Saturday, September 10, 2011

TALAKA SI SURUHISHO LA MATATIZO YA UHUSIANO, SURUHISHO NI KUONGEA NA MWENZA WAKO

Watu bwana, wakikwaruzana ‘Nenda kwenu mbwa wee’…wengine ‘Nipe talaka hunifai!”
“MBWA wewe, najuta sijui kwanini nilikuoa, yaani kati ya wanawake, wewe si lolote, pumbavu kabisa….” Ni kati ya kauli ambazo wanawake wamekuwa wakikumbana nazo kwenye ndoa.

Kama wewe mwanamke uko kwenye ndoa ambayo haina majuto na kero, ni suala la kumshukuru Mungu. Ukweli ni kwamba kuna wanawake wengi wanateswa na wanaume.

Usione wanaume mitaani, usifikiri mwanaume ambaye unakwenda naye gesti na kuachana, ndivyo anavyokuwa kwenye ndoa, wengi ni kero. Si wengi ambao wanawaheshimu wake zao.

Baadhi ya wanaume ni wasomi, ni watu maarufu, lakini kwenye nyumba zao ni takataka. Hawana heshima kwa familia, ndio unaweza kuona kwa mfano baba mtu mzima, anakataa kutoa huduma kwa watoto, eti kisa kagombana na mkewe. Akili iko wapi ndugu yangu kama sio upumbavu?

Kuna wanaume, eti mkewe haruhisiwi kupanda kwenye gari, anapandisha machangudoa…huu ni upumbavu. Dalili kwamba huna akili ni kuendekeza vitu ambavyo haina maana katika maisha. Kuna wanaume wengi hawana akili. Wanachojua wao ni kutembea kwenye nyumba nzuri za starehe na makahaba.

“Mke wangu amekuwa kero, dawa yake naona ni ndogo tu kumchukua nyumba ndogo” ndivyo wengi wanavyojidanganya. Wanafikiri kwamba nyumba ndogo ni mali, lakini nyumba ndogo hawa ni wafanyabiashara, wanachokifanya ni kwamba anakusikiliza eeeh mke wangu hana maana, hanipi raha, eeeh ooh na ujinga mwingine mwingi unamwambia.
Yeye yuko kibiashara zaidi, kwamba anaangalia matatizo uliyonayo kisha anajitahidi kufanya kila linalowezekana kuhakikisha unapata raha, hasa kwa sababu anaamini yuko kibiashara kwa maana kuwa utampa fedha na mambo mengine kama haya.
Nyumba ndogo ni wezi, ni majambazi, na ni wafanyabiashara, baadhi yao huwa wanakuwa bize kujifunza namna ya kuwanasa wanaume. Kuna wengine wanasoma vitabu mbalimbali vya mahaba, ili kumnasa mwanaume asikumbuke kwao.
Kwa wanaume wasio na akili, wanafikiri wanayofanyiwa ni kwa upendo, kumbe hakuna lolote la maana. Bali kinachofanywa na nyumba ndogo ni kusaka njia za kuishi kupitia migongo ya hao wanaume.
Mwanaume mwenye akili timamu ataangalia namna ya kuondoa kasoro zilizoko kwenye nyumba yake. Ndugu zangu tunapokuwa na shamba kama kwa mfano umepanda mahindi na kumeota magugu, kinachofanyika sio kwamba huwa tunang’oa mahindi na kwenda kuyapanda kwenye shamba jingine, bali tunasaka dawa ya kuua magugu ili mahindi yaweze kuota vizuri.

Kuna wanawake pia wana kauli za ujeuri, eeeh kuna wengine kama ulimgusa jana, ukimwambia na leo tena nataka ‘tupigane’ anaanza kulalamika “aaah bwana eeeh nataka kupumzika, aaah jana umetaka na leo unataka kwani mimi ng’ombe, hata ng’ombe huwa wanapumzika’.

Kauli chafu hazitakiwi katika suala zima la ndoa. Kama kweli unaumwa au una jambo linakusumbua, ni suala la msingi kuzungumza taratibu. Acha kuwa mwenye kauli chafu kwa mkeo, acha kuwa na kauli chafu kwa mumeo.
Kuna watu wengeine, wakikwaruzana kidogo ‘Nenda kwenu mbwa wee’…wengine utawasikia wanasema ‘Nipe talaka hunifai!” Ndoa nzuri huwa inajengwa kwa maneno na fikra za kila mtu kuamini kuwa hata kama kunatokea migogoro, cha msingi ni kuangalia chanzo cha mgogoro na kuumaliza. Utaachana na wangapi?
Kuringa kwenye ndoa kwa sababu eti una mwanamke mwingine nje ya ndoa ni upumbavu…kuringa labda una mwanaume mwingine nje ya ndoa ni ujinga.Mtu mwenye akili sahihi na iliyo timamu, baada ya ndoa anachokiangalia ni namna ya kuboresha maisha yake.

Kuna wanaume wanawapiga sana wake zao, wanasema maneno mabaya. Lakini mwanaume kama kichwa cha familia, anapaswa kuwa na akili nzuri, anapaswa kuwa mfano wa kuigwa, kwa kuwa na kauli nzuri, sio ndio jamani?

Sasa kwabahati mbaya kuna watu ni vichwa, lakini matendo yao ni sawa na unyayo sijui maana hata nikisema ni sawa na kiuno bado hawafai. Je wewe mwanaume unaishije na mkeo au watoto kwenye familia yako? Eti kuna wanaume wanaamini nyumba ndogo ni kila kitu katika maisha…eti akigombana na mkewe ndio atakwenda kupata faraja!!!

Ndugu yangu mbona unakuwa huna akili kiasi hiki. Unapotoka nje, kwanza ni kwamba uniaibisha mwenyewe, yule ambaye uko naye kwa asilimia kubwa hata kama anakuchekea, kwanza anajua yuko kibiashara, lakini katika nafsi yake anaamini wewe ni mwanaume usiyefaa, kama uliyeweza kumdharau mkeo na watoto, utashindwa nini kumdharau yeye ambaye hauna naye mikataba yoyote?

Kama ni suala ni migogoro ndio inakumbikiza nyumbani, kwani unafikiri ni mtu gani ambaye unaweza kuishi naye bila kukwaruzana? Wewe umeishi kwenye tumbo la mama yako kwa miezi sijui tisa au chini ya hapo, na bado kuna wakati mnakwaruzana, iwe mtu tu mmekutana mitaani?

Migogoro ni jambo la kawaida katika uhusiano wa kimapenzi au ndoa. Cha msingi ni kufungua milango ya kujadiliana. Tatizo kubwa kuna watu wana kiburi kichafu kabisa, kwamba hawezi kusema nimekosa nisamehe….hata kama kweli amekosa. Ndoa haiwezi kwenda kokote kama watu wake hawako tayari kusameheana au kuomba msamaha

No comments:

Post a Comment