Thursday, June 9, 2011

JAMANI HIVI KUBORESHA MASLAHI YA WAFANYA KAZI NI DHAMIRA YA KWELI?

Wednesday, 08 June 2011 
Mtumishi wa lililokuwa Shirika la Reli la Afrika Mashariki, Kituo cha Kigoma, Said Luziga (88) akifuatilia kupitia radio hotuba ya Bajeti ya mwaka wa fedha 2011/12, Dar es Salaam jana. Picha na Said Powa
Patricia Kimelemeta   SERIKALI  imeahidi kuboresha maslahi ya wafanyakazi wa sekta binafsi na watumishi wa umma ili waweze kuondokana na hali ngumu ya maisha.  Hayo yalisemwa na Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo wakati wa akiwasilisha bajeti ya mwaka 2011/12 kwenye kikao cha Bunge  kilichofanyika mjini Dodoma jana.

Mkulo alisema kuboreshwa  kwa maslahi ya watumishi wa umma kutatokana na uwezo wa mapato yake, jambo ambalo litawasaidia kumudu gharama za maisha.  “Serikali imeahidi kuboresha maslahi ya watumishi ikiwa ni pamoja na kuongeza mishahara kwa watumishi hao, lengo ni kuhakikisha kuwa wanamudu gharama zilizopo za maisha,"alisema Mkulo.  Alisema maeneo ambayo yatatiliwa mkazo ni pamoja na malipo ya mishahara na likizo kwa wakati, na kwamba watahakikisha watumishi hao wanalipwa mafao yao mara baada ya kustaafu, pamoja na pensheni zao za kila mwezi.

 Alisema sambamba na hilo,serikali itatoa mafunzo kwa maofisa wa Hazina ndogo na mahakama zote zinazoshughulikia mirathi, na kuweka mikakati ya pamoja kuwaondolea kero wasimamizi na warithi wa mali za marehemu ambao walikuwa watumishi wa serikali enzi za uhai wao.

 Mwaka jana, serikali ilitumia zaidi ya Sh2.332 trilioni kwa ajili ya kugharimia malipo ya mishahara,ajira mpya, upandishwaji vyeo na kulipia madai ya malimbikizo na mapunjo ya mishahara kwa watumishi wa Serikali Kuu na Serikali za Mitaa.  Katika bajeti hiyo ya mwaka jana, Mkulo alitangaza punguzo la asilimia moja kwa kodi ya mishahara kutoka asilimia 15 hadi 14 ya mishahara hiyo.

Nalo Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi(Tucta), liliwahi kuwasilisha mapendekezo ya mishahara ya watumishi wa umma na sekta binafsi ambapo kiwango cha chini lilitaka kiwe  Sh315,000 kwa mwezii, lakini serikali ilishindwa kuongeza kiasi hicho badala yake iliongeza  hadi Sh135,000  mwaka jana

No comments:

Post a Comment