Tuesday, December 11, 2012

KUMEKUCHA CCM NA CHADEMA VITANI TENA


“Lengo la kutoa mafunzo kwa wenyeviti na makatibu wa ni kuwajengea uwezo wa uwajibikaji, kudai haki zao ili kuleta hamasa kwa Watanzania kushiriki kikamilifu kwenye mchakato wa mabadiliko,” anasema Kigaila"

KUMALIZIKA kwa chaguzi za ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM kumeamsha joto la kisiasa nchini.
CCM na Chadema ndio hasa vyama vinavyoonekana kutolala. Kila kimoja kimeanzisha mbinu mpya ya kujijenga na kujiongezea wafuasi wanaokiunga mkono.
Nia ya vyama hivi ni moja, kujiongezea mtaji wa kukivusha katika uchaguzi mkuu wa 2015 na kushika dola.
Wakati CCM ‘mpya’ ikitajwa kuanza harakati za kupita mikoani na kutangaza mikakati ya kurejesha imani yake kwa wananchi, Chadema imeingia kambini kwa mbinu mpya za mashambulizi, hasa ngazi ya vijijini ili kuikaba koo CCM.
Safu mpya ya CCM
Katika kile walichokiita kurejesha imani ya wananchi kwa chama hicho, viongozi wa Sekretarieti wamefanya ziara ya kutathmini utekelezwaji wa ahadi zake kama zilivyoelekezwa katika ilani yake ya uchaguzi.
Wakiongozwa na Katibu wake, Abdulrahman Kinana, Makamu mwenyekiti, Philip Mangula wameanza mkakati huo kwa nia ya kuwaeleza wananchi kile kilichofanywa na Serikali yao inayoongoza.
Katika hatua ya kwanza ziara ilianzia Mtwara, ikihusisha mikoa minne, mingine ikiwa ni  Rukwa, Geita, kumalizia Arusha.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, anasema lengo la ziara hiyo katika maeneo hayo yenye fursa nyingi za maendeleo ni kuhakikisha wananchi wanapata majibu ya jinsi utekelezwaji wa ahadi za chama hicho tawala ulivyofanyika.
Anasema ziara hiyo inawahusisha mawaziri wa Serikali ambao wanatoa ufafanuzi wa masuala kadhaa, yakiwemo utekelezaji wa ahadi zikiwemo zilizotolewa mwaka 2010 wakati wa kampeni.
Harakati hizo za CCM zinakuja muda mfupi baada ya kupata viongozi wapya, ambao kwa nyakati tofauti, wameahidi kupambana na rushwa iliyokithiri nchini na ndani ya chama hicho.
Wakiwa mkoani Mtwara, kete ya viongozi hao ilichezwa kwenye matatizo ya wakulima wa korosho, zao ambalo ndilo tegemeo kwa wananchi wa mkoa huo. Pia waligusia bandari na miundombinu mingine ambapo waliahidi kuyafanyia kazi maeneo yote yaliyoonekana kusababisha kero kwa wananchi hao.
Mtindo huo wa CCM kutembea na mawaziri wa Serikali unaelezwa kuwa na manufaa kwani hutakiwa kutolea ufafanuzi utekelezaji uliofanywa na chama hicho, na pale ambapo kuna tatizo, hukumbushwa ili kuhakikisha kasoro hizo zinaondolewa haraka.
Katika baadhi ya maeneo katika mkoa huo viongozi hao wapya wamembana na changamoto ikiwemo kuzomewa kwa mawaziri, ambapo Kinana na Nape waliweza kutuliza hali hiyo kwa kukubali kasoro zilizoainishwa na wananchi na kuahidi kuzirekebisha.
Mawaziri waliokumbana na zomea zomea mni Hawa Ghasia (Serikali za Mitaa na tawala za Mikoa), Naibu wake, Aggrey Mwanri na Waziri Kilimo na Uahirika, Christopher Chiza.
Wananchi walieza kukerwa na hatua ya Serikali kuipeleka gesi inayochimbwa Dar es Salaam huku wananchi wa Mtwara wakikosa kunufaika na rasilimali hiyo.

No comments:

Post a Comment