Wednesday, December 14, 2011

WABUNGE MMECHAGULIWA KUWAWAKILISHA WANANCHI NA KUTATUA KERO ZAO, JE UGUMU WA MAISHA NI KWENU TU?

Nyongeza ya posho za wabunge yaibua mjadala mzito  Send to a friend
Wednesday, 14 December 2011 10:45
0digg
Na Joyce Mmasi
NYONGEZA ya posho za wabunge imekuwa gumzo na kuzua mijadala isiyo na kikomo katika jamii ya Tanzania.
Tofauti na mijadala ya awali ya kupinga ama kuiunga mkono, sasa kinachojadiliwa ni kauli tata za viongozi waandamizi wa bunge juu ya jambo hilo.
Kauli tata ni zile za Spika wa Bunge, Anne Makinda na Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashillilah ambazo zimeonekana kutofautiana kana kwamba zimetolewa na watu wasiofanya kazi katika taasisi moja.
Utata huu unatokana na ukweli kuwa viongozi hao wanatoa majibu yanayotofautiana kuhusiana na suala moja.
Viongozi hao ambao wanafanya kazi katika ofisi moja wamezua maswali kufuatia kutoa matamko tofauti kuhusiana na suala moja ambapo wakati mmoja anapinga habari ya kuwapo kwa nyongeza hiyo ya posho kwa wabunge mwingine anaibuka na kueleza kuwa nyongeza inayozungumzwa ipo na imefanywa kwa makubaliano baina ya ofisi, serikali na wabunge wenyewe.
Mparaganyiko huo wa mawazo unatokana na taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari kuhusu kuongezeka kwa posho za wabunge kutoka Sh70,000 hadi 200,000 kutwa hivyo kufanya bajeti ya posho hizo kwa mwaka kufikia Sh28 bilioni.

Kutokana na ongezeko hilo, kila mbunge atakuwa akilipwa Sh 80,000 kama posho ya kujikimu (per diem) anapokuwa nje ya jimbo lake, posho ya vikao,  Sh200,000 na mafuta ya gari Sh50,000 kila siku, sawa na Sh330,000 kwa siku huku mshahara jumla kabla ya makato ukielezwa kuwa ni sh 2.3 milioni.

Kauli tata za viongozi
Kwa mujibu wa Dk Kashillilah, mapendekezo ya kutaka posho za wabunge zipande, yaliibuka katika mkutano wa wabunge mjini Dodoma Novemba 8 mwaka huu, lakini hadi wakati anatoa tamko anasema yalikuwa hayajaanza kutekelezwa.
Siku kadhaa baadaye, Spika wa Bunge, Anne Makinda akaibika na kauli inayoonekana kupingana na ile ya katibu wake na akakiri kuwa ni kweli posho za wabunge zilikuwa zimeongezeka kutoka Sh 70,000 hadi Sh 200,000 kwa kikao na zilikuwa zimeanza kutumika.
Mbunge huyu alikuwa anapata Sh 70000 kwa hiyo tumemwongezea Sh130,000 na hupati 'unless' (isipokuwa) umefanya kazi ya Bunge na umesaini asubuhi na jioni hujafanya hivyo hupati hizo hela, anasema Makinda katika kauli inayokinzana na ile ya Dk Kashillilah ambaye wanafanya kazi katika ofisi moja.
Utata huu wa kauli toka kwa watendaji wakuu wa taasisi hii nyeti ya Bunge ndio ulioongeza kasi ya mjadala wa nyongeza za posho za wabunge. Waliopata fursa ya kuchangia wanahoji sababu ya kukinzana kwa majibu katika suala nyeti kama hilo.
Wengine wanaenda mbali zaidi kwa kusema utata huo unaonyesha ni jinsi gani suala hilo lilivyo tata na ambalo huenda likawa halikuwa na ‘baraka’ hata na baadhi ya watendaji hao na kwamba utekelezaji wake huenda umepelekwa haraka haraka bila kupata baraka za wahusika.
Utata huo unazungumziwaje?
Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila (NCCR- Mageuzi), anasema suala la kupishana kauli kwa viongozi wawili wa taasisi moja, ni udhaifu mkubwa kwa taasisi hiyo. 
Suala la posho linatakiwa litazamwe upya katika mihimili yote ya dola, panapokuwa hakuna kanuni ya kuweka uwiano miongoni mwa mihimili hii, kunasababisha manung’uniko na malalamiko kwa wananchi, inatakiwa itazamwe upya,  hili suala la posho lipatiwe ufumbuzi kabisa,” anasema Kafulila. 
Kwa upande wake, Profesa Ruth Meena ambaye ni mwanaharakati wa masuala ya kijamii na msomi aliyebobea anasema ni jambo la kusikitisha kuwa viongozi wa bunge wanapishana kauli juu ya suala hilo la posho.
Inasikitisha sana hawa wawakilishi wetu kujiongezea posho wakisema kuwa gharama za maisha zimepanda, kwenye hali kama hii ya sasa hakuna njia yeyote utakayo weza kutumia kuhalalisha ongezeka kama hili,  anasema.
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia anasema mfumo mzima wa utoaji wa posho nchini ni wa kifisadi.
Mbatia anasema ipo haja ya kuutizama upya mfumo huo ambao umeacha pengo kubwa kati ya mwenye nacho na asiyekua nacho.
Jambo hili halitendi haki kwa watanzania, linaweka tofauti kubwa kati ya wenye nacho na wasiokuwa nacho hii si sawa, mfumo mzima wa utoaji posho unatakiwa kutizamwa upya, anasema.
Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba Mkoani Kagera, Dk Methodius Kilani anasema ongezeko hilo la posho limekuja ghafla na kwamba kiwango hicho ni kikubwa na hakiendani na hali halisi ya uchumi wa nchi.
Watanzania wengi wanalalamika maisha magumu sasa Wabunge wanapoongezewa posho kwa kiwango kinachofikia Sh 200,000 watambue kwamba kuna wananchi wanaohitaji msaada, hizo nyongeza za posho zingeweza kuwasaidia kwa namna moja ama nyingine ambapo ongezeko la posho hizo zingeweza kuwasaidia anasema Askofu Kilaini.
Kwa upande wake, Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Alhad Mussa Salum  anasema kwamba haoni tatizo posho za wabunge kuongezeka na kwamba  kutokana na majukumu yao mazito ya kuwahudumia wananchi.
Ni jambo jema lakini wabunge watambue kwamba wananchi waliowachagua wana matatizo mengi ya kiuchumi sasa wanaposikia wabunge wameongezewa posho lazima nao watahoji lakini kinachotakiwa ni kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa kutatua matatizo ya wananchi wao”anasema Sheikh Alhad.
Lakini, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (Chadema)  anasema ongezeko hilo ni batili kwa sababu halina baraka za Rais Jakaya Kikwete.
Spika wa Bunge anajua kwamba posho zote hulipwa baada ya rais kuidhinisha. Anasema ongezeko la posho halikuidhinishwa kwakuwa uthibitisho wa kuidhinisha ni Masharti Mapya ya kazi kwa wabunge ambayo hayajatolewa na Ofisi ya Rais.
Anasema kitendo cha kuanza kulipa posho mpya bila masharti mapya ya kazi za wabunge ni kukiuka sheria ya utawala wa Bunge kifungu cha 19 na kwamba kutokana na hali hiyo, Tume ya Bunge inapaswa kuwajibika kwa kutumia vibaya mamlaka yake.
Anapendekeza posho mpya zifutwe na zilizolipwa zirejeshwe mara moja kwani zimelipwa kinyume na sheria. “Spika anapaswa kuheshimu sheria ambazo Bunge limepitisha na kwenda kinyume na sheria kwa makusudi ni kosa la kuvuliwa uspika, anaeleza.
Mbunge wa Jimbo la Ubungo,  John Mnyika (Chadema) anasema ongezeko hilo linatakiwa kusitishwa kwa kuwa mchakato wake umefanyika kinyume na taratibu.
Anasema kauli ya Spika Makinda kwamba nyongeza hiyo inatokana na kupanda kwa gharama za maisha mkoani Dodoma haina ukweli, wala mantiki na ina mwelekeo wa upendeleo

No comments:

Post a Comment