Wednesday, December 14, 2011

SERIKALI IKITAMBUA MCHANGO WA WALIMU,ITAWAJALI HATA KWA MASLAHI

CWT: Hakuna mwalimu aliyelipwa mpaka sasa  Send to a friend
Tuesday, 13 December 2011 19:45
0digg
Rais wa CWT, Gratian Mukoba
Pamela Chilongola
CHAMA Cha Walimu Tanzania (CWT), kimesema hakuna mwalimu yoyote aliyelipwa malimbikizo ya stahili mbalimbali na mishahara kama ilivyotangazwa  na baadhi ya vyombo vya habari.

Juzi Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Philip Mulugo alipozungumza na gazeti moja la kila siku siyo Mwananchi, alisema Novemba, mwaka huu, serikali ilikuwa imelipa Sh29 bilioni, kati ya Sh49.6 bilioni zinazodaiwa na walimu. Lakini jana Rais wa CWT, Gratian Mukoba alisema: “Hadi leo (jana) hakuna mwalimu yeyote ambaye alikuwa amelipwa malimbikizo ya stahili zao au mishahara yao.”

Alisema tangu Juni mwaka huu, CWT na Serikali wamekuwa na vikao kadhaa kuhusu madai hayo.

“Sisi tunadai mishahara yetu  tuliyodhulumiwa, tunakandamizwa sisi walimu tunashangaa badala ya kutulipa hela tunazodai, tunashangaa kusikia wabunge wameongezewa posho na vitu vingine ambavyo vimefikia Sh330,000 milioni.“Msimamo wetu wa kugoma Januari mwakani uko palepale, hivyo hakuna mtu ambaye atatulaumu,  imeshapita miezi mine, serikali haijafanya kitu chochote kuhusu sisi walimu,”alisema Mukoba.

Alisema madai hayo yanawahusu walimu zaidi ya 3,000 ambao hawajalipwa kuanzia mwaka 2008.Mukoba alisema kero nyingine ambayo itawafanya wagome ni walimu walioshushwa vyeo mwaka 2007 na kutopandishwa mpaka sasa.“Na hii imetokana na waraka kandamizi uliotolewa na serikali mwaka 2007 ambao uliwashusha vyeo baada ya kujiendeleza kielimu.

“Serikali ilikubali kuufuta waraka huo baada ya kuridhika kwamba ulikuwa unawakandamiza walimu, lakini hadi sasa unaendelea kutumika, haujafutwa,” alisema Mukoba.   
Alisema kuna walimu ambao wanapata mishahara inayolingana na kwamba haijarekebishwa. “Utakuta mwalimu anaanza kazi anakuwa sawa na yule mwalimu aliyeanza muda mrefu.“Utakuta mwalimu amepanda daraja, lakini mshahara wake haujarekebishwa huku akiendela kupokea mshahara wa zamani,”alisema Mukoba

No comments:

Post a Comment