Friday, June 10, 2011

CHADEMA WAIKOSOA BAJETI YA TANZANIA 2011-2012

Thursday, 09 June 2011 23:
Neville Meena, Dodoma
KAMBI ya Upinzani Bungeni imedai kwamba kuna upotoshaji mkubwa katika Bajeti ya S 200erikali iliyowasilishwa bungeni juzi na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, huku ikidai kwamba bajeti hiyo ni ya kulipa posho na madeni.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Kambi hiyo mjini Dodoma na kusainiwa na Waziri Kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe inabainisha kuwa upembuzi uliofanywa umebaini kuwapo kwa upotoshaji mkubwa wa kitakwimu na kimaudhui uliofanywa kwalengo la kuwajengea matumaini wananchi.
"Kambi ya Upinzani Bungeni imeshtushwa na kushangazwa na hatua ya Serikali kutenga zaidi ya robo ya bajeti kulipa madeni na kulipana posho (asilimia 27), asilimia 14 kulipa madeni na asilimia 13 kulipa posho mbalimbali," ilisema taarifa hiyo.
Miongoni mwa maeneo ambayo yanadaiwa kuwa na upotoshaji ni kiasi cha fedha zilizotengwa kwa ajili ya kukabiliana na tatizo la umeme, ongezeko la jumla la Bajeti ya Serikali ikilinganishwa na ile ya mwaka 2010/11, posho mbalimbali, faini kwa madereva wazembe na ulipaji wa madeni ya Serikali.

Hakuna mradi mpya wa umeme
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, tamko la Serikali kwamba imetenga kiasi cha Sh537 bilioni kwa ajili ya kutatua tatizo la umeme, si kweli kwani kwa jumla Wizara ya Nishati na Madini, imetengewa Sh402.071 bilioni na kwamba hakuna mradi mpya wa umeme hata mmoja utakaoanzishwa.

"Fedha hizo zimegawanywa katika mafungu ya matumizi ya kawaida Sh76,953,934,000  na  kwa upande wa bajeti ya maendeleo zimetengwa Sh325,448,137,000. Sh325 bilioni zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo ya Wizara ya Nishati na Madini zinatosha kwa mradi mmoja tu wa umeme wa 160 MW, 100 Dar es Salaam na 60 Mwanza,"inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Zitto ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, alisema katika taarifa hiyo kuwa, kutokana na hali hiyo hakuna mradi mpya wa umeme unaoonekana katika bajeti hiyo na kwamba kauli ya Mkulo ililenga zaidi kuwajengea wananchi matumaini hewa na si hatua za kweli kumaliza matatizo ya umeme nchini.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hakuna ongezeko lolote halisia la fedha katika bajeti ya mwaka huu, kwani kati ya Sh13.525 trilioni zilizotengwa, Sh1.901 trilioni, sawa na asilimia 14.06 ya bajeti yote ni kwa ajili ya kulipa madeni ya Taifa.
"Kwa mantiki hiyo, mtaona kuwa fedha kwa ajili ya kuendesha Serikali pamoja na kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo zitabaki Sh11.624 trilioni ambazoni ni sawa na fedha za bajeti ya mwaka unaomalizika wa 2010/2011," alisema Zitto katika taarifa yake hiyo na kuongeza: "Kwa kuzingatia kwamba thamani ya shilingi imekuwa ikishuka, bajeti iliyotangazwa ni ya kulipa madeni".
Bajeti ya posho sasa Sh987 bilioni
Kuhusu hatua za kupunguza posho, kiongozi huyo alisema hakuna ukweli wa kauli hiyo kwani Serikali imetenga kiasi cha Sh987 bilioni kwa ajili ya kulipa posho mbalimbali, fedha ambazo ni sawa na asilimia 13 ya bajeti nzima.

 Taarifa hiyo ilibainisha kuwa kutokuwapo kwa nia ya dhati ya kupunguza posho, inaonekana katika hatua za kufanya marekebisho katika sheria ya kodi sura ya 332 ili kusamehe kodi ya mapato katika posho wanazolipwa wafanyakazi wa Serikali na wanaofanya kazi katika taasisi zinazopata ruzuku kutoka kwenye Bajeti ya Serikali.
"Hii inaonyesha kuwa kauli ya kufuta au kupunguza posho ilitolewa na Serikali ili kupumbaza wananchi, lakini haina udhati,"alisema.

 Taarifa hiyo ilieleza kuwa bajeti imeongeza mzigo mkubwa kwa wananchi kutokana na hatua yake ya kuongeza kiwango cha faini kwa madereva wazembe kutoka Sh20,000 hadi Sh300,000, na kwamba kiasi cha Sh50,000 kilichotangazwa na Waziri Mkulo juzi kinatofautia na maelezo kwenye vitabu vya bajeti.
Alisema hatua hiyo itawaathiri wananchi hasa vijana walioajiriwa ama kujiajiri katika huduma za usafiri na usafirishaji na kwamba kipengele hicho pia kinalenga kuuhadaa umma.
Serikali juzi ilitangaza hatua kadhaa za kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima katika mwaka wa fedha wa 2011/2012, lakini fedha za matumizi mengineyo, maarufu kama Other Charges (OC), zimeongezwa kwa asilimia 8.62 ikilinganishwa na Bajeti ya Serikali inayofikia ukomo tarehe 30 mwezi huu.
 Fedha za OC katika bajeti mwaka ujao wa fedha ni Sh3.089 trilioni ikilinganishwa na kiasi cha Sh2.823 kilichotengwa katika mwaka wa fedha wa 2010/2011, likiwa ni ongezeko la Sh266.599 bilioni.
Fungu la fedha za OC ndilo hutumika kugharimia posho mbalimbali kwa watumishi wa umma na uendeshaji wa semina, warsha na makongamano pamoja na kugharimia safari za viongozi ndani na nje ya nchi.
 Kafulila adai bajeti haijazingatia  vigezo vya uchumi
Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila aliliambia Mwananchi katika viwanja vya Bunge kuwa, hali hiyo inadhihirisha kwamba bajeti iliyowasilishwa na Mkulo ililenga zaidi kutafuta kuungwa mkono kuliko kuzingatia vigezo vya kiuchumi.

"Kama mwaka wa fedha unaoishia mwishoni mwa mwezi huu fedha za OC ni kidogo kuliko zile ambazo zimetengwa mwaka ujao wa fedha, basi ni dhahiri kwamba hatuwezi kusema posho zitapunguzwa, hapa nadhani kuna tatizo,"alisema Kafulila.
 Alisema fungu la fedha za OC lazima lipitiwe upya kwani fedha zilizotengwa ni zaidi ya kiasi cha fedha ambazo Serikali imeomba kutoka kwa nchi wahisani kwa ajili ya kutekeleza miradi  ya maendeleo.
"Iwapo fedha za OC ni Sh3 trilioni na fedha za miradi ya maendeleo tunazoomba kutoka kwa wafadhili ni kiasi hicho hicho, utaona kwamba ni jambo la kushangaza, hapa kuna mambo mengi ya kuweka sawa,"alisema Kafulila, huku akibainisha kuwa bajeti hiyo ya Serikali si mbaya sana kwani imekumbuka umuhimu wa miundombinu ya usafirishaji.
Akiwasilisha bungeni juzi Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/12, Waziri Mkulo alibainisha hatua kadhaa za Serikali kudhibiti matumizi yasiyokuwa ya lazima akiahidi kupunguza posho zisizo na tija, safari za ndani na nje za viongozi na ukubwa wa misafara ya viongozi hao ili fedha husika ziweze kutumika kugharimia shughuli nyingine za maendeleo.
"...........Serikali itasitisha ununuzi wa samani za ofisi, hususan zile zinazoagizwa kutoka nje ya nchi, kupunguza malipo ya posho mbalimbali yasiyokuwa na tija, kupunguza matumizi ya mafuta kwa magari ya Serikali, kupunguza safari za ndani na nje ya nchi, ikiwa ni pamoja na ukubwa wa misafara na kuendelea kupunguza semina na warsha, isipokuwa pale inapobidi na kwa kibali cha Ofisi ya Waziri Mkuu..," alisema Mkulo.
Sh3 trilioni kutoka nchi wahisani
Kadhalika majedwali ya ufupisho wa hesabu za bajeti ya Serikali kwa mwaka 2011/12 yanabainisha kuwa fedha za maendeleo zinazotarajiwa kutoka kwa nchi wahisani ni kiasi cha Sh3.054 trilioni. Kiasi hicho kinazidiwa kwa asilimia 18.9 sawa na Sh5.853 bilioni kikilinganishwa na fedha za OC ambazo ni Sh3.089 trilioni.

 Katika bajeti hiyo, fedha zote zilizotengwa na Serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo ni Sh4.925 trilioni, ambapo fedha za ndani ni Sh1.871 trilioni.
 Mchanganuo mzima wa bajeti hiyo unaonyesha kuwa fedha za miradi ya maendeleo zilizotengwa ni sawa na asilimia 31 ya bajeti nzima, wakati fedha za matumizi mengineyo (OC) ni sawa na asilimia 32, mishahara asilimia 23, malipo ya madeni asilimia 8, madeni mengine asilimia 3 na riba ya madeni ya ndani na nje asilimia 3.

KIZURI CHAPASWA KULIWA NA WOTE WANAOKIHITAJI

 The Mandela Rhodes Scholarships
  BUILDING EXCEPTIONAL LEADERSHIP IN AFRICA
Mandela Rhodes Foundation logo
  
  
   Image of 2005 Mandela Rhodes Scholar Jacques Conradie Image of 2006 Mandela Rhodes Scholar Pie-Pacifique Kabalira-Uwase Image of 2007 Mandela Rhodes Scholar Judy Sikuza Image of 2008 Mandela Rhodes Scholar Anton Botha
The Mandela Rhodes Scholarships aim to help in building leadership excellence in Africa.
A Mandela Rhodes Scholarship is more than a bursary, though the costs of Scholars are generously covered during their period of study.
The Mandela Rhodes Foundation offers young Africans who exhibit academic prowess as well as broader leadership potential an educational opportunity unique on the continent. While pursuing their chosen post-graduate degree, each Scholar benefits from access to leadership development programmes, rooted in the principles underpinning the Foundation.
In addition to the opportunity to interact with a diverse group of fellow-Scholars that spans the continent and academic disciplines, they become part of a wide-ranging network of young Africans of excellence who are expected to play leadership roles in their fields and societies in the years following their time ‘in residence’. More... 

Since the selection of the first cohort of eight Scholars in 2005, a total of 123 Mandela Rhodes Scholarships has been awarded. More...

The intention to establish The Mandela Rhodes Foundation was announced in February 2002 when The Rhodes Trust, as part of its centenary celebrations, entered into a partnership with Mr Mandela and pledged a founding benefaction over 10 years.
The Mandela Rhodes Foundation is a unique partnership seeking to close a circle of history for the benefit of current and future generations of Africans. It brings together the 20th century legacy of leadership and reconciliation embodied by Nelson Rolihlahla Mandela, and Cecil John Rhodes's 19th century legacy as it relates specifically to education and entrepreneurship
The overarching mission of The Mandela Rhodes Foundation is to help build exceptional leadership capacity in Africa, by providing excellent educational and leadership development opportunities to individual Africans with leadership potential; as well as by creating over time a network of well-rounded leaders of talent, effectiveness and integrity across African society. More...

©2010 Mandela Rhodes Foundation, all rights reserved 
    Image of Mandela
I would like to take this opportunity of thanking all of you around the world who are assisting in the great project of building The Mandela Rhodes Foundation.
The central purpose of The Mandela Rhodes Foundation is to build exceptional leadership capacity in Africa.
The bringing together of these two names represents a symbolic moment in the closing of the historic circle; drawing together the legacies of reconciliation and leadership and those of entrepreneurship and education.
Already the Mandela Rhodes Scholarships are changing the lives of young Africans, who will play vital roles in the future of the continent.
The achievements of The Mandela Rhodes Foundation so far have been remarkable, but it is its future potential that is most exciting.
I urge you to help in every way you can, knowing that you have my personal appreciation.
Nelson Rolihlahla Mandela
Johannesburg, South Africa

TUNAHITAJI WABUNGE WALO NA UCHUNGU NA NCHI YAO KAMA ZITO KABWE, HAKIKA ZITO NI MWAKILISHI WA WATU MASKINI

Zitto ajitoa kupokea posho za Bunge  Send to a friend
Thursday, 09 June 2011 23:25
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe
Exuper Kachenje
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ameiandikia barua Ofisi ya Bunge kuiomba isimamishe kumlipa posho zake zinazotokana na vikao vya Bunge kuanzia juzi.Zitto ametoa ombi hilo kwa barua rasmi aliyoiwakilisha kwa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah Juni 7 mwaka huu.
Katika barua hiyo, ambayo gazeti hili limefanikiwa kuiona, Zitto alisema anaamini kuwa watumishi wa Serikali na wabunge, hawastahili kulipwa posho wanapohudhuria vikao rasmi vya uwajibikaji wao wa kawaida.
Zitto alisema kuwa posho hiyo haistahili kulipwa kwake, wabunge wengine wala watumishi wa umma kwa kuwa kuhudhuria vikao ni sehemu ya kazi zao.

"Kwa mujibu wa Sheria ya Utawala wa Bunge (National Assembly Act of 2008) na kwa mujibu wa Masharti ya Kazi za Mbunge niliyokabidhiwa, ninastahili kupata posho za vikao, (sitting allowances) kila ninapohudhuria vikao vya Bunge na Kamati zake,"alisema Zitto na kuongeza:
"Ni imani yangu kuwa posho ya kikao haistahili kulipwa kwa mbunge na mtumishi mwingine yeyote wa Serikali kwani kuhudhuria kikao ni sehemu ya kazi yangu,".

Kupitia barua hiyo, Zitto ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Fedha, alieleza kwamba amekuwa akipendekeza posho za vikao hivyo ifutwe, jambo ambalo pia limo katika mapendekezo ya chama chake (Chadema) katika Bajeti ya 2011/2012.
"Nimekuwa nikipendekeza kuwa posho hii ifutwe. Chama changu cha Chadema pia kimependekeza jambo hili katika mapendekezo yake ya Bajeti 2011/2012," alisema Zitto na kuendelea:
"Mpaka hapo mfumo wa kulipana posho za vikao utakapofutwa, ninaelekeza kwamba stahili zangu zote za posho zielekezwe katika Taasisi ya Kigoma Development Initiative (KDI).., utaratibu huu uanze kuanzia tarehe 8/6/2011."


Katibu wa Bunge agoma kuizungumzia
Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alipoulizwa jana kama amepokea barua hiyo ya Zitto, alisema kuwa, yeye kama mtendaji wa mhimili huo wa Dola, anapokea barua nyingi, hivyo si rahisi kukumbuka kama barua hiyo imefika ofisini kwake.

Lakini akasema, hata kama barua hiyo itakuwa imemfikia ofisini, kanuni na taratibu haziruhusu Bunge kutangaza habari za mtu binafsi.Alisema ofisi yake hairuhusiwi kuandika masuala binafsi ya wabunge yanayofikishwa ofisini na kwamba hilo linawezekana ikiwa mhusika (Zitto), ameruhusu lifanyike kwa maandishi.
"...Haturuhusiwi kuandika habari  za mtu. Nikiwa Katibu wa Bunge, napokea barua nyingi 'personal' (binafsi), lakini kama yeye mwenyewe amewaambieni kuwa kaleta barua hiyo, basi mwambieni pia atuandikie barua kuturuhusu na sisi ili tulitangaze hilo," alisema Dk Kashililah.
Bajeti ya posho kulipa walimu laki moja
Uamuzi huo wa Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, umekuja huku taarifa za utafiti wa taasisi ya Policy Forum inayojihusisha na tafiti mbalimbali za sera zikionyesha kuwa, katika mwaka 2008/2009, Serikali katika bajeti yake ilitenga Sh506 bilioni kwa ajili ya malipo ya posho.

Kwa mujibu wa utafiti huo, ambao taarifa yake ilitolewa mwaka uliopita, fedha hizo ni sawa na mishahara ya mwaka mzima kwa walimu 109,000 ambao ni robo tatu ya walimu wote nchini.
Kwa mujibu wa utafiti huo mwaka 2009/10 kiasi cha fedha zilizotengwa kwa ajili ya posho za watumishi wa umma kilikuwa sawa na asilimia 59 ya malipo ya wafanyakazi wa ngazi ya chini .  

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #85 @y2k 2011-06-10 13:40
Quoting Japhary Lyimo:
That is political KIINI MACHO,HOW IS HE SURVIVING??????? Kwa hela zake binafsi? Hela za Chama? Or kunamfadhili anamlipa kichini chini ili siku akitoka aanze kulipa fadhila? Tumeona Dr. SLAA alivyoingia kwenye mkataba na CHADEMA ili ajitoe muhanga kuachia Jimbo na kugombea Urais aliojua hata pata, na leo CHADEMA wanalazimika kumlipa posho na malupulupu kama mbunge. The same to ZITTO, "WE CALL IT A POLITICAL MOVE"

we mzee naona bado akili yako ijakomaa hata kama umezeeka basi umezeeka vibaya kama wazee wenzio wa CCM kama huna cha kusema bora kukaa kimya m-s.n.g.e
Quote
 
 
0 #84 Godson Galasi 2011-06-10 13:37
kwa kweli ztto anatambua nini anakifanya na ni kwa nini yyeye yuko bungeni,zitto ametambua wajibu wake kwa uwepo wake bungeni,ametamb ua thamani ya wapiga kura wake pamoja na watanzania wote waanaoishi maisha magumu kwa sababu ya u-mimi/ubinafsi wa wachache na kutotambua wajibu wao kwa watu waliowapatia kazi.kimsingi malipo ya posho ni wizi mtupu kwa mtu anayetekeleza wajibu wake kama sehemu ya kazi yake,na mimi nashangaa waziri mkuu kuto yaanglia haya kwa u-makini mkubwa!!?halafu pia nafikiri kupitia bajeti hii,kama waziri mkuu anauchungu na maisha ya watanzania tulitarajia kusikia ununuzi wa magari ya kifahri kwa kila mtu sasa basi ili kuokoa fedha za watanzania kupotea na badala yake kufanya kazi nyingine za maendeleo kam alivyofanya zitto kwa maana ya yeye kuonyesha mfano kwa wengine
Quote
 
 
0 #83 zabronsimon 2011-06-10 13:33
Fara John, tatizo wewe huna hoja , usiangalie mtu ametokea chama gani au kabila gani angalia amesema nini, na alichosema kinamaslahi kwa taifa zima na sio kwa wachache? John vip rafiki yangu mbona ishu ya Zitto ipo wazi kabisa haihitaji kuumiza kichwa? badilikeni jaman,achana na uchadema, uccm, u-cuf, lamsingi tujenge nchi yetu.
Quote
 
 
0 #82 JOHN 2011-06-10 13:25
we zanbron iringa mnadanganyika tu wachAGA WAPO TANZANIA NZIMA NYIE MNAFUATA UPEPO TU KWANI HUJUI CUF cha wapemba UDP cha bariadi na DP pekee ndo cha watanganyika. ULIZA WALID KABURU WA kigma mjini ambaye ndo alikuaga mbunge pekee wa chadema yupo wapi baada yan kuingia anga za wachaga. we wa liniiii mbona kama mjanja lakini huelewi mambo
Quote
 
 
0 #81 maskini wa kipato. 2011-06-10 13:16
Kabwe hongera sana,heri yako ukumbukae wenye shida,jaman hebu fikiria mwalimu na kamshahara kake ni sawa na posho ya wabunge ya kikao ya siku moja na nusu,kabwe ameliona hilo.Aisee zitto anaona mbali,huyu ndie yupo kwa maslah ya wananchi,wengin e ni kwa maslahi yao.wananch tunataka vitendo kama zito s maneno tu majukwaani.
Quote
 
 
0 #80 zabronsimon 2011-06-10 13:13
Wewe John htofautiani na John Chiligati(CCM) mbona majina ya akina John wanaakili nyie vipi? Zitto amefanya uamuzi mzuri. Halafu hiyo tabia ya kusema chadema ni cha wachaga ife mbona sisi tupo Iringa sio wachaga? Toweni hoja za msingi msimuige JK maana ni yeye alianzisha kwamba cdm ni cha wachaga baada ya kuishiwa sela wakati wa uchaguz.
Quote
 
 
-1 #79 JOHN 2011-06-10 13:02
CHADEMA WWOTE KUTOKA UCHAGANI LAZIMA WAITISHE KIKAO KUKUJADILI, WE HAYA SHAURI YAKO YALIYOKUKUTA MARA BAADA YA UCHAGUZI BADO HUJAKOMA. NAKUONEA HURUMA SANA NDUGU. HAO WACHAGA HAWATAKUSAMWE KWA HILI UNAACHA PESAA MEKU AISE
Quote
 
 
+2 #78 Lucas Haule 2011-06-10 12:54
Zitto Kabwe, natamani kuzaa mtoto nimwite, Zitto Kabwe. Hizi ndiyo akili, huu ndiyo ufahamu, haya ndiyo majukumu ya kiongozi. watawla hawawezi kufanya hivyo. BABA MUNGU, NAAMINI UNANISIKIA, MWONGOZE KIJANA HUYU ILI AFIKIE KILE AMBACHO WENYE FIKRA HABA HAWATAKI AFIKE, MWEKE AWE KIONGOZI WETU KWA AJILI YA UTUKUFU WA JINA LAKO, AMINAA!
Quote
 
 
+2 #77 Hellen Gupta 2011-06-10 12:54
Hakika Zitto una upendo wa dhati kwa nchi yetu na wananchi wetu. Wachache wako tayari kuachia pesa zao binafsi ili wengine wanufaike. Hongera sana. Tunakuombea Mungu akulinde, uzidi kufanya maajabu kama haya. Naye atakubariki sana.
Ciao.
Quote
 
 
+1 #76 zabronsimon 2011-06-10 12:53
hongera!!!!!!!! !!!!!!!!!!!!!!! ! Zitto. John chiligati (CCM)ziiiiiiiii iiiiiiii umeleta kichefuchefu.
Quote
 
 
+2 #75 Rasvin 2011-06-10 12:44
Mh Zitto Safi sana uliona mifano ya bunge la Germany. Sasa kama kweli wabunge wetu wanataka maendeleo basi huo ni mfano tosha wa kukubalina na mahamuzi aliyofanya Zitto. Sio kupenda posho tu, kwani masaa ya kazi ni wajibu wako kufanya kazi si unalipwa mshaara wako wa kila mwezi. Ndio wenzetu uku wanavyo fanya, na shangaa Nnchi kama Tanzania ina malipo mengi sana ya posho za vikao sio Bunge tu, ata kwenye ofisi za serikali. Bless Up Zitto kwa uamuzi wako.
Ras Vin. Medical Instute Heidelberg.
Quote
 
 
+1 #74 macso 2011-06-10 12:33
Zitto anakubalika. Initiative kama hizi ndio tunataka Tanzania. Hongera Zitto. Hata kwenye tathmini watu wengi wanamkubali sana. Ukurasa wake umejaa sifa tofauti na za mafisadi tathmini.com/.../...
Quote
 
 
+2 #73 pechi 2011-06-10 12:32
kweli zito umenenea
Quote
 
 
+2 #72 zabronsimon 2011-06-10 12:26
hayo ni mawazo yako hafifu, haiwezekani mtu upo ofisini kwako eti ulipwe posho, Hongera Zitto, okoeni hizo bilion 280 za posho.
Quote
 
 
+2 #71 zabronsimon 2011-06-10 12:19
BIG UP!!!!!!!!!!!!! !!!!!!! ZITTO, JOHN CHILIGATI(CCM), NI FISADI, MNYONYAJI, HANA HURUMA, ETI POSHO WAANZE KUTOLIPWA UPINZANI, HALAFU CCM WATAANZA KUTOLIPWA MIAKA IJAYO, HUYO KIONGOZI NI FARA
Quote