Saturday, September 10, 2011

FAINALI ZA MASHINDANO YA MISS TANZANIA NI LEO JUMAPILI TAREHE 11, 2011


KITENDAWILI cha nani ataibuka kuwa Vodacom Miss Tanzania 2011 kitateguliwa leo usiku ambapo warembo 30 kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania wakichuana kuwania taji hilo.

Ni ukweli usiofichika kuwa mashindano ya mwaka huu ambayo ni ya 18 tokea kuanzishwa kwake mwaka 1994 ni ya kihistoria kutokana na sababu mbali mbali. Mbili kubwa ni mashindano ambayo yatakuwa moja ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru na pili ni mshindi wa mwaka huu atazawadiwa zawadi nono tokea kunzishwa kwa mashindano hayo.

Mwaka huu mrembo atapewa zawadi ya Jeep Patriot model ya mwaka huu yenye thamani ya shs. Milioni 72 huku akipewa fedha taslimu sh. Milioni 8. Hii ni zawadi ya kihistoria kwani imevunja rekodi ya mwaka 2003 ya Sylvia Bahame ambaye alizawadiwa gari aina ya Nissan Hardbody yenye thamani ya shs milioni 55 na fedha taslimu shs. 7 million.

Ikumbukwe mwaka jana ambapo mrembo anayemaliza muda wake, Geneieve Mpangala alipewa gari maarufu kwa jina la Mkoko na fedha taslim shs milioni 10 na kufanya jumla ya zawadi zote kufikia milioni 20.

Hii ni hatua kubwa kwani tofauti ya shs milioni 60 si haba na zawadi ya kwanza imewafanya warembo wengi kupagawa kwani hawakuamini macho yao kile walichokuwa wanakiona.

Zawadi nyingine za washindi ni sh. Milioni 6.2 kwa mshindi wa pili, sh. 4 millioni kwa mshindi wa tatu na sh. Milioni 3 kwa mshindi wane. Mshindi wa tano atapewa sh. Milioni 2.4.

Warembo watakaoshika nafasi ya sita mpaka 15 watapewa sh. Milioni 1.2 na waliobaki (16-30) watapewa kifuta jasho cha sh. 700,000.

ìTunatarajia kuwa mashindano magumu sana, hii inatokana na zawadi ya mshindi wa kwanza ambayo warembo wengi wameelekeza nguvu zao huko kwa sababu ya ukubwa wake na vile vile kiu ya kuiwakilisha nchi katika mashindano ya Dunia (Miss world) mjini London,î alisema meneja masoko wa kampuni ya kuuza magari ya CFAO zamani DT Dobie, Alfred Minja.

Minja alisema kuwa wametambua na kuamua kurudisha hadhi ya mashindano hayo ili kuleta mvuto wake wa awali kwani mwaka 2005, Nancy Sumari alizawadiwa nyumba iliyojengwa kule Tabata.

Tofauti na miaka ya nyuma, mashindano ya mwaka huu ni yana ugumu wa aina yake kutokana na ukweli kuwa imekuwa vigumu kujua nani ataibuka mshindi tofauti na mwaka jana, juzi na miaka ya nyuma.

Genevieve Mpangala ambaye atalivua taji lake alionekana wazi wazi kuwa hana mpinzani na hata wakati wa Miriam Gerald na Nasreem Karim. Ukali wa warembo hao ulikuwa wa aina yake na kupewa nafasi hata kabla ya kupanda jukwaani.

Ni vigumu kutabiri nani mshindi, nimefuatilia maonyesho mbali mbali ya televisheni wakiwa kwenye nyumba na mengine, ushindani ni mkubwa sana, lakini mshindi ni mmoja tu,alisema Rodrick Mwambene ambaye kupitia duka la Mama Tike aliwahi kudhamini mashindano mbali mbali ya vituo.


WALIOINGIA TOP 15:
Mwajabu Juma (Temeke, Miss Top Model), Rose Hurbert (Kaskazini, Vipaji), Alexia Williams (Ilala, Miss Personality), Tracy Mabula (Kanda ya Ziwa, Miss Photogenic), Loveness Flavian (Kanda ya Mashariki, Mrembo bora wa michezo).


WANAOWANIA TOP 15:
Weirungu David, Neema Mtitu (Chuo Kikuu Huria), Cynthia Kinasha (Temeke), Zerulia Manoko, Christina Mwenegoha (Kanda ya Kati), Jeniffer Kakolaki, Salha Israel (Ilala), Dalila Ghribu, Maua Kimambo (Kanda ya Kati), Blessing Ngowi, Glory Lory (Elimu ya Juu), Stacey Alfred, Zubeda Seif (Kanda Kaskazini), Stella Mbuge, Husna Maulid, Hamisa Hussein (Kinondoni), Princess Chiaro Masonobo (Udsm), Atu Daniel, Leila Juma, Christine William (Nyanda za Juu Kusini) , Mariaclara Mathayo, Asha Saleh (Mashariki), Irene Karugaba, Glory Samwel (Kanda ya Ziwa).


Warembo wanaoiwakilisha Dar es Salaam:

Weirungu David, Neema Mtitu (Open University), Mwajabu, Cynthia Kinasha, Husna Twalib (Temeke), Alexia Williams, Jeniffer Kakolaki, Salha Israel (Ilala), Blessing Ngowi (Institute of Social work), Glory Lory (IFM), Stella Mbuge, Husna Maulid, Hamisa Hussein (Kinondoni), Princess Chiaro Masonobo (Udsm).


KIINGILIO: SHS. 100,000

BURUDANI
Diamond, kidumu, Juliana, Akili the Brains, Bob Junior maarufu kama Rais w Sharobaro,

MAJAJI WA MWAKA HUU:
Prashant Patel, Crescentius Magori, Victoria Lukindo, Cynthia Masaki, John Njoroge, Benard Mlunya , Javier Diz Rio, Martin Ngadada, Pratma Shah.

WAREMBO WA MIAKA YA NYUMA:
1994 -Aina Maeda,
1995- Emily Adolf
1996- Shose Sinare
1997 - Saida Kessy
1998- Basila Mwanakuzi
1999- Hoyce Temu
2000 - Jacqueline Ntuyabaliwe
2001- Happiness Magese
2002- Angela Damas
2003- Sylvia Bahame
2004- Faraja Kotta
2005 - Nancy Sumari alishinda taji la Miss World Africa
2006- Wema Sepetu
2007- Richa Adhia
2008- Nasreen Karim
2009- Miriam Gerald
2010 - Genevieve Emmanuel

No comments:

Post a Comment