Thursday, May 12, 2011

SI HAKI KUFUNGA SHULE KWA UTOFAUTI WA ITIKADI ZA VYAMA

Wabunge Chadema wageuka mbogo  Send to a friend
Wednesday, 11 May 2011 21:27
0diggsdigg
Boniface Meena, Kwela
WABUNGE wawili wa Chadema jana walikuwa mbogo baada ya kufanya ziara katika Kijiji cha Lusaka, Jimbo la Kwela, mkoani Rukwa na kubaini  Shule ya Sekondari Lusaka imefungwa bila maelezo.Mbali na hilo wabunge hao waliwaeleza wananchi kwamba wamebaini mbolea ya ruzuku inayotolewa na serikali ni ufisadi mtupu kwa sababu wananchi wanatozwa fedha nyingi kununua mbolea ya ruzuku.

Wananchi wa Kijiji cha Lusaka walilalamika mbele ya wabunge hao kwamba Serikali imekuwa ikiwanyanyasa na kibaya zaidi imefunga Shule ya Sekondari ya Kijiji hicho baada ya wananchi wa eneo hilo kumchagua Diwani wa Chadema.

Mbali na hilo wananchi hao walilalamika mbele ya wabunge hao kwamba shule hiyo iko moja tu katika eneo hilo na ilifungwa ghafla miezi mitatu iliyopita na viongozi wa Seriklali wa Manispaa ya Sumbawanga Vijijini bila kutoa maelezo yoyote.

Baada ya kusikia malalamiko ya  wananchi wa eneo hilo, Mbunge wa Viti Maalumu kutoka mkoani Arusha, Joyce Mukya na Raya Ibrahimu kutoka Zanzibar walikwenda katika shule hiyo na kuwaona madiwani wakiendelea na kikao na kushindwa kupata maelezo kutoka kwa madiwani na mbunge wa jimbo hilo.

Mukya aliwaambia wananchi hao kwamba atapambana na viongozi wa halimashauri hiyo ili ajue ni kwa nini shule hiyo imefungwa bila maelezo na kusababisha wanafunzi kutokwenda shuleni.

"Yani ni aibu, nitakufa nao kwa kuwa wamefunga shule halafu wanafanyia vikao vya madiwani kwenye majengo ya shule bila kujali haki za wanafunzi kusoma, hawa watu sijui ni wa aina gani,"alisema Mukya.

Alisema hilo ni moja ya maswali atakayowasilisha bungeni kwenye maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu ili aelezwe ni kwa nini shule hiyo imefungwa."Kata ina vijiji vitano, tunataka tujue ni kwa nini shule imefungwa, tutaliwasilisha bungeni kutaka kujua hilo. Inashangaza sana kwa nini mbunge wenu ananyamaza kuhusu shule kufungwa na anafanya mikutano huko ndani bila hata kujali,"alisema.

Raya Ibrahimu alionekana kuchukizwa na kitendo hicho na kuishambulia serikali kwa kushindwa kuwajali wananchi wake hasa wanachanga fedha zao kujenga shule, lakini zimekuwa zikifungwa bila wananchi kuelezwa sababu za kufanya hivyo.

"Unajua hawa watu wanatia aibu, mimi sijui ni wa aina gani watu wazima wanafunga shule bila kufikiria madhara gani wanafunzi wanapata, halafu wakikimbilia mijini wanalalamika," alisema.

Alisema kitendo kilichofanywa na Serikali kinatia aibu kwa kuwa kinasababisha vijana kukimbilia mijini kwa ajili ya kuuza pipi na biskuti.

Raya alisema suala la huduma za jamii limekuwa ni vituko kijijini ambako kuna barabara mbovu na aliwashauri wananchi kuipunzisha CCM ili wajifunze kuwajali wananchi wao.

Kuhusu mbolea alisema ni bora serikali ikaondoa ruzuku kwenye mbolea ili ishuke bei na wananchi wanunue kwa bei ya chini."Serikali iondoe vocha za ruzuku kwa kuwa zinafaidisha watu wachache na kuwaumiza wananchi wengi ambao ni masikini,"alisema Mukya.

Alisema nchi inanuka rushwa kwa sababu wananchi wamekwua wakilalamika kutopata mbolea kwa kuwa kila mtu ni mla rushwa."Viongozi wa CCM wanachukua zile vocha wanajigawia. mwananchi maskini akitaka vocha mpaka utoe rushwa, mbolea ni kwa ajili yenu ninyi watu maskini ili mjikomboe kwa vijana kufanya shughuli za kilimo, lakini inashindikana kutokana na ufisadi unaofanyika kwenye vocha hizo,"alisema Mukya.

LOLIONDO IKIWEKEWA MIKAKATI MIZURI INAWEZA KULIINGIZIA TAIFA PESA NYINGI ZA KIGENI,WAZIRI WA UTALII UNAMPANGO GANI?

Marais, mfalme watarajiwa kutua Samunge kwa Babu  Send to a friend
Wednesday, 11 May 2011 21:50
0diggsdigg
Abiria waliofika kwa mchungaji Ambilikile Mwasapila katika kijiji ch Samunge kunywa dawa jana, wakiteremka kutoka katika helikopta inayomilikiwa na kampuni ya Akagera aviation ya Rwanda. Picha na Mussa Juma
Mussa Juma, Samunge
MARAIS kadhaa wa nchi za Afrika akiwamo mfalme, wanatarajiwa kwenda Samunge, Loliondo kupata tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Ambilikile Mwasapila.

Kutokana na ujio huo, ulinzi umeimarishwa kuanzia jana. Ofisa mmoja wa polisi wa Wilaya ya Ngorongoro, alithibitisha ujio wa wakuu hao bila ya kutaka kutoa maelezo zaidi. Hakutaja siku wala muda ambao watawasili hapa.
Jana kulikuwa na idadi kubwa zaidi ya polisi kijijini hapa. Ofisa mwingine wa polisi ambaye pia hakutaka jina lake liandikwe alisema, wamepokea taarifa za ujio wa marais hao na walitegemea kwamba wangewasili Samunge kuanzia jana.

 "Ni kweli, kuna wageni watakuja. Nadhani ni wakubwa bado taarifa kamili hazijatufikia watatua lini," alisema.
Helikopta kutoka Rwanda inayomilikiwa na Kampuni ya Akagera Aviation, imeanzisha safari za kwenda Samunge kila siku ikitokea Uwanja wa Ndege wa Arusha.

Helikopta hiyo ni kubwa kuliko nyingine ambazo zimekuwa zikitua Samunge kuleta wagonjwa kupata tiba ya kikombe kwa Babu.Ujio wa helikopta hiyo, sasa unalifanya anga la Samunge kutawaliwa na helikopta nne, zinazofanya safari takriban mara tatu kwa siku kwenda na kutoka Samunge.

Gharama za nauli kwa abiria mmoja kutoka Arusha hadi Samunge kwa helikopta hiyo ya Rwanda ni Dola za Marekani 1,000 hivyo kufanya usafiri huo kuwa wa watu wenye uwezo mkubwa kifedha.
 Baada ya kuongezeka wimbi la viongozi kutoka nchi jirani ya Kenya wanaofika Samunge na habari zao kuandikwa, sasa vigogo wengi wa huko wamebuni njia nyingine ya kufika kijijini hapo bila kujulikana.

Vigogo hao sasa wanafika Samunge kupitia mpaka wa Narock ambako huenda moja kwa moja hadi Loliondo na kukodi magari ya wenyeji ili kuwapaleka Samunge.  Kwa takriban wiki mbili sasa, viongozi kadhaa wa Serikali ya Kenya, wakiwamo maofisa wa Ikulu ya Kenya, mawaziri na wabunge wamekuwa wakitua Samunge.

Babu: Wagonjwa waruhusiwe
Mchungaji Mwasapila ameomba vituo vinavyoratibu magari yanayokwenda Samunge, kuruhusu magari zaidi kupeleka wagonjwa ili wapate huduma kutokana na kupungua kwa foleni.Msaidizi wa Mchungaji Mwasapila, Frederick Nisajile alisema jana kwamba kutokana na huduma kuboreshwa, idadi ya magari yanayopaswa kuingia Samunge kwa siku yanapaswa kuongezeka.

"Tunaomba wawe na mawasiliano na sisi ya mara kwa mara kwani sasa kama unavyoona hakuna foleni, lakini kuna magari yamezuiwa maeneo ya vituo yasije huku," alisema Nisajile.

Jana, zaidi ya magari 500 yakiwamo mabasi makubwa kutoka Mikoa ya Kigoma, Dodoma, Mwanza na Arusha yalifika Samunge na abiria kupata kikombe na kuondoka.Hadi majira ya tisa jioni jana, foleni ya magari ilielekea kumalizika kabisa.

Bei ya kikombe iko palepale
Mchungaji Mwasapila jana alitoa ufafanuzi kuhusu malipo ya kikombe akieleza kuwa hajawahi kupandisha gharama zake tangu mwanzo. Alisema Watanzania wanalipa Sh500 na wageni kutoka nje ya nchi, wanalipa Dola moja au Sh1,500.

JE KAULI NAPE WA CCM INAATHARI KWA CHADEMA?

Chadema, CCM sasa ni kulipuana  Send to a friend
Wednesday, 11 May 2011 21:53
0diggsdigg
Gasper Andrew, Singida na Boniface Meena, Nkasi
VITA ya maneno baina ya vyama vikubwa vya siasa nchini CCM na Chadema, imezidi kushika kasi kwa vyama hivyo kurushiana tuhuma katika mikutano ya hadhara inayoendelea katika maeneo mbalimbali nchini.CCM kinawaita Chadema wanafiki na Chadema kinaendelea kudai kuwa chama hicho tawala ndicho kinachoisababishia nchi umasikini.

Jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM, Nape Nnauye alidai kuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa ni mnafiki kwa kula matapishi yake anapodai kuwa chama tawala kinafuja mali ya umma huku naye (Dk Slaa) akiwa katika mwelekeo huohuo.

Alidai kuwa Dk Slaa ameingia mikataba ya kukishinikiza chama chake kimlipe Sh7.5 milioni kila mwezi wakati alipokuwa mbunge alikuwa akiilalamikia serikali kwamba inawabebesha wananchi mzigo mkubwa kwa kuwalipa wabunge kila mmoja Sh milioni sita. Nape alisema hayo jana alipokuwa akizungumza kwenye mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika katikia Kituo Kikuu cha mabasi cha zamani mjini Singida.

Alisema anazo nyaraka halali za chama hicho zinazoonyesha kwamba baada ya Dk Slaa kuukosa urais, sasa amekigeukia chama chake na kuanza kukishinikiza kimlipe mshahara mkubwa kuliko aliokuwa akiupata alipokuwa mbunge.Nape alisema madai kwamba Dk Slaa haombi alipwe si ya kweli akidai kwamba ndiye anayeshiniza kulipwa kiasi hicho kwa vile ameachishwa ubunge na ameukosa urais.

"Anashangaza sana bungeni alikuwa akipanua mdomo hadi mwisho kupotosha jamii kuwa wabunge pamoja na posho, mishahara na marupurupu mengine, wanalipwa shilingi milioni sita kiasi ambacho alidai kuwa kinawaumiza wananchi. Kwa hiyo ndiyo tuseme Sh7.5 milioni ni kiwango ambacho hakitawaumiza wanachama wa Chadema na walipa kodi wengine," alihoji Nape huku akishangiliwa na wananchi waliohudhuria.

 Katibu huyo alisema kwa kitendo chake hicho cha kushinikiza alipwe kila mwezi mamilioni hayo, anapaswa kuwaomba radhi Watanzania kwa kuwadanganya alipokuwa bungeni kuwa Sh milioni sita ni mshahara mkubwa mno.
 Aidha, alisema kuwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe naye aliwahi kutoa msaada wa Fuso (malori aina ya Mitsubishi Fuso) tatu ili zikisaidie chama hicho katika shughuli mbalimbali za ustawi wake lakini sasa anakidai Sh500 milioni za ununuzi.

Madai ya Nape kuhusu mshahara wa Dk Slaa yaliwahi kutolewa maelezo na Chadema ambacho kilisema kilifikia uamuzi wa kumlipa, Dk Slaa mshahara na maslahi yanayolingana na anayopata mbunge kwa sababu ndicho kilichomshawishi aache kugombea ubunge katika Jimbo la Karatu mkoani Arusha, ambako alikuwa na nafasi kubwa ya kushinda na kumtaka agombee nafasi ya urais ambayo mgombea wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alishinda.

Kilisema uamuzi huo ulifuata taratibu zote ikiwa ni pamoja na vikao vikuu vya chama hicho, kama vile Kamati Kuu, kuidhinisha malipo hayo.Kuhusu malori Chaadema kilisema kiliamua kufanya mkakakti wa kununua magari matatu ambayo Mbowe aliyanunua na kuyatoa kwa muda ili yakisaidie kwenye kampeni.

Mbowe: CCM wanajipa mamlaka ya uungu mtu
Wakati Nape akisema hayo Mbowe amesema viongozi wa Serikali ya CCM wamelewa madaraka na kujivika mamlaka ya uungu watu na kusahau kuwatumikia Watanzania: "viongozi wa nchi hii, wanajipa mamlaka ya umungu-mtu na wananchi wanawaogopa."
Mbowe, ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alisema hayo jana alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika Uwanja wa mji mdogo wa Namanyere, Wilaya ya Nkasi, Rukwa, ikiwa ni sehemu ya operesheni ya Chadema ya kuishinikiza serikali kusikiliza kilio cha wananchi.

Alitoa mfano akisema, iwapo wananchi wa Wilaya ya Nkasi watajengewa barabara, wajue kuwa hiyo ni haki yao na pia wana haki ya kuiuliza serikali sababu za kuchelewa kujengewa kwa miaka 50 ya uhuru.
Alisema katika mkoa kama wa Kilimanjaro, wamekuwa wakijengewa barabara za lami kwa kadri inavyohitajika, tofauti na Mikoa kama ya Rukwa, Iringa, Mbeya na Ruvuma ambayo imeachwa nyuma kimaendeleo, licha ya kuzalisha chakula kinachohifadhiwa katika Hifadhi ya Chakula ya Taifa.

Kutokana na hali hiyo, alisema iwapo wananchi wa Mkoa wa Rukwa hawatapiga kelele kudai maendeleo, kamwe hawezi kushuka Malaika Gabriel kuwapigia kelele."Kwa hiyo ndugu zangu, si kila kitu ni cha kupongeza, muwatume wabunge wenu wakapige kelele," alisema Mbowe.Alisema tangu Chadema ianze kupiga kelele Rukwa, imefanikiwa kutoa Mbunge mmoja tu, Said Arfi na barabara zikianza kutengenezwa.

Mbowe alisema serikali imeshindwa kusimamia reli ya kati kiasi ambacho wananchi wanaotaka kusafiri kulazimika kutumia gharama kubwa kupata usafiri wa ndege.Alisema kuwa baadhi ya wabunge kutumia muda mwingi bungeni kuishukuru serikali katika mambo ambayo ni wajibu wake kuwatekelezea wananchi.Alisema wabunge hao wamekuwa wakifanya hivyo, huku wakijua wazi kuwa ni kinyume na jukumu la mbunge, ambalo ni kuisimamia serikali kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi.
"Kitendo cha kuishukuru serikali, ndicho kinatuchelewesha kupata maendeleo. Wananchi wanaiomba serikali, wabunge wanaishukuru..." alisema.Alisema vitendo hivyo vimechangia kwa kiasi kikubwa kuwafanya viongozi wa serikali nchini kujiona kuwa ni miungu kwa sababu wanatukuzwa.

Waliopewa siku 90 CCM wataaibika karibuni
Katika hatua nyingine, Nape alisema kuwa viongozi walioombwa na chama wajipime wenyewe na kuchukua uamuzi wa kuachia nyadhifa zao mapema kutokana na kutuhumiwa na wananchi juu ya tabia zao za kifisadi, kwamba sasa siku zao za kuja kuaibishwa, zinahesabika.

"Watu sasa wameanza kusema kuwa Nape hana nguvu tena za kupambana na ufisadi nchini, nawaambia kuwa si kweli. Sijalala wala sijaishiwa nguvu za kutokomeza ufisadi. Hawa wanaotuhumiwa kwa ufisadi wanakipa chama machungu na kuanza kukikosesha imani kwa wananchi, wanapaswa kujiondoa wenyewe na wasisubiri kuja kuapishwa kwa kufukuzwa kwa nguvu," alisema.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), John Chilingati aliwataka viongozi na wanachama wa chama hicho ngazi ya wilaya na mikoa kusaidia kukirudisha kwenye misingi yake ya awali ili wananchi waendelee kukiamini.
Chiligati ambaye pia ni Mbunge wa Manyoni Mashariki, alitoa wito huo juzi alipozungumza na wananchi wa Kata ya Ikungi, Singida.
Alisema vikao vya Halmashauri Kuu vilivyofanyika hivi karibuni mjini Dodoma, vilibaini kuwa CCM imefika mahali pabaya kwa kuanza kuacha misingi yake na kusababisha baadhi ya wanachama wake na wananchi kwa ujumla, kuanza kukosa imani nacho.