
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo akiendelea kuwasilisha hotuba yake. (Picha na Youtube)
Katika makaka hiyo tulionyesha makosa yaliyokuwa ndani ya hotuba ya naibu waziri huyo wa elimu aliyoitoa katika mkutano wa wataalam wa elimu huko Afrika Kusini mwanzoni mwa mwezi huu.
Baada ya wimbi kubwa la malalamiko ya umma kuhusu hotuba yake hiyo iliyokuwa imejaa dosari nyingi, waziri huyo leo alizungumza na kituo cha Clouds FM akikiri dosari hizo japokuwa kwa kujitetea kijanja.
Katika kuonyesha kwamba umakini kwa watumishi wa umma nchini ni mdogo sana,  ni jinsi waziri huyo alivyokuwa akiisoma hotuba hiyo bila hata kushitukia chochote.
Kwanza kabisa, kwa ufahamisho, ni kwamba mfumo wa sasa wa hotuba duniani ni kwamba msemaji anaposoma hotuba yake wakati huohuo huonyeshwa na kompyuta katika kiwambo ambapo washiriki wengine wanaweza kuifuatilia pia kwa kuisoma.
Mtandao huu umeandika yote yafuatayo kwa kufuatilia matamko ya hotuba ya Mulugo ambayo yalikwenda sambamba na hotuba yake ambayo ilionekana kwa ajili ya kusomwa.
Mfano wa kosa la kizembe la Mulugo ni pale aliposema kwamba Tanzania inapakana na nchi nane.  Miongoni mwa nchi hizo nane alizozitaja ajabu ni kwamba nchi ya Burundi haikuandikwa katika hotuba yake japokuwa aliitaja toka kichwani!
Jambo jingine, ni kwamba miongoni mwa nchi hizo zinazopakana na Tanzania aliitaja nchi moja kwa jina la “Congo DRC”, hii ni kwa mujibu wa alivyotamka katika hotuba yake na jinsi ilivyokuwa imeandikwa katika hotuba hiyohiyo.
Kiuhalisia, hakuna nchi kama hiyo inayopakana na Tanzania.
Nchi inayopakana na Tanzania miongoni mwa nchi nane alizozitaja ni Congo DR au Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.  Si “Congo DRC” aliyoitaja waziri Mulugo.
Kama Mulugo hakuliona kosa lake na alikuwa bado hajaliona hadi leo wakati anaongea na Clouds FM ni kwamba kirefu cha “Congo DRC” (kama kweli nchi hiyo ipo) ni “Congo Democratic Republic of Congo”!
Waziri Mulugo alisema kwamba neno Zanzibar alilitaja kimakosa kama Zimbabwe wakati wa hotuba yake akielezea nchi zilizounda muungano wa Tanzania, kwa vile msemaji aliyekuwa amemaliza kusema kabla yake alikuwa ametoka Zimbabwe.
Hata hivyo, katika kuisoma hotuba yake iliyokuwa imeandikwa “…islands of Pemba and Zanzibar…” aliisoma kama “…islands of Zimbabwe and Pemba…”.
Angalau kama kweli ni kwa kukosea angeisoma kama “…islands of Pemba and Zimbabwe…”, lakini  kwa vile hakuwa makini, jicho na akili zake vilikimbilia neno ‘Zimbabwe’ kwanza kabla ya kuitaja Pemba ambayo ndiyo ilikuwa ianze, kama hotuba yake ilivyokuwa imeandikwa!
Hebu ona hili lifuatalo!
Katika hotuba ileile, kuna aya iliyokuwa imeandikwa ifuatavyo: “The United Republic of Tanzania is located on the east cost of Africa.”
Hapa kuna makosa mawili yaliyokuwemo katika hotuba hiyo aliyoisoma.   Kosa kubwa la kwanza hapa ni neno “cost” ambalo ni la Kiingereza, maana yake ni “gharama” (likiwa ni nomino) au “kugharimu” (kitenzi).
Hivyo, hilo ni kosa la waziwazi na la kuchekesha na kuchefua lililokuwa katika hotuba ya Mheshimiwa Mulugo!
Neno sahihi lilibidi liwe “coast” yaani “pwani”.  Kwa mujibu wa hotuba hiyo ya Mulugo ambayo huenda aliiandika yeye mwenyewe au kuandikiwa, sentensi hiyo ya “The United Republic of Tanzania is located on the east cost of Africa” ingemaanisha nini?
Ingemaanisha kwamba “Jamhuri ya Muungano ya Tanzania iko mashariki mwa “gharama” (au “gharimu”) mwa Afrika!
Unaona kichekesho hicho?!  Hiyo ni hotuba ya waziri wa Tanzania aliyoiweka kwenye mkoba, akapanda ndege, akafikia hoteli ya kisasa, akala na kulala ambapo kesho yake akaenda mbele ya wasomi wenzake na kupeleka hotuba hiyo ya kusikitisha!
Siyo hivyo tu, Mulugo aliingiza maneno mengine kutoka kichwani ambayo hayakuwemo kwenye hotuba yake hiyo.  Mfano, aliingiza neno “geographically” katika sentensi hiyo kabla ya neno “located”, kitu ambacho kilionyesha wazi hakuwa anaiamini au aliipuuza hotuba yake hiyo iliyokuwa imeandikwa!
Makosa ni mengi ajabu.  La pili ni  kwamba sentensi hiyohiyo aliisoma hivi: “The United Republic of Tanzania is geographically located in east Africa.”
Kwa aliyeisoma vizuri sentensi hii atangundua kwamba ilikuwa na kasoro mbili.  Ya kwanza ni kwamba Mulugo aliongeza neno “geographically” ambalo halikuwa limeandikwa katika hotuba hiyo.  Pili, ukiisoma vizuri sentensi hiyo kuna maneno ambayo aliyaacha katika hotuba hiyo ambayo yalikuwa yameandikwa.
Makosa ni mengi, na yote ni mfano mzuri wa uzembe na kazi za kulipua zinazofanywa na watumishi wa umma karibu katika kila kona.
Cha kusikitisha zaidi ni kwamba uzembe huu wa kisomi umefanywa na mtu ambaye akiwa anazungumza na Clouds FM alijisifu kuwa ni msomi na mtu ambaye aliwahi kuwa mwalimu, lakini uhalisia umeonyesha mapungufu yake makubwa!
Waziri Mulugo ni mmoja tu ya mifano ya kusikitisha na kuudhi inayokwenda kwa jina la viongozi, watu ambao wengi wao wamekuwa ni kichocheo cha kuwakatisha tamaa wananchi wenzao kwa kuwaongezea majonzi ya kiuchumi, kijamii na kisiasa kutokana na kukosa umakini katika kazi zao.
Pia tukio hilo la Mulugo linachochea madai lukuki kwamba uongozi wa nchi hii ni jambo la “kupeana” kirafiki na si lenye kutokana na utaalam au utendaji bora!
Kwa Mulugo, njia ya kujitoa katika aibu hii na kupunguza hasira za Watanzania ni KUACHIA NGAZI MARA MOJA!

WAREMBO WA REDD'S MISS TANZANIA 2012 WATEMBELEA TBL

Wednesday, September 5, 2012

Dr. Dre Aongoza kwa utajili katika mziki wa Hip Hop 2012

Dr. Dre (photo: Johnny Nunez, WireImage)Six years ago Dr. Dre was walking along the beach with Interscope Records chief Jimmy Iovine, pondering whether or not he should launch his own shoe line. "[Forget] sneakers," said Iovine. "Let's sell speakers!"
It might have been the best piece of advice the rapper-producer ever received. In 2008 he teamed with Iovine and a handful of other partners to launch Beats By Dr. Dre, which now sells more than half of the country's premium headphones ($100 and up). That's music to the ears of Dr. Dre, who collected $100 million pretax when handset maker HTC paid $300 million for a 51% stake in the company last year.

With $110 million in pretax earnings, Dr. Dre is this year's Hip-Hop Cash King—despite the fact that his long-awaited album, Detox, remains on the shelf. He's not the only one on the list who banks the bulk of his bucks outside the recording studio. Diddy ranks No. 2 with $45 million, thanks mostly to a share of profits from Diageo's Ciroc vodka; Jay-Z ranks third with $38 million, pulling in more than half his annual earnings from ventures including ownership stakes in cosmetics company Carol's Daughter, the Brookyln Nets and a joint venture with battery maker Duracell. Last year, Jay-Z topped the list with $37 million.
Jay-Z and New Jersey Nets owner Lewis Katz (photo: Johnny Nunez, WireImage)"The reality of it is, you want to do something that you own," says frequent Jay-Z collaborator Timbaland, who ranks No. 20 on the list with $6 million. "You want to own what you put your heart into. That's how you make money."
Kanye West ranks fourth on the list with $35 million, fueled by his Watch the Throne album with Jay-Z and the ensuing tour, followed by Lil Wayne at $27 million. The diminutive rhymester's latest album, Tha Carter IV, sold a million copies in its first week; he also launched clothing line Trukfit and a partnership with Pepsi's Mountain Dew, the first major product endorsement in the veteran rapper's career.
Lil Wayne is joined on the Cash Kings list by labelmates Drake (No. 6) and Nicki Minaj (No. 8), who banked $20.5 million and $15.5 million, respectively, thanks to new albums, tours and product endorsements with companies like Kodak and Pepsi. Their boss, Cash Money co-founder Bryan "Birdman" Williams, ranks seventh with $20 million. Even lower down on the list, artists are getting paid considerable sums to shill products.
"We've received a lot of income based around endorsements," says former Def Jam President Kevin Liles, who now manages a host of artists including No. 18 Young Jeezy. "A lot of brands are saying, 'Hey, there's a value proposition, instead of this freewheeling spending … I have some guaranteed curators and travel agents that can help me reach the consumer in a better way.'"
Yet for a few artists, music alone is a viable path to earning millions. No. 9 Eminem sold more albums last decade than any artist in the world, and continues to cash in from his extensive back catalog and occasional tour dates, pulling in $15 million.
Ludacris rounds out the top ten with earnings of $12 million. The multihyphenate mogul's non-musical ventures include Conjure cognac, headphone line Soul, voiceovers for RadioShack and roles in movies such as Fast Five and New Year's Eve.
"We work so hard that we never get a real chance to stop and reflect on what we've done sometimes," says Ludacris. "So the FORBES list is a great representation of, 'You know what, wow, we are out here working as hard as hell!'"

To compile the Cash Kings list, which charts pretax earnings for all living artists whose work is primarily classified as hip-hop or rap, we looked at income from touring, record sales, publishing, films, merchandise sales, endorsements and other ventures. Management, agent and attorney fees are not deducted; earnings are tabulated from May 2011 to May 2012 and based on data from Pollstar, the Recording Industry Association of America and Nielsen SoundScan, and from interviews with numerous managers, lawyers, record executives and some of the artists themselves.
All in all, hip-hop's top 20 earners pulled in $415 million last year, the most since 2008's $515 million. The more recent total got a heavy boost from Dr. Dre's impressive haul, but it doesn't mean he's resting on his financial laurels. Earlier this summer, he and his partners bought back half of the 51% stake in Beats that they sold to HTC nearly a year ago—meaning that fans waiting for his new album might have to hold out a little longer.
"I understand why Dre didn't finish Detox," says Liles, with a laugh. "It's called Beats."

Sunday, July 1, 2012

FEDHA ZA MATIBABU ZAPATIKANA,MADAKTARI WAKATAA MSAADA WA SERIKALI

Ulimboka apelekwa nje kutibiwa  Send to a friend
Sunday, 01 July 2012 08:12
0digg
Wananchi wakiwa wamelizunguka gari la wagonjwa lililompeleka Dk Steven Ulimboka kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya kupelekwa nje kwa matibabu.Picha na Silvan Kiwale

Geofrey Nyang’oro
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka amesafirishwa kwenda nje ya nchi kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.Kusafirishwa kwake kunafuatia hatua ya jopo la madaktari waliokuwa wakimhudumia, kueleza mabadiliko ya hali ya afya yake, yaliyosababisha figo kushindwa kufanya kazi, hali iliyolazimu pamoja na matibabu mengine, kwenda   kusafishwa damu.

Ingawa madaktari hao wamekataa kuweka wazi nchi anayopelekwa, kuna taarifa kwamba huenda amesafirishwa kwenda nchini Afrika Kusini.

Katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi) jana makundi mbalimbali ya watu yalifurika wakiwamo wanaharakati na ndugu wa Dk Ulimboka,  waliofika kwa lengo la kumsindikiza Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Watu hao waliofika hospitalini hapo kuanzia asubuhi, waliendelea kubaki  eneo hilo hadi saa 6:45 mchana msafara ulipoanza.

Dk Ulimboka alisafirishwa kwa gari la kubebea wagonjwa la kampuni ya AAR. Alipofika uwanjani, alisafirishwa kwa  ndege ya kukodi ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini, akisindikizwa na watu watatu.

Usiri safari ya Dk Ulimboka

Mapema jana asubuhi, taarifa za kusafirishwa kwake zilizagaa, lakini hapakuwa na mtu wa kuthibitisha safari hiyo na namna atakavyosafiri.

Katika safari hiyo, Dk Ulimboka amesindikizwa na  Dk Pascal Lugajo, kaka yake, Dk Hobakile Ulimboka na mke wake,  Dk Judith Mzovela.

Madaktari watoa tamko

Baada ya Ulimboka kusafirishwa, madaktari walilaani kitendo cha kutekwa na kupigwa mwenzao na kuitaka Serikali itoe tamko juu ya usalama wao.

Katibu wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Edwan Chitage aliwaambia waandishi wa habari kuwa tukio hilo na vitisho vya kufukuzwa kazi wanataaluma hao kunakofanywa na Serikali, kumezua  hofu kwa  madaktari wote nchini.

“Tunaamini Serikali inawajibika kwa watu wake, kwa hali ilivyo sasa madaktari wapo kwenye hofu kubwa, tunataka itoe tamko juu ya usalama wa madaktari,” alisema Dk Chitage.

Akizungumzia hali ya Dk Ulimboka, alisema imekuwa ikibadilika mara kwa mara hali ambayo imesababisha kumpeleka nje ya nchi kwa matibabu zaidi .

Chitage alisema kama Serikali ingekuwa na nia ya kuboresha huduma hospitalini hapo ingeweza kununua mashine ya CT Scan ambayo alisema bei yake ni sawa na Toyota ‘Shangingi’ moja.

Kwa upande wao wanaharakati wa haki za binadamu, jana walifika Uwanja wa Ndege wakiwa na mabango yenye ujumbe tofauti wakilaani kitendo alichofanyiwa Dk Ulimboka.

Dk Chitega alisema hadi kufikia jana, walikuwa wamepata fedha zilizokuwa zikihitajika kwa ajili ya matibabu yake. Juzi madaktari hao walisema wanahitaji Dola za Marekani 40,000 (Sh63.2 milioni) ili kumtibu mwenzao nje ya nchi.


Serikali na tiba ya Ulimboka


Wakati mgomo wa madaktari ukiingia siku ya nane leo, Serikali imesema ilikuwa tayari kugharimia matibabu ya Dk Ulimboka.

Msemaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Nsachris Mwamwaja jana alisema Serikali ilikuwa tayari kugharimia matibabu ya daktari huyo.

Mwamaja aliliambia Mwananchi Jumapili kuwa ni haki ya mgonjwa anayepewa rufani ya kutibiwa nje, kugharimiwa na Serikali, lakini
msaada huo wa Serikali ulikataliwa na madaktari hao na kuitaka ikae mbali na matibabu ya kiongozi wao.

“Sisi tulishaanza maandalizi ya kugharimia matibabu yake, lakini madaktari wenyewe walikataa msaada wa Serikali,” alisema Mwamwaja.

Hali yazidi kuwa tete

Kutokana na mgomo huo, uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC mjini Moshi, umewatimua zaidi ya madaktari 80 walioko kwenye mafunzo kwa vitendo.

Hadi kufikia juzi, madaktari 146 walikuwa wamefukuzwa kutokana na mgomo huo katika hospitali za Bugando na Sekou Toure mkoani Mwanza na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya na ile ya Mkoa wa Dodoma.

Mbeya

Habari kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mbeya zinadai kwamba, baada ya uongozi wa hospitali hiyo kulazimika kuomba madaktari wengine kutoka hospitali za jijini Mbeya ili kuongeza nguvu, madaktari hao nao wameonekana kutoridhishwa na ombi hilo.

Habari hizo zinasema kwamba, licha ya madaktari hao kupatikana na kwenda hospitalini hapo, walisikika wakilalamika kwamba wao hawapo tayari kufanya kazi sehemu yenye mgogoro na kwamba wao hawawezi kufanywa kama chambo kwa kuhofia usalama wao.

Akizungumza kwa njia ya simu Mkurugenzi wa Hospitali hiyo,  Dk Eliuter Samky alikiri kuzidiwa na kusuasua kwa utoaji huduma kwa wagonjwa ambapo alisema kuwa hadi sasa huduma zinazotolewa ni zile za dharura pekee na zile za kawaida wagonjwa wanaambiwa waende Hospitali ya Mkoa.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya, Dk Seif Mhina, alisema kwa sasa hali inaendelea vizuri kutokana na kujipanga vyema kukabiliana nayo, licha ya kuwa bado kuna tatizo la upungufu wa vitanda hivyo kusababisha wagonjwa kulala chini.

Tanga

Baadhi ya wagonjwa katika Hospitali ya Mkoa wa Tanga ya  Bombo, wameitaka Serikali kukaa pamoja na madaktari ili kumaliza tatizo hilo.

Wamesema hali iliyofikia sasa ni mbaya hivyo ni busara pande hizo mbili kukaa meza moja kutatua mgogoro huo bila kujali nani kati yao amesababisha.

Sakina Abdallah ambaye amelazwa katika wodi ya wazazi ya Gallanis, alisema amesikitishwa na baadhi ya wanasiasa wanaoshabikia kutekwa Dk  Ulimboka.

“Binafsi hali inayoendelea ya mgomo wa madaktari inanihuzunisha sana kwani tunaoumia ni sisi wananchi tunaotibiwa katika hospitali hizi,” alisema Sakina.


Godfrey Jambia ambaye ni majeruhi aliyelazwa katika hospitali hiyo, alisema Serikali inatakiwa kutatua madai ya madaktari hao ili kuwanusuru raia wasio na hatia.

                   
NCCR yaivaa Serikali

Chama cha NCCR-Mageuzi kimesema Serikali ina maswali ya kujibu kutokana na kushindwa kutatua mgomo wa madaktari nchi nzima.

Chama hicho kimesema Serikali haitakiwi kutumia nguvu ya dola kumaliza mgomo na kuitaka ifute kesi iliyofunguliwa mahakamani ili kukaa meza ya majadiliano na madaktari hao kwa kuwa raia wasio na hatia, wanapoteza maisha kwa kukosa matibabu.

Akizungumza wakati akifungua mkutano wa Halmashauri Kuu (Nec) ya chama hicho Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa chama, James Mbatia, alisema hata kama suala hilo limefika mahakamani, bado linazungumzika kwa kuwa afya za Watanzania zinawahusu wote.

“Hivi Serikali inashindwa kuliondoa jambo hilo mahakamani na kukaa meza moja na madaktari kumaliza tatizo hili..., katika hili lazima tuseme, yaani watu wanakufa tukae kimya, haiwezekani hata kidogo,” alisema Mbatia na kuongeza:

“Ubabe hauwezi kuingizwa katika uhai wa Watanzania, kama majadiliano ya awali hayakufanikiwa basi wawekwe watu makini watakaosimamia majadiliano haya, hata wabunge wanaweza kusimamia suala hili, mgomo huu hauna itikadi za vyama unawahusu wananchi wote.”


Habari Hii imeandaliwa na Fidelis Butahe, Claud Mshana, Dar, Burhani Yakub,Tanga na Godfrey Kahango, Mbeya

Sunday, June 10, 2012

NAPE ASHIDWA KUKANUSHA MADAI YA CHADEMA KTK VIWANJA VYA CHADEMA-SQUARE

Saturday, 09 June 2012 08:13
0digg
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye
Dotto Kahindi na Leon Bahati
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amesema chama chake hakina mpango wa kuutumia mkutano wake wa leo kwenye Viwanja vya Jangwani kujibizana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na badala yake, kitajikita zaidi katika kutoa somo kwa wajumbe wapya wa mashina na viongozi wa matawi Mkoa wa Dar es Salaam.

Kauli hiyo ya Nape inatoa mtazamo tofauti na tetesi kwamba  CCM kitatumia mkutano huo kukijibu chama hicho kikuu cha upinzani ambacho nacho kilifanya mkutano kwenye viwanja hivyo hivi karibuni.
Katika mkutano huo ambao Chadema kilizindua Mpango wake wa Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) mwishoni mwa mwezi uliopita, kiliorodhesha shutuma nyingi dhidi ya Serikali ya CCM zikiwemo za kusababisha maisha magumu kwa Watanzania.

Nape alisema mkutano huo uliandaliwa na CCM Mkoa wa Dar es Salaam hata kabla ya huo wa Chadema na lengo lake ni kuwakutanisha viongozi wapya wa chama hicho tawala na viongozi wa juu wa chama na Serikali, wakiwemo mawaziri watakaofafanua shughuli zao za kiutendaji.
“Mkutano huu unalenga kuwafundisha wajumbe wa nyumba kumi na viongozi wa mashina waliochaguliwa hivi karibuni namna ya utendaji wa Serikali, kwa kuwa wao bado ni  wapya kiuongozi na wanahitaji kupewa somo,” alisema Nape.

Alipoulizwa kama mkutano huo ni moja ya hatua za kufuta nyayo za Chadema hasa baada ya kuzindua M4C, Nape alisema: “Mkutano huu tuliuandaa mapema kabla hata ya Chadema hawajafanya mkutano wao. Ila kilichochelewesha ni Mkutano wa Halmashauri Kuu (Nec) ya CCM,” alisema Nape na kuongeza:

“Mkutano huu awali, ulikuwa ufanyike ndani ya ukumbi lakini kwa kuwa watu wengi walipenda kushiriki tumeamua kuufanyia Jangwani ambako wanachama na viongozi wa CCM watapata fursa ya kusikia sera za viongozi wa chama na watendaji wa Serikali.”

Aliwataja mawaziri ambao watakuwa katika mkutano huo kuwa ni pamoja na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe ambaye atazungumzia masuala ya usafiri wa reli, bandari na anga na Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli ambaye atazungumzia masuala ya miundombinu na barabara.

Wengine ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira ambaye atazungumzia hatima ya Watanzania katika masuala ya ajira na vijana na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ambaye atazungumzia mipango ya wizara yake.

M4C
Mei 25 mwaka huu, Chadema kilizindua mkakati wake mpya wa ‘Movement For Change-M4C’ ukiwa na lengo la kukiandaa chama hicho kushinda Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliwataka wanachama na wananchi kwa ujumla kukichangia fedha chama hicho ili kufanikisha kampeni aliyoielezea ni ya kukiondoa CCM madarakani mwaka 2015.

Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa alisema maisha ya Watanzania si mazuri, vyakula vinaongezeka bei kutokana na Serikali ya CCM kutokuwa makini hivyo akawataka wabunge wa chama hicho kuibana kupitia Bunge lijalo la Bajeti.

Aliilaumu Serikali kwa kutotumia vizuri kodi za Watanzania kwa ajili ya shughuli za maendeleo kwa kuwalipa watumishi ambao nafasi zao hazina manufaa kwa wananchi.
Dk Slaa alilalamikia kitendo cha kuongeza kodi katika mafuta ya taa ili watu wasichakachue mafuta ya dizeli akisema ni mwiba kwa Watanzania.

R.I.P BOB MAKANI, TUTAUENZI MCHANGO WAKO KATIKA KUPIGANIA DEMOKRASIA NA MAENDELEO NCHINI TANZANIA


 Send to a friend
Sunday, 10 June 2012 09:38
0digg
Mzee Bob Makani
Na Mwandishi Wetu
MWASISI wa Chadema na Mwanasheria mkongwe nchini Bob Makani, amefariki dunia usiku katika hospitali ya Aga khan, jijini Dar es Salaam.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe, Makani alizidiwa ghafla saa 3: 00 usiku wa kuamkia leo na kukimbizwa katika Hospitali ya Aga Khan ambako alifariki dunia saa 4.15 usiku.

“Amekuwa anaumwa muda mrefu, mara kadhaa akipelekwa hospitali na baada ya muda anaruhusiwa, lakini hii ya sasa alikua nyumbani akazidiwa ghafla wakampeleka hospitali na ilipofika saa 4.15 wakasema amefariki,” alisema Zitto.

Zitto alisema kuwa, suala la wapi utakapozikwa Makani ambaye ni Katibu Mkuu wa Kwanza na Mwenyekiti wa pili wa Chadema, litajulikana baada ya kujadiliana na familia ya marehemu.

“Suala la wapi atazikwa kama ni Shinyanga ama Dar es Salaam, litajulikana baada ya kuzungumza na familia yake, kwa sasa tunashughulika kwanza na kuhifadhi mwili wa mzee wetu,” alisema Zitto.
Zitto alisema msiba wa utakuwa nyumbani kwa marehemu eneo la Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam.

Kwa siku za hizi karibuni afya yake imekuwa ikizorota na kumfanya kuripotiwa kuanguka mara kwa mara alipokuwa akifanya shughuli zake.

Januari 17 mwaka huu katika msiba wa aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum wa Chadema Regia Mtema, Makani alianguka muda mfupi baada ya kuuaga mwili wa marehemu.

 Baada ya tukio hilo, alibebwa na kupelekwa pembeni ambako alipepewa kwa takriban dakika tano kisha kurejea katika hali yake ya kawaida na kurudi kwenye kiti chake

Alikuwa Katibu Makuu wa kwanza wa Chadema kati ya mwaka 1993 hadi 1998, alikuwa Mwenyekiti wa chama hicho kuanzia mwaka 1998 hadi 2004 na amegombea ubunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini kwa mara tatu kati ya mwaka 1995 na 2000 na mwaka 2005.

Kazi ambazo amewahi kuzifanya serikalini; alikuwa naibu mwanasheria mkuu wa serikali, Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) mwaka 1966 na elimu yake ana shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu Cha Makarere nchini Uganda.

Ni mzaliwa wa Wilaya ya Kishapu, mkoani Shinyanga akitokea kwenye ukoo wa kichifu wa Makani.

Sunday, April 8, 2012

KANUMBA WATANZANIA WALIKUPENDA SANA, LAKINI MUNGU AMEKUPENDA ZAIDI, R.I.P KANUMBA THE GREAT

Kanumba afariki  Send to a friend
Saturday, 07 April 2012 21:45
Marehemu Steven Kanumba
MAELFU ya wapenzi wa sanaa ya filamu nchini, alfajiri ya kuamkia jana waliduwaa mithili ya watu waliopigwa sindano ya ganzi baada ya kuenea kwa taarifa za kifo cha ghafla cha msanii namba moja wa filamu nchini, Steven Charles Kanumba (28).

Taarifa za kifo cha Kanumba zilisambaa kwa kasi mithili ya moto katika nyika kavu na kuikuta alfajiri ya jana, ikigeuka kibarua kigumu kwa idadi kubwa ya watu, kusaka stesheni mbalimbali za redio, televisheni mitandao ya kompyuta huku wengine wakihangaika kupiga simu huku na kule, kutafuta ukweli wa tukio hilo,lililotikisa si Tanzania tu bali ukanda mzima wa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla.


Kanumba alifariki usiku wa kuamkia jana nyumbani kwake, Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi, Kanda ya Kinondoni, Charles Kenyela, ziinaeleza kuwa kifo cha msanii huyo kilitokana na ugomvi uliotokea kati yake na mpenzi wake ndani ya nyumba yake.

Taarifa za kifo cha Kanumba zilianza kusambaa kuanzia saa 10.00 alfajiri na kuenea kwa kasi ambapo hadi kufikia saa moja asubuhi, mamia ya watu walikuwa wamejazana nyumbani Kanumba kutaka kuthibitisha habari hizo.

Kadri muda ulivyozidi kusogea ndivyo idadi ya watu ilizidi kuongezeka nyumbani kwa msaani huyo ambaye amejizolea umaarufu mkubwa kutoka na filamu zake kuuzwa na kuoneshwa katika vituo mbalimbali vya televisheni, ndani na nje ya nchi.

Miongoni mwa watu waliomiminika kwa haraka nyumbani kwa kanumba jana ni wasanii wa fani mbalimbali nchini,  wanasiasa na viongozi mbalimbali wa Serikali

Chanzo cha kifo chake

Kwa mujibu wa maelezo ya mdogo wake aitwaye Seth ambaye alikuwepo eneo la tukio, alisema kaka yake alishinda nyumbani na baada ya kula chakula cha jioni, alimwambia wajiandae kutoka.

Seth alisema kuwa wakati Kanumba akiwa tayari amejiandaa, walisikia mlio wa gari lifunga breki nje ya nyumba.

Alisema gari hilo lilikuwa limemleta mpenzi wa kaka yake msanii wa filamu, Elizabeth Michael maarufu kwa jina la Lulu ambaye aliingia ndani na kwenda moja kwa moja chumbani kwa Kanumba.

Baada ya kuingia ndani, muda mfupi alisikia sauti zilizoashiria kuwa kulikuwa na ugomvi kati ya wapenzi hao.

“Ghafla ulizuka mzozo ndani na dakika chache baadaye, Lulu alitoka na kuja kuniambia kuwa Kanumba amedondoka baada ya kujigonga ukutani na kwamba yupo taabani hajitambui,” alisema Seth.

Alisema alipoingia chumbani, alimkuta kaka yake akiwa katika hali mbaya hivyo akaamua kumpigia simu daktari wake, ambaye alipofika na kuwashauri wampeleke haraka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kupatiwa matibabu.

Seth alisema kabla ya kufika Muhimbili  walipitia Kituo cha Polisi cha Oysterbay kupatiwa Fomu ya matibabu (PF3).

Hata hivyo, baada ya polisi kupata maelezo ya awali ya ugomvi huo, walimshikilia Lulu kituoni hapo na kumwacha Seth akimpeleka Kanumba hospitali.

Alisema walipofikia Hospitali ya Muhimbili, madakati waligundua kuwa tayari Kanumba alishaaga dunia.

Kamanda Kenyela

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alisema Kanumba alikufa kutokana na ugomvi uliotokea kati yake na rafiki yake wa kike Lulu.

 "Kanumba amefariki usiku wa kuamkia leo (jana) majira ya saa tisa usiku, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni ugomvi kati yake na rafiki yake wa kike anayejulikana kwa jina la Elizabeth Michael 'Lulu' mwenye umri wa miaka 18.

Alisema kabla ya ugomvi huo kutokea kati yao wakiwa chumbani, simu ya Lulu iliita na akaamua kutoka nje kupokea kitendo kilichomuudhi Kanumba.

Kamanda Kenyela alisema Kanumba aliamua kumfuata Lulu nje huku akifoka kwa sauti akitaka aelezwe kwanini alitoka nje kupokea simu huku akimtuhumu kuwa huenda alikuwa akizungumza na mwanaume mwingine.

Aliongeza baada ya Lulu kuona Kanumba akimfuata aliamua kukimbia kutoka nje ya geti , lakini kabla hajafanikiwa kufungua geti, Kanumba  alimkamata na kumrudishwa ndani.

Kamanda Kenyela, alisema Kanumba akiwa amemshikilia waliingia wote chumbani na kufunga mlango.

Hata hivyo, alisema haijulikani nani aliyefunga mlango, ingawa maelezo ya Lulu anadi kuwa aliyefunga mlango ni Kanumba.

Kamanda huyo alisema Lulu anaeleza kuwa baada ya Kanumba kufunga mlango, alimuona akilegea na kujigonga kisogo chake kwenye ukuta wa chumba hicho kabla ya kuanguka chini.

Alibainisha kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa Kanumba alikuwa amekunywa Whisky (pombe kali) aina ya Jacky Daniel, hata hivyo, bado wanachunguza zaidi kujua kama kweli Kanumba alilegea tu na kuanguka, ama alipigwa na kitu kizito kichwani au alisukumwa kwa nguvu na kumfanya aangukie kisogo.

“Uchunguzi ukikamilika tutampeleka mahakamani kwa tuhuma za mauaji,” aliongeza Kamanda Kenyela.

Rais Kikwete atoa pole

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania –TAFF kuomboleza kifo cha Kanumba,

Katika taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, Rais Kikwete ameelezea kushtushwa na kuhuzunishwa na kifo cha msanii huyo ambaye amemtaja kuwa mahiri na mwenye kipaji kikubwa.

“Nimepokea kwa mshtuko na huzuni nyingi taarifa za kifo cha Ndugu Steven Charles Kanumba. Kupitia filamu zake, ameburudisha na kuelimisha jamii yetu kwa namna ambayo haiwezi kupimika. Alikuwa msanii mahiri na mwenye kipaji kikubwa ambaye mchango wake mkubwa katika kuanzisha, kukuza na kuimarisha sanaa ya filamu nchini hautasahaulika,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Rais Kikwete alisema Kanumba ametoa mchango mkubwa kupitia sanaa ya filamu na kutokana na uwezo mkubwa wa kisanii, Watanzania wataendelea kumkumbuka kwa mchango wake.

“Nakutumia wewe Rais wa TAFF salamu zangu za rambirambi na kupitia kwako kwa wasanii wote wa filamu na sanaa nyingine kufuatia msiba huu mkubwa kwa fani yetu ya sanaa.

Mama wa Kanumba azungumza

Mama mzazi wa Kanumba, Flora Mutegoa amesema alizungumza na Kanumba kwenye simu saa chache kabla ya kifo chake, huku akimtaka arudi Dar es Salaam haraka, kutoka Kagera alikokwenda kumsalimia mama yake (bibi wa Kanumba), ili aje amuage kabla hajasafiri kwenda Marekani.

 Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana katika Uwanja wa Ndege wa Bukoba wakati akijiandaa kusafi kwenda jijini Dar es Salaam, Flora alisema alizungumza na mwanawe  kwa simu usiku huo huo saa chache kabla ya kufikwa na mauti kumkuta.

Mama huyo ni mzaliwa wa Kijiji cha Itoju, Kata ya Izigo, Wilaya ya Muleba, mkoani Kagera lakini kwa sasa anaishi  Dar es Salaam .

 "Mwanangu niliongea naye usiku akiwa mwenye furaha na tulitaniana sana,alisema anatuma nauli nirudi Dar es Salaam tuagane, kwani alikuwa na safari ya kwenda Marekani,"alisema Flora.

 "Sina cha kuongea naomba mniombee katika kipindi hiki kigumu jana nimeongea naye kwenye simu leo naambiwa mwanangu amekufa,"alisema huku akibubujikwa machozi.
Aliongeza kuwa Kanumba aliwahi kumdokeza kuhusu ndoto zake za baadaye kuwa alikuwa na matarajio ya kufika mbali zaidi katika sanaa ya uigizaji.

Maneno ya mwisho ya Kanumba

Siku za hivi karibuni Kanumba alikuwa akichapisha habari mbalimbali katika mitandao ya kijamii zilizokuwa zikisisitiza  upendo.

Katika mtandao wake wa Twiter na Blog yake  juzi saa sita mchana alichapisha habari akiwasi watu kufanya mambo mema kwa watu wengine ili wapate baraka.

"Tunavyofanya kwa ajili yetu huwa yanakufa nasi, lakini tunayoyafaya kwa ajili ya wengine hubaki duniani," sehemu ya maneno yake ya mwisho aliyoyaweka katika Balog yake juzi kabla ya kifo chake .


Mbali na ujumbe alioandika siku moja kabla ya kufikwa na mauti, Kanumba amekuwa akichapisha katika mitandoa yake ya kijamii maneno ya busara na kukemea chuki miongoni mwa jamii tangu mwanzoni mwa mwaka huu.

Maneno ya mwisho kwa wasanii wenzake

Kanumba mbali ya kutoa maneno ya busara kwa jamii, pia alikuwa akitumia mitandao yake kutoa maneno ya kuwapa moyo wasanii wenzake.

Kwa mfano Januari 24 mwaka huu baada ya kutwaa Tuzo ya ZIFF, aliandika kwenye mtandao maneno aliyoyaelekeza kwa wasanii wenzake akisema,:

 "Maneno yangu ya mwisho, hata tukiwa na uwezo wa kuhamisha milima kama hatupendani katika tasnia ni kazi bure,kile kilicho moyoni ndio kioneshe usoni na si vinginevyo".

"Kama wanichukia moyoni basi onyesha usoni na kama wanipenda moyoni basi onyesha usoni na si vinginevyo,Isiwe moyoni wanichukia halafu usoni wanichekea,Hii sanaa ni karama tuliyobarikiwa na Mungu tuitumie vyema kwa ajili ya utukufu wake maana ipo siku atatuuliza na kutudai,kama katupa bure basi anao uwezo wa kutuny'ang'anya pia','soma Wakorintho uone jinsi Mungu alivyogawa karama hizi na ni kwanini katugawia." sehemu ya maneno yake kwa wasanii wenzake nchini.

Mamia wafurika nyumbani kwake

Mamia ya watu jana walifurika nyumbani kwa msanii huyo kiasi cha barabara ya Sinza Uzuri inayopita karibu na nyumba hiyo kufungwa.

Watu kutoka kona mbalimbali za jiji la Dar es Salaam baadhi yao wakiwa wanabubujikwa, machozi walifika kushuhudia kwa macho yao kile wanachokisikia kwenye vyombo vya habari. Kulikuwa na msongamano mkubwa pia wa magari katika eneo hilo.

Historia yake

Kanumba alizaliwa Januari 8, 1984  mkoani Shinyanga,  ni mtoto wa tatu katika familia yao akiwa na dada zake wawili.

Alisoma Shule ya Msingi Kaboya, mjini Bukoba na baadaye akahamia Shinyanga ambako alimalizia elimu yake ya msingi katika Shule ya Bugoi.

Alijiunga kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari, Christian Seminari iliyopo Kongowe na baadaye akaendelea na masomo ya kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari ya Jitegemee.

Dada wa marehemu

Dada wa marehemu, Abela Kajumolo alisema kuwa mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa marehemu Sinza Vatican.

Alisema familia imepanga mazishi ya Kanumba yatafanyika Jumanne wiki ijayo na kwamba bado hawajaamua kama atazikwa Dar es Salaam au Bukoba," alisema.

Tayari kamati ya mazishi imeundwa na ikiwajumuisha Gabriel Mtitu,  Stephen Jacob (JB) William Mtitu na Issa Mussa (Cloud) ambao wote ni wasanii wa filamu nchini.

Kamati ya usafiri itakuwa na Meneja wa  Clouds Media Group,  Ruge Mutahaba na Vincent Kigosi (Ray).

Enzi za Uhai wake

Marehemu alianza uigizaji miaka ya 2000 akiwa na Kundi la Kaole na baadaye kuingia katika fani ya filamu wakati huo akifanya kazi zake chini ya Kampuni ya Game First Quality.

Hata hivyo, alifanya kazi na kampuni hiyo hadi alipofanikiwa kumiliki kampuni yake binafsi ya Kanumba The Great Film.

Marehemu Kanumba pia ameshirikiana na wasanii wakubwa barani Afrika katika uingizaji akiwamo Ramsey Nouah wa Nigeria ambaye amecheza naye filamu ya Devil’s Kingdom na ambayo imezinduliwa mapema mwezi huu nchini Ghana.

Pia hadi mauti yanamkuta, Kanumba alikuwa akiendelea kutengeneza filamu ya Ndoa yangu ambayo alikuwa akiiandaa na mwigizaji mahiri wa kike, Jackline Wolper.

Kuingia kwenye siasa

Marehemu Kanumba pia katika siku za hivi karibuni aliwahi kukaririwa akisema atagombea Ubunge katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, akini hakuweka bayana kupitia chama gani wala jimbo.

Kanumba amekuwa  msanii wa kwanza nchini kuitangaza Tanzania ndani na nje ya bara la Afrika kupitia filamu.

Wasanii wenzake wanasemaje?

Suzan Lewis maarufu kama 'Natasha'  ambaye ni msanii mkongwe anasema kifo cha Kanumba kimemwachia kumbukumbu ambayo haiwezi kusahaulika.

“Nitamkumbuka Kanumba daima katika maisha yangu, alikuwa ni mtu wa watu alikuwa ni msanii pekee aliyepiga hatua na kuishi maisha ya wasanii wa kimataifa.

Yvonne Cherryl (Monalisa): “Kifo cha Kanumba kimefifisha ndoto zangu za kuigiza pamoja na wasanii maarufu kutoka Hollywood, tulikuwa na maandalizi hayo na Kanumba ndio alikuwa kila kitu katika suala hilo sikutegemea kama hili lingetokea.”

Wema Sepetu: "Siamini, na sitaki kuamini kabisa, nipo ndotoni sijui niseme nini,"alisema Wema huku akiangua kilio kilichomfanya ashindwe kuendelea kuongea.

Hatman Mbilinyi: " Alikuwa ni mcheshi sana, alipenda watu waliofanya naye kazi, nimepokea kwa ugumu, siamni kwa sababu ni saa chache tu tulikuwa pamoja, hakuumwa ni bora angeumwa tukajua aliumwa."

Jerison Tegete ambaye ni Mchezaji wa Yanga alisema alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kupata habari za msiba, na kwamba ameguswa sana na kifo cha Kanumba.

"Inasikitisha sana kwani tumepoteza kijana mdogo na ambaye alikua na nafasi kubwa katika kuielimisha jamii kupitia filamu zake.
Single Mtambalike maarufu Richie alisema ana mwachia Mungu kuhusu kifo cha Kanumba. "Sijui nizungumze vipi kuhusu marehemu kwanza siamini kama kweli Kanumba hatutakua naye katika tasnia hii na si filamu tu hata katika kazi nyingine ambazo tumekua naye karibu yote namwachia Mungu.”

Jacob Steven  amarufu JB alisema ni vigumu kuamini kuwa kanumba kafa kwa vile saa chcahe walikuwa pamoja.

“Ni pigo lisiloelezeka kwa sasa na ni vigumu kuamini kilichotokea kwani saa chache kabla ya kifo chake tuliwasiliana na alioongea kwa furaha bila kutambua nini kitatokea mbele yake katika muda mchache ujao.”

Tangana Iringa wamlilia
Naye Burhani Yakub kutoka Tanga anaripoti kuwa waandaaji wa filamu wa Mkoa wa Tanga wameleza kuguswa kwao na taarifa za kifo cha Kanumba na kuwataka wasanii wa tasnia hiyo kuwa watulivu katika kipindi hiki cha majonzi.
Wakizungumza na Mwananchi Jumapili mara baada ya kusikika taarifa za kifo cha Kanumba jana asubuhi, walisema kifo cha Kanumba ni pigo kubwa kwa tasnia hiyo nchini.
Mtunzi Mkongwe  wa riwaya na mwandishi wa hadithi za Filam wa Jijini Tanga, Faki A. Faki  alisema taarifa za kifo cha Kanumba zimeshtua kwa kuwa ni msanii aliyeikuza sanaa ya filamu nchini.

Tumaini Msowoya anaripoti kutoka Iringa kuw Tumaini Msowoya, Iringa
Wakazi wa Mkoa wa Iringa wakiwamo wasanii wa filamu wamesema kuwa wamepokea kwa masikitiko msiba wa msanii nyota wa filamu Tanzania, Steven Kanumba na kwamba taifa limepata pigo kwa kumpoteza mtu muhimu aliyeweza kutangaza filamu za Kitanzania ndani na nje ya nchi.
Baadhi ya maduka, kati kati ya mji wa Iringa wameamua kuomboleza kifo cha msanii huyo kwa kutoa nje televisheni zao ili kusaidia watu kuona filamu ambazo zimeigizwa na msanii huyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi hao walisema msiba huo umewashtua na kwamba msanii huyo alikuwa na mchango mkubwa kwenye sanaa sanaa kupitia filamu zake.
Katibu wa kundi la sanaa la Mundu, mkoani Iringa, Athanas Kipera alisema hata kundi lake limepata mchango mkubwa kutoka kwa marehemu Kanumba.

Basata wahuzunika
Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) amesema kuwa baraza lake limepokea kwa masikitiko makubwa  kifo cha Kanumba.
"BASATA inaungana na familia za wafiwa na wasanii wote nchini kwa maombolezo  ya msiba huu mkubwa na wa kihistoria, kufiwa na msanii huyu mahili kwenye tasnia ya filamu ni pengo kubwa kwa familia, Sekta ya sanaa na Taifa kwa ujumla kutokana na ukweli kuwa, aliweza kuutangaza utamaduni na sanaa yetu nje ya mipaka,"alisema Gonche Materego ambaye ni katibu mkuu wa Basata.

Alisema Kanumba atakumbukwa kwa moyo wake wa kujituma na kuthamini kazi ya Sanaa toka akiwa Kundi la Maigizo la Kaole ambapo moyo wake huo ulimfanya awe miongoni mwa wasanii walioleta mageuzi kwenye tasnia ya filamu kwa kuifanya kuanza kupendwa na wadau wengi zaidi.

Imeandaliwa na Julieth Kulangwa, Jesca Nangawe, Vicky Kimaro na Phinias Bashaya, Bukoba

Thursday, March 22, 2012

MAWAZIRI MUACHE SIASA KATIKA MATATIZO MAZITO YANAYOHITAJI UTEKELEZAJI, NI NANI ASIJEJUA MATATIZO YA AJIRA TANZANIA?

 Send to a friend

Waziri wa Kazi na Ajira,Kabaka gaudencia

YASEMA AJIRA KWA VIJANA SIYO BOMU, WAZIRI KABAKA AMWAGA TAKWIMU, AELEZA MAANA YA AJIRA

Geofrey Nyangoro

SERIKALI imetoa takwimu za ajira kwa vijana nchini  ikiwa ni majibu kwa kauli za mara kwa mara za Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa ambaye amekuwa akisema tatizo hilo ni kubwa akililinganisha na bomu linalosubiri kulipuka.

Lowassa amenukuliwa katika matukio manne tofauti kuanzia mwishoni mwa mwaka jana na mwaka huu, akionya tatizo hilo la ajira kwa vijana kwamba linahitaji kupatiwa ufumbuzi wa haraka.


Jana, Waziri wa Kazi na Ajira alisema tatizo hilo haliwezi kufafanishwa na bomu na kusema wanaosambaza uvumi huo hawaitendei haki Serikali, kwani tatizo hilo limepungua kutoka asilimia 12.9 mwaka 2000/1 hadi asilimia 11.7, mwaka 2006.


Katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika ofisini kwake Dar es Salaam jana, Kabaka alitoa ufafanuzi wa hali ya ajira nchini na hatua ambazo Serikali inachukua kushughulikia tatizo hilo.

“Hali halisi ya ukuaji wa uchumi nchini ni nzuri lakini, haiwezi kuonekana kama wananchi wake ni maskini na hawana ajira. Hata hivyo, Serikali imekua ikichukua hatua mbalimbali kushughulikia suala hilo ikiwamo la kuhimiza uwekezaji nchini,” alisema Kabaka na kuongeza:


“Kitendo cha wanasiasa kuendelea kusema tatizo la ajira kwa vijana ni bomu linalosubiri kulipuka, siyo kweli na kudai Serikali hayaijafanya kitu wanakuwa hawaitendei haki.”

Alisema utafiti uliofanywa na wizara yake kwa kushirikiana na Taasisi ya Takwimu ya Taifa (NBS), unaonyesha kuwa tatizo hilo limepungua kwa asilimia 1.2.


Mikakati

Waziri Kabaka alisema utafiti uliofanywa na NBS mwaka 2006 ikishirikiana na wizara hiyo unabainisha kuwa nguvu kazi ya Tanzania ni 20.6milioni kati ya watu 37.5 milioni, kwa wakati huo.


Alisema kutokana na utafiti huo, watu 18.3milioni sawa na asilimia 88.3 ya watu hao 20.6milioni walikuwa na ajira huku waliokuwa kwenye ajira ya sekta rasmi wakiwa ni 17milioni sawa na asilimia 92.7.


Kabaka alisema katika utafiti huo, watu 1.3milioni walikuwa kwenye ajira isiyo rasmi huku utafiti ukibaini kuwa kila mwaka watu 800,000 hadi milioni moja wanaingia kwenye soko la ajira.


“Utafiti unaonyesha hali ya ukosefu wa ajira nchini umeshuka kidogo kutoka asilimia 12.9 mwaka 2000/1 na kufikia asilimia 11.7 mwaka 2006, hata hivyo kiwango hicho ni cha juu kwa nchi kama Tanzania ambayo haina huduma za kinga kwa watu wasio na ajira,” alisema Kabaka.


Waziri Kabaka alisema pamoja na kushuka kwa kiwango cha ajira, bado kiwango cha ukosefu wa ajira ni kikubwa huku kikitofatutiana baina ya kundi moja na jingine akisema Tanzania siyo kisiwa hivyo, tatizo linaloikumba dunia la ukosefu wa ajira pia linaikumba nchi hiyo.


Alitaja mikakati ya Serikali kuwa ni pamoja na utekelezaji wa mipango mbalimbali yenye lengo la kukuza ajira ambayo ni pamoja na mpango wa mafunzo yenye kuwezesha vijana kujiajiri, mfuko wa maendeleo ya vijana, mpango wa kukuza ajira kwa vijana na mpango wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na kukuza ajira.


Kabaka alitaja mipango mingine kuwa ni ule wa uwekezaji katika elimu na mafunzo, kujengea uwezo mamlaka za Serikali za mitaa (LGAs) na ajira za moja kwa moja zinazotolewa na Serikali kupitia sekta mbalimbali.


“Serikali imetoa ajira kwa walimu 15,000 wa shule za sekondari na msingi na pia kwa kipindi cha miaka mitano 2007 hadi 2011, ajira 414,679 zimepatikana kupitia Kituo cha Uwekezaji (TIC),” alisema Kabaka.


Waziri Kabaka alibainisha mpango kabambe uliowekwa na Serikali katika kukabiliana na tatizo la ajira, ambao alisema hadi kufikia mwaka 2015, itakuwa imepunguza tatizo la ajira kutoka asimilia 11.6 ya mwaka 2006 hadi kufikia asilimia tano.


Alisema katika kutekeleza hilo, Serikali imeanza kuchukua hatua na kwamba imeanda programu ya kwanza itakayolenga kutambua vijana wote wenye taaluma  aina ya ujuzi walionao katika kila wilaya hapa nchini.


“Programu hii ambayo utekelezaji wake unatarajia kuanza mwaka wa fedha wa 2012/13, imejikita katika kuwatambua vijana na shughuli zao ili kuwajengea uwezo katika kukuza tabia ya kijasiriamali, kuwawezesha kupata ujuzi wa kujiajiri na kukuza soko la bidhaa za ndani kwa kuweka mazingira kutumia bidhaa za Tanzania,” alisema Kabaka.


Alisema pia mpango huo umejikita kuwezesha kijana mmojamoja au kikundi kujiajiri, vijana wasomi na wenye ujuzi wanaohitimu katika vyuo vya elimu ya juu kujiajiri na kutengeneza mazingira ya kuajiri wengine na pia kuwezesha sekta binafsi na taasisi za umma kuwekeza katika sekta zenye kipaumbele katika kutoa ajira.


Waziri Kabaka alisema Serikali imejipanga kutekeleza mpango wa kukuza ajira katika maeneo ya mikoa na wilaya ili kuwezesha kupunguza tatizo la ajira na kuwafanya vijana wasikimbilie mijini.


Maana ya ajira

Akinuuku tafsiri inayotumika duniani na kutambuliwa na Shirika la Kazi la Kimataifa (ILO), Waziri Kabaka alisema maana ya ajira ni shughuli yoyote halali anayoifanya mtu mwenye umri wa kufanya kazi kwa kujipatia kipato na kwa kawaida shughuli hiyo ni ya hiari inayotambuliwa kisheria na hufanywa kwa saa 40 hadi 45 kwa wiki.


Alisema ukosefu wa ajira ni hali ambayo hutokea wakati watu walioko kwenye umri wa kufanya kazi na ambao wangependa kufanya kazi wanatafuta bila ya kuipata.


“Tafisiri hii ya kimataifa haiwajumuishi wale wasiotafuta kazi, wasiopenda kufanya kazi hata kama hawana kazi,” alisema Kabaka na kuongeza:

“Lakini tafisiri inayotumika zaidi Tanzania inatambua wote wasio na kazi na ambao wako tayari kufanya kazi  bila kujali wanatafuta kazi au la na inawahusisha hata  wasio na uhakika wa kufanya kazi hata ya siku moja.”

Alitaja aina tatu za ajira ambazo ni kazi ya staha, kazi chini ya kiwango na ajira maskini.


Alisema ajira za staha ni zile ambazo zina tija kiusalama, heshima haki za wafanyakazi na kipato cha kutosha, wakati ya ile ya chini ya kiwango ni ile ambayo haitoshelezi kutumia uwezo, muda na taaluma yote ambayo ambayo mhusika anayo. Ajira maskini ni ile ambayo kipato kinachopatikana ni cha chini ya kiwango kisichomwezesha mtu kuishi.


Akirejea utafiti wa ILO wa mwaka 2010/11, Waziri Kabaka alisema ripoti hiyo inaonyesha hali ya umaskini na ukosefu wa ajira duniani ni kubwa. Watu 205 milioni dunia kote mwaka 2010 hawakuwa na ajira.

Alisema idadi hiyo ilikuwa sawa na ongezeko la nguvu kazi isiyo na ajira duniani ya watu 27.7 milioni kulinganisha na ile ya mwaka 2007.


Alisema sababu za ongezeko la ukosefu wa ajira kwa mujibu wa ripoti hiyo, ni kutokana na utandawazi, maendeleo ya mawasiliano, mabadiliko ya teknolojia ambayo hayahitaji nguvu kazi nyingi katika utendaji kazi na kudidimia kwa nguvu za kiuchumi hasa katika nchi zinazoendelea.


Lowassa na ajira

Novemba 15, mwaka jana akiwa katika harambee ya ujenzi wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Makasa, Parokia ya Nyakato, Mwanza, Lowassa alionya kuhusu tatizo hilo na kulitaka lisaidie kujenga vyuo vya ufundi.


Alitoa takwimu akisema utafiti wa mwaka 2006, ambao hata hivyo, hakusema ulifanywa na taasisi gani, ulionyesha tatizo hilo kwa sasa limekuwa na kufikia asilimia 15 huku likigusa zaidi vijana wenye umri wa miaka kati ya 15 hadi 24 ambao ndiyo nguvukazi ya taifa... “Ninapozungumza hili siyo nia yangu kumlenga mtu. Mimi ni Yohana Mbatizaji, hii ni sauti inayolia nyikani.”


Novemba 29, mwaka huo wa jana akiwa harambee ya ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKT), Usharika wa Amani Sabasaba, Singida, Lowassa alirudia tena suala hilo la tatizo ajira.


Mapema mwaka jana, Lowassa pia alifanya mkutano na waandishi wa habari Mjini Arusha na kuzungumzia tatizo hilo la ajira ambalo alilifananisha na bomu.


Jumatatu iliyopita, Lowassa alirejea kauli hiyo alipokuwa katika sherehe za uzinduzi wa Jimbo jipya la Kanisa Katoliki Ifakara akisema: “Nawaomba maaskofu katika miradi yenu mlipe kipaumbele suala la tatizo la ajira kwa vijana.... hili kama tulivyosema ni bomu linalosubiri kulipuka...”

Monday, March 19, 2012

Wananchi tunaitaka chadema

Default

Kuna upotoshaji mkubwa sana unafanyika hivi sasa ambao unafanyika katika namna ya hatari sana, naiweza kuifafanisha namna hiyo sawa sawa na mtu anaesema moto ni joto au upofu ni usingizi. Wanasiasa waliomadarakani wanajaribu kuyawekea mahitaji ya wananchi dhana ya kisiasa.

Wakati wananchi wanasema tunataka Mfumo bora wa elimu watawala wanasema CHADEMA haiwezi kuuleta, sababu DR SLAA Aliiba pesa kanisani.


Wananchi wanasema tunataka mfumuko wa bei udhibitiwe, watawala wanasema CHADEMA haiwezi kudhiti mfumuko wa bei sababu MBOWE ni DJ


Wananchi wanasema tunataka huduma bora za afya, watawala wanasema, DR Slaa anampenda sana Josephine.


Wananchi walia wanakufa njaa, watawala wanasema, CHADEMA ni chama cha Kichaga.


Wananchi wanapiga kelele wanalalamika mariasiri za Taifa letu zinanufaisha wachache na nyingi zinaibiwa na wageni, watawala wetu wanasema Ushindi ni Lazima.


Naomba tukumbushane historia mbichi kabisa, waliomfurumusha Hussein Mubarak kutoka Madarakani sio wanasiasa, Kijana aliyejichoma moto tunisia na kuacha laana nyuma yake hakuwa analalamikia wizi wa kura, waliomkamata Gadafi kwenye mtaro wa daraja walikuwa hawajebaba bendera ya chama chochote kile cha siasa, Hata sasa huko Siria wananchi hawapiganii kuundwa katika mpya wala kuwa na tume huru ya Uchaguzi.


Wito wangu kwa viongozi wa CCM ni huu ufuatao.

Kwanza, kuna ushahidi wa kutosha kwamba hivi sasa duniani, mabadiriko yanatokea kwa kasi ambayo haijawahi kutokea huko nyuma katika kila nyanja ya maisha.

Pili na mwisho, Muda si mrefu watanzania watagundua kwamba wanachokihitaji sio katiba mpya na wala sio tume huru ya uchaguzi wala sio maridhiano ya kitaifa ya namna yoyote ile wala sio ushindi wa wagombea wao.


Narudia tena, Punde kidogo, upepo wa mabadiriko utabidiri mkondo wake, watu watakapoamua kuweka magwanda na kuachana na ustaarabu wa kuonyeshana alama ya V sijui mtawaambia nini