Saturday, April 30, 2011

MUUNGANO NIUTAKAO MIMI MWANANCHI WA KAWAIDA

Kumekuwa na hoja nyingi kuhusu muungano viswa vya Zanzibar na Tanganyika,ambavyo vyot kwa pamoja viliiunda Tanzania,waasisi wa muungano huo marehemu mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Shehe Abeid Karume walilenga kukuza na kudumisha undungu baina ya watanganyika na wazanzibara. Muungano ambao juzi umetimiza miaka 47 umepoteza malengo ya awali ya kujenga na kudumisha undugu,nionavyo mimi ubinafsi wa viongozi wa kisiasa walioshika dola baada ya waasisi Nyerere na karume ndio chanzo cha chokochoko za muungano.Nionavyo mimi waasisi wa muungano walifikia hatua ya kwanza ambayo ilizaa serikari ndogo ya Zanzibar na Serikari ya muungano wa Tanzania, hivyo ingekuwa jukumu la viongozi wa sasa kuendelea kujenga na kudumisha undugu kwa kendeleza hatua ya pili kwa kufanya serikari mbili kuwa serikari moja ya Tanzania yenye raisi mmoja tu badala ya serikari tatu au mbili ambazo zimekuwa zikipigiwa upato. Sioni kwanini viongozi wa kisiasa wanaendeleza kuweka vitu ambavyo kwa namna moja au nyingine ndio vyanzo vya chokochoko za muungano wetu? kulikuwa na na haja ipi kwa zanzibar sehemu ya Tanzania kuwa na Bendera yake,wimbo wake wa taifa,majeshi yake na serikari yake? viongozi wa kisiasa tuache ubinafsi, sisi wananchi wa kawaida tungependa kuona muungano wa zanzibar na Tanganyika unazaa serikari moja chini ya raisi mmoja ili kuwa na nguvu za kuharakisha maendeleo ya Tanzania kwa ujumla wake! Kuna ugumu upi zanzibar ambayo wakazi wake ni takribani millioni moja sawa na idadi ya watu katika mikoa mingine tanzania,kuongozwa na wakuu wa mikoa kama ilivyo kwa mikoa mingine?hakika kero za muungano zitakoma pale ambapo tanzania itakuwa na serikari moja tu.

No comments:

Post a Comment