Tuesday, March 22, 2011

JE NIRAHISI KWA WANAWAKE KUWAKATALIA WANAUME?

Dayna:Kukubali au kukataa ni uamuzi wako!!!!!!!!  Send to a friend
Saturday, 19 March 2011 12:20
0diggsdigg
Dayna
Na Julieth KulangwaWASANII wa kike wanalalamikia kutakwa kimapenzi pale wanapohitaji msaada wowote wa kikazi, lakini Dayna anasema kukubali au kukataa ni jambo lililo ndani ya uwezo wa yule anayeombwa penzi.

Dayna ambaye jina lake halisi ni Mwanaisha Said anasema suala hilo lilikuwepo tangu enzi na haliwezi kukoma kamwe, kinachotakiwa ni kwa mwanamke kuwa na busara na kujua siku zote atakuatana na viumbe hawa wakiwa na ombi hilohilo.

Akiwa na wimbo wake mpya redio na kideoni uitwao Fimbo ya Mapenzi anasema kuwa hata yeye amepambana sana kufikia hapo alipo sasa, kwani wanaume wa aina hii amekutana nao lakini siku zote alijua nini alikuwa akitaka.

"Unajua kuna mwanamume mwingine ukimfuata na kumweleza nia yako, yeye moja kwa moja akili yake inamtuma kuwa unamtaka kimapenzi la yeye ataanzisha biashara za hivyo,

Sasa ndugu yangu kwa mwendo huu mwisho wa siku utajikuta unaingia kwenye biashara nyingine na kusahau kilichokupeleka pale," alisema Dayna.

No comments:

Post a Comment